Romani: New Testament

Swahili: New Testament

1 Corinthians

15

1Dav tume goji phrale, mangav te phenav tumenge e lashi viasta mai iek data sar phendem tumenge mai anglal, tume lian les, ai cho pachamos zuriarde.
1Sasa ndugu, napenda kuwakumbusha ile Habari Njema niliyowahubirieni nanyi mkaipokea na kusimama imara ndani yake.
2Ai pa kodo san skepime, te ninkerena les sar phendem les tumenge.
2Kwa njia yake mnaokolewa, ikiwa mnayazingatia maneno niliyowahubirieni, na kama kuamini kwenu hakukuwa bure.
3Sichardem tume mai anglal sa sar vi me sichilem, ke O Kristo mulo anda amare bezexa. Sar phenel o ramomos.
3Mimi niliwakabidhi ninyi mambo muhimu sana ambayo mimi niliyapokea: kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu kufuatana na Maandiko Matakatifu;
4Ke sas gropome, ai zhuvindisailo o trito dies sar phenel o ramomos.
4kwamba alizikwa, akafufuka siku ya tatu kama ilivyoandikwa;
5Ai ke sikadilo ka Cephas, porme le desh u donge.
5kwamba alimtokea Kefa, na baadaye aliwatokea wale kumi na wawili.
6Porme sikadilo mai but de pansh shela phralen iek data, ai mai but anda lende inker zhuvinde le, ai uni mule.
6Kisha aliwatokea ndugu zaidi ya mia tano kwa mara moja; wengi wao wanaishi bado, lakini baadhi yao wamekwisha kufa.
7Porme sikadilo ka Iakov, ai sa le apostluria.
7Baadaye alimtokea Yakobo kisha akawatokea mitume wote.
8Pala lende savorhe vi mange sikadilo, sar le bi vriamako.
8Baada ya wote, akanitokea hata mimi, mimi niliyekuwa kama mtu aliyezaliwa kabla ya wakati.
9Ke sim o mai tsigno andal apostluria, chi trobul te akharen ma apostle, ke chinuisardem e khangeri le Devleski.
9Maana mimi ni mdogo kabisa miongoni mwa mitume na wala sistahili kuitwa mtume, kwa sababu nililidhulumu kanisa la Mungu.
10Katar o mishtimos le Devlesko sim so sim: ai o mishtimos le Devlesko karing mande nas intaino, dur kotsar, kerdem mai but buchi lendar savorhe, na me, numa o mishtimos le Devlesko kai si mansa.
10Lakini, kwa neema yake Mungu, nimekuwa kama nilivyo. Na neema yake kwangu haikuwa bure. Mimi nimefanya kazi kuliko wote; si mimi hasa, ila ni neema ya Mungu ifanyayo kazi pamoja nami.
11No kadia te avela me vai te aven won, eta, so das duma pa Del, ai pachaie tume.
11Lakini hata hivyo, iwe wao ndio wahubirio au mimi nihubiriye, haidhuru, hiki ndicho tunachuhubiri, na hiki ndicho mnachoamini.
12Fin phenas ke Kristo zhuvindisailo andal mulen. Sar uni anda tumende phenen ke nai zhuvindimos le mulen?
12Sasa, maadam inahubiriwa kwamba Kristo amefufuliwa kutoka wafu, baadhi yenu wanawezaje kusema kwamba hakuna ufufuo wa wafu?
13Te na avela zhuvindimos le mulengo, chi O Kristo chi zhuvindisailo.
13Kama hakuna ufufuo wa wafu, basi, Kristo naye hakufufuka;
14Ai te Kristo nai zhuvindime, amaro divano antunchi intaino, ai vi tumaro pachamos intaino le.
14na kama Kristo hakufufuka, basi mahubiri yetu hayana maana na imani yenu haina maana.
15Antunchi vi sam xoxamne marturia ke phendiam ke O Del zhuvindisardia le Kristos: numa O Del chi zhuvindisardia les anda le mule te na wushten le mule andai martia.
15Zaidi ya hayo sisi tungekuwa mashahidi wa uongo mbele ya Mungu, maana tulisema kwamba Mungu alimfufua Kristo kutoka wafu na kumbe yeye hakumfufua--kama ni kweli kwamba wafu hawafufuliwi.
