Polish

Swahili: New Testament

2 Peter

3

1Najmilsi! już ten drugi list do was piszę, którym wzbudzam przez napominanie uprzejmą myśl waszę,
1Wapenzi wangu, hii ni barua ya pili ninayowaandikia. Katika barua hizo mbili nimejaribu kufufua fikira safi akilini mwenu kwa kuwakumbusheni mambo haya.
2Abyście pamiętali na słowa przepowiedziane od świętych proroków, i na przykazanie nasze, którzyśmy Apostołami Pana i Zbawiciela:
2Napenda mkumbuke maneno yaliyosemwa na manabii watakatifu, na ile amri ya Bwana na Mwokozi mliyopewa na mitume wenu.
3To najpierwej wiedząc, że przyjdą w ostateczne dni naśmiewcy, według własnych swoich pożądliwości chodzący,
3Awali ya yote jueni kwamba siku za mwisho watakuja watu ambao mienendo yao inatawaliwa na tamaa zao mbaya. Watawadhihaki ninyi
4I mówiący: Gdzież jest obietnica przyjścia jego? Bo jako ojcowie zasnęli, wszystko tak trwa od początku stworzenia.
4na kusema: "Aliahidi kwamba atakuja! Je, sasa yuko wapi? Mambo ni yaleyale tangu babu zetu walipokufa; hali ya vitu ni ileile kama ilivyokuwa mwanzo wa ulimwengu!"
5Tego zaiste umyślnie wiedzieć nie chcą, że się niebiosa dawno stały i ziemia z wody i w wodzie stanęła przez słowo Boże,
5Watu hao, kwa makusudi, husahau kwamba zamani Mungu alinena, nazo mbingu na nchi zikaumbwa. Dunia iliumbwa kutoka katika maji na kwa maji;
6Dlaczego on pierwszy świat wodą będąc zatopiony, zginął.
6na kwa maji hayo, yaani yale maji ya gharika kuu, dunia ya wakati ule iliangamizwa.
7Lecz te niebiosa, które teraz są i ziemia temże słowem odłożone są i zachowane ogniowi na dzieó sądu i zatracenia niepobożnych ludzi.
7Lakini mbingu na nchi za sasa zahifadhiwa kwa neno la Mungu kwa ajili ya kuharibiwa kwa moto. Zimewekwa kwa ajili ya Siku ile ambapo watu wasiomcha Mungu watahukumiwa na kuangamizwa.
8Ale ta jedna rzecz niech wam nie będzie tajna, najmilsi! iż jeden dzieó u Pana jest jako tysiąc lat, a tysiąc lat, jako jeden dzieó.
8Lakini, wapenzi wangu, msisahau kitu kimoja! Mbele ya Bwana, hakuna tofauti kati ya siku moja na miaka elfu; kwake yote ni mamoja.
9Nie omieszkiwać Pan z obietnicą, (jako to niektórzy mają za omieszkanie), ale używa cierpliwości przeciwko nam, nie chcąc, aby którzy zginęli, ale żeby się wszyscy do pokuty udali.
9Bwana hakawii kutimiza yale aliyoahidi kama watu wengine wanavyofikiri kuwa atakawia. Yeye ana saburi kwa ajili yenu, maana hapendi hata mmoja wenu apotee, bali huwavuta wote wapate kutubu.
10A on dzieó Paóski przyjdzie jako złodziej w nocy, w który niebiosa z wielkim trzaskiem przeminą, a żywioły rozpalone ogniem stopnieją, a ziemia i rzeczy, które są na niej, spalone będą.
10Siku ya Bwana itakuja kama mwizi. Siku hiyo, mbingu zitatoweka kwa kishindo kikuu; vitu vyake vya asili vitateketezwa kwa moto, nayo dunia itatoweka pamoja na kila kitu kilichomo ndani yake.
11Ponieważ się tedy to wszystko ma rozpłynąć, jakimiż wy macie być w świętych obcowaniach i pobożnościach?
11Maadamu kila kitu kitaharibiwa namna hiyo, je, ninyi mnapaswa kuwa watu wa namna gani? Mnapaswa kuishi kitakatifu na kumcha Mungu,
12Którzy oczekujecie i spieszycie się na przyjście dnia Bożego, w który niebiosa gorejące rozpuszczą się i żywioły pałające stopnieją.
12mkiingojea Siku ile ya Mungu na kuifanya ije upesi--Siku ambayo mbingu zitateketezwa kwa moto na kuharibiwa, na vitu vyake vya asili vitayeyushwa kwa joto.
13Lecz nowych niebios i nowej ziemi według obietnicy jego oczekujemy, w których sprawiedliwość mieszka.
13Lakini sisi, kufuatana na ahadi yake, twangojea mbingu mpya na dunia mpya ambayo imejaa uadilifu.
14Przetoż najmilsi! tego oczekując, starajcie się, abyście bez zmazy i bez nagany od niego znalezieni byli w pokoju;
14Kwa hiyo wapenzi wangu, mkiwa mnangojea Siku ile, fanyeni bidii kuwa safi kabisa bila hatia mbele ya Mungu, na kuwa na amani naye.
15A nieskwapliwość Pana naszego miejcie za zbawienie wasze, jako wam i miły brat nasz Paweł według danej sobie mądrości pisał,
15Mnapaswa kuuona uvumilivu wa Bwana kuwa ni nafasi anayowapeni mpate kuokolewa, kama Paulo ndugu yetu mpenzi alivyowaandikia akitumia hekima aliyopewa na Mungu.
16Jako i we wszystkich listach swoich mówiąc o tych rzeczach, między któremi są niektóre rzeczy trudne ku wyrozumieniu, które nieumiejętni i niestateczni wykręcają jako i inne pisma, ku swemu własnemu zatraceniu.
16Hayo ndiyo asemayo katika barua zake zote anapozungumzia suala hilo. Yapo mambo kadhaa katika barua zake yaliyo magumu kuyaelewa, mambo ambayo watu wajinga, wasio na msimamo, huyapotosha kama wanavyopotosha sehemu nyingine za Maandiko Matakatifu. Hivyo wanasababisha maangamizi yao wenyewe.
17Wy tedy, najmilsi! wiedząc to przedtem; strzeżcie się, abyście błędem tych niezbożników nie byli zwiedzeni i nie wypadli z waszej stateczności;
17Lakini ninyi, wapenzi wangu, mmekwisha jua jambo hili. Basi, muwe na tahadhari msije mkapotoshwa na makosa ya waasi, mkaanguka kutoka katika msimamo wenu imara.
18Ale rośćcie w łasce i w znajomości Pana naszego i Zbawiciela, Jezusa Chrystusa, któremu niech będzie chwała i teraz, i na czasy wieczne. Amen.
18Lakini endeleeni kukua katika neema na katika kumjua Bwana wetu na Mwokozi Yesu Kristo. Utukufu uwe kwake, sasa na hata milele! Amina.