1I ja, bracia! nie mogłem wam mówić jako duchownym, ale jako cielesnym i jako niemowlątkom w Chrystusie.
1Ndugu, mimi sikuweza kusema nanyi kama watu mlio na huyo Roho. Nilipaswa kusema nanyi kama watu wa kidunia, kama watoto wachanga katika maisha ya Kikristo.
2Napawałem was mlekiem, a nie karmiłem was pokarmem; boście jeszcze nie mogli znieść, owszem i teraz jeszcze nie możecie,
2Ilinibidi kuwalisheni kwa maziwa, na si kwa chakula kigumu, kwani hamkuwa tayari kukipokea. Hata sasa hamko tayari.
3Gdyż jeszcze cielesnymi jesteście. Bo ponieważ między wami jest zazdrość i swary, i rozterki, azażeście nie cieleśni i według człowieka nie chodzicie?
3Maana bado mu watu wa kidunia. Je, si kweli kwamba bado uko wivu na magombano kati yenu? Mambo hayo yanaonyesha wazi kwamba ninyi bado ni watu wa kidunia, mnaishi mtindo wa kidunia.
4Albowiem gdy kto mówi: Jam jest Pawłowy, a drugi: Jam Apollosowy, azaż cielesnymi nie jesteście?
4Mmoja wenu anaposema, "Mimi ni wa Paulo", na mwingine, "Mimi ni wa Apolo", je, hiyo haionyeshi kwamba mnaishi bado kama watu wa dunia hii tu?
5Bo któż jest, Paweł? Kto Apollos? jedno słudzy, przez którycheście uwierzyli, a to jako każdemu Pan dał.
5Apolo ni nani? na Paulo ni nani? Sisi ni watumishi tu ambao tuliwaleteeni ninyi imani. Kila mmoja wetu anafanya kazi aliyopewa na Bwana.
6Jam szczepił, Apollos polewał, ale Bóg wzrost dał.
6Mimi nilipanda mbegu, Apolo akamwagilia maji; lakini aliyeiotesha mbegu ni Mungu.
7A tak, ani ten, co szczepi, jest czem, ani ten, co polewa, ale Bóg, który wzrost daje.
7Wa maana si yule aliyepanda mbegu, au yule aliyemwagilia maji; wa maana ni Mungu aliyeiwezesha mbegu kuota.
8Lecz ten, który szczepi, i ten, który polewa, jedno są, a każdy swoję zapłatę weźmie według pracy swojej.
8Yule aliyepanda na yule aliyemwagilia maji wote ni sawa, ingawa kila mmoja atapokea tuzo lake kufuatana na jitihada yake mwenyewe.
9Albowiem jesteśmy pomocnikami Bożymi, wy Bożą rolą, Bożym budynkiem jesteście.
9Maana sisi ni ndugu, wafanyakazi pamoja na Mungu; na ninyi ni shamba lake; ninyi ni jengo lake.
10Według łaski Bożej, która mi jest dana, jako mądry budownik założyłem grunt, a drugi na nim buduje: wszakże każdy niechaj baczy, jako na nim buduje.
10Kwa msaada wa neema aliyonipa Mungu, nimefaulu, kama mwashi stadi mwenye busara, kuweka msingi ambao juu yake mtu mwingine anajenga. Basi, kila mmoja awe mwangalifu jinsi anavyojenga juu yake.
11Albowiem gruntu innego nikt nie może założyć, oprócz tego, który jest założony, który jest Jezus Chrystus.
11Hakuna mtu awezaye kuweka msingi mwingine badala ya ule uliokwisha wekwa, yaani Yesu Kristo.
12A jeźli kto na tym gruncie buduje złoto, srebro, kamienie drogie, drwa, siano, słomę,
12Juu ya msingi huo mtu anaweza kujenga kwa dhahabu, fedha au mawe ya thamani; anaweza kutumia miti, majani au nyasi.
13Każdego robota jawna będzie; bo to dzieó pokaże, gdyż przez ogieó objawiona będzie, a każdego roboty, jaka jest, ogieó doświadczy.
13Iwe iwavyo, ubora wa kazi ya kila mmoja utaonekana wakati Siku ile ya Kristo itakapoifichua. Maana, Siku hiyo itatokea na moto, na huo moto utaipima na kuonyesha ubora wake.
14Jeźli czyja robota zostanie, którą na nim budował, zapłatę weźmie.
14Ikiwa alichojenga mtu juu ya huo msingi kitaustahimili huo moto, atapokea tuzo;
15Jeźli czyja robota zgore, ten szkodę podejmie; lecz on sam będzie zachowany, wszakże tak jako przez ogieó.
15lakini kama alichojenga kitaunguzwa, basi, atapoteza tuzo lake; lakini yeye mwenyewe ataokolewa kana kwamba ameponyoka kutoka motoni.
16Azaż nie wiecie, iż kościołem Bożym jesteście, a Duch Boży mieszka w was?
16Je, hamjui kwamba ninyi ni hekalu la Mungu, na kwamba Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?
17A jeźli kto gwałci kościół Boży, tego Bóg skazi, albowiem kościół Boży święty jest, którym wy jesteście.
17Basi, mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu; maana hekalu la Mungu ni takatifu, na hekalu hilo ni ninyi wenyewe.
18Niechajże nikt samego siebie nie zwodzi; jeźli się kto sobie zda być mądrym między wami na tym świecie, niech się stanie głupim, aby się stał mądrym.
18Msijidanganye! Mtu yeyote miongoni mwenu akijidhania mwenye hekima mtindo wa kidunia, heri awe mjinga kusudi apate kuwa na hekima ya kweli.
19Albowiem mądrość tego świata głupstwem jest u Boga; bo napisano: Który chwyta mądrych w chytrości ich;
19Maana, hekima ya kidunia ni upumbavu mbele ya Mungu. Kwani Maandiko Matakatifu yasema: "Mungu huwanasa wenye hekima katika ujanja wao."
20I zasię: Pan zna myśli mądrych, iż są marnością.
20Na tena: "Bwana ajua kwamba mawazo ya wenye hekima hayafai."
21A tak niech się nikt nie chlubi ludźmi; albowiem wszystkie rzeczy są wasze.
21Basi, mtu asijivunie watu. Maana kila kitu ni chenu.
22Bądź Paweł, bądź Apollos, bądź Kiefas, bądź świat, bądź żywot, bądź śmierć, bądź przytomne, bądź przyszłe rzeczy, wszystkie są wasze;
22Paulo, Apolo na Kefa, ulimwengu, maisha na kifo; mambo ya sasa na ya baadaye, yote ni yenu.
23Aleście wy Chrystusowi, a Chrystus Boży.
23Lakini ninyi ni wa Kristo naye Kristo ni wa Mungu.