16Te na zhuvindila le mule chi O Kristo nai zhuvindime.
16Maana, ikiwa ni kweli kwamba wafu hawafufuki, basi naye Kristo hakufufuka.
17Ai te O Kristo nai zhuvindime, tumaro pachamos intainalo, inker san ande tumare bezex.
17Na kama Kristo hakufufuliwa, basi, imani yenu ni ya bure; mngali bado katika dhambi zenu.
18Ai vi kodola kai mule ando Kristo, xasarde le.
18Zaidi ya hayo, wale wote waliokufa wakiwa wameungana na Kristo wamepotea kabisa.
19Te si ferdi ande kado traio ke jinas po Kristo, sam le mai nekezhime andal sa manush.
19Kama matumaini yetu katika Kristo yanahusu tu maisha haya ya sasa, basi, sisi ni watu wa kusikitikiwa zaidi kuliko wengine wote duniani.
20Numa akana O Kristo zhuvindime lo andal mule, ai angluno lo anda kodola kai mule.
20Lakini ukweli ni kwamba Kristo amefufuliwa kutoka wafu, limbuko lao wale waliolala katika kifo.
21Ke te avili e martia katar iek manush, vi katar iek manush avilo o zhuvindimos le mulenge.
21Maana kama vile kifo kilivyoletwa duniani na mtu mmoja, vivyo hivyo nako kufufuka kutoka wafu kumesababishwa na mtu mmoja.
22Ai sar savorhe meren ando Adam, savorhe zhuvindina ando Kristo.
22Kama vile watu wote wanavyokufa kwa kujiunga na Adamu, vivyo hivyo wote watafufuliwa kwa kuungana na Kristo.
23Numa swako pe pesko rhindo, O Kristo sar le anglune, porme kodola kai si le Kristoske kana avela, porme avela o getomos.
23Lakini kila mmoja kwa mpango wake: Kristo kwanza, halafu wale walio wake Kristo wakati Kristo atakapokuja.
24Kana dela amperetsia ka kado kai si Del, ai Dat; pala kodia kai peravela swako barimos, swako poronchimos ai swako zor.
24Baada ya hayo, mwisho utafika wakati ambapo Kristo atamkabidhi Mungu Baba Utawala, baada ya kufutilia mbali kila tawala na mamlaka na nguvu.
25Ke trobul te poronchil, zhi kai thola sa le duzhmanon telai leske punrhe.
25Maana Kristo sharti atawale mpaka Mungu atakapowashinda adui zake na kuwaweka chini ya miguu yake.
26O paluno duzhmano kai avela perado si e martia.
26Adui wa mwisho atakayeangamizwa ni kifo.
27O Del chaches sa thodia tela leske punrhe. Numa kana phenel, ke swako fialo si tela leste, chaches ke kodo kai thodiape pala leste swako fialo wo nai.
27Maana, Maandiko yasema: "Mungu ameweka vitu vyote chini ya miguu yake." Lakini, Maandiko yanaposema: "Vitu vyote vimewekwa chini ya miguu yake avitawale" ni dhahiri kwamba Mungu haingii katika kundi hilo la vitu, maana yeye ndiye anayeviweka vitu hivyo chini ya Kristo.
28Ai kana swako fialo avena tela leste, porme O Shav vi wo avela tela kodo kai thodai tela leste, kashte te avel O Del sa ando swako fialo.
28Lakini vitu vyote vitakapowekwa chini ya Utawala wa Kristo, ndipo naye Mwana atakapojiweka chini ya Mungu, aliyeweka vyote chini ya Utawala wake; ili Mungu atawale juu ya vyote.
29Te na, nichi, so keren kodola ke bolenpe le mulenge, te na zhuvindila vov si le mule? Sostar bolenpe anda lende?
29Kama hakuna ufufuo, je watu wale wanaobatizwa kwa ajili ya wafu wanatumainia kupata nini? Kama wafu hawafufuliwi, ya nini kubatizwa kwa ajili yao?
30Ai ame sostar sam swako chaso ande dar?
30Na sisi, ya nini kujitia hatarini kila saa?
