1A zalecam wam Febę, siostrę naszę, która jest służebnicą zboru Kienchreeóskiego;
1Napenda kumjulisha kwenu dada yetu Foibe ambaye ni mtumishi katika kanisa la Kenkrea.
2Abyście ją przyjęli w Panu, jako przystoi świętym, i stali przy niej, w którejkolwiek by was rzeczy potrzebowała; albowiem i ona wielom gospody użyczała, aż i mnie samemu.
2Mpokeeni kwa ajili ya Bwana kama iwapasavyo watu wa Mungu. Mpeni msaada wowote atakaohitaji kutoka kwenu, maana yeye amekuwa mwema sana kwa watu wengi na kwangu pia.
3Pozdrówcie Pryscyllę i Akwilę, pomocniki moje w Chrystusie Jezusie;
3Salamu zangu ziwafikie Priska na Akula, wafanyakazi wenzangu katika utumishi wa Kristo Yesu.
4(Którzy za duszę moję swojej własnej szyi nadstawiali; którym nie ja sam dziękuję, ale i wszystkie zbory pogaóskie.)
4Wao walihatarisha maisha yao kwa ajili yangu. Wanastahili shukrani; si tu kutoka kwangu, bali pia kutoka kwa makanisa yote ya watu wa mataifa mengine.
5Także zbór, który jest w domu ich. Pozdrówcie Epeneta miłego mojego, który jest pierwiastkiem Achai do Chrystusa.
5Salamu zangu pia kwa kanisa linalokutana nyumbani kwao. Salamu zangu zimfikie rafiki yangu Epaineto ambaye ni kwa kwanza katika mkoa wa Asia kumwamini Kristo.
6Pozdrówcie Maryję, która wiele pracowała dla nas.
6Nisalimieni Maria ambaye amefanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu.
7Pozdrówcie Andronika i Junijasza, krewnych moich i spółwięźni moich, którzy znacznymi są między Apostołami, którzy i przede mną byli w Chrystusie.
7Salamu zangu kwa Androniko na Yunia, wananchi wenzangu waliofungwa gerezani pamoja nami; wao wanajulikana sana kati ya mitume; tena walikuwa Wakristo kabla yangu mimi.
8Pozdrówcie Amplijasa, miłego mojego w Panu.
8Salamu zangu kwa Ampliato, rafiki yangu katika kuungana na Bwana.
9Pozdrówcie Urbana, pomocnika naszego w Chrystusie i Stachyna mnie miłego.
9Salamu zangu zimfikie Urbano, mfanyakazi mwenzangu katika utumishi wa Kristo; salamu zangu pia kwa rafiki yangu Staku.
10Pozdrówcie Apellesa doświadczonego w Chrystusie. Pozdrówcie tych, którzy są z domu Arystobulowego.
10Nisalimieni Apele ambaye uaminifu wake kwa Kristo umethibitishwa. Salamu zangu kwa wote walio nyumbani mwa Aristobulo.
11Pozdrówcie Herodijona, pokrewnego mojego. Pozdrówcie tych, którzy są z domu Narcyssowego, tych, którzy są w Panu.
11Salamu zangu kwa Herodiana, mwananchi mwenzangu; na kwa jamaa yote ya Narkisi iliyojiunga na Bwana.
12Pozdrówcie Tryfenę i Tryfosę, które pracują w Panu. Pozdrówcie Persydę miłą, która wiele pracowała w Panu.
12Nisalimieni Trufena na Trufosa wanaofanya kazi katika utumishi wa Bwana, na rafiki yangu Persi ambaye amefanya mengi kwa ajili ya Bwana.
13Pozdrówcie Rufa, wybranego w Panu i matkę jego, i moję.
13Nisalimieni Rufo, mtu hodari sana katika kazi ya Bwana, na mama yake ambaye ni mama yangu pia.
14Pozdrówcie Asynkryta, Flegonta, Hermana, Patrobę, Hermena i braci, którzy są z nimi.
14Nisalimieni Asunkrito, Flegoni, Herme Patroba, Herma na ndugu wote walio pamoja nao.
