1Paweł, powołany Apostoł Jezusa Chrystusa przez wolę Bożą, i Sostenes brat.
1Mimi Paulo, niliyeitwa kuwa mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na ndugu Sosthene,
2Zborowi Bożemu, który jest w Koryncie, poświęconym w Chrystusie Jezusie, powołanym świętym, ze wszystkimi, którzy wzywają imienia Pana naszego Jezusa Chrystusa na wszelkiem miejscu, i ich, i naszem.
2tunawaandikia ninyi mlio kanisa la Mungu huko Korintho. Ninyi mmefanywa watakatifu katika kuungana na Kristo Yesu, mkaitwa muwe watu wa Mungu, pamoja na watu wote popote wanaomwomba Bwana wetu Yesu Kristo aliye Bwana wao na wetu pia.
3Łaska wam i pokój niech będzie od Boga, Ojca naszego, i od Pana Jezusa Chrystusa.
3Nawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana wetu Yesu Kristo.
4Dziękuję Bogu mojemu zawsze za was dla łaski Bożej, która wam jest dana w Chrystusie Jezusie,
4Ninamshukuru Mungu wangu daima kwa ajili yenu kwa sababu amewatunukia ninyi neema yake kwa njia ya Kristo Yesu.
5Iżeście we wszystkiem ubogaceni w nim we wszelkiej mowie i we wszelkiej znajomości;
5Maana, kwa kuungana na Kristo mmetajirishwa katika kila kitu. Mmejaliwa elimu yote na uwezo wote wa kuhubiri,
6Jako świadectwo Chrystusowe utwierdzone jest w was,
6kwani, ujumbe juu ya Kristo umethibitishwa ndani yenu,
7Tak iż wam na żadnym darze nie schodzi, którzy oczekujecie objawienia Pana naszego Jezusa Chrystusa.
7hata hampungukiwi kipaji chochote cha kiroho mkiwa mnangojea kufunuliwa kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
8Który was też utwierdzi aż do koóca, abyście byli bez nagany w dzieó Pana naszego, Jezusa Chrystusa.
8Yeye atawaimarisha ninyi mpaka mwisho mpate kuonekana bila hatia Siku ile ya Bwana wetu Yesu Kristo.
9Wiernyć jest Bóg, przez którego jesteście powołani ku społeczności Syna jego, Jezusa Chrystusa, Pana naszego.
9Mungu ni mwaminifu; yeye aliwaita ninyi muwe na umoja na Mwanae Yesu Kristo Bwana wetu.
10A proszę was, bracia! przez imię Pana naszego, Jezusa Chrystusa, abyście toż mówili wszyscy, a iżby nie były między wami rozerwania, ale abyście byli spojeni jednakim umysłem i jednakiem zdaniem.
10Ndugu, ninawasihi kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo: pataneni nyote katika kila jambo msemalo; yasiweko mafarakano kati yenu; muwe na fikira moja na nia moja.
11Albowiem oznajmiono mi o was, bracia moi! od domowników Chloi, iż poswarki są między wami.
11Ndugu zangu, habari nilizopata kutoka kwa watu kadhaa wa jamaa ya Kloe, zaonyesha wazi kwamba kuna kutoelewana kati yenu.
12A to powiadam, iż każdy z was mówi: Jamci jest Pawłowy, a jam Apollosowy, a jam Kiefasowy, alem ja Chrystusowy.
12Nataka kusema hivi: kila mmoja anasema chake: mmoja husema, "Mimi ni wa Paulo," mwingine: "Mimi ni wa Apolo," mwingine: "Mimi ni wa Kefa," na mwingine: "Mimi ni wa Kristo,".
13Rozdzielonyż jest Chrystus? Azaż Paweł za was ukrzyżowany? Alboście w imię Pawłowe ochrzczeni?
13Je, Kristo amegawanyika? Je, Paulo ndiye aliyesulubiwa kwa ajili yenu? Au je, mlibatizwa kwa jina la Paulo?
14Dziękuję Bogu, żem żadnego z was nie chrzcił, oprócz Kryspa i Gajusa;
14Namshukuru Mungu kwamba sikumbatiza mtu yeyote miongoni mwenu isipokuwa tu Krispo na Gayo.
15Aby kto nie rzekł, żem chrzcił w imię moje.
15Kwa hiyo hakuna awezaye kusema amebatizwa kwa jina langu.
16Ochrzciłem też i dom Stefanowy; nadto nie wiem, jeźlim kogo drugiego ochrzcił.
16(Samahani, nilibatiza pia jamaa ya Stefana; lakini zaidi ya hawa, sidhani kama nilimbatiza mtu mwingine yeyote.)
17Boć mnie nie posłał Chrystus chrzcić, ale Ewangieliję kazać, wszakże nie w mądrości mowy, aby nie był wyniszczony krzyż Chrystusowy.
