1Le tu pala e dragostia, ai roden le podarki le Devleske, mai but kucha le profesia, chaches.
1Jitahidini kuwa na upendo. Vilevile fanyeni bidii ya kupata vipaji vingine vya kiroho, hasa kipaji cha kutangaza ujumbe wa Mungu.
2Kodo kai del duma pel shiba chi del duma le manushensa, numa le Devlesa; ke khonik chi haliarel leske; ai ando duxo phenel shodenia.
2Mwenye kunena lugha ngeni hasemi na watu bali anasema na Mungu. Yeye hunena kwa nguvu ya Roho mambo yaliyofichika.
3Kodo kai del profesia aver fial del duma le manushensa, zuralel le, zhutil le, pechil le.
3Lakini mwenye kipaji cha kutangaza ujumbe wa Mungu, husema na watu kwa ajili ya kuwajenga, kuwafariji na kuwatia moyo.
4Kodo kai del duma pel shiba vazdel pek korkorho, kodo kai profetil vazdel e khangeri.
4Mwenye kunena lugha ngeni anajijenga mwenyewe. Lakini mwenye kipaji cha kutangaza ujumbe wa Mungu, analijenga kanisa.
5Mangav te den duma savorhe pel shiba, numa mai but te profetis, kodo kai profetil mai baro lo sar kodo kai del duma pel shiba. De ferdi kodo vi te haliarela le shiba. Kashte te vazdel e khangeri.
5Basi, ningependa ninyi nyote mseme kwa lugha ngeni lakini ningependelea hasa muwe na kipaji cha kutangaza ujumbe wa Mungu, maana mtu mwenye kipaji cha kutangaza ujumbe wa Mungu, ni wa maana zaidi kuliko yule mwenye kusema lugha ngeni, isipokuwa tu kama yupo hapo mtu awezaye kuyafafanua hayo mambo asemayo, ili kanisa lipate kujengwa.
6Akana, phrala le, che mishtimos kerava tumenge te avavas tumende te dav duma pel shiba, ai te na dav duma katar O Del, vai pa zhanglimos, vai pa profesia, vai pai zakono.
6Hivyo, ndugu zangu, kama nikija kwenu na kusema nanyi kwa lugha ngeni itawafaa nini? Haitawafaa chochote, isipokuwa tu kama nitawaelezeni ufunuo wa Mungu au ujuzi fulani au ujumbe wa Mungu au mafundisho fulani.
7Le dieluria kai chi mishkin, ai kai bashen sar iek fishtoko vai iek tsitura, chi bashen but fialuri, sar haliarasa so diilaben po flishtoko vai pe tsitura?
7Ndivyo ilivyo kwa vyombo visivyo na uhai vyenye kutoa sauti kama vile filimbi au kinanda. Je, mtu anawezaje kuutambua wimbo unaochezwa kama vyombo hivyo havitoi sauti waziwazi vinapopigwa?
8Ai e tutraza te bashela bi goresko, kon lashardiol po marimos?
8La mgambo likilia bila kufuata taratibu zake, nani atajiweka tayari kwa vita?
9Vi tume, iek fialo la shibasa te na den iek vorba vorta sar zhangliape, so phenen? Dena duma pe barval.
9Hali kadhalika na ninyi, kama ulimi wenu hausemi kitu chenye kueleweka, nani ataweza kufahamu mnayosema? Maneno yenu yatapotea hewani.
10Makar ke but shiba si ande lumia, chi iek nai te na avel iek shib.
10Zipo lugha mbalimbali ulimwenguni, na hakuna hata mojawapo isiyo na maana.
11No te na haliarava kodia shib, sim iek sirbatiko kodo leske kai del duma, ai kodo kai del duma si mange sirbatiko.
11Lakini ikiwa mimi sifahamu maana ya lugha asemayo mtu fulani, mimi ni mgeni kwake mtu huyo naye pia ni mgeni kwangu.
12Saikfialo tume, roden le podarki le Devleske te vazden e khangeri.
12Hali kadhalika na ninyi, maadam mna hamu ya kupata vipaji vya Roho, jitahidini hasa kujipatia vile vinavyosaidia kulijenga kanisa.
13Kodo kai del duma pa shiba, rhugilpe te mothol so phendia.
