Polish

Swahili: New Testament

1 John

4

1Najmilsi! nie każdemu duchowi wierzcie; ale doświadczajcie duchów, jeźli z Boga są. Bo wiele fałszywych proroków wyszło na świat.
1Wapenzi wangu, msimsadiki kila mtu asemaye kwamba ana Roho wa Mungu, bali chunguzeni kwa makini kama huyo mtu anaongozwa na Roho wa Mungu au la, Maana manabii wengi wa uongo wamezuka ulimwenguni.
2Przez to poznawajcie Ducha Bożego: Wszelki duch, który wyznaje, iż Jezus Chrystus w ciele przyszedł, z Boga jest.
2Hii ndiyo njia ya kujua kama mtu anaongozwa na Roho wa Mungu: Kila anayekiri kwamba Kristo alikuja, akawa binadamu, mtu huyo anaye Roho wa Mungu.
3Ale wszelki duch, który nie wyznaje, że Jezus Chrystus w ciele przyszedł, nie jest z Boga; ale ten jest on duch antychrystowy, o którymeście słyszeli, iż idzie i teraz już jest na świecie.
3Lakini mtu yeyote asiyemkiri Kristo hivyo, hana huyo Roho atokaye kwa Mungu. Mtu huyo ana roho ambaye ni wa Adui wa Kristo; nanyi mlikwisha sikia kwamba anakuja, na sasa tayari amekwisha wasili ulimwenguni!
4Wy z Boga jesteście, dziateczki! i zwyciężyliście ich; iż większy jest ten, który w was jest, niż ten, który jest na świecie.
4Lakini ninyi, watoto, ni wake Mungu na mmekwisha washinda hao manabii wa uongo; maana Roho aliye ndani yenu ana nguvu zaidi kuliko roho aliye ndani ya hao walio wa ulimwengu.
5Onić są z świata; przetoż o świecie mówią, a świat ich słucha.
5Wao husema mambo ya ulimwengu, nao ulimwengu huwasikiliza kwani wao ni wa ulimwengu.
6My z Boga jesteśmy. Kto zna Boga, słucha nas; kto nie jest z Boga, nie słucha nas. Przez to poznajemy ducha prawdy i ducha błędu.
6Lakini sisi ni wake Mungu. Mtu anayemjua Mungu hutusikiliza, mtu asiye wa Mungu hatusikilizi. Basi, kwa njia hiyo tunaweza kutambua tofauti kati ya Roho wa ukweli na roho wa uongo.
7Najmilsi! miłujmyż jedni drugich, gdyż miłość jest z Boga; i każdy, co miłuje, z Boga jest narodzony i zna Boga.
7Wapenzi wangu, tupendane, maana upendo hutoka kwa Mungu. Kila mtu aliye na upendo ni mtoto wa Mungu, na anamjua Mungu.
8Kto nie miłuje, nie zna Boga; gdyż Bóg jest miłość.
8Mtu asiye na upendo hamjui Mungu, maana Mungu ni upendo.
9Przez to objawiona jest miłość Boża ku nam, iż Syna swego jednorodzonego posłał Bóg na świat, abyśmy żyli przez niego.
9Na Mungu alionyesha upendo wake kwetu kwa kumtuma Mwanae wa pekee ulimwenguni, ili tuwe na uzima kwa njia yake.
10W tem jest miłość, nie iżbyśmy my umiłowali Boga, ale iż on umiłował nas i posłał Syna swego, aby był ubłaganiem za grzechy nasze.
10Hivi ndivyo upendo ulivyo: si kwamba sisi tulikuwa tumempenda Mungu kwanza, bali kwamba yeye alitupenda hata akamtuma Mwanae awe sadaka ya kutuondolea dhambi zetu.
11Najmilsi! ponieważ nas tak Bóg umiłował, i myśmy powinni jedni drugich miłować.
11Wapenzi wangu, ikiwa Mungu alitupenda hivyo, basi, nasi tunapaswa kupendana.
12Boga żaden nigdy nie widział; ale jeźli miłujemy jedni drugich, Bóg w nas mieszka, a miłość jego doskonała jest w nas.
12Hakuna mtu aliyekwisha mwona Mungu kamwe; lakini kama tukipendana Mungu anaishi katika muungano nasi, na upendo wake unakamilika ndani yetu.
13Przez to poznajemy, iż w nim mieszkamy, a on w nas, iż z Ducha swego nam dał.
13Tunajua kwamba tunaishi katika umoja na Mungu, naye Mungu anaishi katika umoja nasi, kwani yeye ametupa Roho wake.
14A myśmy widzieli i świadczymy, iż Ojciec posłał Syna, aby był Zbawicielem świata.
14Sisi tumeona na kuwaambia wengine kwamba Baba alimtuma Mwanae awe Mwokozi wa ulimwengu.
15Ktobykolwiek wyznał, iż Jezus jest Synem Bożym, Bóg w nim mieszka, a on w Bogu.
15Kila mtu anayekiri kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu, Mungu anaishi katika muungano na mtu huyo, naye anaishi katika muungano na Mungu.
16I myśmy poznali i uwierzyli o miłości, którą Bóg ma ku nam. Bóg jest miłość; a kto mieszka w miłości, w Bogu mieszka, a Bóg w nim.
16Basi, sisi tunajua na tunaamini upendo alio nao Mungu kwetu sisi. Mungu ni upendo, na kila mtu aishiye katika upendo, anaishi katika muungano na Mungu, na Mungu anaishi katika muungano naye.
17W tem doskonała jest miłość Boża z nami, abyśmy ufanie mieli w dzieó sądny, iż jaki on jest, tacy i my jesteśmy na tym świecie.
17Upendo umekamilika ndani yetu kusudi tuweze kuwa na ujasiri Siku ile ya Hukumu; kwani maisha yetu hapa duniani ni kama yale ya Kristo.
18Nie maszci bojaźni w miłości, ale miłość doskonała precz wyrzuca bojaźó: bo bojaźó ma udręczenie, a kto się boi, nie jest doskonały w miłości.
18Palipo na upendo hapana uoga; naam, upendo kamili hufukuza uoga wote. Basi, mtu mwenye uoga hajakamilika bado katika upendo, kwani uoga huhusikana na adhabu.
19My go miłujemy, iż on nas pierwej umiłował.
19Sisi tuna upendo kwa sababu Mungu alitupenda kwanza.
20Jeźliby kto rzekł: Miłuję Boga, a brata by swego nienawidził, kłamcą jest; albowiem kto nie miłuje brata swego, którego widział, Boga, którego nie widział, jakoż może miłować?
20Mtu akisema kwamba anampenda Mungu, hali anamchukia ndugu yake, huyo ni mwongo. Maana mtu asiyempenda ndugu yake ambaye anamwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hamwoni.
21A toć rozkazanie mamy od niego, aby ten, co miłuje Boga, miłował i brata swego.
21Basi, hii ndiyo amri aliyotupa Kristo: Anayempenda Mungu anapaswa pia kumpenda ndugu yake.