1Byli też i fałszywi prorocy między ludem, jako i między wami będą fałszywi nauczyciele, którzy z sobą wprowadzą kacerstwa zatracenia i Pana, który ich kupił, zaprzą się, sami na się przywodząc prędkie zginienie.
1Palitokea manabii wa uongo kati ya watu, na vivyo hivyo walimu wa uongo watatokea kati yenu. Watu hao wataingiza mafundisho maharibifu na kumkana Bwana aliyewakomboa, na kwa njia hiyo watasababisha ghafla maangamizi yao wenyewe.
2A wiele ich naśladować będą zginienia ich, przez których droga prawdy będzie bluźniona.
2Tena watu wengi watazifuata hizo njia zao mbaya, kwa sababu yao, wengine wataipuuza Njia ya ukweli.
3I przez łakomstwo zmyślonemi słowami kupczyć będą, którym sąd z dawna nie omieszkuje i zatracenie ich nie drzemie.
3Kwa tamaa yao mbaya watajipatia faida kwa kuwaambieni hadithi za uongo. Lakini kwa muda mrefu sasa Hakimu wao yu tayari, na Mwangamizi wao yu macho!
4Albowiem jeźli Bóg Aniołom, którzy byli zgrzeszyli, nie przepuścił, ale strąciwszy ich do piekła, podał łaócuchom ciemności, aby byli zachowani na sąd:
4Malaika walipotenda dhambi, Mungu hakuwahurumia, bali aliwatupa katika moto wa Jehanamu ambako wamefungwa wakingojea Siku ile ya Hukumu.
5Także i pierwszemu światu nie przepuścił, ale Noego samoósmego, kaznodzieję sprawiedliwości, zachował, przywiódłszy potop na świat niepobożnych;
5Mungu hakuihurumia dunia ya hapo kale, bali alileta gharika kuu juu ya nchi ile ya watu wasiomcha Mungu; lakini Noa ambaye alihubiri uadilifu, Mungu alimwokoa pamoja na watu wengine saba.
6I miasta Sodomczyków i Gomorry w popiół obróciwszy podwróceniem potępił, wystawiwszy je na przykład tym, którzy by niepobożnie żyli;
6Mungu aliadhibu miji ya Sodoma na Gomora, akaiteketeza kwa moto, akaifanya iwe mfano wa mambo yatakayowapata watu wasiomcha Mungu.
7A sprawiedliwego Lota, onych niezbożników rozpustnem obcowaniem strapionego, wyrwał.
7Alimwokoa Loti, mtu mwema, ambaye alisikitishwa sana na mwenendo mbaya wa watu hao waasi.
8Albowiem widzeniem i słyszeniem on sprawiedliwy mieszkając między nimi, dzieó po dniu duszę sprawiedliwą uczynkami ich niezbożnymi trapił.
8Loti aliishi miongoni mwa watu hao, na kwa siku nyingi moyo wake ulikuwa katika wasiwasi mkuu aliposikia matendo yao maovu.
9Umie Pan pobożnych z pokuszenia wyrywać, a niesprawiedliwych na dzieó sądu ku karaniu chować;
9Kwa hiyo, basi, Bwana anajua jinsi ya kuwaokoa katika majaribu watu wanaomcha Mungu, na jinsi ya kuwaweka waovu katika adhabu hadi Siku ile ya hukumu,
10A najwięcej tych, którzy za ciałem w pożądliwości plugastwa chodzą, a zwierzchnością pogardzają, śmieli i sobie się podobający, nie wzdrygają się bluźnić przełożeóstw.
10hasa wale wanaofuata tamaa mbaya za mwili na kupuuza mamlaka. Watu hao ni washupavu na wenye majivuno, huvitukana na hawaviheshimu viumbe vitukufu vya juu.
11Chociaż Aniołowie będąc większymi siłą i mocą, nie przynoszą przeciwko nim przed Pana bluźnierczego sądu.
11Lakini malaika, ambao wana uwezo na nguvu zaidi kuliko hao walimu wa uongo, hawawashtaki na kuwatukana hao mbele ya Bwana.
12Ale ci, jako bydło bezrozumne, które za przyrodzeniem idzie, sprawione na ułowienie i skazę, bluźniąc to, czego nie wiedzą, w tej skazie swojej zaginą.
