Romani: New Testament

Swahili: New Testament

Acts

5

1Iek manush kai busholas Ananias, ai leski zhuvli kai busholas Sapphira, bichinde penge phuv.
1Mtu mmoja aitwaye Anania na mkewe Safira waliuza shamba lao vilevile.
2Ai garade andal love, leski rhomni zhanelas, ai angerde so ashilia andel love kal punrhe le apostlonge.
2Lakini, mkewe akiwa anajua, Anania akajiwekea sehemu ya fedha alizopata na ile sehemu nyingine akawakabidhi mitume.
3Numa o Petri phendia leske, "Ananias, Sostar o beng lia cho ilo ai te kerel tu te xoxaves le Swuntone Duxos, ai kai garadian andal love kana bichindian e phuv?
3Basi, Petro akamwuliza, "Anania, mbona Shetani ameuingia moyo wako na kukufanya umdanganye Roho Mtakatifu kwa kujiwekea sehemu ya fedha ulizopata kutokana na lile shamba?
4Mai anglal sar te bichines kodia phuv chiro sas, ai kana bichindian les le love chire sas, sarta thodian ande cho ilo? Kasaviatar buchi, chi xoxadian le manushen numa le Devles."
4Kabla ya kuliuza lilikuwa mali yako, na baada ya kuliuza, bado hizo fedha zilikuwa zako uzitumie utakavyo. Kwa nini basi, uliamua moyoni mwako kufanya jambo la namna hii? Hukumdanganya mtu; umemdanganya Mungu!"
5O Ananias kana ashundia kodola vorbi, pelo tele ai mulo; ai sa o narodo kai sas kotse daraile.
5Anania aliposikia hayo, akaanguka chini, akafa. Watu wote waliosikia habari ya tukio hilo waliogopa sana.
6Le mai terne wushtilo opre, vulisarde les andek tsol, ai angerde les te gropon les.
6Vijana wakafika wakaufunika mwili wake, wakamtoa nje, wakamzika.
7Trin chasuria pala kodia leski rhomni avili kotse, ai chi zhanelas so kerdilia.
7Baada ya muda wa saa tatu hivi, mke wake, bila kufahamu mambo yaliyotukia, akaingia mle ndani.
8O Petri divinil lasa, ai phushel la, "Phen mange, pe ka savo pretso bichindian tumare phuv?" E, woi mothol pe kado pretso.
8Petro akamwambia, "Niambie! Je, kiasi hiki cha fedha ndicho mlichopata kwa kuuza lile shamba?" Yeye akamjibu, "Naam, ni kiasi hicho."
9Antunchi o Petri mothol lake, "Sarta akordisailian te xoxaven le Swuntsone Duxos kai si le Devlesko? Ashun kodola kai groposarde che rhomes angla wudar le, ai vi tu te angeren.
9Naye Petro akamwambia, "Mbona mmekula njama kumjaribu Roho wa Bwana? Sikiliza! Wale watu waliokwenda kumzika mume wako, sasa wako mlangoni na watakuchukua wewe pia."
10Strazo peli kal punrhe le apostlonge, ai muli; kana le terne avile andre, arakhle la muli, angerde la, ai groposarde la pasha lako rhom.
10Mara Safira akaanguka mbele ya miguu ya Petro, akafa. Wale vijana walipoingia, walimkuta amekwisha kufa; hivyo wakamtoa nje, wakamzika karibu na mume wake.
11Savorhe daraile kai sas kotse, ai vi kodola kai ashunde so kerdilia.
11Kanisa lote pamoja na wote waliosikia habari ya tukio hilo, waliogopa sana.
12But mirakluria ai but bucha kerdionas mashkar o narodo katar le vas le apostlonge. Savorhe beshenas andek than anglal o wudara kodoleske kai busholas Solomon.
12Mitume walifanya miujiza na maajabu mengi kati ya watu. Waumini walikuwa wakikutana pamoja katika ukumbi wa Solomoni.
13Ai chi iek andal kolaver chi mai tromanas te zhan lensa; numa o narodo bariarenas le zurales.
13Mtu yeyote mwingine ambaye hakuwa mwamini hakuthubutu kujiunga nao. Hata hivyo, watu wengine wasiokuwa wa imani hiyo waliwasifu.
14But narodo mai but ai mai but mursh ai zhuvlia pachanaspe ando Del, ai buntionas.
14Idadi ya watu waliomwamini Bwana, wanaume kwa wanawake, iliongezeka zaidi na zaidi.
15Anenas le naswalen pel droma, an thonas le pel paturia, saxke kana o Petri nakhela leski vushalin te sai sastiarel vulen.
15Kwa sababu hiyo, watu walikuwa wakipeleka wagonjwa barabarani na kuwalaza juu ya vitanda na mikeka ili Petro akipita, walau kivuli chake kiwaguse baadhi yao.
16But narodo zhalas, uni andel gava kai sas pashe ande Jerusalem, anenas le naswalen, ai le manushenge kai sas o bi vuzho ande lende, ai savorhe sastionas.
16Watu wengi walifika kutoka katika miji ya kando kando ya Yerusalemu, wakiwaleta wagonjwa wao na wale waliokuwa na pepo wachafu, nao wote wakaponywa.
17Antunchi o baro rashai, ai sa kodola kai sas lesa le Saduseanuria, xoliariko sas pe apostluria.
