1I zatrąbił piąty Anioł i widziałem, że gwiazda spadła z nieba na ziemię, a dano jej klucz studni przepaści.
1Kisha malaika wa tano akapiga tarumbeta yake. Nami nikaona nyota iliyokuwa imeanguka juu ya nchi kutoka mbinguni. Nayo ikapewa ufunguo wa shimo la Kuzimu.
2I otworzyła studnię przepaści; i wystąpił dym z onej studni, jakoby dym pieca wielkiego, i zaćmiło się słoóce i powietrze od dymu onej studni.
2Basi, nyota hiyo ikafungua shimo la Kuzimu, kukatoka moshi wa tanuru kubwa. Jua na anga vikatiwa giza kwa moshi huo wa Kuzimu.
3A z onego dymu wyszły szaraócze na ziemię i dano im moc, jako mają moc niedźwiadki ziemskie;
3Nzige wakatoka katika moshi huo, wakaingia duniani wakapewa nguvu kama ya ng'e.
4A rzeczono im, żeby nie szkodziły trawie ziemi, ani żadnej rzeczy zielonej, ani żadnemu drzewu, ale tylko samym ludziom, którzy nie mają pieczęci Bożej na czołach swoich.
4Wakaamrishwa wasiharibu nyasi za nchi wala majani wala miti yoyote, bali wawaharibu wale tu ambao hawakupigwa mhuri wa Mungu katika paji la uso.
5A dano im, nie żeby ich zabijały, ale aby ich dręczyły przez pięć miesięcy, a udręczenie ich, aby było jako udręczenie od niedźwiadka, gdy człowieka ukąsi.
5Nzige hao hawakuruhusiwa kuwaua watu, ila kuwatesa tu kwa muda wa miezi mitano. Maumivu watakayosababisha ni kama maumivu yanayompata mtu wakati anapoumwa na ng'e.
6Przetoż w one dni szukać będą ludzie śmierci, ale jej nie znajdą; i będą chcieli umrzeć, ale śmierć od nich uciecze.
6Muda huo watu watatafuta kifo lakini hawatakipata; watatamani kufa lakini kifo kitawakimbia.
7A kształt onych szaraóczy podobny był koniom zgotowanym do bitwy, a na głowach ich były jakoby korony podobne złotu, a twarze ich jako twarze ludzkie;
7Kwa kuonekana, nzige hao walikuwa kama farasi waliowekwa tayari kwa vita. Juu ya vichwa vyao walikuwa na taji zilizo kama za dhahabu, na nyuso zao zilikuwa kama za binadamu.
8I miały włosy jako włosy niewieście, a zęby ich były jako lwie;
8Nywele zao zilikuwa kama nywele za wanawake, na meno yao yalikuwa kama meno ya simba.
9A miały pancerze jako pancerze żelazne, a szum skrzydeł ich, jako grzmot wozów, gdy wiele koni bieży do bitwy.
9Vifua vyao vilikuwa vimefunikwa kitu kama ngao ya chuma. Sauti ya mabawa yao ilikuwa kama sauti ya msafara wa magari ya farasi wengi wanaokimbilia vitani.
10A ogony miały podobne niedźwiadkom, a żądła były w ogonach ich, a moc ich była szkodzić ludziom przez pięć miesięcy;
10Walikuwa na mikia na miiba kama ng'e, na kwa mikia hiyo, walikuwa na nguvu ya kuwadhuru watu kwa muda wa miezi mitano.
11A miały nad sobą króla, anioła przepaści, któremu imię po żydowsku Abaddon, a po grecku ma imię Apolijon.
11Tena wanaye mfalme anayewatawala, naye ndiye malaika wa kuzimu; jina lake kwa Kiebrania ni Abadoni, na kwa Kigiriki ni Apolioni, yaani mwangamizi.
12Biada jedno przeszło, a oto jeszcze idą dwa biada potem.
12Maafa ya kwanza yamepita; bado mengine mawili yanafuata.
13Tedy zatrąbił Anioł szósty, a słyszałem głos jeden ze czterech rogów ołtarza złotego, który jest przed oblicznością Bożą,
13Kisha malaika wa sita akapiga tarumbeta yake. Nami nikasikia sauti moja kutoka katika pembe nne za madhabahu ya dhahabu iliyokuwa mbele ya Mungu.
14Mówiący szóstemu Aniołowi, który miał trąbę: Rozwiąż onych czterech Aniołów związanych u wielkiej rzeki Eufrates.
14Sauti hiyo ikamwambia huyo malaika wa sita mwenye tarumbeta, "Wafungulie malaika wanne waliofungwa kwenye mto mkubwa Eufrate!"
15I rozwiązani są oni czterej Aniołowie, zgotowani na godzinę i na dzieó, i na miesiąc, i na rok, aby pobili trzecią część ludzi.
15Naye akawafungulia malaika hao wanne ambao walikuwa wametayarishwa kwa ajili ya saa hiyo ya siku ya mwezi huo, wa mwaka huohuo, kuua theluthi moja ya wanaadamu.
16A liczba wojska jezdnego była dwieściekroć tysiąc tysięcy; bom słyszał liczbę ich.
16Nilisikia idadi ya majeshi wapanda farasi ilikuwa milioni mia mbili.
17Widziałem także konie w widzeniu, a ci, którzy siedzieli na nich, mieli pancerze ogniste hijacyntowe i siarczane; a głowy onych koni były jako głowy lwie, a z gęby ich wychodził ogieó i dym i siarka.
17Hivi ndivyo nilivyowaona hao farasi na wapanda farasi katika hiyo njozi: Walikuwa na ngao vifuani zilizokuwa moto mtupu, zenye rangi ya samawati na njano kama kiberiti. Vichwa vya hao farasi vilikuwa kama vya simba; na moto, moshi, na kiberiti vilikuwa vinatoka kinywani mwao.
18A od tego trojga pobita jest trzecia część ludzi od ognia i od dymu, i od siarki, które wychodziły z gąb ich.
18Theluthi moja ya wanaadamu waliuawa kwa mabaa hayo matatu yaani, moto, moshi na kiberiti, yaliyokuwa yanatoka katika vinywa vyao;
19Albowiem moc ich jest w gębach ich i w ogonach ich; bo ogony ich wężom są podobne, mając głowy, któremi szkodzą.
19maana nguvu ya farasi hao ilikuwa vinywani mwao na katika mikia yao. Mikia yao ilikuwa na vichwa kama nyoka, na waliitumia hiyo kuwadhuru watu.
20A inni ludzie, którzy nie są pobici temi plagami, ani pokutowali od uczynków rąk swoich, aby się nie kłaniali dyjabłom i bałwanom złotym i srebrnym, i miedzianym, i kamiennym i drewnianym, którzy ani widzieć nie mogą, ani słyszeć, ani chodzić;
20Wanaadamu wengine waliobaki ambao hawakuuawa na mabaa hayo, hawakugeuka na kuviacha vitu walivyokuwa wametengeneza kwa mikono yao wenyewe; bali wakaendelea kuabudu pepo, sanamu za dhahabu, fedha, shaba, mawe na miti, vitu ambavyo haviwezi kuona, kusikia wala kutembea.
21Ani pokutowali z mężobójstw swoich, ani z czarów swoich, ani z wszeteczeóstw swoich, ani z złodziejstw swoich.
21Wala hawakutubu na kuacha kufanya mauaji, uchawi, uzinzi, na wizi.