13Kwa hiyo, mwenye kunena lugha ngeni na aombe apate uwezo wa kuzifafanua.
14Te rhugiva ma pel shiba, murho duxo rhugilpe, numa murhi goji chi kerel kanchi.
14Maana, nikisali kwa lugha ngeni roho yangu ndiyo inayosali, lakini akili yangu hubaki bure.
15So te kerav? Rhugiv ma le duxosa, ai rhugiv ma vi la gojako, jilabav le duxosa, ai jilabav vi la gojasa.
15Nifanye nini, basi? Nitasali kwa roho yangu, nitasali pia kwa akili yangu; nitaimba kwa roho yangu, nitaimba pia kwa akili yangu.
16Te na nichi, te naisisaras le Devles, pa le duxosa sar phenela o manush and narodo, Amen, kai naisardia, ke chi zhanel so phenes?
16Ukimsifu Mungu kwa roho yako tu, atawezaje mtu wa kawaida aliye katika mkutano kuitikia sala yako ya shukrani kwa kusema: "Amina," kama haelewi unachosema?
17Chaches mishto naisis, numa kaver nai vazdino.
17Sala yako ya shukrani yaweza kweli kuwa bora, lakini huyo mwingine haitamfaidia.
18Naisiv le Devleske, ke dav duma pel shiba mai but sar tume savorhe.
18Namshukuru Mungu kwamba mimi nasema kwa lugha ngeni zaidi kuliko ninyi nyote.
19Numa ande khangeri mai drago mange te phenav panzh vorbi murhe gojasa, kashte te sicharav vi le kavren, de sar desh mi vorbi pel shiba.
19Lakini katika mikutano ya waumini napendelea zaidi kusema maneno matano yenye kueleweka ili niwafundishe wengine, kuliko kusema maneno elfu ya lugha ngeni.
20Phrala le, te na aven shavorhe po haliarimos, aven manush numa keren sar le shavorhe kai chi zhanen sar te keren bezex.
20Ndugu, msiwe kama watoto katika fikira zenu. Kuhusu uovu muwe kama watoto wachanga lakini katika kufikiri ni lazima muwe kama watu waliokomaa.
21Ramome ande zakono, katar manush avre shibake ai andal mursh streino dava duma kadale narodos, ai chi kadia chi ashunena mande, phenel O Del.
21Imeandikwa katika Sheria: "Bwana asema hivi: Kwa njia ya wenye kunena lugha ngeni, na kwa midomo ya wageni, nitasema na watu hawa, hata hivyo, hawatanisikiliza."
22Anda kadia le shiba si semno, na kodolenge kai pachanpe, numa kodolenge kai chi pachanpe. E profesia aver fialo semno si, na kodolenge kai chi pachanpe, numa kodolenge ka pachanpe.
22Hivyo basi, kipaji cha kusema lugha ngeni ni ishara, si kwa ajili ya watu wenye imani, bali kwa ajili ya wale wasioamini; lakini kipaji cha kutangaza ujumbe wa Mungu ni kwa ajili ya wale wanaoamini na si kwa ajili ya wasioamini.
23Te ande khangeri kana si chidine savorhe, den duma pel shiba, ai te avena manush anda narodo, vai kai chi pachanpe, chi phenena ke dile san?
23Basi, kanisa lote linapokutana pamoja, na wote wakaanza kusema kwa lugha ngeni, kama wakija watu wa kawaida au wasioamini, je, hawatasema kwamba ninyi mna wazimu?
24Numa savorhe te profetina, ai te avela iek manush kai chi pachanpe, vai iek manush anda narodo, savorhe keren les te haliarel, ai savorhe keren kris pe leste.
24Lakini, wote wakiwa wanautangaza ujumbe wa Mungu, akija mtu wa kawaida au asiyeamini, yote atakayosikia yatamhakikishia ubaya wake mwenyewe; yote atakayosikia yatamhukumu.
25O garaimata anda lesko ilo sikadiol, kadia ke perela tele mosa te rhugilape ka Del, ai vestila ke O Del chaches mashkar tumende lo.
25Siri za moyo wake zitafichuliwa, naye atapiga magoti na kumwabudu Mungu akisema: "Kweli Mungu yupo pamoja nanyi."
