Polish

Swahili: New Testament

Revelation

21

1Potemem widział niebo nowe i ziemię nową; albowiem pierwsze niebo i pierwsza ziemia przeminęła, a morza już więcej nie było.
1Kisha nikaona mbingu mpya na dunia mpya. Mbingu ile ya kwanza na dunia ile ya kwanza vilikuwa vimetoweka, nayo bahari pia haikuweko tena.
2A ja Jan widziałem ono święte miasto, Jeruzalem nowe, zstępujące z nieba od Boga zgotowane, jako oblubienicę ubraną mężowi swemu.
2Nikaona mji mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka kwa Mungu mbinguni. Ulikuwa umetayarishwa vizuri kama bibi arusi aliyepambwa tayari kukutana na mumewe.
3I słyszałem głos wielki z nieba mówiący: Oto przybytek Boży z ludźmi, i będzie mieszkał z nimi; a oni będą ludem jego, a sam Bóg będzie z nimi, będąc Bogiem ich.
3Kisha nikasikia sauti kubwa kutoka katika kiti cha enzi ikisema, "Tazama! Mungu amefanya makao yake kati ya watu. Atakaa kati yao, nao watakuwa watu wake, naye atakuwa Mungu wao.
4I otrze Bóg wszelką łzę z oczów ich; a śmierci więcej nie będzie, ani smutku, ani krzyku, ani boleści nie będzie; albowiem pierwsze rzeczy pominęły.
4Yeye atayafuta machozi yao yote; maana hakutakuwako tena na kifo, wala uchungu, wala kilio, wala maumivu; maana ile hali ya kale imepita!"
5I rzekł ten, który siedział na stolicy: Oto wszystko nowe czynię. I rzekł mi: Napisz: bo te słowa są wierne i prawdziwe.
5Kisha yule aliyeketi juu ya kiti cha enzi akasema, "Tazama, nafanya yote mapya." Tena akaniambia, "Andika hili, maana maneno haya ni ya kuaminika na ya kweli!"
6I rzekł mi: Stało się. Jam jest Alfa i Omega, początek i koniec. Ja pragnącemu dam darmo ze źródła wody żywej.
6Kisha akaniambia, "Yametimia! Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Aliye na kiu nitampa kinywaji cha bure kutoka katika chemchemi ya maji ya uzima.
7Kto zwycięży, odziedziczy wszystko i będę mu Bogiem, a on mi będzie synem.
7Yeyote atakayeshinda atapokea hiki, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu.
8Lecz bojaźliwym i niewiernym, i obmierzłym, i mężobójcom, i wszetecznikom, i czarownikom, i bałwochwalcom, i wszystkim kłamcom część ich dana będzie w jeziorze gorejącem ogniem i siarką: Tać jest śmierć wtóra.
8Lakini watu waoga, wasioamini, wapotovu, wauaji, wazinzi, wachawi, waabudu sanamu, na waongo wote, mahali pao patakuwa ndani ya lile ziwa linalowaka moto na kiberiti; hicho ndicho kifo cha pili."
9Tedy przyszedł do mnie jeden z onych siedmiu Aniołów, którzy mieli siedm czasz napełnionych siedmioma plagami ostatecznemi, i mówił ze mną, i rzekł: Chodź sam, okażę ci oblubienicę, małżonkę Barankową.
9Kisha mmoja wa wale malaika saba waliokuwa na yale mabakuli saba yaliyokuwa yamejaa mabaa saba ya mwisho, akaja na kuniambia, "Njoo! Mimi nitakuonyesha bibi arusi, mkewe Mwanakondoo!"
10I zaniósł mię w duchu na górę wielką i wysoką, i okazał mi miasto wielkie, ono święte Jeruzalem, zstępujące z nieba od Boga,
10Basi, Roho akanikumba, naye malaika akanipeleka juu ya mlima mrefu sana. Akanionyesha mji mtakatifu, ukishuka kutoka kwa Mungu mbinguni,
11Mające chwałę Bożą, którego światłość podobna była kamieniowi najkosztowniejszemu, jako kamieniowi jaspisowi, na kształt kryształu przezroczystemu;
11uking'aa kwa utukufu wa Mungu. Mwangaza wake ulikuwa kama wa jiwe la thamani kubwa kama yaspi, angavu kama kioo.
12I mające mur wielki i wysoki, mające bram dwanaście, a na onych bramach dwanaście Aniołów i imiona napisane, które są dwanaście pokoleó synów Izraelskich.
12Ulikuwa na ukuta mrefu na mkubwa, wenye milango kumi na miwili, na malaika wanangojea kumi na wawili. Majina ya wangoja milango kumi na mawili ya Israeli yalikuwa yameandikwa juu ya milango hiyo.
13Od wschodu bramy trzy, od północy bramy trzy, od południa bramy trzy, od zachodu bramy trzy.