31Ke swako dies sai merav, phenav phrala le pala putiera ke sam mange ando Jesus Kristo amaro Del.
31Ndugu, mimi nakikabili kifo kila siku! Fahari niliyo nayo juu yenu katika kuungana na Kristo Yesu Bwana wetu inanifanya nitangaze jambo hili.
32Te si sar manushenge dikhimos ke marde ma le zhigeniensa ando Ephesus, che mishtimos lav anda kodia, te na zhuvindin le mulen? Xas, piias, ke terhara meras.
32Kama kusudi langu lingalikuwa la kibinadamu tu, kule kupigana kwangu na wanyama wakali hapa Efeso kungalinifaa kitu gani? Kama wafu hawafufuki, basi, "Tule na tunywe, maana kesho tutakufa."
33Na shubin tume, le chorhe ginduria rimon vi lasho zakono.
33Msidanganyike! Urafiki mbaya huharibu tabia njema.
34Ambolden palpale tumende so si mishto, ai na keren bezex, ke uni chi zhanen le Devles: phenav tumaro lazhav.
34Amkeni! Anzeni kuishi vema, na acheni kutenda dhambi. Baadhi yenu hawamjui Mungu kabisa. Hii nawaambieni, ni aibu kubwa kwenu!
35No vari kon phenela, sar le mule zhuvindin? Ai che statosa ambolden?
35Lakini mtu anaweza kuuliza: "Wafu watafufuliwaje? Watakuwa na mwili wa namna gani wakati watakapokuja tena?"
36Dilia, e sumuntsa kai thos chi zhuvindil, te na merel.
36Hayo ni maswali ya kijinga! Ukipanda mbegu, isipokufa kwanza haitaota.
37Soste bariol, nai o stato kai bariol, ferdi iek sumuntsa jiveske amborim, vai aver sumuntsa.
37Unachopanda ni mbegu tu, labda ya ngano au nafaka nyingine, na si mmea mzima ambao hutokea baadaye.
38Porme O Del del les iek stato sar mangel, ai swako sumuntsa del iek stato kai si leske.
38Mungu huipa hiyo mbegu mwili anaoutaka mwenyewe; kila mbegu hupata mwili wake wa pekee.
39Swako mas nai iek mas, numa aver si o mas le manushenge, aver si le shtare punrhenge, aver le chirikliange, aver le masenge.
39Miili ya viumbe vyote si sawa. Miili ya binadamu ni ya namna moja, ya wanyama ni ya namna nyingine, ya ndege ni ya namna nyingine na miili ya samaki pia ni ya namna nyingine.
40Si vi staturia chereske, ai staturia phuviake: numa aver si o strefiamos le staturia le chereske, aver si le staturia la phuviake.
40Iko miili ya mbinguni na miili ya duniani; uzuri wa miili ya mbinguni ni mwingine, na na uzuri wa miili ya duniani ni mwingine.
41Aver si o strefiamos la khamesko, aver si o strefiamos le shunutosko, ai aver si o strefiamos le cherhaiengo. Iek chererhai strefial aver fialo katar aver chererhai.
41Uko uzuri wa jua, wa mwezi na wa nyota; hata nyota nazo huhitilafiana kwa uzuri.
42Kadia si anda zhuvindimos le mulenge, o stato bariardo kai rimolpe, zhuvindil kai chi mai rimol.
42Ndivyo ilivyo kuhusu ufufuo wa wafu. Kama vile mbegu, mwili huzikwa ardhini ukiwa katika hali ya kuharibika, lakini hufufuliwa katika hali ya kutoharibika.
43Bariol gratsia, zhuvindil vuzho: bariol kovlo, zhuvindil pherdo zor.
43Huzikwa katika hali duni, hufufuliwa katika hali tukufu; huzikwa katika hali dhaifu, hufufuliwa ukiwa wenye nguvu.
44Bariol zhigania, zhuvindil swuntsome stato. Si iek stato zhigania, si vi iek stato swuntso.
44Unapozikwa ni mwili wa kawaida, unapofufuliwa ni mwili wa kiroho. Kuna mwili wa kawaida na kutakuwa na mwili wa kiroho.
