1A roku piętnastego panowania Tyberyjusza Cesarza, gdy Poncki Piłat był starostą Judzkim, a Herod Tetrarchą Galilejskim, a Filip, brat jego, Tetrarchą Iturejskim i krainy Trachonickiej, a Lizanijasz Tetrarchą Abileóskim,
1Mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberio, Pontio Pilato alikuwa anatawala mkoa wa Yudea. Herode alikuwa mkuu wa mkoa wa Galilaya, na Filipo, ndugu yake, alikuwa mkuu wa mikoa ya Iturea na Trakoniti. Lusania alikuwa mkuu wa mkoa wa Abilene,
2Za najwyższych kapłanów Annasza i Kaifasza, stało się słowo Boże do Jana, Zacharyjaszowego syna, na puszczy.
2na Anasi na Kayafa walikuwa makuhani wakuu mjini Yerusalem. Wakati huo ndipo neno la Mungu lilipomjia Yohane, mwana wa Zakariya, kule jangwani.
3I przyszedł do wszystkiej krainy leżącej około Jordanu, każąc chrzest pokuty na odpuszczenie grzechów.
3Basi, Yohane akaenda katika sehemu zote zilizopakana na mto Yordani, akihubiri watu watubu na kubatizwa ili Mungu awaondolee dhambi.
4Jako napisano w księgach proroctw Izajasza proroka, mówiącego: Głos wołającego na puszczy; gotujcie drogę Paóską, proste czyócie ścieżki jego.
4Ndivyo ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: "Sauti ya mtu imesikika jangwani: Mtayarishieni Bwana njia yake; nyosheni mapito yake.
5Każdy padół będzie wypełniony, a każda góra i pagórek będzie zniżony, i miejsca krzywe wyprostują się, a ostre drogi będą gładkiemi;
5Kila bonde litafukiwa, kila mlima na kilima vitasawazishwa; palipopindika patanyooshwa, njia mbaya zitatengenezwa.
6I ogląda wszelkie ciało zbawienie Boże.
6Na, watu wote watauona wokovu utokao kwa Mungu."
7Mówił tedy ludowi, który wychodził, aby był ochrzczony od niego: Rodzaju jaszczurczy! któż wam pokazał, żebyście uciekali przed przyszłym gniewem?
7Basi, Yohane akawa anawaambia watu wengi waliofika ili awabatize: "Enyi kizazi cha nyoka! Ni nani aliyewadokezea kwamba mngeweza kuiepuka ghadhabu inayokuja?
8Przynoścież tedy owoce godne pokuty, a nie poczynajcie mówić sami w sobie: Ojca mamy Abrahama; albowiem powiadam wam, że Bóg może i z tych kamieni wzbudzić dzieci Abrahamowi.
8Basi, onyesheni kwa matendo kwamba mmetubu. Msianze sasa kusema: Sisi ni watoto wa Abrahamu. Nawaambieni hakika, Mungu anaweza kuyageuza mawe haya yawe watoto wa Abrahamu!
9A już siekiera do korzenia drzew przyłożona jest; przetoż każde drzewo, które nie przynosi owocu dobrego, bywa wycięte i w ogieó wrzucone.
9Lakini, sasa hivi shoka limewekwa tayari kukata mizizi ya miti. Kila mti usiozaa matunda mazuri utakatwa na kutupwa motoni."
10I pytał go lud mówiąc: Cóż tedy czynić będziemy?
10Umati wa watu ukamwuliza, "Tufanye nini basi?"
11A on odpowiadając rzekł im: Kto ma dwie suknie, niechaj udzieli temu, co nie ma; a kto ma pokarm niech także uczyni.
11Akawajibu, "Aliye na nguo mbili amgawie yule asiye na nguo; aliye na chakula afanye vivyo hivyo."
12Przyszli też i celnicy, aby byli chrzczeni, i rzekli do niego: Nauczycielu! a my cóż czynić będziemy?
12Nao watoza ushuru wakaja pia ili wabatizwe, wakamwuliza, "Mwalimu, tufanye nini?"
13A on rzekł do nich: Nic więcej nie wyciągajcie nad to, co wam postanowiono.
13Naye akawaambia, "Msitoze ushuru zaidi ya kima kilichowekwa."
14Pytali go też i żołnierze, mówiąc: A my cóż czynić będziemy? I rzekł do nich: Nikomu gwałtu nie czyócie, i nikogo nie potwarzajcie, a przestawajcie na żołdzie waszym.
14Nao askari wakamwuliza, "Na sisi tufanye nini?" Naye akawajibu, "Msichukue vitu vya mtu yeyote kwa nguvu wala kumshtaki yeyote kwa uongo. Toshekeni na mishahara yenu."
15A gdy lud oczekiwał, i myślili wszyscy w sercach swych o Janie, jeśliby snać on nie był Chrystusem,
15Wote walikuwa wanatazamia kitu fulani; basi, wakaanza kujiuliza mioyoni mwao kuhusu Yohane: kuwa labda yeye ndiye Kristo.
16Odpowiedział Jan wszystkim, mówiąc: Jać was chrzczę wodą; lecz idzie mocniejszy nad mię, któremum nie jest godzien rozwiązać rzemyka u butów jego; ten was chrzcić będzie Duchem Świętym i ogniem.
16Hapo Yohane akawaambia wote, "Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini anakuja mwenye uwezo zaidi kuliko mimi ambaye sistahili hata kumfungulia kamba za viatu vyake. Yeye atawabatizeni kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
17Którego łopata jest w ręku jego, a wyczyści bojewisko swoje, i zgromadzi pszenicę do gumna swego, ale plewy spali ogniem nieugaszonym.