12Watu hao ambao hutukana chochote kile wasichoelewa, ni sawa na wanyama wasio na akili, ambao huzaliwa na baadaye hukamatwa na kuchinjwa! Wataangamizwa kutokana na uharibifu wao wenyewe,
13I odniosą zapłatę niesprawiedliwości jako ci, którzy mają za rozkosz każdodzienne lubości, będąc plugastwem i zmazą, rozkosz mają w zdradach swoich z wami bankietując:
13na watalipwa mateso kwa mateso ambayo wameyasababisha. Furaha yao ni kufanya, tena mchana kabisa, chochote kinachotosheleza anasa zao za mwili. Hao ni fedheha na aibu tupu kwa jumuiya yenu wakati wanapojiunga nanyi katika karamu zenu, bali wakifurahia njia zao za udanganyifu.
14Oczy mają pełne cudzołóstwa i bez przestania grzeszące, przyłudzając dusze niestateczne, mając serce wyćwiczone w łakomstwie, synowie przeklęstwa,
14Macho yao yamejaa uzinzi na uwezo wao wa kutenda dhambi hauna kikomo. Huwaongoza watu walio dhaifu mpaka mitegoni. Mioyo yao imezoea kuwa na tamaa ya mali. Wapo chini ya laana ya Mungu!
15Którzy opuściwszy prostą drogę, zbłądzili, naśladując drogi Balaama, syna Bosorowego, który zapłatę niesprawiedliwości umiłował;
15Wameiacha njia iliyonyoka, wakapotoka na kuifuata njia aliyofuata Balaamu, mwana wa Beori, ambaye alipendelea kupata faida kwa kufanya udanganyifu,
16Ale miał karanie za swój występek, ponieważ jarzmu niema oślica poddana, człowieczym głosem przemówiwszy, zahamowała szaleóstwo proroka.
16akakaripiwa kwa ajili ya uovu wake. Punda ambaye hasemi alinena kwa sauti ya binadamu, akaukomesha wazimu wa huyo nabii.
17Ci są studniami bez wody, obłoki od wichru pędzone, którym chmura ciemności na wieki jest zachowana.
17Watu hao ni kama chemchemi zilizokauka, kama mawingu yanayopeperushwa na tufani; makao yao waliyowekewa ni mahali pa giza kuu.
18Albowiem nadętą próżność mówiąc, przyłudzają przez pożądliwość ciała i rozpusty tych, którzy byli prawdziwie uciekli od obcujących w błędzie,
18Husema maneno ya majivuno na yasiyo na maana, na kutumia tamaa zao mbaya za kimwili kuwatega wale ambao wamejitenga hivi karibuni na watu waishio katika udanganyifu.
19Wolność im obiecując, a sami będąc niewolnikami skazy. Albowiem kto jest od kogo przezwyciężony, temu też jest zniewolony.
19Huwaahidi watu wengine eti watakuwa huru, kumbe wao wenyewe ni watumwa wa upotovu--maana mtu ni mtumwa wa chochote kile kinachomtawala.
20Bo ponieważ oni uszli plugastw świata przez poznanie Pana i zbawiciela, Jezusa Chrystusa, a znowu się zaś niemi uwikławszy, zwyciężeni bywają; stały się ich ostateczne rzeczy gorsze niż pierwsze.
20Watu waliokwisha ponyoka katika upotovu wa ulimwengu kwa kupata kumjua Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, kisha wakakubali kunaswa na kutawaliwa tena na upotovu huo, hali yao itakuwa mbaya zaidi kuliko awali.
21Bo by im było lepiej, nie uznać drogi sprawiedliwości, niżeli poznawszy ją, odwrócić się od podanego im rozkazania świętego.
21Ingalikuwa afadhali kwao kama wasingalijua kamwe njia hiyo ya uadilifu kuliko kujua na kisha kuiacha na kupoteza amri takatifu waliyopokea.
22Aleć się im przydało według onej prawdziwej przypowieści: Pies wrócił się do zwracania swego, a świnia umyta do walania się w błocie.
22Ipo mithali isemayo: "Mbwa huyarudia matapishi yake mwenyewe," na nyingine isemayo: "Nguruwe aliyekwisha oshwa hugaagaa tena katika matope!" Ndivyo ilivyo kwao sasa.