Polish

Swahili: New Testament

1 Corinthians

6

1Śmież kto z was, mając sprawę z drugim, sądzić się przed niesprawiedliwymi, a nie przed świętymi?
1Anathubutuje mmoja wenu kumshtaki ndugu muumini mbele ya mahakama ya watu wasiomjua Mungu badala ya kumshtaki mbele ya watu wa Mungu?
2Azaż nie wiecie, iż święci będą sądzili świat? A jeźli świat od was będzie sądzony, czyliście niegodni, abyście sądy mniejsze odprawiali?
2Je, hamjui kwamba watu wa Mungu watauhukumu ulimwengu? Ikiwa basi, ulimwengu utahukumiwa nanyi, kwa nini hamstahili kuhukumu hata katika mambo madogo?
3Azaż nie wiecie, iż Anioły sądzić będziemy? A cóż tych doczesnych rzeczy?
3Je, hamjui kwamba, licha ya kuhukumu mambo ya kawaida ya kila siku, tutawahukumu hata malaika?
4Przeto jeźlibyście mieli sądy o rzeczy doczesne, tych, którzy są najpodlejsi we zborze, na sąd wysadzajcie.
4Mnapokuwa na mizozo juu ya mambo ya kawaida, je, mnawaita wawe mahakimu watu ambao hata hawalijali kanisa?
5Ku zawstydzeniu waszemu to mówię. Nie maszże między wami mądrego i jednego, który by mógł rozsądzić między braćmi swoimi?
5Aibu kwenu! Ndiyo kusema hakuna hata mmoja miongoni mwenu mwenye hekima kiasi cha kuweza kutatua tatizo kati ya ndugu waumini?
6Ale się brat z bratem prawuje, i to przed niewiernymi?
6Badala yake, kweli imekuwa mtindo ndugu kumpeleka ndugu yake mahakamani, tena mbele ya mahakimu wasioamini.
7Już tedy zapewne jest między wami niedostatek, że się z sobą prawujecie. Czemuż raczej krzywdy nie cierpicie? Czemuż raczej szkody nie podejmujecie?
7Kwa kweli huko kushtakiana tu wenyewe kwa wenyewe kwabainisha kwamba mmeshindwa kabisa! Je, haingekuwa jambo bora zaidi kwenu kudhulumiwa! Haingekuwa bora zaidi kwenu kunyang'anywa mali yenu?
8Owszem wy krzywdzicie i do szkody przywodzicie, a to braci.
8Lakini, badala yake, ninyi ndio mnaodhulumu na kunyang'anya; tena, hayo mnawafanyia ndugu zenu!
9Azaż nie wiecie, iż niesprawiedliwi królestwa Bożego nie odziedziczą? Nie mylcie się: ani wszetecznicy, ani bałwochwalcy, ani cudzołożnicy, ani pieszczotliwi, ani samcołożnicy,
9Au je, hamjui kwamba watu wabaya hawataurithi Utawala wa Mungu? Msijidanganye! Watu wanaoishi maisha ya uasherati, wanaoabudu sanamu, wazinzi, au walawiti,
10Ani złodzieje, ani łakomcy, ani pijanicy, ani złorzeczący, ani ździercy królestwa Bożego nie odziedziczą.
10wevi, wachoyo, walevi, wasengenyaji, wanyang'anyi, hao wote hawatashiriki Utawala wa Mungu.
11A takimiście niektórzy byli; aleście omyci, aleście poświęceni, aleście usprawiedliwieni w imieniu Pana Jezusa i przez Ducha Boga naszego.
11Baadhi yenu mlikuwa hivyo; lakini sasa mmeoshwa, mkafanywa watakatifu, na kupatanishwa na Mungu kwa jina la Bwana Yesu Kristo na kwa Roho wa Mungu wetu.
12Wszystko mi wolno, ale nie wszystko pożyteczno; wszystko mi wolno, ale ja się nie dam zniewolić żadnej rzeczy.
12Mtu anaweza kusema: "Kwangu mimi kila kitu ni halali." Sawa; lakini si kila kitu kinafaa. Nakubali kwamba kila kitu ni halali kwangu lakini sitaki kutawaliwa na kitu chochote.
13Pokarmy brzuchowi należą, a brzuch pokarmom; ale Bóg i brzuch i pokarmy skazi; lecz ciało nie należy wszeteczeóstwu ale Panu, a Pan ciału.
13Unaweza kusema: "Chakula ni kwa ajili ya tumbo, na tumbo ni kwa ajili ya chakula." Sawa; lakini Mungu ataviharibu vyote viwili. Mwili wa mtu si kwa ajili ya uzinzi bali ni kwa ajili ya kumtumikia Bwana, naye Bwana ni kwa ajili ya mwili.
14Bo Bóg i Pana wzbudził, i nas wzbudzi mocą swoją.
14Basi, Mungu aliyemfufua Bwana kutoka wafu atatufufua nasi pia kwa nguvu yake.
15Azaż nie wiecie, iż ciała wasze są członkami Chrystusowymi? Wziąwszy tedy członki Chrystusowe, czyli je uczynię członkami wszetecznicy? Nie daj tego Boże!
15Je, hamjui kwamba miili yenu ni viungo vya mwili wa Kristo? Je, mnadhani naweza kuchukua sehemu ya mwili wa Kristo na kuifanya kuwa sehemu ya mwili wa kahaba? Hata kidogo!
16Azaż nie wiecie, iż ten, co się złącza z wszetecznicą, jednem ciałem z nią jest? albowiem mówi: Będą dwoje jednem ciałem.
16Maana, kama mjuavyo, anayeungana na kahaba huwa mwili mmoja naye--kama ilivyoandikwa: "Nao wawili watakuwa mwili mmoja."
17A kto się złącza z Panem, jednym duchem jest z nim.
17Lakini aliyejiunga na Bwana huwa roho moja naye.
18Uciekajcie przed wszeteczeóstwem. Wszelki grzech, który by człowiek popełnił, oprócz ciała jest; lecz kto wszeteczeóstwo płodzi, przeciwko swemu własnemu ciału grzeszy.
18Jiepusheni kabisa na uzinzi. Dhambi nyingine zote hutendwa nje ya mwili lakini mzinzi hutenda dhambi dhidi ya mwili wake mwenyewe.
19Azaż nie wiecie, iż ciało wasze jest kościołem Ducha Świętego, który w was jest, którego macie od Boga? a nie jesteście sami swoi;
19Je, hamjui kwamba miili yenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, ambaye mlimpokea kutoka kwa Mungu? Ninyi basi, si mali yenu wenyewe.
20Albowiemeście drogo kupieni. Wysławiajcież tedy Boga w ciele waszym i w duchu waszym, które są Boże.
20Mlinunuliwa kwa bei kubwa. Kwa hiyo, itumieni miili yenu kwa ajili ya kumtukuza Mungu.