1Phrala le, chi mangav te na zhanen, ke sa amare dada sas tela nuvero, ai savorhe nakhle andai maria.
1Ndugu, nataka mjue kwamba babu zetu wote walikuwa chini ya ulinzi wa lile wingu, na kwamba wote walivuka salama ile bahari.
2Savorhe sas bolde ando Moses tela o nuvero ai ande maria.
2Wote walibatizwa katika umoja na Mose kwa lile wingu na ile bahari.
3Kai savorhe xale iek fielo xamos Devleske.
3Wote walikula chakula kilekile cha kiroho,
4Kai pile savorhe iek pai anda Swunto Duxo; ke penas ka stana baxreske kai avela pala lende: ai kadia stana baxreske sas O Kristo.
4wakanywa pia kinywaji kilekile cha kiroho, maana walikunywa kutoka ule mwamba wa kiroho uliowafuata; mwamba huo ulikuwa Kristo mwenyewe.
5Numa mai but anda lende nai drago le Devleske: ke but xasaile ande pusta.
5Hata hivyo, wengi wao hawakumpendeza Mungu, na maiti zao zilisambazwa jangwani.
6Akana kodola dieluria kerdile ame kashte te podain amenge te zhanas so kerdilia, kaste te na aven ame chorhe ginduria sar sa le len.
6Sasa, mambo hayo yote ni mfano tu kwetu; yanatuonya sisi tusitamani ubaya kama wao walivyotamani.
7Na kerdion kodolendar kai lenpe pala ikoni, sar uni anda lende kai si ramome, le manush beshle tele te xan ai te pen, porme wushtilo opre veselisaile.
7Msiwe waabudu sanamu kama baadhi yao walivyokuwa; kama yasemavyo Maandiko: "Watu waliketi kula na kunywa, wakasimama kucheza."
8Na ingeras amaro stato kai kurvia, sar uni anda lende kerde, ai mule anda lende ande iek dies bishtai trin mi.
8Wala tusizini kama baadhi yao walivyozini, wakaangamia siku moja watu ishirini na tatu elfu.
9Na zumaven O Krisro sar kerde uni anda lende, ai le sapa xale le.
9Tusimjaribu Bwana kama baadhi yao walivyomjaribu, wakauawa na nyoka.
10Na divinin kontra O Del sar divinisarde won, ai mule anda lende but.
10Wala msinung'unike kama baadhi yao walivyonung'unika, wakaangamizwa na Mwangamizi!
11Kodola dieluria kerdile lenge kaste te podain amenge: ai ramome le kaste te sicharen amen, ame kai sam aresliam kai getolpe e lumia,
11Basi, mambo hayo yaliyowapata wao ni kielelezo kwa wengine, na yaliandikwa ili kutuonya sisi, ambao mwisho wa nyakati unatukabili.
12anda kodia kodo kai gindilpe ande punrhende te arakhelpe te na perel.
12Anayedhani amesimama imara ajihadhari asianguke.
13Chi iek zumaimos chi kerdiol tumenge te na sai rhevdila: numa O Del kai si chacho, chi mekel te aven zumade mai but sar sode si e zor, numa kana kerdilia amenge vari so, wo lasharel le dieluria te anklia avri anda kodo nasulimos, kashte te sai rhevdisaras les.
13Majaribu mliyokwisha pata ni ya kawaida kwa binadamu. Mungu ni mwaminifu, naye hataruhusu mjaribiwe kupita nguvu zenu, ila pamoja na majaribu, yeye atawapeni pia nguvu ya kustahimili na njia ya kutoka humo salama.
14Anda kodia murhe drazhe, nashen katar le dela chorhe.
14Kwa hiyo, wapenzi wangu, epeni ibada za sanamu.
15Dav duma sar le manushensa le gojavrensa; keren tume kris so phenav.
15Naongea nanyi, watu wenye busara; jiamulieni wenyewe hayo nisemayo.
16Kana das o rhugimos pala o daxtai ai piias e mol kai skafidi le Devleski, nai kodia o rat le Kristosko? O manrho kai xas kai skafidi le Devleski nai kodia andek than ando stato le Kristosko?
16Tunapomshukuru Mungu kwa kikombe kile cha baraka, je, huwa hatushiriki damu ya Kristo? Na tunapoumega mkate, je, huwa hatushiriki mwili wa Kristo?
17Ke si iek manrho ame kai sam but, kerdilia iek stato lestar: ke keras kodia diela ieke manrhesa.
17Kwa kuwa mkate huo ni mmoja, sisi, ingawa ni wengi, tu mwili mmoja; maana sote twashiriki mkate huohuo.
