1Sas ando Caesarea iek manush kai busholas Cornelius, wo sas baro mashkar le Romanonge ketani, mothonas lenge le ketani le Italianonge.
1Kulikuwa na mtu mmoja huko Kaisarea aitwaye Kornelio, Jemadari wa kikosi kimoja kiitwacho "Kikosi cha Italia."
2Kodo manush pachalaspe ando Del, ai pachalas o mui le Devlesko ai vi leski familia, wo zhutilas but le chorhe manushen, ai rhugilaspe ka Del sagda.
2Alikuwa mtu mwema; naye pamoja na jamaa yake yote walimcha Mungu; alikuwa anafanya mengi kusaidia maskini wa Kiyahudi na alikuwa anasali daima.
3Kal trin pala miazutso dikhlia iazhno ek vizion, ek angelo le Devlesko avilo leste ando kher, ai mothol leske, "Cornelius."
3Yapata saa tisa mchana, aliona dhahiri katika maono malaika wa Mungu akiingia ndani na kumwambia, "Kornelio!"
4Ai dikhlia pe leste darasa, ai phendia, "So si, Devla?" Ai o angelo phendia leske, "O Del ashundia che rhugimata ai dikhlia ke zhutisardian le chorhen ai diape goji pe tute.
4Kornelio alimkodolea macho huyo malaika kwa hofu, akamwambia, "Kuna nini Mheshimiwa?" Huyo malaika akamwambia, "Mungu amezipokea sala na sadaka zako kwa maskini.
5Trade akana manushen ando Joppa te anen le Simonos kai akharel les Petri.
5Sasa, watume watu Yopa wakamwite mtu mmoja aitwaye Simoni, kwa jina lingine Petro.
6Wo beshel le manushensa kai bushol Simon, wo kerel buchi morchaki, ai lesko kher pashai maria; wo phenel tuke so te keres."
6Yeye yumo nyumbani kwa Simoni mtengenezaji wa ngozi ambaye nyumba yake iko karibu na bahari."
7Kana o angelo kai dia lesa duma gelotar, o Cornelius akhardia duie slugen, ai ek ketana kai kerelas leski buchi ai kai pachalaspe ando Del.
7Huyo malaika aliyesema hayo alipokwisha kwenda zake, Kornelio aliwaita watumishi wawili wa nyumbani na mmoja wa askari zake ambaye alikuwa mcha Mungu,
8Ai kana phendia lenge so kerdilia, tradia le ando Joppa.
8akawaeleza yote yaliyotukia, akawatuma Yopa.
9Pe terharin, sar zhanas pa drom, ai sar pashonas pasha foro, o Petri anklisto po kher kal desh u dui te rhugilpe.
9Kesho yake, hao watu watatu wakiwa bado safarini, lakini karibu kufika Yopa, Petro alipanda juu ya paa la nyumba yapata saa sita mchana ili kusali.
10Bokhailo, ai mangelas te xal, zhi kai lasharenas leske te xal, dikhlia ek vizion.
10Aliona njaa, akatamani kupata chakula. Chakula kilipokuwa kinatayarishwa, alipatwa na usingizi mzito akaona maono.
11Dikhlia o cheri sar phuterdilo, ai vari so hulelas tele, sar ek bari selia kai sas phangli katar le shtar koltsuria, kai hulelas ai bufliolas pe phuv;
11Aliona mbingu zimefunguliwa na kitu kama shuka kubwa inateremshwa chini ikiwa imeshikwa pembe zake nne.
12Ai andre sas but failuria zhigeni shtar punrhensa, ai sapa, shuporli (chorhe zhigeni), ai but fialuria chiriklia.
12Ndani ya shuka hiyo kulikuwa na kila aina ya wanyama: wanyama wenye miguu minne, wanyama watambaao na ndege wa angani.
13Ai ek glaso mothol leske, Wushti, Petri, Mudar, ai xa,"
13Akasikia sauti ikimwambia: "Petro, amka uchinje, ule!"
14Numa o Petri phendia, "Nichi, Devla, ke shoxar chi xalem vari so kai si bi vuzho vai marime."
14Petro akajibu, "La, Bwana; mimi sijaonja kamwe chochote ambacho ni najisi au kichafu."
15Ai o glaso mai phendia leske, "So O Del vuzhardo, na dikh tu sar te avino marime."
15Ile sauti ikasikika tena ikimwambia: "Usiviite najisi vitu ambavyo Mungu amevitakasa!"
16Ai o trio data phendia leske, ai strazo kodola diela anklisti opre ando cheri.
16Jambo hili lilifanyika mara tatu, kisha ile shuka ikarudishwa juu mbinguni.
17O Petri delaspe goji so znachil kodia vizion kai dikhlia, eta le trin manush kai sas tradine katar o Cornelius phushenas te arakhen kai sas o kher le Simonosko, ai won vorta angla o wudar sas.
17Petro alipokuwa bado anashangaa juu ya maana ya hilo maono alilokuwa ameliona, wale watu waliotumwa na Kornelio, baada ya kuigundua nyumba ya Simoni, walifika mlangoni,
18Ai phushle zurales te sas kotse kai beshel o Simon kai akharen les Petri.