17Kristo hakunituma kubatiza, bali kuhubiri Habari Njema; tena, niihubiri bila kutegemea maarifa ya hotuba za watu kusudi nguvu ya kifo cha Kristo msalabani isibatilishwe.
18Albowiem mowa o krzyżu tym, którzy giną, jest głupstwem; ale nam, którzy bywamy zbawieni, jest mocą Bożą.
18Maana ujumbe kuhusu kifo cha Kristo msalabani ni jambo la kipumbavu kwa wale walio katika mkumbo wa kupotea, lakini kwetu sisi tulio katika njia ya wokovu ujumbe huo ni nguvu ya Mungu.
19Bo napisano: Wniwecz obrócę mądrość mądrych, a rozum rozumnych odrzucę.
19Maana Maandiko Matakatifu yasema: "Nitaiharibu hekima yao wenye hekima, na elimu ya wataalamu nitaitupilia mbali."
20Gdzież jest mądry? Gdzież jest uczony w Piśmie? Gdzież badacz wieku tego? Izali w głupstwo nie obrócił Bóg mądrości świata tego?
20Yu wapi basi, mwenye hekima? Yu wapi basi, mwalimu wa Sheria? Naye bingwa wa mabishano wa nyakati hizi yuko wapi? Mungu ameifanya hekima ya ulimwengu kuwa upumbavu.
21Albowiem ponieważ w mądrości Bożej świat nie poznał Boga przez mądrość, upodobało się Bogu przez głupie kazanie zbawić wierzących,
21Maana, kadiri ya hekima ya Mungu, watu hawawezi kumjua Mungu kwa njia ya hekima yao wenyewe. Badala yake, Mungu amependa kuwaokoa wale wanaoamini kwa njia ya kile ambacho wenye hekima wanakiona kuwa ni upumbavu, yaani ujumbe tunaohubiri.
22Gdyż i Żydowie się cudów domagają, a Grekowie mądrości szukają.
22Wayahudi wanataka ishara, na Wagiriki wanatafuta hekima;
23Ale my każemy Chrystusa ukrzyżowanego, Żydom wprawdzie zgorszenie, a Grekom głupstwo;
23lakini sisi tunamhubiri Kristo aliyesulubiwa. Kwa Wayahudi jambo hili ni kikwazo, na kwa watu wa mataifa ni upumbavu;
24Lecz samym powołanym i Żydom, i Grekom każemy Chrystusa, który jest mocą Bożą i mądrością Bożą.
24lakini kwa wale walioitwa, Wayahudi kwa Wagiriki, Kristo ni nguvu ya Mungu na hekima ya Mungu.
25Albowiem głupstwo Boże jest mędrsze niż ludzie; a mdłość Boża jest mocniejsza niż ludzie.
25Maana kinachoonekana kuwa ni upumbavu wa Mungu, kina busara zaidi kuliko hekima ya binadamu; na kinachoonekana kuwa ni udhaifu wa Mungu, kina nguvu zaidi kuliko nguvu za binadamu.
26Widzicie zaiste powołanie wasze, bracia! iż niewiele mądrych według ciała, niewiele możnych, niewiele zacnego rodu;
26Ndugu, kumbukeni wakati mlipoitwa: wengi wenu hawakuwa wenye hekima hata kwa fikira za binadamu; wengi hawakuwa wenye nguvu au watu wa tabaka ya juu.
27Ale co głupiego jest u świata tego, to wybrał Bóg, aby zawstydził mądrych, a co mdłego u świata, wybrał Bóg, aby zawstydził mocnych.
27Ndiyo kusema, Mungu aliyachagua yale ambayo ulimwengu huyaona ni upumbavu, ili awaaibishe wenye hekima; na aliyachagua yale ambayo ulimwengu huyaona ni dhaifu, ili awaaibishe wenye nguvu.
28A podłego rodu u świata i wzgardzone wybrał Bóg, owszem te rzeczy, których nie masz, aby te, które są, zniszczył.
28Mungu ameyachagua yale ambayo kwa fikira za dunia ni mambo yaliyo duni na yanayodharauliwa, mambo ambayo hata hayakuwako, ili kwa hayo ayafutilie mbali yale ambayo kwa fikira za binadamu ni mambo ya maana.
29Aby się nie chlubiło żadne ciało przed obliczem jego.
29Basi, hakuna mtu awezaye kujivunia chochote mbele ya Mungu.
30Lecz z niego wy jesteście w Chrystusie Jezusie, który się nam stał mądrością od Boga i sprawiedliwością, i poświęceniem, i odkupieniem,
30Mungu mwenyewe ndiye aliyewaunganisha ninyi na Kristo Yesu. Mungu amemfanya Kristo awe hekima yetu; kwa njia yake sisi tunapatanishwa na Mungu, tunakuwa watu wake Mungu na kukombolewa.
31Aby, jako napisano: Kto się chlubi, w Panu się chlubił.
31Basi, kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Mwenye kutaka kujivuna, basi, na ajivunie kazi ya Bwana."