13Kila upande ulikuwa na milango mitatu: upande wa mashariki, milango mitatu, kaskazini milango mitatu, kusini milango mitatu na magharibi milango mitatu.
14A mur miasta miał gruntów dwanaście, a na nich dwanaście imion dwunastu Apostołów Barankowych.
14Kuta za mji huo zilikuwa zimejengwa juu ya mawe ya msingi kumi na mawili, na juu ya mawe hayo yalikuwa yameandikwa majina na mitume kumi na wawili wa Mwanakondoo.
15A ten, co mówił ze mną, miał trzcinę złotą, a zmierzył miasto i bramy jego, i mur jego.
15Basi, yule malaika aliyekuwa anasema nami alikuwa na kijiti cha dhahabu cha kupimia, kwa ajili ya kuupima huo mji, milango yake na kuta zake.
16A położenie miasta onego jest czworograniaste, a długość jego taka jest, jako i szerokość. I pomierzył miasto ono trzciną na dwanaście tysięcy stajan; a długość i szerokość i wysokość jego równe są.
16Mji wenyewe ulikuwa wa mraba, upana na urefu wake sawa. Basi, malaika akaupima mji huo kwa kijiti chake: ulikuwa na urefu, upana na urefu wa kwenda juu, kama kilomita elfu mbili na mia nne.
17I zmierzył mur jego na sto czterdzieści cztery łokcie miary człowieczej, która jest miara Aniołowa.
17Kisha akaupima ukuta wake pia; nao ulikuwa mita sitini kwa kipimo cha macho cha kibinadamu ambacho malaika alitumia.
18A było budowanie muru jego z jaspisu; a samo miasto było złoto czyste, podobne szkłu czystemu.
18Ukuta huo ulikuwa umejengwa kwa mawe mekundu ya thamani, na mji wenyewe ulikuwa umejengwa kwa dhahabu safi, angavu kama kioo.
19A grunty muru miasta ozdobione były wszelkim kamieniem drogim. Pierwszy grunt był jaspis, wtóry szafir, trzeci chalcedon, czwarty szmaragd.
19Mawe ya msingi wa ukuta huo yalikuwa yamepambwa kwa kila aina ya mawe ya thamani. Jiwe la kwanza la msingi lilikuwa jiwe la thamani jekundu, la pili yakuti samawati, la tatu kalkedoni, la nne zamaradi,
20Piąty sardoniks, szósty sardyjusz, siódmy chrysolit, ósmy beryllus, dziewiąty topazyjusz, dziesiąty chrysopras, jedenasty hijacynt, dwunasty ametyst.
20la tano sardoniki, la sita akiki, la saba krisolito, la nane zabarijadi, la tisa topazi, la kumi krisopraso, la kumi na moja yasinto, na la kumi na mbili amethisto.
21A dwanaście bram jest dwanaście pereł: a każda brama była z jednej perły, a rynek miasta złoto czyste jako szkło przezroczyste.
21Na ile milango kumi na miwili ilikuwa lulu kumi na mbili; kila mlango ulikuwa umetengenezwa kwa lulu moja. Barabara kuu ya mji ilikuwa imetengenezwa kwa dhahabu safi, angavu kama kioo.
22Alem kościoła nie widział w niem; albowiem Pan, Bóg wszechmogący, jest kościołem jego, i Baranek.
22Sikuona hekalu katika mji huo, maana Bwana Mungu Mwenye Uwezo na yule Mwanakondoo ndio Hekalu lake.
23A nie potrzebuje to miasto słoóca ani księżyca, aby świeciły w niem; albowiem chwała Boża oświeciła je, a świecą jego jest Baranek.
23Mji huo hauhitaji jua wala mwezi kuangazia, maana utukufu wa Mungu huuangazia, na taa yake ni yule Mwanakondoo.
24A narody, które będą zbawione, będą chodziły w świetle jego, a królowie ziemscy chwałę i cześć swoję do niego przyniosą.
24Watu wa mataifa watatembea katika mwanga wake, na wafalme wa dunia watauletea utajiri wao.
25A bramy jego nie będą zamknięte we dnie; albowiem tam nocy nie będzie.
25Milango ya mji huo itakuwa wazi mchana wote; maana hakutakuwa na usiku humo.
26I wniosą do niego chwałę i cześć narodów.
26Fahari na utajiri wa watu wa mataifa utaletwa humo ndani.
27I nie wnijdzie do niego nic nieczystego i czyniącego obrzydliwość i kłamstwo, tylko ci, którzy są napisani w księgach żywota Barankowych.
27Lakini hakuna chochote kilicho najisi kitakachoingia humo; wala mtu yeyote atendaye mambo ya kuchukiza au ya uongo hataingia humo. Ni wale tu walioandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwanakondoo ndio watakaoingia ndani.