Paite

Swahili: New Testament

Romans

2

1Huaijiakin, mihing aw, mi selhat kuapeuh himahlechin, pau lam himhim na neikei hi; midang na selna mahah nangmah leh nangmah siamlouh kitang sak na hi; nang selhatin leng huchibang thilte tuh na hih sam ngala.
1Basi, rafiki, kama unawahukumu wengine, huwezi kamwe kujitetea haidhuru wewe ni nani. Kwa maana, kwa kuwahukumu wengine, unajilaani wewe mwenyewe kwa vile nawe unayafanya mambo yaleyale unayohukumu.
2Huchibang thil hih nakte tungah Pathian vaihawmna tuh diktak in a tung chih i thei ngala.
2Tunajua kwamba hukumu ya Mungu kwa wale wanaofanya mambo kama hayo ni hukumu ya haki.
3Mihing aw, huchibang thil hih nakte gensia, nang leng huchibang na hih sam ngal naka Pathian vaihawmna pelh na kigingta ahia?
3Lakini wewe, rafiki, unayewahukumu wale wanaofanya mambo kama hayo bali wewe pia unayafanya, je unadhani utaiepa hukumu ya Mungu?
4A hihkeileh, Pathian hoihna tuh kisiknaa nang honpi dinga om ahi chih theilouin, a hoihna, a thuaktheihna leh, a dohtheihna hauhnate na ngaineu ahi a?
4Au labda unaudharau wema wake mkuu, uvumilivu wake na saburi yake, bila kutambua kwamba wema wake huo una shabaha ya kukuongoza upate kutubu?
5Na chihmoh leh na lungtang khauh jiakin, hehna leh Pathian vaihawmna diktat hongkilatna ni chiang adingin, na tungah hehna na kikhol khawm tawm ahi.
5Lakini unao ugumu na ukaidi wa moyo, na hivyo unajilundikia adhabu kwa Siku ile ambayo ghadhabu ya Mungu na hukumu zake za haki vitadhihirishwa.
6Pathianin mi chih a thil hih bang jel un a hawmsak dinga;
6Siku hiyo Mungu atamlipa kila mmoja kufuatana na matendo yake.
7thil hoih hih teiteia, thupina leh pahtawina leh manthat theihlouhna zong mite kiangah, khantawn hinna a pe ding;
7Wale wanaozingatia kutenda mema, kutafuta utukufu na heshima ya Mungu na kutokufa, watapata uzima wa milele.
8a hihhangin, genhaka, thutak jui lou a, gitlouhna jui zote tungah, hehna leh thangpaihna te, haksatna leh lungkhamna thupitakte a om dia;
8Lakini wale wengine wenye ubinafsi, wenye kukataa mambo ya haki na kufuata uovu, wataangukiwa na ghadhabu na hasira ya Mungu.
9mihing thil hihkhial tengteng kha tungah a om ding, Juda mi kha tungah a masa dia, huan, Grik mi kha tungah a om nawn ding.
9Mateso na maumivu yatampata binadamu yeyote atendaye uovu. Yatawapata Wayahudi kwanza, na watu wa mataifa mengine pia.
10Ahihhangin, thil hoih hih peuhmah kiangah thupinate, pahtawina te, khamuanna te piak ahi ding, Juda mi kiangah piak ahi masa dia, huan, Grik mi kiangah ahi nawn ding.
10Lakini Mungu atawapa utukufu, heshima na amani wale wanaotenda mema; Wayahudi kwanza, na watu wa mataifa mengine pia.
11Pathianin mi deihsk tuam a nein gal keia.
11Maana Mungu hambagui mtu yeyote.
12Kuapeuh dan neiloua thil hihkhial tuh, dan louin a mangthang ding hi; huan, kuapeuhmah dan neia thil hihkhial tuh, dana vaihawmin a om ding.
12Wale wanaotenda dhambi bila kuijua Sheria ya Mose wataangamia ingawaje hawajui Sheria. Na wale wanaotenda dhambi wakiwa wanaijua Sheria watahukumiwa kisheria.
13Dan zami phette tuh Pathian mitmuhin mi dik ahi kei ua; dan juite tuh mi dik a hizo ding uh.
13Mtu hafanywi kuwa mwadilifu mbele yake Mungu kwa kuisikia Sheria, bali kwa kuitii Sheria.
14Dan neilou Jentelten amau pianpiha dan thilte a hih un, huaiten dan neikeimahleh uh, amau leh amau danin a kinei tawm ngal ua.
14Mathalan: watu wa mataifa mengine hawana Sheria ya Mose; lakini kila wanapotimiza matakwa ya Sheria wakiongozwa na dhamiri zao, wao wenyewe wanakuwa kipimo cha Sheria ingawa hawaijui Sheria.
15A lungtang uah dan thilhih gelh ahi chih a ensak uh, huai tuh a sia leh pha theihna un a theihpih hi; a lungsimte uh tuh a kisela, a thupukna-un siamlouh a tan hiam siam a tan hiam ahi ding,