18Dikhen le Zhiduvuria kodola kai xan le masa le zhigeni kai mudaren le, vov si andek than le altariosa.
18Chukueni, kwa mfano, Wayahudi wenyewe: kwao, wenye kula vilivyotambikiwa madhabahuni waliungana na hiyo madhabahu.
19So phenav? Ke kodola masa kai shinavel le le devlenge si vari so, vai ke kokola dela lenge si vari so?
19Nataka kusema nini, basi? Kwamba chakula kilichotambikiwa sanamu ni kitu zaidi ya chakula? Na hizo sanamu, je, ni kitu kweli zaidi ya sanamu?
20Kanchi nai. Phenav ka kodo kai shinavel les, na le devlenge numa le bengeske, me chi mangav te aven andek than le bengensa.
20Hata kidogo! Ninachosema ni kwamba tambiko wanazotoa watu wasiomjua Mungu wanawatolea pepo, sio Mungu. Sipendi kamwe ninyi muwe na ushirika na pepo.
21Nashti pen anda daxtai le Devlesko, ai anda daxtai le bengenge: nashti zhan kai skafidi le Devleski, ai kai skafidi le bengenge.
21Hamwezi kunywa kikombe cha Bwana na kikombe cha pepo; hamwezi kushiriki katika meza ya Bwana na katika meza ya pepo.
22Manges te xoliaras le Devles? Sam ame mai zurales lestar?
22Au je, tunataka kumfanya Bwana awe na wivu? Mnadhani tuna nguvu zaidi kuliko yeye?
23Swako fielo slobodo mange, numa swako fielo chi trobul; swako fielo slobodo, numa swako fielo chi maladiol le manushes.
23Vitu vyote ni halali, lakini si vyote vinafaa. Vitu vyote ni halali lakini si vyote vinajenga.
24Porme te na rodel peske mishtimos korkorho, numa savorhe te roden kodo le kavrenge.
24Mtu asitafute faida yake mwenyewe, ila faida ya mwenzake.
25Xan swako fielo, so godi bichindiol po bazari, bi te phushen so si katar avel.
25Kuleni chochote kile kiuzwacho sokoni bila ya kuulizauliza kwa sababu ya dhamiri zenu;
26Ke e phuv si le Devleski, ai so godi si pe late.
26maana Maandiko yasema: "Dunia na vyote vilivyomo ni mali ya Bwana."
27Te si vari kon kai chi pachalpe ai akharel tume, ai te mangena te xan. Xan so godi anena tume, bi te phushen te dar si vari so kai chi trobul.
27Kama mtu ambaye si muumini akiwaalikeni nanyi mkakubali kwenda, basi, kuleni vyote atakavyowaandalieni bila kuulizauliza kwa sababu ya dhamiri zenu.
28Numa te phenela tumenge vari kon, kako sas shinado andal le devlenge, na xan, na anda kodo kai shinadia les, ke e phuv si le Devleski, ai so godi si pe phuv.
28Lakini mtu akiwaambieni: "Chakula hiki kimetambikiwa sanamu," basi, kwa ajili ya huyo aliyewaambieni hivyo na kwa ajili ya dhamiri, msile.
29Kai del duma, na anda tumende, numa anda kodo kai phenel: ande soste keren kris pe murhi ivia anda aver vari kon?
29Nasema, "kwa ajili ya dhamiri," si dhamiri yenu, bali dhamiri yake huyo aliyewaambieni. Mtaniuliza: "Kwa nini uhuru wangu utegemee dhamiri ya mtu mwingine?
30Te xala ai naisiv le Devleske, sostar lav sama?
30Ikiwa mimi nashiriki chakula hicho huku namshukuru Mungu, kwa nini nilaumiwe kwa chakula ambacho kwa ajili yake nimemshukuru Mungu?"
31Vai xana, vai pena, so godi keren, keren les te bariaren o anav le Devlesko.
31Basi, chochote mfanyacho iwe ni kula au kunywa, fanyeni yote kwa ajili ya utukufu wa Mungu.
32Numa na len vorbi kai nai lashe, chi le Grekonge, chi le Zhidovonge, vai chi la khangeriake le Devleski.
32Msiwe kikwazo kwa Wayahudi au kwa Wagiriki au kwa kanisa la Mungu.
33Sar kai chi sim me, mangav te kerav so godi vorta, chi rodav so si mange mishto, numa so si o mishtimos savorhen.
33Muwe kama mimi; najaribu kuwapendeza wote kwa kila njia, bila kutafuta faida yangu mwenyewe ila faida ya wote, wapate kuokolewa.