1Patrzcie, jaką miłość dał nam Ojciec, abyśmy dziatkami Bożemi nazwani byli. Dlategoć świat nie zna nas, iż onego nie zna.
1Oneni basi, jinsi Baba alivyotupenda mno hata tunaitwa watoto wa Mungu! Na kweli, ndivyo tulivyo. Ndiyo maana ulimwengu haututambui sisi, kwani haumjui Mungu.
2Najmilsi! teraz dziatkami Bożemi jesteśmy, ale się jeszcze nie objawiło, czem będziemy; lecz wiemy, iż gdy się on objawi, podobni mu będziemy; albowiem ujrzymy go tak, jako jest.
2Wapenzi wangu, sisi ni watoto wa Mungu sasa, lakini bado haijaonekana wazi jinsi tutakavyokuwa. Lakini tunajua kwamba wakati Kristo atakapotokea, tutafanana naye kwani tutamwona vile alivyo.
3A ktokolwiek ma tę nadzieję w nim, oczyszcza się, jako i on czysty jest.
3Basi, kila mtu aliye na tumaini hili katika Kristo, hujiweka safi kama vile Kristo alivyo safi kabisa.
4Każdy, co czyni grzech, ten i zakon przestępuje; albowiem grzech jest przestępstwo zakonu.
4Kila mtu atendaye dhambi anavunja sheria ya Mungu, maana dhambi ni uvunjaji wa sheria.
5A wiecie, iż się on objawił, aby grzechy nasze zgładził, a grzechu w nim nie masz.
5Mnajua kwamba Kristo alikuja kuziondoa dhambi zetu, na kwamba kwake hamna dhambi yoyote.
6Wszelki tedy, kto w nim mieszka, nie grzeszy; ale ktokolwiek grzeszy, nie widział go, ani go poznał.
6Basi, kila aishiye katika muungano na Kristo hatendi dhambi; lakini kila mtu atendaye dhambi hakupata kamwe kumwona, wala kumjua Kristo.
7Dziateczki! niechaj was nikt nie zwodzi; kto czyni sprawiedliwość, sprawiedliwy jest, jako i on sprawiedliwy jest;
7Basi, watoto wangu, msikubali kupotoshwa na mtu yeyote. Mtu atendaye matendo maadilifu ni mwadilifu kama vile Kristo alivyo mwadilifu kabisa.
8Kto czyni grzech, z dyjabła jest; gdyż od początku dyjabeł grzeszy. Na to się objawił Syn Boży, aby zepsował uczynki dyjabelskie.
8Lakini atendaye dhambi ni wa Ibilisi, maana Ibilisi ametenda dhambi tangu mwanzo. Lakini Mwana wa Mungu alikuja duniani kuiharibu kazi ya Ibilisi.
9Wszelki, co się narodził z Boga, grzechu nie czyni, iż nasienie jego w nim zostaje, i nie może grzeszyć, iż z Boga narodzony jest.
9Kila aliye mtoto wa Mungu hatendi dhambi, maana anayo hali ya kimungu ndani yake; hawezi kutenda dhambi kwa sababu yeye ni mtoto wa Mungu.
10Po tem poznać dziatki Boże i dzieci dyjabelskie. Wszelki, który nie czyni sprawiedliwości, nie jest z Boga, i który nie miłuje brata swego.
10Lakini yeyote asiyetenda mambo maadilifu, au asiyempenda ndugu yake, huyo si mtoto wa Mungu. Hiyo ndiyo tofauti iliyoko kati ya watoto wa Mungu na watoto wa Ibilisi.
11Albowiem to jest poselstwo, któreście słyszeli od początku, abyśmy jedni drugich miłowali.
11Na, ujumbe mliousikia tangu mwanzo ndio huu: Tunapaswa kupendana!
12Nie jako Kain, który był z tego złośnika i zabił brata swego. A dlaczegoż go zabił? Iż uczynki jego złe były, a brata jego sprawiedliwe.