15Mwenendo wao unaonyesha kwamba matakwa ya Sheria yameandikwa mioyoni mwao. Dhamiri zao zinashuhudia pia jambo hilo, maana fikira zao mara nyingine huwashtaki, na mara nyingine huwatetea.
16ka Tanchin Hoih gen banga, mihingte thugukte Pathianin, Jesu Krisa, a ngaihtuah ni chiangin.
16Hivyo, kufuatana na hii Habari Njema ninayohubiri, ndivyo itakavyokuwa wakati Mungu atakapohukumu mambo ya siri ya binadamu kwa njia ya Yesu Kristo.
17Himahleh, nang Juda kichi na hi a, dan na muanga, Pathian na suanga,
17Na wewe, je? Wewe mwenyewe unajiita Myahudi; unaitumainia Sheria na kujivunia kuwa wa Mungu;
18a deihlam na theia, thil hoihjaw te hoih na saa, dana hilhin na om a,
18kwa njia ya Sheria unajua matakwa ya Mungu na unaweza kuchagua jambo jema;
19nangmah mah mittawte pipa, mial laka omte vakna hiin na kigingta a;
19wewe unajiona kuwa kiongozi wa vipofu na mwanga kwa wale walio gizani;
20dan ah pilna leh thutak omdan na theih jiakin, mi pilloute hilhpilpa, naungekte hilhpain nakigingta hi;
20unajiona kuwa mkufunzi wa wajinga na mwalimu wa wale wasiokomaa bado. Unayo katika Sheria picha kamili ya elimu na ukweli.
21huchibang na hih ngal leh, nang, midangte hilhpa, nangmah na kihilh ka hia? Nang, mi guta lou dia hilhpa, nang nag u nak maw?
21Basi, wewe unawafundisha wengine; kwa nini hujifundishi wewe mwenyewe? Unawahubiria wengine wasiibe, lakini kumbe wewe mwenyewe unaiba.
22Nang, angkawm lou dia hilhpa, nang ang na kawm nak maw? Nang, milim hopa, nang milim biakina thilte nag u nak maw?
22Unasema: "Msizini," na huku wewe unazini; unachukia sanamu za miungu hali wewe unajitajirisha kwa kuiba katika nyumba za miungu.
23Nang, dan suangpa, nang dana na tatlek jiakin Pathian na hihminse jel ahi maw?
23Kwa kujigamba ati unayo Sheria ya Mungu, je huoni kwamba kwa kuivunja Sheria unamdharau Mungu?
24A gelh bang ngei un Pathian min tuh noumau jiakin Jentelte lakah hihsiatin a om ta hi.
24Kama vile Maandiko Matakatifu yasemavyo: "Watu wa mataifa mengine wamelikufuru jina la Mungu kwa sababu yenu ninyi Wayahudi!"
25Dan juipa na hih leh zeksum a phatuam ngial hi; dana talekpa na hih lebel, na zeksum tuh sum louh bang phet a honghita hi.
25Kutahiriwa kwako kutakuwa na maana kama ukiitii Sheria. Lakini kama unaivunja Sheria, basi, ni afadhali ungalibaki bila kutahiriwa.
26Huaijiakin, zeksum lou miin dan thu sehte a zuih leh, a zeksum louh tuh sum banga sim ahi kei dia hia?
26Kama mtu wa mataifa mengine ambaye hakutahiriwa akitimiza matakwa ya Sheria, hakika atafikiriwa kana kwamba ametahiriwa.
27Huan, amau saa zeksum louhin dan a zuih kim uleh, nang, danthu gelh leh zeksum nei ngala, dana talekpa a honmohpaih kei ding ua hia?
27Watu wa mataifa mengine watakuhukumu wewe Myahudi kama ukiivunja Sheria, ingawaje unayo maandishi ya Sheria na umetahiriwa, hali wao wanaitii Sheria ingawa hawakutahiriwa.
28Alang lela Juda mi hi jaw Juda mi tak ahi kei hi; a langa sa lela zeksum jaw zeksum tak leng ahi sam kei hi.Ahihhangin, a lang lel hi loua, Juda mi hi, Juda mi tak ahi; huan, zeksum tak tuh, lungsim lama sum ahi, lai thu phetah hi louin, kha ah ahi; huai miin tuh mihing phat a loh keia, Pathian phat a loh jaw ahi.
28Ndiyo kusema, si kila anayeonekana kwa nje kuwa Myahudi ni Myahudi wa kweli, wala mtu hawi Myahudi wa kweli ati kwa kuwa ametahiriwa kimwili.
29Ahihhangin, a lang lel hi loua, Juda mi hi, Juda mi tak ahi; huan, zeksum tak tuh, lungsim lama sum ahi, lai thu phetah hi louin, kha ah ahi; huai miin tuh mihing phat a loh keia, Pathian phat a loh jaw ahi.
29Myahudi wa kweli ni yule aliye Myahudi kwa ndani, yaani yule ambaye ametahiriwa moyoni. Hili ni jambo la Roho, na si jambo la maandishi ya Sheria. Mtu wa namna hiyo anapata sifa, si kutoka kwa watu, bali kutoka kwa Mungu.