1Przetoż, bracia święci, powołania niebieskiego uczestnicy! obaczcie Apostoła i najwyższego kapłana wyznania naszego, Chrystusa Jezusa,
1Ndugu zangu watu wa Mungu ambao mmeitwa na Mungu, fikirini juu ya Yesu ambaye Mungu alimtuma awe Kuhani Mkuu wa imani tunayoiungama.
2Wiernego temu, który go postanowił, jako i Mojżesz był we wszystkim domu jego.
2Yeye alikuwa mwaminifu kwa Mungu aliyemteua kufanya kazi yake kama vile Mose alivyokuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Mungu.
3Albowiem tem większej chwały ten nad Mojżesza godzien, im większą cześć ma budownik domu, niżeli sam dom.
3Mjenzi wa nyumba hupata heshima zaidi kuliko hiyo nyumba yenyewe. Hali kadhalika naye Yesu anastahili heshima kubwa zaidi kuliko Mose.
4Bo każdy dom bywa budowany od kogo; ale który wszystkie rzeczy zbudował, Bóg jest.
4Kila nyumba hujengwa na mjenzi fulani--na Mungu ndiye mjenzi wa vitu vyote.
5A byłci Mojżesz wiernym we wszystkim domu jego, jako sługa, na świadectwo tego, co potem miało być mówione.
5Mose alikuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Bwana kama mtumishi, na alinena juu ya mambo ambayo Mungu atayasema hapo baadaye.
6Ale Chrystus jako syn nad domem swoim panuje, którego domem my jesteśmy, jeźli tylko tę pewną ufność i tę chwałę nadziei aż do koóca stateczną zachowamy.
6Lakini Kristo ni mwaminifu kama Mwana mwenye mamlaka juu ya nyumba ya Mungu. Sisi ni nyumba yake kama tukizingatia uhodari wetu na uthabiti wetu katika kile tunachotumainia.
7Przetoż jako mówi Duch Święty: Dziś, jeźlibyście głos jego usłyszeli,
7Kwa hiyo, basi, kama asemavyo Roho Mtakatifu: "Kama mkisikia sauti ya Mungu leo,
8Nie zatwardzajcież serc waszych, jako w rozdrażnieniu, w dzieó onego pokuszenia na puszczy.
8msiifanye mioyo yenu kuwa migumu kama wazee wenu walivyokuwa wakati walipomwasi Mungu; kama walivyokuwa siku ile kule jangwani,
9Gdzie mię kusili ojcowie wasi i doświadczali mię, i widzieli sprawy moje przez czterdzieści lat.
9Huko wazee wenu walinijaribu na kunichunguza, asema Bwana, ingawa walikuwa wameyaona matendo yangu kwa miaka arobaini.
10Dlategom się rozgniewał na ten naród i rzekłem: Ci zawsze błądzą sercem, a oni nie poznawają dróg moich.
10Kwa sababu hiyo niliwakasirikia watu hao nikasema, Fikira za watu hawa zimepotoka, hawajapata kamwe kuzijua njia zangu.
11Jakom przysiągł w gniewie moim, że nie wnijdą do odpocznienia mojego.
11Basi, nilikasirika, nikaapa: Hawataingia huko ambako ningewapa pumziko."
12Patrzcież, bracia! by snać nie było w którym z was serce złe i niewierne, które by odstępowało od Boga żywego;
12Basi ndugu, jihadharini asije akawako yeyote miongoni mwenu aliye na moyo mbaya hivyo na asiyeamini hata kujitenga na Mungu aliye hai.
13Ale napominajcie jedni drugich na każdy dzieó, póki się Dziś nazywa, aby kto z was nie był zatwardzony oszukaniem grzechu.
13Maadamu hiyo "Leo" inayosemwa katika Maandiko bado inatuhusu sisi, mnapaswa kusaidiana daima, ili mtu yeyote miongoni mwenu asidanganywe na dhambi na kuwa mkaidi.
14Albowiem staliśmy się uczestnikami Chrystusa, jeźliże tylko początek tego gruntu aż do koóca stateczny zachowamy.
14Maana sisi tunashirikiana na Kristo ikiwa tutazingatia kwa uthabiti tumaini tulilokuwa nalo mwanzoni.
15Przetoż póki bywa rzeczone: Dziś, jeźlibyście głos jego usłyszeli, nie zatwardzajcież serc waszych, jako w onem rozdrażnieniu.
15Maandiko yasema hivi: "Kama mkisikia sauti ya Mungu leo, msiifanye mioyo yenu kuwa migumu kama wazee wenu walivyokuwa wakati walipomwasi Mungu."
16Albowiem niektórzy usłyszawszy, rozdrażnili Pana, ale nie wszyscy, którzy byli wyszli z Egiptu przez Mojżesza.
16Ni akina nani basi, waliosikia sauti ya Mungu wakamwasi? Ni wale wote walioongozwa na Mose kutoka Misri.
17A na którychże się gniewał przez czterdzieści lat? Izali nie na tych, którzy grzeszyli, których ciała poległy na puszczy?
17Mungu aliwakasirikia akina nani kwa miaka arobaini? Aliwakasirikia wale waliotenda dhambi, maiti zao zikatapakaa kule jangwani.
18A którymże przysiągł, że nie mieli wnijść do odpocznienia jego? Azaż nie tym, którzy byli nieposłusznymi?
18Mungu alipoapa: "Hawataingia huko ambako ningewapa pumziko," alikuwa anawasema akina nani? Alikuwa anasema juu ya hao walioasi.
19I widzimy, iż tam nie mogli wnijść dla niedowiarstwa.
19Basi, twaona kwamba hawakuingia huko kwa sababu hawakuamini.