Polish

Swahili: New Testament

1 Corinthians

9

1Izalim nie jest Apostołem? Izalim nie jest wolnym? Izalim Jezusa Chrystusa, Pana naszego nie widział? Izali wy nie jesteście pracą moją w Panu?
1Je, mimi si mtu huru? Je, mimi si mtume? Je, mimi sikumwona Yesu Bwana wetu? Je, ninyi si matokeo ya kazi yangu kwa ajili ya Bwana?
2Choćbym innym nie był Apostołem, alem wam jest; albowiem pieczęcią apostolstwa mego wy jesteście w Panu.
2Hata kama kwa watu wengine mimi si mtume, lakini walau kwenu ninyi mimi ni mtume. Ninyi ni uthibitisho wa mtume wangu kwa sababu ya kuungana kwenu na Bwana.
3Tać jest obrona moja przeciwko tym, którzy mię sądzą.
3Hoja yangu kwa wale wanaonipinga ndiyo hii:
4Izali nie mamy wolności jeść i pić?
4Je, hatuna haki ya kula na kunywa?
5Izali nie mamy wolności wodzić z sobą siostry żony, jako i drudzy Apostołowie i bracia Paóscy, i Kiefas?
5Je, hatuna ruhusa kumchukua mke Mkristo katika ziara zetu, kama vile wafanyavyo mitume wengine, ndugu zake Bwana, na pia Kefa?
6Izali ja tylko i Barnabasz nie mamy wolności, abyśmy nie pracowali?
6Au ni mimi tu na Barnaba ambao tunapaswa kujipatia maslahi yetu kwa kufanya kazi?
7Któż kiedy służy żołnierkę swoim kosztem? Któż sadzi winnicę, a owocu jej nie pożywa? Albo któż trzodę pasie, a mleka trzody nie pożywa?
7Je, mwanajeshi gani anayelipia utumishi wake jeshini? Mkulima gani asiyekula matunda ya shamba lake la mizabibu? Mchungaji gani asiyekunywa maziwa ya mifugo yake?
8Izali to obyczajem ludzkim mówię? Izali i zakon tegoż nie mówi?
8Je, nasema mambo haya kibinadamu tu? Je, Sheria nayo haisemi hivyo?
9Albowiem w zakonie Mojżeszowym napisano: Nie zawiążesz gęby wołowi młócącemu; izali się Bóg o woły stara?
9Imeandikwa katika Sheria ya Mose: "Usimfunge kinywa ng'ombe anapoliwata nafaka." Je, ndio kusema Mungu anajishughulisha na ng'ombe?
10Czyli zgoła dla nas to mówi? Albowiem dla nas to napisano; gdyż w nadziei ma orać ten, co orze, a kto młóci w nadziei, nadziei swojej ma być uczestnikiem.
10Je, hakuwa anatufikiria sisi aliposema hivyo? Naam, haya yaliandikwa kwa ajili yetu; kwani yule anayelima na yule anayevuna, wote wawili wana haki ya kutumaini kupata sehemu ya mavuno.
11Ponieważeśmy my wam duchowne dobra siali, wielkaż to, gdybyśmy wasze cielesne żęli?
11Ikiwa sisi tumepanda mbegu ya kiroho kati yenu, je, ni jambo kubwa tukichuma kwenu faida ya kidunia?
12Jeźliż insi tej wolności nad wami używają, czemuż nie raczej my? A wszakżeśmy tej wolności nie używali, ale wszystko znaszamy, abyśmy jakiego wstrętu Ewangielii Chrystusowej nie uczynili.
12Ikiwa wengine wanayo haki ya kutazamia hayo kutoka kwenu, je, sisi hatuna haki zaidi kuliko hao? Lakini, sisi hatukuitumia haki hiyo, Badala yake, tumestahimili kila kitu ili tusiiwekee kizuizi chochote Habari Njema ya Kristo.
13Azaż nie wiecie, iż ci, którzy około rzeczy świętych pracują, z świętych rzeczy jadają? a którzy ołtarza pilnują, spólną cząstkę z ołtarzem mają?
13Je, hamjui kwamba wanaotumikia Hekaluni hupata chakula chao Hekaluni, na kwamba wanaotolea sadaka madhabahuni hupata sehemu ya hiyo sadaka?
14Tak też Pan postanowił tym, którzy Ewangieliję opowiadają, aby z Ewangielii żyli.
14Bwana aliagiza vivyo hivyo; wahubiri wa Habari Njema wapate riziki zao kutokana nayo.
15Alem ja nic z tych rzeczy nie używał. I nie pisałem tego, aby się tak przy mnie działo; bo mnie daleko lepiej umrzeć, niżby kto przechwalanie moje miał próżnem uczynić.
