Romani: New Testament

Swahili: New Testament

2 Corinthians

4

1O Del ande pesko lashimos, dia ame kadia buchi, ai anda kodia chi xasaras zor.
1Basi, Mungu, kwa huruma yake, ametukabidhi kazi hii na hivyo hatufi moyo.
2Shudiam le dieli le chorhe kai kerdionas chordanes, ai chi keras buchi bi malades, ai chi parhuvas E Vorba le Devleski. Numa phenas o chachimos, ai ame tasame angla sako manush te dikhen amaro traio kai thodiam angla Del.
2Tumeyaacha kabisa mambo yote ya aibu na ya kisirisiri. Hatuishi tena kwa udanganyifu, wala kwa kulipotosha neno la Mungu; bali tunaudhihirisha ukweli kwa kuufanya ukweli, na hivyo kujiweka chini ya uamuzi wa dhamiri za watu mbele ya Mungu.
3Numa te si e lashi viasta kai phenas garadi, garadi la ferdi kodolenge kai xzasavon.
3Maana, kama Habari Njema tunayohubiri imefichika, imefichika tu kwa wale wanaopotea.
4Chi pachanpe ke O Del o nasul kadala lumiako korhardia lenge goji, kodo del (o beng) chi mekel le te dikhen e vediara kai si andini katar e lashi viasta le Kristosko kai phenel pa lesko barimos, wo si o patreto le Devlesko.
4Hao hawaamini kwa sababu yule mungu wa ulimwengu huu amezitia giza akili zao wasipate kuuona wazi mwanga wa Habari Njema ya utukufu wa Kristo, ambaye ni mfano kamili wa Mungu.
5Ke chi das duma pa amende; numa das duma pa Jesus Kristo le Devles; ai ame jinas ame sar tumare slugi pala Kristo.
5Maana hatujitangazi sisi wenyewe, ila tunamhubiri Yesu Kristo aliye Bwana, sisi wenyewe tukiwa watumishi wenu kwa ajili ya Yesu.
6O Del kai phendia, "Te strefial e vediara mashkar o tuniariko," ai vi kado si, kai kerdia te strefial peski vediara ande amare ile, te zhanas e vediara kai si o barimos le Devlesko, kai strefial po mui le Jesus Kristosko.
6Mungu ambaye alisema, "Mwanga na uangaze kutoka gizani," ndiye mwenye kuiangaza mioyo yetu, na kutupatia mwanga wa ujuzi wa utukufu wa Mungu uangazao katika uso wa Kristo.
7Numa ame kai ingeras kodo barvalimos le Devlesko, sam sar kanta chikaki, te sai dichol mishto ke kodia putiera e bari si le Devleski, ai na amari.
7Basi, sisi tulio na hazina hii tuko tu kama vyombo vya udongo, ili ionekane wazi kwamba nguvu hiyo kuu yatoka kwa Mungu wala si kwetu sisi wenyewe.
8But chinuimata si pe amende, numa chi sam licharde; nekezhisaras, numa chi rimovsavas;
8Daima twapata taabu, lakini hatugandamizwi; twapata mashaka, lakini hatukati tamaa;
9Chinuin ame, numa O Del chi mekel ame, shudiam tele, numa na xasarde.
9twateseka, lakini hatuachwi bila msaada; na ingawa tumeangushwa chini, hatukuangamizwa.
10Si ame sagda ande amaro stato e martia le Jesus Kristoski, saxke te sikadiol lesko traio ande amaro stato.
10Kila wakati tumekuwa tukichukua mwilini mwetu kifo cha Kristo, ili uhai wake Yesu pia udhihirike katika miili yetu.
11Ande amaro traio sagda sam angla e martia pala Kristo, saxke lesko traio te sikadiol ande amaro stato kai merel.
11Naam, katika maisha yetu yote tunakabiliwa na kifo daima kwa ajili ya Yesu, ili uzima wake Yesu udhihirike katika miili yetu inayokufa.
12E martia kerel buchi ande amende; numa o traio kerel buchi ande tumende.
12Hii ina maana kwamba ndani yetu kifo kinafanya kazi, lakini ndani yenu uhai unafanya kazi.
13E Vorba le Devleski mothol, "Pachaie ma, anda kodia dem duma." Vi ame ande sa kodo duxo pachamasko pachas ame, ai anda kodo das duma.
13Maandiko Matakatifu yasema: "Niliamini, ndiyo maana nilinena." Nasi pia, tukiwa na moyo huohuo wa imani, tunaamini, na kwa sababu hiyo twanena.
14Zhanas ke O Del, kai andia le Devles O Jesus katar e martia ka traio, anela iamen ka traio le Kristosa, ai kerela ame te sikadiuas tumensa angla leste.
14Tunajua kwamba yule aliyemfufua Bwana Yesu atatufufua sisi pia pamoja na Yesu na kutuweka mbele yake pamoja nanyi.
15Sa kadia tumenge; saxke o lashimos le Devlesko aresel te skepil mai bute manushen, saxke mai but rhugimata naisimaske te aven angla barimos le Devlesko.
15Yote haya ni kwa faida yenu; ili kama vile neema ya Mungu inavyoenea kwa watu wengi zaidi na zaidi vivyo hivyo watu wengi zaidi watoe shukrani nyingi kwa utukufu wa Mungu.
16Anda kodia shoxar chi xasaras zor. Marka ke rimolape amaro stato xantsi po xantsi, amaro traio kai dia ame O Del neviol swako dies.
16Kwa sababu hiyo hatufi moyo; na hata kama maumbile yetu ya nje yataoza, lakini kwa ndani tunafanywa wapya siku kwa siku.
17Ke amaro chinuria le tsinorhe, kai si ame akana, lasharen amenge iek mai baro lashimos kai chi mai getolpe, but mai but ke so chinuisaras.
17Taabu tunayopata ni kidogo, tena ya muda tu: lakini itatupatia utukufu upitao matazamio yote, utukufu ambao hauna mwisho.
18Ke chi las sama pel dieli kai dichon, numa pel dieli kai chi dichon: so dichol ferdi xantsi vriama inkerel, numa so chi dichol inkerel sagda.
18Hivyo tunatazamia kwa makini si vitu vinavyoonekana, bali visivyoonekana. Maana vinavyoonekana ni vya muda tu; lakini vile visivyoonekana ni vya milele.