Paite

Swahili: New Testament

Romans

1

1Paula, Jesu Kris sikha, sawltak hi dinga sap, Pathian Tanchin Hoih lama khenkhiak,
1Kutoka kwangu mimi Paulo, mtumishi wa Kristo Yesu, na mtume niliyeteuliwa na kuitwa kwa ajili ya kuhubiri Habari Njema ya Mungu.
2huai tuh Pathianin tuma lama laisiangthoua a jawlneitea achiamsa,
2Hapo kale, Mungu aliwaahidia watu hii Habari Njema kwa njia ya manabii wake katika Maandiko Matakatifu.
3A tapa, sa lama David suana piang tungtang tanchin hoih.
3Hii Habari Njema inamhusu Mwana wa Mungu, Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye mintarafu ubinadamu wake, alikuwa mzawa wa Daudi;
4Siangthouna kha lam thua misi laka thohnawnnaa Pathian Tapa thilhihtheihna toh hi dinga genkhiak thu; Jesu Kris i Toupa ngei tuh,
4mintarafu utakatifu wake wa kimungu, alithibitishwa kwa uwezo mkuu kwamba ni Mwana wa Mungu kwa kufufuliwa kutoka wafu.
5a min jiaka ginna nam chih laka mi gingta sak dingin, amah jiakin hehpihna leh sawltak hihna i tangta hi;
5Kwa njia yake, mimi nimepewa neema ya kuwa mtume, ili kwa ajili yake niwaongoze watu wa mataifa yote wapate kuamini na kutii.
6huai lakah nou leng Jesu Kris sapte na hi uhi:
6Ninyi ni miongoni mwa watu hao; mmeitwa muwe watu wake Yesu Kristo.
7Rome khua Pathian deihtak, mi siangthoua om dinga sapte tengteng kiangah: Pathian i Pa leh Toupa Jesu Kris kianga kipan hehpihna leh lemna na kiang uah om hen.
7Basi, ninawaandikia ninyi nyote mlioko Roma ambao Mungu anawapenda, akawateua muwe watu wake. Nawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.
8Khovel tengtengah na ginna thu uh a than jiakin na vek ua tungah ka kipahnathu Jesu Kris jiakin ka Pathian kiangah ka gen masa phot ahi.
8Awali ya yote, namshukuru Mungu wangu kwa njia ya Yesu Kristo kwa ajili yenu nyote, kwa sababu imani yenu inasikika duniani kote.
9Ka thumnate ah, tawplouin na min uh ka lou nilouhlouh hi, chih, a Tapa Tanchin Hoiha ka khaa a na ka sep gige Pathian tuh kei hontheihpihpa ahi ngala;
9Mungu, ambaye ninamtumikia kwa moyo wangu wote katika kuhubiri Habari Njema ya Mwanae, ni shahidi wangu kwamba ninawakumbukeni
10Tu beka na kiang ua ka hongna dingin Pathian thuthua zin hun lemtang ka muh teitei theihna ding ngenin.
10daima katika sala zangu. Namwomba Mungu akipenda, anipatie nafasi nzuri ya kuja kwenu sasa.
11Na kipna ding ua kha lam thilpiak bang hiam nou ka honpiak theihna dingin nou honmuh ka ut thei mahmah ngala;
11Kwa maana ninatamani sana kuwaoneni ili nipate kuwagawieni zawadi ya kiroho na kuwaimarisha.
12Huai tuh na ginna uh leh ka ginnaa i kikhamuan tuah theihna dingin, ka chihna ahi.
12Ndiyo kusema, tutaimarishana: imani yenu itaniimarisha mimi, na yangu itawaimarisha ninyi.
13Huan, unaute aw, Jentel dangte kianga ka sep gim gah ka muh tak bangmahin, noumau lakah leng gahte ka muh theihna dingin na kiang uah tamvei pi hong ka tumta chih na theih louh uh ka deih kei hi; himahleh, tuma tengin dalin ka om gige nak hi.
13Ndugu zangu, nataka mjue kwamba mara nyingi nilikusudia kuwatembeleeni, lakini mpaka sasa nimezuiwa. Ningependa kupata mafanikio mema kati yenu kama nilivyopata kati ya watu wa mataifa mengine.
14Grik mite leh melmakte kiangah bat ka nei a; mi pil leh mi pilloute kiangah leng.
14Ninalo jukumu kwa watu wote, waliostaarabika na wasiostaarabika, wenye elimu na wasio na elimu.
15Huchiin, nou Rome khuaa omte kiang ah leng Tanchin Hoih gen ka ut mahmah hi.
15Ndiyo maana ninatamani pia kuihubiri Habari Njema kwenu ninyi mlioko huko Roma.
16Tanchin Hoih tuh ka zahpih keia; kuapeuh a gingta phota dingin hotdamna dinga Pathian thilhihtheihna ahi ngala; atungin Juda mi adin ahi a, huan, Grik mi adingin leng a honghi nawn hi.
16Sioni aibu kutangaza Habari Njema; yenyewe ni nguvu ya Mungu inayowaokoa wote wanaoamini: Wayahudi kwanza, na wasio Wayahudi pia.
17Huaiah tuh gin semsemna dingin, ginnain Pathian diktatna latsakin a om; Ginna jiaka midiktat tuh a hing ding, chi-a gelh bangin.
17Kwa maana Habari Njema inaonyesha wazi jinsi Mungu anavyowakubali watu kuwa waadilifu; jambo hili hufanyika kwa imani, tangu mwanzo mpaka mwisho. Kama ilivyoandikwa: "Mwadilifu kwa imani ataishi."
18Thutak diklou taka dalte Pathian limsaklouhna leh diktatlouhna tengteng tungah van akipanin Pathian hehna a hongkilangta ngala;
