Polish

Swahili: New Testament

James

5

1Nuż teraz, bogacze! płaczcie, narzekając nad nędzami waszemi, które przyjdą.
1Na sasa sikilizeni enyi matajiri! Lieni na kuomboleza kwa sababu ya taabu zitakazowajieni.
2Bogactwo wasze zgniło, a szaty wasze mole zgryzły.
2Mali zenu zimeoza, na nguo zenu zimeliwa na nondo.
3Złoto wasze i srebro wasze pordzewiało, a rdza ich będzie na świadectwo przeciwko wam i pożre ciała wasze jako ogieó; zgromadziliście skarb na ostatnie dni.
3Dhahabu yenu na fedha vimeota kutu, na kutu hiyo itakuwa ushahidi dhidi yenu, nayo itakula miili yenu kama vile moto. Ninyi mmejilundikia mali katika siku hizi za mwisho!
4Oto, zapłata robotników, którzy żęli krainy wasze, od was zatrzymana woła, a wołania żeóców weszły do uszów Pana zastępów.
4Hamkuwalipa mishahara watumishi waliofanya kazi katika mashamba yenu. Sikilizeni malalamiko yao! Kilio cha hao wanaovuna mashamba yenu kimefika masikioni mwa Bwana, Mwenye Nguvu.
5Żyliście w rozkoszach na ziemi i bujaliście; wytuczyliście serca wasze jako na dzieó zabijania ofiar.
5Mmeishi duniani maisha ya kujifurahisha na ya anasa. Mmejinenepesha tayari kwa siku ya kuchinjwa.
6Potępiliście, zamordowaliście sprawiedliwego, a nie sprzeciwia się wam.
6Mmemhukumu na kumwua mtu asiye na hatia, naye hakuwapigeni.
7Przetoż, bracia! bądźcie cierpliwymi aż do przyjścia Paóskiego. Oto, oracz oczekuje drogiego pożytku ziemi, cierpliwie go oczekując, ażby otrzymał deszcz ranny i wieczorny.
7Basi, ndugu zangu, muwe na subira mpaka Bwana atakapokuja. Tazameni mkulima anavyongoja kwa subira mimea yake itoe mavuno mazuri. Yeye hungojea kwa subira mvua za masika na za vuli.
8Bądźcież i wy cierpliwymi, a utwierdzajcie serca wasze; albowiem się przybliża przyjście Paóskie.
8Nanyi pia mnapaswa kuwa na subira; imarisheni mioyo yenu, maana siku ya kuja kwake Bwana inakaribia.
9Nie wzdychajcie jedni przeciwko drugim, bracia! abyście nie byli osądzeni. Oto, sędzia już przede drzwiami stoi.
9Ndugu zangu, msinung'unikiane ninyi kwa ninyi msije mkahukumiwa na Mungu. Hakimu yu karibu, tayari kuingia.
10Bierzcie za przykład, bracia moi! utrapienia i cierpliwości proroków, którzy mówili w imieniu Paóskiem.
10Ndugu, mkitaka kuona mfano wa subira na uvumilivu katika mateso, fikirini juu ya manabii ambao walinena kwa jina la Bwana.
11Oto za błogosławionych mamy tych, którzy cierpieli. O cierpliwości Ijobowej słyszeliście i koniec Paóski widzieliście, iż wielce miłosierny jest Pan i litościwy.
11Tunawaita hao wenye heri kwa sababu walivumilia. Mmesikia habari za uvumilivu wa Yobu, na mnajua jinsi Bwana alivyomtendea mwishoni. Maana Bwana amejaa huruma na rehema.
12A przed wszystkiemi rzeczami, bracia moi! nie przysięgajcie ani przez niebo, ani przez ziemię, ani żadną inszą przysięgą; ale niech będzie mowa wasza: Tak, tak; i Nie, nie; abyście w obłudę nie wpadli.
12Zaidi ya hayo yote, ndugu zangu, msiape kwa mbingu, wala kwa dunia, wala kwa kitu kingine chochote. Semeni "Ndiyo" kama maana yenu ni ndiyo, na "La" kama maana yenu ni la, na hapo hamtahukumiwa na Mungu.
13Jest kto utrapiony między wami, niechże się modli; jest kto dobrej myśli, niechajże śpiewa.
13Je, pana mtu yeyote miongoni mwenu aliye na shida? Anapaswa kusali. Je, yuko mwenye furaha? Anapaswa kuimba nyimbo za sifa.
14Choruje kto między wami, niechże zawoła starszych zborowych, a niech się modlą za nim, pomazując go olejkiem w imieniu Paóskiem;
14Je, yuko mgonjwa kati yenu? Anapaswa kuwaita wazee wa kanisa, nao watamwombea na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana.
15A modlitwa wiary uzdrowi chorego i podniesie go Pan; a jeźliby się grzechu dopuścił, będzie mu odpuszczone.
15Wakiomba kwa imani mgonjwa ataponyeshwa; Bwana atampatia nafuu, na dhambi alizotenda zitaondolewa.
16Wyznawajcie jedni przed drugimi upadki, a módlcie się za drugimi; abyście byli uzdrowieni. Wiele może uprzejma modlitwa sprawiedliwego.
16Basi, ungamanianeni dhambi zenu, na ombeaneni, ili mpate kuponywa. Sala ya mtu mwema ina nguvu ya kutenda mengi.
17Elijasz był człowiek tymże biedom poddany jako i my, a modlitwą modlił się, żeby deszcz nie padał; i nie padał deszcz na ziemię trzy lata i sześć miesięcy,
17Eliya alikuwa binadamu kama sisi. Aliomba kwa moyo mvua isinyeshe, nayo haikunyesha nchini kwa muda wa miaka mitatu na miezi sita.
18I zaś się modlił, a wydało niebo deszcz i ziemia zrodziła owoce swoje.
18Kisha akaomba tena, mvua ikanyesha kutoka angani na nchi ikatoa mazao yake.
19Bracia! jeźliby się kto z was obłądził od prawdy, a nawróciłby go kto,
19Ndugu zangu, mmoja wenu akipotoka kuhusu ukweli, na mwingine akamrudisha,
20Niechże wie, że kto by odwrócił grzesznika od błędnej drogi jego, zachowa duszę od śmierci i zakryje mnóstwo grzechów.
20fahamuni kwamba, huyo anayemrudisha mwenye dhambi kutoka njia yake ya upotovu, ataiokoa roho yake kutoka kifo, na dhambi nyingi zitaondolewa.