18Wakaita kwa sauti: "Je, kuna mgeni humu aitwaye Simoni Petro?"
19O Petri delaspe goji pe vizion, ai O Swunto Duxo phendia leske, "Ashun, si katse trin manush kai roden tu.
19Petro alikuwa bado anajaribu kuelewa lile maono, na hapo Roho akamwambia, "Sikiliza! kuna watu watatu hapa, wanakutafuta.
20Wushti opre, ai huli tele ai zha lensa, ke me tradem le.
20Shuka upesi na wala usisite kwenda pamoja nao kwa maana ni mimi niliyewatuma."
21O Petri hulisto tele ai phendia kodole manushenge kai avile katar o Cornelius, "Me sim kodo kai roden, ai phenen lenge sostar avilian?"
21Basi, Petro akateremka chini, akawaambia hao watu, "Mimi ndiye mnayemtafuta. Kwa nini mmekuja?"
22Won phenen, "O Cornelius tradia ame, o baro ketanengo, kodo manush lasholo, rhugilpe ka Del, ai sa le Zhiduvuria lazhan lestar, ek angelo le Devlesko phendia leske te ingeras tu leste, te ashunel so si tu te mothos leske."
22Wao wakamjibu, "Jemadari Kornelio ambaye ni mtu mwema, mcha Mungu na mwenye kuheshimika mbele ya Wayahudi wote ametutuma. Aliambiwa na malaika mtakatifu akualike nyumbani kwake ili asikilize chochote ulicho nacho cha kusema."
23O Petri phendia lenge te aven andre, ai te beshen kodia riat.Pe terharin gelotar lensa, uni andal phral le Joppeske gele lensa.
23Petro akawaalika ndani, akawapa mahali pa kulala usiku ule. Kesho yake, Petro alianza safari pamoja nao, na baadhi ya ndugu wa huko Yopa walifuatana naye.
24Aresle ando Caesarea pe terharin, o Cornelius azhukerelas le peske niamonsa ai peske vortachensa.
24Siku ya pili yake, walifika Kaisarea na huko Kornelio alikuwa anawangojea pamoja na jamaa na marafiki aliokuwa amewaalika.
25Sar delas te del andre o Petri ando kher, o Cornelius gelo angla leste, ai shudiape ka leske punrhe, ai bandilo tele pe phuv angle leste.
25Petro alipokuwa anaingia, Kornelio alitoka nje kumlaki, akapiga magoti mbele yake na kuinama chini kabisa.
26Numa o Petri vazdia les opre ai phendia, "Wushti opre, ke i me sim manush."
26Lakini Petro alimwinua, akamwambia, "Simama, kwa maana mimi ni binadamu tu."
27Sar divinilas lesa, dine ando kher, kotse arakhlia bute manushen.
27Petro aliendelea kuongea na Kornelio wakiwa wanaingia nyumbani ambamo aliwakuta watu wengi wamekusanyika.
28Ai phendia lenge, "Zhanen, nai slobodo te phirel ieke streinosa vai te zhal leste; numa O Del sikadia mange te na dikhav chi ieke manush sar marime vai bi vuzho.
28Petro akawaambia, "Ninyi wenyewe mnajua kwamba Myahudi yeyote amekatazwa na Sheria yake ya dini kushirikiana na watu wa mataifa mengine. Lakini Mungu amenijulisha nisimfikirie mtu yeyote kuwa najisi au mchafu.
29Anda kodia kana akhardian ma, avilem vi te mothav vari so, numa manglemas te zhanav sostar kerdian ma te avav?"
29Kwa sababu hiyo, mliponiita nimekuja bila kusita. Basi, nawaulizeni: kwa nini mmeniita?"
30O Cornelius phendia, "De shtar dies palpale kana postivas; kal trin pala miazutso rhugivas ma ando murho kher, ai eta, ek manush kai sas pe leste tsalia kai strefianas avilo angla mande,
30Kornelio akasema, "Siku tatu zilizopita saa kama hii, saa tisa alasiri, nilikuwa nikisali chumbani mwangu. Ghafla, mtu aliyekuwa amevaa mavazi yenye kun'gaa alisimama mbele yangu,
31ai phendia, "Cornelius, O Del ashundia cho rhugimos, ai diape goji ka mishtimos kai kerdian le chorhenge.
31akasema: Kornelio! Sala yako na sadaka zako kwa maskini vimekubaliwa na Mungu.
32Trade, vari kas ando Joppa, ai an le Simonos, kai akharen les Petri; wo beshel ando kher le Simonosko kai kerel buchi morchaki pashai maria.
32Mtume mtu Yopa akamwite mtu mmoja aitwaye Simoni, kwa jina lingine Petroi; yuko nyumbani kwa Simoni mtengenezaji wa ngozi karibu na bahari.
33Wo, kana avela, del duma tuke. Strazo tradem vari kas karing tute, ai mishto kerdian kai avilian. Akana savorhe sam angla Del, te ashunas so godi O Del phendia tuke te phenes amenge."
