1I ukazał mi rzekę czystą wody żywota, jasną jako kryształ, wychodzącą z stolicy Bożej i Barankowej.
1Kisha malaika akanionyesha mto wa maji ya uzima maangavu kama kioo yakitoka kwenye kiti cha enzi cha Mungu na Mwanakondoo.
2A w pośród rynku jego z obu stron rzeki było drzewo żywota, przynoszące owoc dwanaścioraki, na każdy miesiąc wydawające owoc swój, a liście drzewa służyły ku uzdrowieniu pogan.
2Mto huo ulitiririka kupitia katikati ya barabara kuu ya mji. Kandokando ya mto huo kulikuwa na mti wa uzima unaozaa matunda mara kumi na mbili kwa mwaka, yaani kila mwezi; na majani yake ni dawa ya kuwaponya watu wa mataifa.
3I nie będzie więcej żadnego przeklęstwa, ale stolica Boża i Barankowa w niem będzie, a słudzy jego służyć mu będą,
3Hapana kitu chochote kilicholaaniwa kitakachokuwa katika mji huo. Kiti cha enzi cha Mungu na cha Mwanakondoo kitakuwa katika mji huo, na watumishi wake watamwabudu.
4I patrzyć będą na oblicze jego, a imię jego na czołach ich będzie.
4Watauona uso wake, na jina lake litaandikwa juu ya paji za nyuso zao.
5I nocy tam nie będzie i nie będą potrzebować świecy i światłości słonecznej; bo je Pan Bóg oświeca, i królować będą na wieki wieków.
5Usiku hautakuwako tena, wala hawatahitaji mwanga wa taa au wa jua, maana Bwana Mungu atawaangazia, nao watatawala milele na milele.
6I rzekł mi: Te słowa wierne są i prawdziwe, a Pan, Bóg świętych proroków, posłał Anioła swego, aby ukazał sługom swoim, co się ma stać w rychle.
6Kisha malaika akaniambia, "Maneno haya ni ya kweli na ya kuaminika. Bwana Mungu ambaye huwapa manabii Roho wake, alimtuma malaika wake awaonyeshe watumishi wake mambo ambayo lazima yatukie punde.
7Oto przychodzę rychło: Błogosławiony, który zachowuje słowa proroctwa księgi tej.
7"Sikiliza! Naja upesi. Heri yake anayeyazingatia maneno ya unabii yaliyo katika kitabu hiki."
8A ja Jan widziałem i słyszałem te rzeczy. A gdym słyszał i widział, upadłem, abym się pokłonił przed nogami Anioła onego, który mi to pokazywał.
8Mimi Yohane, niliyaona na kusikia mambo haya. Nilipokwisha sikia na kuona nikajitupa chini mbele ya miguu ya huyo malaika aliyenionyesha mambo hayo, nikataka kumwabudu.
9Ale mi on rzekł: Patrz, abyś tego nie czynił; bom jest spółsługa twój i braci twoich proroków, i tych, co chowają słowa księgi tej; Bogu się kłaniaj.
9Lakini yeye akaniambia, "Acha! Mimi ni mtumishi tu kama wewe na ndugu zako manabii na wote wanaoyatii maagizo yaliyomo katika kitabu hiki. Mwabudu Mungu!"
10Potem mi rzekł: Nie pieczętuj słów proroctwa księgi tej; albowiem czas blisko jest.
10Tena akaniambia, "Usiyafiche kama siri maneno ya unabii yaliyomo katika kitabu hiki, maana wakati wa kutimizwa kwake umekaribia.
11Kto szkodzi, niech jeszcze szkodzi; a kto jest plugawy, niech jeszcze będzie plugawszy; a kto jest sprawiedliwy, niech się jeszcze usprawiedliwi; a kto święty, niech jeszcze będzie poświęcony.
11Kwa sasa anayetenda mabaya na aendelee kutenda mabaya, na aliye mchafu aendelee kuwa mchafu. Mwenye kutenda mema na azidi kutenda mema, na aliye mtakatifu na azidi kuwa mtakatifu."
12A oto przychodzę rychło, a zapłata moja jest ze mną, abym oddał każdemu według uczynków jego.
12"Sikiliza!" Asema Yesu, "Naja upesi, pamoja na tuzo nitakalompa kila mmoja kufuatana na matendo yake.
13Jam jest Alfa i Omega, początek i koniec, pierwszy i ostateczny.
13Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho, wa kwanza na wa mwisho."
14Błogosławieni, którzy czynią przykazania jego, aby mieli prawo do drzewa żywota, i aby weszli bramami do miasta.
14Heri yao wale wanaoosha mavazi yao, kwani watakuwa na haki ya kula tunda la mti wa uzima, na haki ya kuingia mjini kwa kupitia milango yake.
15A na dworze będą psy i czarownicy, i wszetecznicy, i mężobójcy, i bałwochwalcy, i każdy, który miłuje i czyni kłamstwo.
15Lakini mbwa, wachawi, wazinzi, wauaji, waabudu sanamu na wote wanaopenda kusema uongo, watakaa nje ya mji.
16Ja Jezus posłałem Anioła mojego, aby wam świadczył o tych rzeczach we zborach. Jam jest korzeó i rodzaj on Dawidowy, gwiazda jasna i poranna.
16"Mimi, Yesu, nimemtuma malaika wangu awathibitishieni mambo haya katika makanisa. Mimi ni mzawa wa ukoo wa Daudi. Mimi ni nyota angavu ya asubuhi!"
17A Duch i oblubienica mówią: Przyjdź! A kto słyszy, niech rzecze: Przyjdź! A kto pragnie, niech przyjdzie; a kto chce, niech bierze wodę żywota darmo.
17Roho na Bibiarusi waseme, "Njoo!" Kila mtu asikiaye hili, na aseme, "Njoo!" Kisha, yeyote aliye na kiu na aje; anayetaka maji ya uzima na apokee bila malipo yoyote.
18A oświadczam się każdemu słuchającemu słów proroctwa księgi tej: Jeźliby kto przydał do tego, przyda mu też Bóg plag opisanych w tej księdze;
18Mimi Yohane nawapa onyo wote wanaosikia maneno ya unabii yaliyomo katika kitabu hiki: mtu yeyote akiongeza chochote katika mambo haya, Mungu atamwongezea mabaa yaliyoandikwa katika kitabu hiki.
19A jeźliby kto ujął ze słów księgi proroctwa tego, odejmie też Bóg część jego z księgi żywota i z miasta świętego, i z tych rzeczy, które są napisane w tej księdze.
19Na mtu yeyote akipunguza chochote katika maneno ya unabii yaliyomo katika kitabu hiki, Mungu atamnyang'anya sehemu yake katika ule mti wa uzima, na sehemu yake katika mji mtakatifu, ambavyo vimeelezwa katika kitabu hiki.
20Tak mówi ten, który świadectwo daje o tych rzeczach: Zaiste, przyjdę rychło. Amen. I owszem przyjdź, Panie Jezusie!
20Naye anayetoa ushahidi wake juu ya mambo haya asema: "Naam! Naja upesi." Amina. Na iwe hivyo! Njoo Bwana Yesu!
21Łaska Pana naszego, Jezusa Chrystusa, niech będzie z wami wszystkimi. Amen.
21Nawatakieni nyote neema ya Bwana Yesu. Amen.