17Yeye ni kama mtu anayeshika mikononi mwake chombo cha kupuria nafaka, aipure nafaka yake, akusanye ngano ghalani mwake, na makapi ayachome kwa moto usiozimika."
18A tak wiele i innych rzeczy napominając, odpowiadał ludowi.
18Hivyo, pamoja na mawaidha mengine mengi, Yohane aliwahimiza watu akiwahubiria Habari Njema.
19A Herod Tetrarcha, będąc strofowany od niego dla Herodyjady, żony Filipa, brata jego, i dla wszystkich złych spraw, które czynił Herod.
19Lakini Yohane alimgombeza Herode, mkuu wa mkoa, kwa sababu alikuwa amemchukua Herodia, mke wa ndugu yake, na kumfanya mke wake; na pia kwa ajili ya mabaya yote aliyokuwa amefanya.
20Przydał i to nade wszystko, iż wsadził Jana do więzienia.
20Kisha Herode akazidisha ubaya wake kwa kumtia Yohane gerezani.
21I stało się, gdy był ochrzczony wszystek lud, i gdy Jezus był ochrzczony, i modlił się, że się niebo otworzyło;
21Watu wote walipokuwa wamekwisha batizwa, Yesu naye alibatizwa. Na alipokuwa akisali, mbingu zilifunguka,
22I zstąpił naó Duch Święty w kształcie cielesnym jako gołębica, i stał się głos z nieba, mówiąc: Tyś jest on Syn mój miły; w tobie mi się upodobało.
22na Roho Mtakatifu akamshukia akiwa na umbo kama la njiwa. Sauti ikasikika kutoka mbinguni: "Wewe ndiwe Mwanangu mpendwa, nimependezwa nawe."
23A Jezus poczynał być jakoby w trzydziestu latach, będąc (jako mniemano,)synem Józefa, syna Helego,
23Yesu alipoanza kazi yake hadharani, alikuwa na umri upatao miaka thelathini, na watu walidhani yeye ni mwana wa Yosefu, mwana wa Heli.
24Syna Matatowego, syna Lewiego, syna Melchyjego, syna Jannego, syna Józefowego,
24Heli alikuwa mwana wa Mathati, mwana wa Lawi, mwana wa Melki, mwana wa Yanai, mwana wa Yosefu,
25Syna Matatyjaszowego, syna Amosowego, syna Naumowego, syna Eslego, syna Naggiego,
25mwana wa Matathia, mwana wa Amosi, mwana wa Nahumu, mwana wa Hesli, mwana wa Nagai,
26Syna Maatowego, syna Mattatyjaszowego, syna Semejego, syna Józefowego, syna Judowego,
26mwana wa Maathi, mwana wa Matathia, mwana wa Shemeni, mwana wa Yoseki, mwana wa Yuda,
27Syna Joannowego, syna Resowego, syna Zorobabelowego, syna Salatyjelowego, syna Neryjego,
27mwana wa Yohanani, mwana wa Resa, mwana wa Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, mwana wa Neri,
28Syna Melchyjego, syna Addyjego, syna Kosamowego, syna Elmodamowego, syna Irowego,
28mwana wa Melki, mwana wa Adi, mwana wa Kosamu, mwana wa Elmadamu, mwana wa Eri,
29Syna Jozego, syna Elijezerowego, syna Jorymowego, syna Mattatego, syna Lewiego,
29mwana wa Yoshua, mwana wa Eliezeri, mwana wa Yorimu, mwana wa Mathati, mwana wa Lawi,
30Syna Symeonowego, syna Judowego, syna Józefowego, syna Jonanowego, syna Elijakimowego,
30mwana wa Simeoni, mwana wa Yuda, mwana wa Yosefu, mwana wa Yonamu, mwana wa Eliakimu,
31Syna Meleowego, syna Mainanowego, syna Mattatanowego, syna Natanowego, syna Dawidowego,
31mwana wa Melea, mwana wa Mena, mwana wa Matatha, mwana wa Nathani, mwana wa Daudi,
32Syna Jessego, syna Obedowego, syna Boozowego, syna Salmonowego, syna Nasonowego,
32mwana wa Yese, mwana wa Obedi, mwana wa Boazi, mwana wa Salmoni, mwana wa Nashoni,
33Syna Aminadabowego, syna Aramowego, syna Esromowego, syna Faresowego, syna Judowego,
33mwana wa Aminadabu, mwana wa Admini, mwana wa Arni, mwana wa Hesroni, mwana wa Feresi, mwana wa Yuda,
34Syna Jakóbowego, syna Izaakowego, syna Abrahamowego, syna Tarego, syna Nachorowego,
34mwana wa Yakobo, mwana wa Isaka, mwana wa Abrahamu, mwana wa Tera, mwana wa Nahori,
35Syna Saruchowego, syna Ragawowego, syna Falekowego, syna Heberowego, syna Salego,
35mwana wa Serugi, mwana wa Reu, mwana wa Pelegi, mwana wa Eberi, mwana wa Sala,
36Syna Kainowego, syna Arfaksadowego, syna Semowego, syna Noego, syna Lamechowego,
36mwana wa Kainani, mwana wa Arfaksadi, mwana wa Shemu, mwana wa Noa, mwana wa Lameki,
37Syna Matusalemowego, syna Enochowego, syna Jaredowego, syna Malaleelowego, syna Kainanowego,
37mwana wa Mathusala, mwana wa Henoki, mwana wa Yaredi, mwana wa Mahalaleli, mwana wa Kenani,
38Syna Enosowego, syna Setowego, syna Adamowego, syna Bożego.
38mwana wa Enosi, mwana wa Sethi, mwana wa Adamu, aliyekuwa wa Mungu.