Polish

Swahili: New Testament

2 Thessalonians

3

1Na ostatek, bracia! módlcie się za nas, aby się słowo Paóskie szerzyło i rozsławiało, jako i u was;
1Hatimaye, ndugu, tuombeeni ili ujumbe wa Bwana uzidi kuenea upesi na kupokelewa kwa heshima kama vile ulivyo kati yenu.
2I abyśmy byli wyrwani od niezbędnych i złych ludzi; albowiem nie wszystkich jest wiara.
2Ombeni pia ili Mungu atuokoe na watu wapotovu na waovu, maana si wote wanaoamini ujumbe huu.
3Aleć wierny jest Pan, który was utwierdzi i strzec będzie od złego.
3Lakini Bwana ni mwaminifu. Yeye atawaimarisheni na kuwalinda salama na yule Mwovu.
4A ufamy w Panu o was, iż to, co wam rozkazujemy, i czynicie i czynić będziecie.
4Naye Bwana anatupatia tumaini kubwa juu yenu, na hatuna shaka kwamba mnafanya na mtaendelea kufanya yale tuliyowaambieni.
5A Pan niech sprawuje serca wasze ku miłości Bożej i ku cierpliwemu oczekiwaniu Chrystusa.
5Bwana aiongoze mioyo yenu katika upendo wa Mungu na katika uvumilivu tunaopewa na Kristo.
6A rozkazujemy wam, bracia! w imieniu Pana naszego, Jezusa Chrystusa, abyście się odłączyli od każdego brata nieporządnie chodzącego, a nie według podanej nauki, którą wziął od nas.
6Ndugu, tunawaamuru kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo, mjiepushe na ndugu wote walio wavivu na ambao hawafuati maagizo tuliyowapa.
7Albowiem sami wiecie, jako nas potrzeba naśladować, ponieważeśmy nie żyli między wami nieporządnie;
7Ninyi wenyewe mnajua kwamba mnapaswa kufuata mfano wetu. Sisi tulipokuwa nanyi hatukuwa wavivu;
8Aniśmy darmo chleba jedli u kogo, ale z pracą i z kłopotem we dnie i w nocy robiąc, abyśmy nikomu z was ciężkimi nie byli;
8hatukula chakula kwa mtu yeyote bila ya kumlipa. Tulifanya kazi kwa bidii na taabu mchana na usiku ili tusiwe mzigo kwa mtu yeyote kati yenu.
9Nie iżbyśmy tej mocy nie mieli, ale żebyśmy wam sami siebie za przykład podali, abyście nas naśladowali.
9Tulifanya hivyo si kwa kuwa hatuna haki ya kutaka msaada wenu, ila kwa sababu tunataka kuwapeni mfano.
10Albowiem gdyśmy byli u was, tośmy wam rozkazali, że jeźli kto nie chce robić, niechajże też nie je.
10Tulipokuwa pamoja nanyi tulikuwa tukiwaambieni, "Mtu asiyefanya kazi, asile."
11Bo słyszymy, iż niektórzy między wami nieporządnie chodzą, nic nie robiąc, ale się niepotrzebnemi rzeczami bawiąc.
11Tunasema mambo hayo kwa sababu tumesikia kwamba wako baadhi yenu ambao ni wavivu na ambao hawafanyi chochote, isipokuwa tu kujiingiza katika mambo ya watu wengine.
12Przetoż takowym rozkazujemy i napominamy ich przez Pana naszego, Jezusa Chrystusa, aby w pokoju robiąc, swój własny chleb jedli.
12Kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo tunawaamuru na kuwaonya watu hao wawe na nidhamu na kufanya kazi ili wajipatie maslahi yao wenyewe.
13A wy, bracia! nie słabiejcie, dobrze czyniąc.
13Lakini ninyi ndugu, msichoke kutenda mema.
14A jeźli kto jest nieposłuszny słowu naszemu przez list pisanemu, tego naznaczcie, a nie mieszajcie się z nim, aby się zawstydził;
14Huenda kwamba huko kuna mtu ambaye hatautii huu ujumbe tunaowapelekeeni katika barua hii. Ikiwa hivyo, basi, mfichueni mtu huyo na msiwe na uhusiano wowote naye kusudi aone aibu.
15Wszakże nie miejcie go za nieprzyjaciela, ale napominajcie jako brata.
15Lakini msimtendee mtu huyo kama adui, bali mwonyeni kama ndugu.
16A sam Pan pokoju niech wam da pokój zawsze i wszelkim sposobem. Pan niech będzie z wami wszystkimi.
16Bwana mwenyewe ndiye chanzo cha amani, awajalieni amani siku zote kwa kila namna. Bwana awe nanyi nyote.
17Pozdrowienie ręką moją Pawłową, co jest znakiem w każdym liście; tak piszę.
17Kwa mkono wangu mwenyewe naandika hivi: Salamu kutoka kwa Paulo! Hivi ndivyo ninavyotia sahihi kila barua; ndivyo ninavyoandika.
18Łaska Pana naszego, Jezusa Chrystusa, niech będzie z wami wszystkimi. Amen.
18Tunawatakieni nyote neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.