Polish

Swahili: New Testament

2 Corinthians

5

1Wiemy bowiem, że jeźli tego naszego ziemskiego mieszkania namiot zburzony będzie, budowanie mamy od Boga, dom nie rękoma urobiony, wieczny w niebiesiech.
1Maana tunajua kwamba hema hii ambayo ndani yake tunaishi sasa hapa duniani, yaani mwili wetu, itakapong'olewa, Mungu atatupa makao mengine mbinguni, nyumba ya milele isiyotengenezwa kwa mikono.
2Albowiem w tym namiocie wzdychamy, domem naszym, który jest z nieba, żądając być przyobleczeni.
2Na sasa, katika hali hii, tunaugua, tukitazamia kwa hamu kubwa kuvikwa makao yetu yaliyo mbinguni.
3Jeźliż tylko przyobleczonymi a nie nagimi znalezieni będziemy.
3Naam, tunapaswa kuvikwa namna hiyo ili tusije tukasimama mbele ya Mungu bila vazi.
4Bo którzyśmy w tym namiocie, wzdychamy, będąc obciążeni, ponieważ nie żądamy być zewleczeni, ale przyobleczeni, aby pożarta była śmiertelność od żywota.
4Tukiwa bado katika hema hii ya duniani, tunalia kwa kukandamizwa; si kwamba tunataka kuuvua mwili huu wa kufa, ila tuna hamu ya kuvalishwa ule usiokufa, ili kile chenye kufa kimezwe kabisa na uhai.
5A ten, który nas ku temuż właśnie przygotował, jestci Bóg, który nam też dał zadatek Ducha.
5Mungu mwenyewe alitutayarishia mabadiliko hayo, naye ametupa Roho wake awe dhamana ya yote aliyotuwekea.
6Przetoż mając zawsze ufność i wiedząc, że póki mieszkamy w tem ciele, pielgrzymujemy od Pana:
6Tuko imara daima. Tunajua kwamba kuishi katika mwili huu tu ni kukaa mbali na Bwana.
7(Bo przez wiarę chodzimy, a nie przez widzenie).
7Maana tunaishi kwa imani, na si kwa kuona.
8Lecz ufamy i wolimy raczej wynijść z ciała, a iść na mieszkanie do Pana.
8Lakini tuko imara na tungependelea hata kuyahama makao haya, tukahamie kwa Bwana.
9Przetoż też usiłujemy, bądź w ciele mieszkamy, bądź z ciała wychodzimy, onemu się podobać.
9Lakini jambo la maana zaidi, tunataka kumpendeza, iwe tunaishi hapa duniani au huko.
10Albowiem musimy się wszyscy pokazać przed sądową stolicą Chrystusową, aby każdy odniósł, co czynił w ciele, według tego, co czynił, lub dobre, lub złe.
10Maana sote ni lazima tusimame mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo, ili kila mmoja apokee anayostahili kwa matendo aliyoyafanya wakati alipokuwa anaishi duniani, mema au mabaya.
11Przetoż wiedząc o tym strachu Paóskim, ludzi do wiary namawiamy, a Bogu jawnymi jesteśmy; i mam nadzieję, iż w sumieniach waszych jawnymi jesteśmy.
11Basi, sisi tunajua umuhimu wa kumcha Bwana, na hivyo tunajitahidi kuwavuta watu. Mungu anatujua waziwazi, nami natumaini kwamba nanyi pia mnatujua kinaganaga.
12Albowiem nie samych siebie wam znowu zalecamy, ale wam dajemy przyczynę, abyście się chlubili nami i żebyście mieli co mówić przeciwko tym, którzy się chlubią z powierzchownych rzeczy, a nie z serca.
12Si kwamba tunajaribu tena kujipendekeza kwenu, ila tunataka kuwapa ninyi sababu zetu za kuona fahari juu yenu, ili mpate kuwajibu wale wanaojivunia hali yao ya nje zaidi kuliko jinsi walivyo moyoni.
13Bo choć od rozumu odchodzimy, Bogu odchodzimy, choć przy rozumie jesteśmy, wam jesteśmy.
13Ikiwa tumeonekana kuwa wendawazimu, hiyo ni kwa ajili ya Mungu; na ikiwa tunazo akili zetu timamu, hiyo ni kwa faida yenu.
14Albowiem miłość Chrystusowa przyciska nas, jako tych, którzyśmy to osądzili, iż ponieważ jeden za wszystkich umarł, tedy wszyscy byli umarłymi;
14Maana mapendo ya Kristo yanatumiliki sisi ambao tunatambua ya kwamba mtu mmoja tu amekufa kwa ajili ya wote, na hiyo ina maana kwamba wote wanashiriki kifo chake.
15A że za wszystkich umarł, aby ci, którzy żyją, już więcej sobie nie żyli, ale temu, który za nich umarł i jest wzbudzony.
15Alikufa kwa ajili ya watu wote, ili wanaoishi wasiishi kwa ajili yao wenyewe, bali kwa ajili yake yeye aliyekufa, akafufuliwa kwa ajili yao.
16Dlatego my od tego czasu nikogo według ciała nie znamy, a chociaśmy też znali Chrystusa według ciała, lecz już teraz więcej nie znamy.
16Basi, tangu sasa, sisi hatumpimi mtu yeyote kibinadamu. Hata kama kwa wakati mmoja tulimpima Kristo kibinadamu, sasa si hivyo tena.
17A tak jeźli kto jest w Chrystusie, nowem jest stworzeniem; stare rzeczy przeminęły, oto się wszystkie nowemi stały.
17Mtu yeyote akiungana na Kristo huwa kiumbe kipya, mambo ya kale yamepita, hali mpya imefika.
18A to wszystko z Boga jest, który nas z samym sobą pojednał przez Jezusa Chrystusa i dał nam usługiwanie tego pojednania,
18Yote ni kazi ya Mungu mwenye kutupatanisha sisi naye kwa njia ya Kristo, akatupa nasi jukumu la kuwapatanisha watu naye.
19Ponieważ Bóg był w Chrystusie, świat z samym sobą jednając, nie przyczytując im upadków ich, i położył w nas to słowo pojednania:
19Ndiyo kusema: Mungu, amekuwa akiupatanisha ulimwengu naye kwa njia ya Kristo, bila kutia maanani dhambi zao binadamu. Yeye ametupa ujumbe kuhusu kuwapatanisha watu naye.
20Przetoż na miejscu Chrystusowem poselstwo sprawujemy, jakoby was Bóg upominał przez nas, prosimy na miejscu Chrystusowem, jednajcie się z Bogiem;
20Basi, sisi tunamwakilisha Kristo, naye Mungu mwenyewe anatutumia sisi kuwasihi ninyi. Tunawaombeni kwa niaba ya Kristo, mpatanishwe na Mungu.
21Albowiem on tego, który nie znał grzechu, za nas grzechem uczynił, abyśmy się my stali sprawiedliwością Bożą w nim.
21Kristo hakuwa na dhambi, lakini Mungu alimfanya ahusike na dhambi kwa ajili yetu, ili sisi kwa kuungana naye, tupate kuushiriki uadilifu wake Mungu.