1Dziatki moje! to wam piszę, abyście nie grzeszyli; i jeźliby kto zgrzeszył, mamy orędownika u Ojca, Jezusa Chrystusa sprawiedliwego;
1Watoto wangu, ninawaandikieni mambo haya, kusudi msitende dhambi. Lakini, ikijatokea mtu akatenda dhambi, tunaye mmoja ambaye hutuombea kwa Baba, ndiye Yesu Kristo aliye mwadilifu kabisa.
2A on jest ubłaganiem za grzechy nasze; a nie tylko za nasze, ale też za grzechy wszystkiego świata.
2Kristo ndiye sadaka iondoayo dhambi zetu; wala si dhambi zetu sisi tu, bali pia dhambi za ulimwengu wote.
3A przez to wiemy, żeśmy go poznali, jeźli przykazania jego zachowujemy.
3Tukizitii amri za Mungu, basi, tunaweza kuwa na hakika kwamba tunamjua.
4Kto mówi: Znam go, a przykazania jego nie zachowuje, kłamcą jest, a prawdy w nim nie masz.
4Mtu akisema kwamba anamjua, lakini hazitii amri zake, basi mtu huyo ni mwongo, na ukweli haumo ndani yake.
5Lecz kto by zachował słowa jego, prawdziwie się w tym miłość Boża wykonała; przez to znamy, iż w nim jesteśmy.
5Lakini mtu yeyote anayeshika neno la Mungu, huyo ndiye aliye na upendo kamili wa Mungu ndani yake. Hivi ndivyo tunavyoweza kuwa na hakika kwamba tunaungana naye:
6Kto mówi, że w nim mieszka, powinien, jako on chodził, i sam także chodzić.
6mtu yeyote anayesema kwamba ameungana na Mungu, anapaswa kuishi kama alivyoishi Yesu Kristo.
7Bracia! nie nowe przykazanie wam piszę, ale przykazanie stare, któreście mieli od początku; a to stare przykazanie jest ono słowo, któreście słyszeli od początku.
7Wapenzi wangu, amri hii ninayowaandikieni si amri mpya; ni amri ileile ya zamani mliyokuwa nayo tangu mwanzo. Amri hiyo ya zamani ni ule ujumbe mliousikia.
8Zasię przykazanie nowe piszę wam, które jest prawdziwe w nim i w was; iż ciemność przemija, a prawdziwa ona światłość już świeci.
8Hata hivyo, amri hii ninayowaandikieni ni amri mpya, na ukweli wake unaonekana ndani ya Kristo na ndani yenu pia. Maana giza linatoweka, na mwanga wa ukweli umekwisha anza kuangaza.
9Kto mówi, iż jest w światłości, a brata swego nienawidzi, w ciemności jest aż dotąd.
9Yeyote asemaye kwamba yumo katika mwanga, lakini anamchukia ndugu yake, mtu huyo bado yumo gizani.
10Kto miłuje brata swego, w światłości mieszka i zgorszenia w nim nie masz.
10Yeyote ampendaye ndugu yake, yuko katika mwanga, na hamna chochote ndani yake kiwezacho kumkwaza mtu mwingine.
11Lecz kto nienawidzi brata swego, w ciemności jest i w ciemności chodzi, a nie wie, gdzie idzie, iż ciemność zaślepiła oczy jego.
11Lakini anayemchukia ndugu yake, yumo gizani; anatembea gizani, na hajui anakokwenda, maana giza limempofusha.
12Piszę wam, dziatki! iż wam są odpuszczone grzechy dla imienia jego.
12Ninawaandikieni ninyi watoto, kwa kuwa dhambi zenu zimeondolewa kwa jina la Kristo.
13Piszę wam, ojcowie! żeście poznali tego, który jest od początku. Piszę wam, młodzieócy! żeście zwyciężyli onego złośnika.
13Nawaandikieni ninyi kina baba kwani mnamjua yeye ambaye amekuwako tangu mwanzo, Nawaandikieni ninyi vijana kwa sababu mmemshinda yule Mwovu.
14Piszę wam, dziateczki! żeście poznali Ojca. Pisałem wam, ojcowie! żeście poznali onego, który jest od początku. Pisałem wam, młodzieócy! że jesteście mocni, a słowo Boże mieszka w was, a żeście zwyciężyli onego złośnika.
14Nawaandikieni ninyi watoto, kwa sababu mnamjua Baba. Nawaandikieni ninyi kina baba, kwa kuwa mnamjua yeye ambaye amekuwako tangu mwanzo. Nawaandikieni ninyi vijana kwa sababu mna nguvu; neno la Mungu limo ndani yenu na mmemshinda yule Mwovu.
15Nie miłujcie świata, ani tych rzeczy, które są na świecie; jeźli kto miłuje świat, nie masz w nim miłości ojcowskiej.
15Msiupende ulimwengu, wala chochote kilicho cha ulimwengu. Mtu anayeupenda ulimwengu, upendo wa Baba hauwezi kuwamo ndani yake.