45Anda kodia ramome, si o angluno manush Adam kerdilo stato zhuvindo, o paluno Adam kerdilo iek duxo kai zhuvindil.
45Maana Maandiko yasema: "Mtu wa kwanza, Adamu, alikuwa kiumbe mwenye uhai;" lakini adamu wa mwisho ni Roho awapaye watu uzima.
46Numa so si swunto nai o angluno so si zhigania, ai so si swunto avela mai palal.
46Lakini unaotangulia kuwako si ule mwili wa kiroho, ila ule mwili wa kawaida kisha ule mwili wa kiroho.
47O angluno manush ankalado andai phuv, phuviako lo, o duito manush si andai rhaio.
47Adamu wa kwanza aliumbwa kwa udongo, alitoka ardhini; mtu wa pili alitoka mbinguni.
48Kadia si la phuviako, kadia si vi le phuviako, ai kadia si le cheresko.
48Wote walio wa dunia wako kama huyo mtu aliyeumbwa kwa udongo; wale walio wa mbinguni wako kama yule aliyetoka mbinguni.
49Ai sar savorhe ningerdiam o patreto la phuviakoresko, vi kadia ningerasa le cheresko.
49Kama vile tulivyofanana na yule aliyeumbwa kwa udongo, vivyo hivyo tutafanana na huyohuyo aliyetoka mbinguni.
50So phenav, phrala le, ke o mas ai o rat nashtil len o rhaio le Devlesko, ai ke o rimome nashti lel kai chi mai rimolpe.
50Basi, ndugu, nasema hivi: kile kilichofanywa kwa mwili na damu hakiwezi kuushiriki Ufalme wa Mungu; na chenye kuharibika hakiwezi kuwa na hali ya kutoharibika.
51Eta, phenav tumenge iek shodenia, chi meras sa, numa savorhe parhuenas sa.
51Sikilizeni, nawaambieni siri: sisi hatutakufa sote, ila sote tutageuzwa
52Ande ek tsikon (momento), ai ande dikhimos iakhako, kai palui tuturaza, ke e tuturaza bashela ai le mule zhuvindila, ke chi mai rimonpe ai ame savorhe avasa parhuenasa.
52wakati wa mbiu ya mwisho, kwa nukta moja, kufumba na kufumbua. Maana mbiu itakapolia, wafu watafufuliwa katika hali ya kutoweza kufa tena, na sisi tutageuzwa.
53Ke trobul kado stato kai rimolpe te vuriarelpe so chi mai rimolpe, ai kado stato kai merel lelpe peste kai chi mai merel.
53Maana ni lazima kila kiharibikacho kijivalie hali ya kutoharibika, mwili uwezao kufa ujivalie hali ya kutokufa.
54Kana kado stato kai rimolpe vuriarelpe kai chi mai rimolpe, ai kado stato kai merel kana vuriarelape kai chi mai merel, antunchi kerdiol e vorba kai si ramome.
54Basi, mwili huu wenye kuharibika utakapojivalia hali ya kutoharibika, na kile chenye kufa kitakapojivalia hali ya kutokufa, hapo ndipo litakapotimia lile neno lililoandikwa: "Kifo kimeangamizwa ushindi umekamilika!"
55E martia sas tasadi ando nirimos. Martio, kai cho nirimos? Martio, kai chi kanrho?
55"Kifo, ushindi wako uko wapi? Uwezo wako wa kuumiza uko wapi?"
56O kanrho la martiako si o bezex, ai e zor le bezexesko si o zakono.
56Ukali wa kifo hutokana na dhambi, nayo dhambi hupata nguvu yake katika Sheria.
57Numa nais le Devleske kai dia ame o nirimos katar amaro Del, O Jesus Kristo.
57Lakini tumshukuru Mungu anayetupatia ushindi kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.
58Kadia, murhe drazhe phral, aven zurale, na parhudion, keren buchi mai mishto, ai mai mishto ande diela le Devleske, te zhanen ke tumari buchi chi avela intaino ando Del.
58Basi, ndugu zangu wapenzi, simameni imara na thabiti. Endeleeni daima kuwa na bidii katika kazi ya Bwana, mkijua kwamba kazi mnayofanya katika utumishi wa Bwana haitapotea bure.