33Kwa hiyo nilikutumia ujumbe bila kuchelewa, nawe umefanya vyema kuja. Sasa, sisi tuko mbele ya Mungu, kusikiliza chochote ambacho bwana amekuamuru kusema."
34Antunchi o Petri phendia, "Chachimasa akana zhanav ke O Del nai leske mai drago iek manush de sar aver.
34Hapo Petro akaanza kusema: "Sasa nimetambua kwamba hakika Mungu hana ubaguzi.
35Numa swako manush ande vari savi vitsa te avela, ai pachala le Devlesko mui, ai kerel so si vorta.
35Mtu wa taifa lolote anayemcha Mungu na kutenda haki anapokelewa naye.
36Drago lo le Devleske. Tradia e vorba kal shave le Zhidovonge, ai andia lenge e pacha katar O Jesus Kristo, kai so O Del savorhenge.
36Huu ndio ule ujumbe Mungu alioupeleka kwa watu wa Israeli, akitangaza Habari Njema iletayo amani kwa njia ya Yesu Kristo ambaye ni Bwana wa wote.
37Zhanen so kerdilia ande sa e Judea, ai kai kerde ande Galilee, mai anglal pala bolimos kai phendia o Iovano.
37Ninyi mnajua jambo lililotukia katika nchi yote ya Wayahudi kuanzia Galilaya baada ya ule ubatizo aliohubiri Yohane.
38Zhanen sar O Del shordia pesko Swunto Duxo ai peski putiera po Jesus andai Nazareth, kai zhalas than thanestar ai kerelas mishtimos, ai sastiarelas kodolen kai sas telai putiera le bengeske; ke O Del lesa sas.
38Mnajua Yesu wa Nazareti na jinsi Mungu alivyomteua kwa kummiminia Roho Mtakatifu na nguvu. Mungu alikuwa pamoja naye; yeye alikwenda huko na huko akitenda mema na kuwaponya wote waliokuwa wamevamiwa na Ibilisi.
39Ame sam marturia ande sa godi kerdia ando them le Zhidovon, ai ande Jerusalem; mudarde les kana karfosarde les po trushul.
39Sisi ni mashahidi wa mambo yote aliyotenda katika nchi ya Wayahudi na katika Yerusalemu. Walimuua kwa kumtundika msalabani;
40Numa O Del zhuvindisardia les o trito dies, ai manglia te sikadiol.
40lakini Mungu alimfufua siku ya tatu, akamfanya aonekane
41Na sa le manushenge, numa le marturia kai sas alome mai anglal katar O Del, ame kai xaliam ai piliam lesa palal o zhuvindimos andal mule.
41si kwa watu wote ila kwa wale Mungu aliokwisha wachagua wawe mashahidi wake, yaani sisi tuliokula na kunywa pamoja naye baada ya kufufuka kwake kutoka wafu.
42Ai O Kristo dia ame ordina te das duma pa Del le narodoske, ai te mothas ke wo si kai sas thodino katar O Del te avel kritsinitori pel zhuvinde ai pal mule.
42Alituamuru kuihubiri Habari Njema kwa watu wote na kushuhudia kwamba yeye ndiye aliyeteuliwa na Mungu awe Mwamuzi wa wazima na wafu.
43Sa le profeturia mothon pa leste, ke kon godi pachalpe anda leste, avena lenge bezexa iertime ando lesko anav."
43Manabii wote waliongea juu yake kwamba kila mtu atakayemwamini atasamehewa dhambi zake zote kwa jina lake."
44Sar o Petri divinilas, O Swunto Duxo hulisto pe sa kodola kai ashunenas kodo divano.
44Wakati Petro alipokuwa bado anasema maneno hayo, Roho Mtakatifu aliwashukia wote waliokuwa wanasikiliza ujumbe huo.
45Ai le shave le Devleske kai avile sas le Petresa chudisaile, ke dikhle kai O Swunto Duxo hulisto vi pe le Nai Zhiduvuria.
45Wale Wayahudi waumini waliokuja pamoja na Petro kutoka Yopa walishangaa kuona kuwa Mungu aliwamiminia zawadi ya Roho Mtakatifu watu wa mataifa mengine pia;
46Ke ashunenas len sar denas duma anda kolaver shiba, ai naisinas le Devles. Antunchi o Petri phendia,
46maana waliwasikia wakiongea kwa lugha mbalimbali wakimtukuza Mungu. Hapo Petro akasema,
47"Sai aterdiaras kadale manushen te aven bolde ando pai. Akana kai hulisto O Swunto Duxo pe lende sar amende?
47"Watu hawa wamempokea Roho Mtakatifu kama sisi wenyewe tulivyompokea. Je, kuna yeyote atakayeweza kuwazuia wasibatizwe kwa maji?"
48Ai dia ordina te bolen le ando anav le Devlesko." Ai porme mangle lestar te beshel lensa trin shtar dies.
48Basi, akaamuru wabatizwe kwa jina la Yesu Kristo. Kisha wakamwomba akae nao kwa siku chache.