16Albowiem wszystko, co jest na świecie, jako pożądliwość ciała i pożądliwość oczu, i pycha żywota, toć nie jest z Ojca, ale jest z świata.
16Vitu vyote vya ulimwengu-tamaa mbaya za mwili, vitu wanavyoviona watu na kuvitamani, majivuno yasababishwayo na mali-vyote hivyo havitoki kwa Baba, bali vyatoka kwa ulimwengu.
17Światci przemija i pożądliwość jego; ale kto czyni wolę Bożą, trwa na wieki.
17Ulimwengu pamoja na vitu vyake vyote vyenye kutamanika unapita; lakini mtu atendaye atakalo Mungu, anaishi milele.
18Dziateczki! ostateczna godzina jest; a jakoście słyszeli, że antychryst przyjść ma, i teraz wiele antychrystów powstało; stąd wiemy, iż jest ostateczna godzina.
18Watoto, mwisho u karibu! Mlikwisha sikia kwamba adui wa Kristo anakuja, na sasa adui wengi wa Kristo wamekwisha fika, na hivyo twajua kwamba mwisho u karibu.
19Z nas wyszli, ale nie byli z nas; albowiem gdyby byli z nas, zostaliby byli z nami; ale wyszli z nas, aby objawieni byli, iż wszyscy nie byli z nas.
19Watu hao wametokea kati yetu lakini hawakuwa kweli wa kwetu na ndiyo maana walituacha; Kama wangalikuwa wa kwetu, wangalibaki nasi. Lakini waliondoka, wakaenda zao, kusudi ionekane wazi kwamba hawakuwa kamwe wa kwetu.
20Ale wy macie pomazanie od onego Świętego i wiecie wszystko.
20Ninyi, lakini, mlipata kumiminiwa Roho Mtakatifu na Kristo, na hivyo mnaujua ukweli.
21Nie pisałem wam, przeto żeście prawdy nie znali, ale że ją znacie, a iż wszelkie kłamstwo nie jest z prawdy.
21Basi, nawaandikieni, si kwa kuwa hamuujui ukweli, bali kwa sababu mnaujua; na pia mnajua kwamba uongo wowote haupatikani katika ukweli.
22Kto jest kłamcą? Azaż nie ten, który zapiera, iż Jezus nie jest Chrystusem? Ten jest antychryst, który się zapiera Ojca i Syna.
22Mwongo ni nani? Ni yule anayekana kwamba Yesu ni Masiha. Mtu wa namna hiyo ni adui wa Kristo--anamkana Baba na Mwana.
23Każdy, co się zapiera Syna, i Ojca nie ma; a kto wyznaje Syna, ma i Ojca.
23Maana yeyote anayemkana Mwana, anamkana pia Baba; na yeyote anayemkubali Mwana, anampata Baba pia.
24Wy tedy, coście słyszeli od początku, to niechaj w was zostaje; jeźliby w was zostawało, coście słyszeli od początku, i wy w Synu i w Ojcu zostaniecie.
24Basi, ujumbe ule mliousikia tangu mwanzo na ukae mioyoni mwenu. Kama ujumbe huo mliousikia tangu mwanzo ukikaa ndani yenu, basi, mtaishi daima katika umoja na Mwana na Baba.
25A tać jest obietnica, którą on nam obiecał, to jest żywot on wieczny.
25Na ahadi aliyotuahidia sisi ndiyo hii: uzima wa milele.
26Tom wam napisał o tych, którzy was zwodzą.
26Nimewaandikieni mambo haya kuhusu wale wanaotaka kuwapotosha ninyi.
27Ale to pomazanie, któreście wy wzięli od niego, zostaje w was, a nie potrzebujecie, aby was kto uczył: ale jako to pomazanie uczy was o wszystkiem, a jest prawdziwe, i nie jest kłamstwem, a jako was nauczyło, tak w niem zostaniecie.
27Lakini, kwa upande wenu ninyi, Kristo aliwamiminieni Roho wake. Na kama akiendelea kukaa ndani yenu, hamhitaji kufundishwa na mtu yeyote. Maana Roho wake anawafundisheni kila kitu na mafundisho yake ni ya kweli, si ya uongo. Basi shikeni mafundisho ya huyo Roho na kubaki katika muungano na Kristo.
28I teraz, dziateczki! zostaócie w niem, abyśmy, gdy się ukaże, ufanie mieli, a nie byli zawstydzeni od niego w przyjściu jego.
28Naam, watoto, kaeni ndani yake kusudi wakati atakapotokea tuwe hodari bila kuwa na sababu ya kujificha kwa aibu Siku ya kuja kwake.
29Ponieważ wiecie, że on sprawiedliwy jest, wiedzcież też, iż każdy, który czyni sprawiedliwość, z niego narodzony jest.
29Mnajua kwamba Kristo ni mwadilifu kabisa; basi, mnapaswa kujua pia kwamba kila mtu atendaye mambo adili ni mtoto wa Mungu.