Polish

Swahili: New Testament

1 Timothy

1

1Paweł, Apostoł Jezusa Chrystusa podług rozrządzenia Boga, zbawiciela naszego, i Pana Jezusa Chrystusa, który jest nadzieja nasza,
1Mimi Paulo, mtume wa Yesu Kristo kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu na Yesu Kristo tumaini letu,
2Tymoteuszowi, własnemu synowi w wierze, niech będzie łaska, miłosierdzie, pokój od Boga, Ojca naszego, i Chrystusa Jezusa, Pana naszego.
2nakuandikia Timotheo mwanangu halisi katika imani. Nakutakia neema, huruma na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Kristo Yesu Bwana wetu.
3Jakom cię prosił, abyś został w Efezie, gdym szedł do Macedonii, patrzże, abyś rozkazał niektórym, żeby inaczej nie uczyli.
3Napenda ukae huko Efeso, kama nilivyokuomba nilipokuwa ninakwenda Makedonia. Wako watu fulani huko wanaofundisha mafundisho ya uongo. Wakomeshe watu hao.
4I nie bawili się baśniami i wywodami nieskoóczonemi rodzaju, które więcej sporów przynoszą, niż zbudowania Bożego, które w wierze zależy.
4Waambie waachane na zile hadithi tupu na orodha ndefu za mababu, ambazo huleta tu ubishi, wala haviwajengi watu katika mpango ujulikanao kwa imani.
5Lecz koniec przykazania jest miłość z czystego serca i z sumienia dobrego, i z wiary nieobłudnej.
5Shabaha ya amri hii ni kuhimiza mapendo yatokayo katika moyo safi, dhamiri njema, na imani ya kweli.
6Czego niektórzy jako celu uchybiwszy, obrócili się ku próżnomówności.
6Watu wengine wamepotoka na kugeukia majadiliano yasiyo na maana.
7Chcąc być nauczycielami zakonu, nie rozumieją ani tego, co mówią, ani co za pewne twierdzą.
7Wanapenda kuwa walimu wa Sheria, lakini hawaelewi maneno yao wenyewe au mambo wanayosisitiza.
8A wiemy, że dobry jest zakon, jeźliby go kto przystojnie używał,
8Twajua kwamba Sheria ni njema, kama ikitumiwa ipasavyo.
9Wiedząc to, że sprawiedliwemu nie jest zakon postanowiony, ale niesprawiedliwym i niepoddanym, niepobożnym i grzesznikom, złośliwym i nieczystym, ojcomordercom i matkomordercom, mężobójcom,
9Lakini tunapaswa kukumbuka kwamba sheria haziwekwi kwa ajili ya watu wema, bali kwa ajili ya wahalifu na wasiotii, wasiomcha Mungu na wenye dhambi, watu wasio na dini na wa kidunia. Watu wanaowaua baba na mama zao, au wauaji wowote wale;
10Wszetecznikom, samcołożnikom, ludokradcom, kłamcom, krzywoprzysiężcom, i jeźli co innego jest przeciwnego zdrowej nauce.
10sheria imewekwa kwa ajili ya waasherati, wafiraji, wanaowaiba watu, waongo, na wanaoapa uongo au wanaofanya chochote ambacho ni kinyume cha mafundisho ya kweli.
11Według chwalebnej Ewangielii błogosławionego Boga, która mi jest zwierzona.
11Mafundisho hayo hupatikana katika Habari Njema ambayo mimi nimekabidhiwa niihubiri, Habari Njema ya Mungu mtukufu na mwenye heri.
12Przetoż dziękuję temu, który mię umocnił, Chrystusowi Jezusowi, Panu naszemu, iż mię za wiernego osądził, na usługiwanie postanowiwszy mię.
12Namshukuru Bwana wetu Yesu Kristo aliyenipa nguvu kwa ajili ya kazi yangu. Namshukuru kwa kuniona mimi kuwa ni mwaminifu, akaniteua nimtumikie,
13Którym pierwej był bluźniercą i prześladowcą, i gwałtownikiem; alem miłosierdzia dostąpił, bom to z niewiadomości czynił, będąc w niewierze.
13ingawa pale awali mimi nilimtukana na kumtesa na kumdhulumu. Lakini Mungu alinionea huruma, kwa sababu sikuwa na imani bado, na hivyo sikujua nilichokuwa ninafanya.
14Lecz nader obfitowała łaska Pana naszego z wiarą i z miłością, która jest w Chrystusie Jezusie.
14Lakini Bwana wetu alinijalia neema yake kwa wingi, akanipa imani na upendo katika kuungana na Kristo Yesu.
15Wierna jest ta mowa i wszelkiego przyjęcia godna, iż Chrystus Jezus przyszedł na świat, aby grzeszników zbawił, z których jam jest pierwszy.
15Usemi huu ni wa kuaminika, na tena unafaa kukubaliwa kabisa: Kristo Yesu alikuja ulimwenguni kuwaokoa wenye dhambi. Nami ni mkosefu zaidi kuliko hao wote,
16Alem dlatego miłosierdzia dostąpił, aby na mnie pierwszym okazał Jezus Chrystus wszelką cierpliwość na przykład tym, którzy weó uwierzyć mają ku żywotowi wiecznemu.
16lakini Mungu alinionea huruma, ili Kristo aonyeshe uvumilivu wake wote kwangu mimi, kama mfano kwa wale wote ambao baadaye watamwamini na kupokea uzima wa milele.
17Przetoż królowi wieków nieśmiertelnemu, niewidzialnemu samemu mądremu Bogu, niech będzie cześć i chwała na wieki wieków. Amen.
17Kwake yeye aliye Mfalme wa milele na asiyekufa, yeye aliye Mungu pekee--kwake viwe heshima na utukufu milele na milele! Amina.
18Toć rozkazanie zalecam, synu Tymoteuszu! abyś według proroctw, które uprzedziły o tobie, bojował w nich on dobry bój,
18Mwanangu Timotheo, nakukabidhi amri hii kufuatana na maneno ya unabii yaliyosemwa zamani juu yako. Yatumie maneno hayo yawe silaha yako katika kupigana vita vizuri,
19Mając wiarę i dobre sumienie, które niektórzy odrzuciwszy, szkodę podjęli w wierze;
19na ushike imani yako na dhamiri njema. Watu wengine hawakusikiliza dhamiri zao na hivyo wakaiharibu imani yao.
20Z których jest Hymeneusz i Aleksander, którychem oddał szatanowi, aby pokarani będąc, nauczyli się nie bluźnić.
20Miongoni mwao ni Humenayo na Aleksanda ambao nimewakabidhi kwa Shetani, ili wafundishwe wasimtukane Mungu.