15Lakini, mimi sikutumia hata mojawapo ya haki hizo. Na wala siandiki nijipatie haki hizo; kwangu mimi ni afadhali kufa kuliko kumfanya yeyote aone kwamba najisifu bure.
16Bo jeźli Ewangieliję opowiadam, nie mam się czem chlubić, gdyż ta powinność na mnie leży; a biada mnie, jeźlibym Ewangielii nie opowiadał.
16Ikiwa ninaihubiri Habari Njema, hilo si jambo la kujivunia; hilo ni jukumu nililopewa. Na, ole wangu kama sitaihubiri Habari Njema!
17Albowiem jeźli to dobrowolnie czynię, mam zapłatę; jeźli poniewolnie, szafarstwa mi powierzono.
17Ningekuwa nimeichagua kazi hii kwa hiari, basi, ningetazamia malipo; lakini maadam naifanya ikiwa ni wajibu, hiyo ina maana kwamba ni jukumu nililopewa nitekeleze.
18Jakąż tedy mam zapłatę? Abym Ewangieliję opowiadając, bez nakładu wystawił Ewangieliję Chrystusową, na to, żebym źle nie używał wolności mojej przy Ewangielii.
18Mshahara wangu ni kitu gani, basi? Mshahara wangu ni fursa ya kuihubiri Habari Njema bure, bila kudai haki ninazostahili kwa kuihubiri.
19Albowiem będąc wolnym od wszystkich, samegom siebie uczynił niewolnikiem wszystkim, abym ich więcej pozyskał.
19Kwa hiyo, ingawa mimi si mtumwa wa mtu yeyote, nimejifanya mtumwa wa kila mtu ili nimpatie Kristo watu wengi iwezekanavyo.
20I stałem się Żydom jako Żyd, abym Żydów pozyskał; a tym, którzy są pod zakonem, jakobym był pod zakonem, abym tych, którzy są pod zakonem, pozyskał;
20Kwa Wayahudi nimeishi kama Myahudi ili niwapate Wayahudi; yaani, ingawa mimi siko chini ya Sheria, nimejiweka chini ya Sheria kwao, ili niwapate hao walio chini ya Sheria.
21Tym, którzy są bez zakonu, jakobym bez zakonu, (nie będąc bez zakonu Bogu, ale będąc pod zakonem Chrystusowi), abym pozyskał tych, którzy są bez zakonu.
21Na kwa wale walio nje ya Sheria, naishi kama wao, nje ya Sheria, ili niwapate hao walio nje ya Sheria. Hii haimaanishi kwamba mimi niko nje ya sheria ya Mungu, maana nabanwa na sheria ya Kristo.
22Stałem się mdłym jako mdły, abym mdłych pozyskał. Wszystkim stałem się wszystko, abym przecię niektórych zbawił.
22Kwao walio dhaifu nimejifanya dhaifu ili niwapate hao walio dhaifu. Nimejifanya kila kitu kwa wote ili nipate kuwaokoa baadhi yao kwa kila njia.
23A to czynię dla Ewangielii, abym się jej stał uczestnikiem.
23Nafanya haya yote kwa ajili ya Habari Njema, nipate kushiriki baraka zake.
24Azaż nie wiecie, iż ci, którzy w zawód bieżą, wszyscyć więc bieżą, lecz jeden zakład bierze? Także bieżcie, abyście otrzymali.
24Je, hamjui kwamba katika uwanja wa michezo, ingawa wapiga mbio wote hukimbia, ni mmoja tu anayejinyakulia zawadi?
25A każdy, który się potyka, we wszystkiem się powściąga, onić wprawdzie, aby wzięli koronę skazitelną, ale my nieskazitelną.
25Wanariadha hujipa mazoezi na nidhamu kali; hufanya hivyo ili wajipatie taji iharibikayo! Lakini sisi twafanya hivyo tupate taji ya kudumu daima.
26Ja tedy tak bieżę, nie jako na niepewne; tak szermuję, nie jako wiatr bijąc.
26Ndivyo basi, ninavyopiga mbio nikiwa na nia ya kushinda; ndivyo ninavyopigana, na si kama bondia anayetupa ngumi zake hewani.
27Ale karzę ciało moje i w niewolę podbijam, abym snać inszym każąc, sam nie był odrzucony.
27Naupa mwili wangu mazoezi magumu na kuutia katika nidhamu kamili, nisije mimi mwenyewe nikakataliwa baada ya kuwahubiria wengine.