Polish

Swahili: New Testament

2 Thessalonians

1

1Paweł i Sylwan, i Tymoteusz zborowi Tesaloniceóskiemu w Bogu, Ojcu naszym, i w Panu Jezusie Chrystusie.
1Mimi Paulo, Silwano na Timotheo tunawaandikia ninyi jumuiya ya kanisa la Thesalonike, ambao ni watu wake Mungu Baba yetu na wa Bwana Yesu Kristo.
2Łaska wam i pokój niech będzie od Boga, Ojca naszego, i Pana Jezusa Chrystusa.
2Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.
3Powinniśmy Bogu zawsze dziękować za was, bracia! tak jako się godzi, iż bardzo rośnie wiara wasza i pomnaża się miłość każdego z was, jednych przeciwko drugim,
3Ndugu, tunapaswa kushukuru Mungu daima kwa ajili yenu. Inafaa kwetu kufanya hivyo kwani imani yenu inakua sana na kupendana kwenu kunaongezeka sana.
4Tak iż i my sami chlubimy się z was we zborach Bożych z waszej cierpliwości i wiary we wszystkich prześladowaniach waszych i w uciskach, które ponosicie.
4Ndio maana sisi tunajivunia ninyi katika makanisa ya Mungu. Tunaona fahari juu ya jinsi mnavyoendelea kuamini na kustahimili katika udhalimu wote na mateso mnayopata.
5Co jest jawnym dowodem sprawiedliwego sądu Bożego, abyście godnymi byli poczytani królestwa Bożego, dla którego też cierpicie,
5Hayo yote yanathibitisha kwamba hukumu ya Mungu ni ya haki, na matokeo yake ninyi mtastahili Utawala wake ambao kwa ajili yake mnateseka.
6Ponieważ sprawiedliwa jest u Boga, żeby wzajem oddał uciśnienie tym, którzy was uciskają;
6Mungu atafanya jambo la haki: atawalipa mateso wale wanaowatesa ninyi,
7A wam, którzyście uciśnieni, odpocznienie z nami przy objawieniu Pana Jezusa z nieba z Aniołami mocy jego,
7na kuwapeni nafuu ninyi mnaoteseka, na sisi pia. Atafanya jambo hilo wakati Bwana atakapotokea kutoka mbinguni pamoja na malaika wake na wakuu
8W ogniu płomienistym oddawając pomstę tym, którzy Boga nie znają i tym, którzy nie są posłuszni Ewangielii Pana naszego, Jezusa Chrystusa;
8na miali ya moto, kuwaadhibu wale wanaomkataa Mungu na wale wasiotii Habari Njema ya Bwana wetu Yesu.
9Którzy pomstę odniosą, wieczne zatracenie od obliczności Paóskiej i od chwały mocy jego.
9Adhabu yao itakuwa kuangamizwa milele na kutengwa mbali na utukufu wake mkuu,
10Gdy przyjdzie, aby był uwielbiony w świętych swoich i aby się dziwnym okazał we wszystkich wierzących (dlatego iż uwierzono naszemu świadectwu u was) w on dzieó.
10wakati atakapokuja Siku ile kupokea utukufu kutoka kwa watu wake na heshima kutoka kwa wote wanaoamini. Ninyi pia mtakuwa miongoni mwao, kwani mmeuamini ule ujumbe tuliowaletea.
11Dlaczego też modlimy się zawsze za was, aby Bóg nasz godnymi was uczynił powołania tego i wypełnił wszystko upodobanie dobrotliwości swojej, i skutek wiary w mocy.
11Ndiyo maana tunawaombeeni daima. Tunamwomba Mungu wetu awawezeshe muyastahili maisha aliyowaitia myaishi. Tunamwomba, kwa uwezo wake, atimize nia yenu ya kutenda mema na kukamilisha kazi yenu ya imani.
12Aby było uwielbione imię Pana naszego, Jezusa Chrystusa w was, a wy w nim, według łaski Boga naszego i Pana Jezusa Chrystusa.
12Kwa namna hiyo, jina la Bwana wetu Yesu litapata utukufu kutoka kwenu, nanyi mtapata utukufu kutoka kwake kwa neema ya Mungu wetu na ya Bwana Yesu Kristo.