26So te keras phralen? Kana chiden tume, iek vai avres si tume iek kantik, vai iek sicharimos, vai iek sikaimos, iek shib, iek parhuimos te kerdiol sa po vazdimos.
26Ndugu, tuseme nini, basi? Mnapokutana pamoja, mmoja aimbe wimbo, mwingine atoe mafundisho, mwingine awe na ufunuo kutoka kwa Mungu, mwingine atumie kipaji cha kusema kwa lugha ngeni na mwingine afafanue yanayosemwa. Yote yawe kwa ajili ya kulijenga kanisa.
27Si kai den duma pa shib, dui vai trin, vai mai but den duma swako te pesko rhindo, vai vari kon te parhuvel.
27Wakiwepo watu wenye vipaji vya kusema kwa lugha ngeni, waseme wawili au watatu, si zaidi, tena mmojammoja; na aweko mtu wa kufafanua yanayosemwa.
28Te na avela vari kon kai parhuvel, te na den duma ande khangeri, ai swako te del duma pe sa, ai le Devles.
28Lakini kama hakuna awezaye kufafanua, basi, mwenye kusema lugha ngeni anyamaze mkutanoni, aseme na nafsi yake mwenyewe na Mungu.
29Andal profeturia dui vai trin te den duma, ai kaver te keren kris.
29Kuhusu wale wenye kipaji cha kutangaza ujumbe wa Mungu, waseme wawili au watatu, na wengine wayapime maneno yao.
30Te avres kai beshel tele avel sikaimos, o pervo te na mai del duma.
30Ikiwa mmoja anaposema mwingine wa wasikilizaji amepata ufunuo kutoka kwa Mungu, basi, yule anayesema anyamaze.
31Ke savorhe sai profetin pala iek kavreske, kashte te aven sicharde. Ai savorhe te aven raduime.
31Maana nyote mwaweza kutangaza ujumbe wa Mungu, mmoja baada ya mwingine, ili nyote mpate kujifunza na kutiwa moyo.
32O duxo le profetongo ninkeren le profeturia.
32Kipaji cha kutangaza ujumbe wa Mungu ni lazima kitawaliwe na huyo mwenye hicho kipaji.
33Ke O Del nai iek Del bi gorasko, numa pacha, sar ande sa le khangeria le Swuntonge.
33Maana Mungu si Mungu wa fujo, ila wa amani.
34Le zhuvlia te na den duma kana si chidine ande khangeri, ke nai lenge slobodo te den duma, o zakono Zhidovisko phenel kodia.
34Kama ilivyo desturi katika makanisa yote ya watu wa Mungu, wanawake wakae kimya katika mikutano ya waumini. Hawana ruhusa kusema; ila wawe watii kama isemavyo Sheria.
35Te mangena te sichon pe vari soste te beshen penge rhomen khere. Ke zhungales ieka zhuvliake te del duma ande khangeri.
35Ikiwa wanayo maswali ya kuuliza, wawaulize waume zao nyumbani, maana ni aibu kwa mwanamke kusema katika mikutano ya waumini.
36Tumendar ankliste le Vorba le Devleski vai ferdi tumende avili?
36Je, mnadhani neno la Mungu limetoka kwenu ninyi au kwamba limewajieni ninyi peke yenu?
37Te gindilpe vari kon profeto, vai ke zhanel te dikhel, ke so ramov tumenge, zakono si katar O Del.
37Kama mtu yeyote anadhani kwamba yeye ni mjumbe wa Mungu au kwamba anacho kipaji cha Roho, na ajue kwamba haya ninayowaandikia ninyi ni amri ya Bwana.
38Ai te na zhanel vari kon, mek te na zhanel.
38Lakini mtu asiyetambua hayo, basi, mtu asimjali mtu huyo.
39Kadia, phrala le, roden e podarka le profesiaki, ai chi aterdion le te den duma pel shiba.
39Hivyo basi, ndugu zangu, mnapaswa kuwa na hamu ya kutangaza ujumbe wa Mungu; lakini msimkataze mtu kusema kwa lugha ngeni.
40Numa swako fialo te kerdiol mishto ai vorta.
40Lakini yote yafanyike kwa heshima na kwa utaratibu.