15Pozdrówcie Filologa i Juliję, Nerego i siostrę jego, i Olimpa, i wszystkich świętych, którzy są z nimi.
15Nisalimieni Filologo na Yulia, Nerea na dada yake, na Olumpa, pamoja na watu wote wa Mungu walio pamoja nao.
16Pozdrówcie jedni drugich z pocałowaniem świętem. Pozdrawiają was zbory Chrystusowe.
16Salimianeni ninyi kwa ninyi kwa ishara ya upendo. Salamu kwenu kutoka kwa makanisa yote ya Kristo.
17A proszę was, bracia! abyście upatrywali tych, którzy czynią rozerwania i zgorszenia przeciwko tej nauce, którejście się wy nauczyli; i chroócie się ich.
17Ndugu zangu, nawasihi muwafichue wote wanaosababisha mafarakano na kuwafanya watu wengine waanguke, kinyume cha mafundisho mliyofundishwa. Jiepusheni na watu hao,
18Albowiem takowi Panu naszemu Jezusowi Chrystusowi nie służą, ale własnemu brzuchowi swemu, a przez łagodną mowę i pochlebstwo serca prostych zwodzą.
18maana watu wa namna hiyo hawamtumikii Kristo Bwana wetu, bali wanayatumikia matumbo yao wenyewe. Kwa maneno yao matamu na hotuba za kubembeleza hupotosha mioyo ya watu wanyofu.
19Bo posłuszeóstwo wasze wszystkich doszło. A przetoż raduję się z was; ale chcę, abyście byli mądrymi na dobre, a prostymi na złe.
19Kila mtu amesikia juu ya utii wenu na hivyo mmekuwa sababu ya furaha yangu. Nawatakeni muwe na hekima katika mambo mema, na bila hatia kuhusu mambo mabaya.
20A Bóg pokoju zetrze szatana pod nogi wasze w rychle. Łaska Pana naszego Jezusa Chrystusa niech będzie z wami. Amen.
20Naye Mungu aliye chanzo cha amani hatakawia kumponda Shetani chini ya miguu yenu. Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi.
21Pozdrawiają was Tymoteusz, pomocnik mój, i Lucyjusz, i Jazon, i Sosypater, pokrewni moi.
21Timotheo, mfanyakazi mwenzangu, anawasalimu. Hali kadhalika Lukio, Yasoni, na Sosipatro, wananchi wenzangu, wanawasalimu.
22Pozdrawiam was w Panu ja Tercyjusz, którym ten list pisał.
22Nami Tertio, ninayeandika barua hii nawasalimuni katika Bwana.
23Pozdrawia was Gajus, gospodarz mój i wszystkiego zboru. Pozdrawia was Erastus, szafarz miejski, i Kwartus brat.
23Gayo, mwenyeji wangu, pamoja na kanisa lote linalokutana kwake, anawasalimu. Erasto, mweka hazina wa mji huu, pamoja na Kwarto, wanawasalimu.
24Łaska Pana naszego Jezusa Chrystusa niech będzie z wami wszystkimi. Amen.
24Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi nyote. Amina.
25A temu, który was może utwierdzić według Ewangielii mojej i opowiadania Jezusa Chrystusa, według objawienia tajemnicy od czasów wiecznych zamilczanej,
25Basi, sasa na tumsifu Mungu! Yeye anaweza kuwaimarisheni katika ile Habari Njema niliyohubiri juu ya ujumbe wa Yesu Kristo, na katika ile siri iliyofunuliwa na ambayo ilikuwa imefichika kwa karne nyinyi zilizopita.
26Lecz teraz objawionej i przez Pisma prorockie według postanowienia wiecznego Boga ku posłuszeóstwu wiary między wszystkimi narody oznajmionej;
26Lakini, sasa ukweli huo umefunuliwa kwa njia ya maandiko ya manabii; na kwa amri ya Mungu wa milele umedhihirisha kwa mataifa yote ili wote waweze kuamini na kutii.
27Temu, samemu mądremu Bogu niech będzie chwała przez Jezusa Chrystusa na wieki. Amen.
27Kwake Mungu aliye peke yake mwenye hekima, uwe utukufu kwa njia ya Yesu Kristo, milele na milele! Amina.