12Tusiwe kama Kaini ambaye, kwa kuongozwa na yule Mwovu, alimuua ndugu yake. Na, kwa nini alimuua? Kwa sababu matendo yake yalikuwa maovu, lakini yale ya ndugu yake yalikuwa mema!
13Nie dziwujcie się, bracia moi! jeźli was świat nienawidzi.
13Basi, ndugu zangu, msishangae kama ulimwengu unawachukia ninyi.
14My wiemy, żeśmy przeniesieni z śmierci do żywota, iż miłujemy braci; kto nie miłuje brata, zostaje w śmierci.
14Sisi tunajua kwamba tumekwisha pita kutoka katika kifo na kuingia katika uzima kwa sababu tunawapenda ndugu zetu. Mtu asiye na upendo hubaki katika kifo.
15Każdy, co nienawidzi brata swego, mężobójcą jest; a wiecie, iż żaden mężobójca nie ma żywota wiecznego w sobie zostawającego.
15Kila anayemchukia ndugu yake ni muuaji; nanyi mnajua kwamba muuaji yeyote yule hana uzima wa milele ndani yake.
16Przez tośmy poznali miłość Bożą, iż on duszę swoję za nas położył; i myśmy powinni kłaść duszę za braci.
16Sisi tumepata kujua upendo ni nini, kwani Kristo aliyatoa maisha yake kwa ajili yetu. Nasi vilevile tunapaswa kuyatoa maisha yetu kwa ajili ya ndugu zetu.
17A kto by miał majętność świata tego i widziałby brata swego potrzebującego, a zawarłby wnętrzności swoje przed nim, jakoż w nim zostaje miłość Boża?
17Basi, mtu akiwa na mali za hapa duniani, halafu akamwona ndugu yake ana shida, lakini akawa na moyo mgumu bila kumwonea huruma, anawezaje kusema kwamba anampenda Mungu?
18Dziateczki moje! nie miłujmy słowem ani językiem, ale uczynkiem i prawdą.
18Watoto wangu, upendo wetu usiwe maneno matupu, bali uwe upendo wa kweli na wa vitendo.
19A przez to poznajemy, iż z prawdy jesteśmy i przed nim uspokojemy serca nasze.
19Hivyo ndivyo tuwezavyo kuwa na hakika kwamba sisi ni watu wa ukweli; na hatutakuwa na wasiwasi mbele ya Mungu.
20Bo jeźliby nas potępiało serce nasze, daleko większy jest Bóg niż serce nasze i wie wszystko.
20Kwa maana, hata kama dhamiri yetu yatuhukumu, twajua kwamba Mungu ni mkuu zaidi kuliko dhamiri, na kwamba yeye ajua kila kitu.
21Najmilsi! jeźliby serce nasze nas nie potępiało, ufanie mamy ku Bogu;
21Wapenzi wangu, kama dhamiri yetu haina lawama juu yetu, basi, twaweza kuwa na uthabiti mbele ya Mungu,
22I o cokolwiek byśmy prosili, bierzemy od niego; bo przykazania jego chowamy i to, co się podoba przed obliczem jego, czynimy.
22na twaweza kupokea kwake chochote tunachoomba, maana tunazitii amri zake na kufanya yale yanayompendeza.
23A toć jest przykazanie jego, abyśmy wierzyli imieniowi Syna jego, Jezusa Chrystusa, i miłowali jedni drugich, jako nam przykazał.
23Na, amri yake ndiyo hii: Kumwamini Mwanae Kristo, na kupendana kama alivyotuamuru.
24Bo kto chowa przykazania jego, w nim mieszka, a on też w nim; a przez to znamy, iż mieszka w nas, to jest z Ducha, którego nam dał.
24Anayezitii amri za Mungu anaishi katika muungano na Mungu na Mungu anaishi katika muungano naye. Kwa njia ya Roho ambaye Mungu ametujalia, sisi twajua kwamba Mungu anaishi katika muungano nasi.