18Ghadhabu ya Mungu imedhihirishwa kutoka mbinguni dhidi ya uasi na uovu wote wa binadamu ambao kwa njia zao mbaya wanaupinga ukweli usijulikane.
19Pathianin a theihsak tak jiakin Pathian tanchin theihtheih ding tuh a lungsim uah chiangtaka theih sakin a om ngala.
19Kwa maana, yote yanayoweza kujulikana juu ya Mungu ni wazi kwao; maana Mungu mwenyewe ameyadhirisha.
20Khovel siamtunga kipan a pianken muhtheihlouh, a tangtawn thilhihtheihna leh a Pathianna, thilsiam te achiantaka muh ahi; huaijiakin paulam ding a neikei uh;
20Tangu Mungu alipoumba ulimwengu, uwezo wake wa milele na uungu wake, ingawa havionekani kwa macho, vinafahamika wazi. Watu wanaweza kuyajua mambo hayo kutokana na vitu hivyo alivyoumba Mungu. Kwa hiyo hawana njia yoyote ya kujitetea!
21Pathian theingala Pathian bangin a pahtawi kei ua, kipahthu leng a gen sam kei uhi; thil thulimlou a ngaihtuah zota ua, a lungtang hai uh a hongmialta hi.
21Ingawa wanajua kuna Mungu, lakini hawampi heshima anayostahili, wala hawamshukuru. Badala yake, fikira zao zimekuwa batili na akili zao tupu zimejaa giza.
22Pil kisa khemin mihai a hongsuak ua,
22Wanajidai kuwa wenye hekima, kumbe ni wapumbavu.
23sitheilou Pathian thupina sethei mihingte leh vasate, gamsate leh bokvak ganhingte limin a suaksak uhi.
23Wanaacha kumwabudu Mungu aishiye milele, na badala yake, wanaabudu sanamu zilizo mfano wa binadamu ambaye hufa, mfano wa wanyama, ndege, au wanyama watambaao.
24Huaijiakin a sa uh zumhuaipia kibawltuah dingin a lungtang uh duhgawlna banga thilnin hih phalin Pathianin a lehngatsan hi.
24Kwa sababu hiyo, Mungu amewaacha wafuate tamaa mbaya za mioyo yao na kufanyiana mambo ya aibu kwa miili yao.
25Pathian thutak tuh juaua tangsakin, a Bawlpa biak sangin a bawl niain a na a sem zota uhi. A Bawlpa tuh khantawna phat tuak ahi, Amen.
25Wanaubadili ukweli juu ya Mungu kwa uongo; wanaheshimu na kuabudu kiumbe badala ya Muumba mwenyewe, ambaye ndiye astahiliye sifa milele! Amina.
26Huai jiakin Pathianin zahhuaipia huk phalin lehlam a ngatsan ahi; a numeite nangawn un leng a omdan pianpih uh danlou banga om dingin a kibawl lamdang ngal ua;
26Kwa hiyo, Mungu amewaacha wafuate tamaa mbaya. Hata wanawake wanabadili matumizi yanayopatana na maumbile.
27pasalten leng numei zatdan ngeina tawpsana, hukin a kienlah ua, pasal leh pasal zummoh thil hihin a om ua, a gitlouh man muh ding uh tuh a satung uah a mu uhi.
27Nao wanaume hali kadhalika, wanaacha kufuata matumizi ya maumbile ya mume na mke wakawakiana tamaa wao kwa wao. Wanaume wanafanyiana mambo ya aibu, na hivyo wanajiletea wenyewe adhabu wanayostahili kwa vitendo vyao viovu.
28Huan, Pathian theih a ut louh jiak un, thil kilawmloute hih dinga a deih louhlam lungsim neih phalin Pathianin a lehngatsante;
28Kwa vile watu walikataa kumtambua Mungu, Mungu amewaacha katika fikira zao potovu, wakafanya yale ambayo hawangestahili kufanya.
29Huchin diktatlouhna tengteng, gitlouhna tengteng, huaihamna tengteng, huatna tengteng khawng in, a nadim ua; hajatna te, tual thahna te, kiselna te, khemna te, nundan hoih lou tein a dim ua;
29Wamejaa kila aina ya uovu, dhuluma, ulafi na ufisadi. Wamejaa wivu, uuaji, ugomvi, udanganyifu na nia mbaya; husengenya,
30gensiatna te, migenna te, Pathian huat lam te, kisaktheihna te, kisatheimite, thil gilou bawlkhete,
30na kusingiziana; ni watu wa kuchukiza kwa Mungu, wafidhuli, wenye kiburi na majivuno; hodari sana katika kutenda mabaya, na hawawatii wazazi wao;
31nu leh pa thu mangloute, theihna beite, thuchiam susete, itna pianpih neiloute, hehpihna neiloute ahi ua.Huchi banga hihte tuh si tak him ahi uh chih Pathian dan tuh thei gigein, amau kiaa hih leng hi louin, mi dang hih jelte tungah leng a kipak uhi.
31hawana dhamiri, hawatimizi ahadi zao, hawana wema wala huruma kwa wengine.
32Huchi banga hihte tuh si tak him ahi uh chih Pathian dan tuh thei gigein, amau kiaa hih leng hi louin, mi dang hih jelte tungah leng a kipak uhi.
32Wanajua kwamba Sheria ya Mungu yasema kwamba watu wanaoishi mithili hiyo, wanastahili kifo. Zaidi ya hayo, siyo tu kwamba wanafanya mambo hayo wao wenyewe, bali hata huwapongeza wale wanaofanya mambo hayohayo.