17Kisha, Kuhani Mkuu na wenzake waliokuwa wa kikundi cha Masadukayo wa mahali hapo, wakawaonea mitume wivu.
18Line le apostluria, ai thode le ande temnitsa.
18Basi, wakawatia nguvuni, wakawafunga ndani ya gereza kuu.
19Numa iek angelo le Devlesko phuterdia e riate le vurotsi la temnisaki, ai lia le avri, ai phendia lenge,
19Lakini usiku malaika wa Bwana aliifungua milango ya gereza, akawatoa nje, akawaambia,
20"Zhan ande tampla ai mothon le narodoske sa le vorbi kai si ande kado nevo traio."
20"Nendeni mkasimame Hekaluni na kuwaambia watu kila kitu kuhusu maisha haya mapya."
21Kana o Petri ai o Iovano ashunde kodia, de diminiatsi gele le ande tampla, ai sicharenas le narodos.O baro rashai ai kodola sas lesa avile, ai chide le mai phuren ai sa le bare pel Zhiduvuria te den duma, porme trade ketanen le apostlonge katar e temnitsa.
21Mitume walitii, wakaingia Hekaluni asubuhi na mapema, wakaanza kufundisha. Kuhani Mkuu na wenzake walipofika, waliita mkutano wa Baraza kuu, yaani halmashauri yote ya wazee wa Wayahudi halafu wakawatuma watu gerezani wawalete wale mitume.
22Numa kana le ketani aresle kai temnitsa, won ma nas kotse, gele palpale kal bare le ketani, ai phende so kerdilia. Phenen,
22Lakini hao watumishi walipofika huko hawakuwakuta mle gerezani. Hivyo walirudi, wakatoa taarifa mkutanoni,
23"Le wudara la temisake phandade sas, ai le ketani kai lenas sama kotse sas anglal wudara; numa kana phuterdiam le wudara, chi arakhlem kanikas andre."
23wakisema, "Tulikuta gereza limefungwa kila upande na walinzi wakilinda milango. Lakini tulipofungua hatukumkuta mtu yeyote ndani."
24Kana o baro le ketanengo kai lenas sama kater e tampla ai le bare le rashange ashunde kodola vorbi, chi zhanenas so kerdilia kai ma nai le slugi ai denas pe duma iek kavresa, so si te kerdiol.
24Mkuu wa walinzi wa Hekalu na makuhani wakuu waliposikia habari hiyo wakawa na wasiwasi, wasijue yaliyowapata.
25Vari kon avilia te mothol lenge, "Eta le manush kai thodian ande temnitsa si ande tamplo, ai sicharen le narodos pa Del."
25Akafika mtu mmoja, akawaambia, "Wale watu mliowafunga gerezani, hivi sasa wamo Hekaluni, wanawafundisha watu."
26O baro le ketanengo gelo peske manushensa, ai andine le, numa chi line le pe zor, ke daranas katar o narodo ke shudel le baxensa pe lende.
26Hapo mkuu wa walinzi wa Hekalu pamoja na watu wake walikwenda Hekaluni, akawaleta. Lakini hawakuwakamata kwa kutumia nguvu, maana waliogopa kwamba watu wangewapiga mawe.
27Kana andine le palpale, angla o narodo kai sas kotse, ai o baro rashai phushlia le, phenelas,
27Basi, wakawapeleka, wakawasimamisha mbele ya Baraza. Kuhani Mkuu akawaambia,
28"Ke phendiamas tumenge te na mai sicharen le narodos ande kado anav? Ai akana sa o Jerusalem si sichardo tumendar, ai tume mangen te perel pe amende o rat kodole manushengo."
28"Tuliwakatazeni waziwazi kufundisha kwa jina la mtu huyu; sasa mmeyaeneza mafundisho yenu pote katika Yerusalemu na mnakusudia kutuwekea lawama ya kifo cha mtu huyo."
29O Petri ai le kaver apostluria phende, "Trobul te pachas o mui, o mui le Devlesko de sar le manushengo.
29Hapo Petro, akiwa pamoja na wale mitume wengine, akajibu, "Lazima tumtii Mungu, na siyo binadamu.
30O Del amare dadengo zhuvindisailo, O Jesus, kai mudardian kana karfosardian les po trushul.
30Mungu wa babu zetu alimfufua Yesu baada ya ninyi kumwua kwa kumtundika msalabani.
31O Del vazdia les pesko chache vastesa sar O Shav le Amperatosko, ai O Skepitori te del ka Israel, te keinpe, ai te aven iertime anda penge bezexa.
31Huyu ndiye yule aliyekwezwa na Mungu mpaka upande wake wa kulia, akawa kiongozi na Mwokozi, ili awawezeshe watu wa Israeli watubu, wapate kusamehewa dhambi zao.
32Ame sam marturia anda kadala dieli, ai vi O Swunto Duxo kai O Del dia ka kodola kai pachan lesko mui."
32Sisi ni mashahidi wa tukio hilo, naye Roho Mtakatifu ambaye Mungu amewapa wale wanaomtii, anashuhudia pia tukio hilo."
33Kana ashunde kodia, le bare mangle te mudaren le.
33Wajumbe wote wa lile Baraza waliposikia hayo, wakawaka hasira, hata wakaamua kuwaua.
34Numa iek manush mashkar o narodo, ek Farisi, kai busholas Gamaliel, kai sicharelas o zakono kai o narodo lazhalas lestar ai pachalas lesko mui, wushtilo opre ai phendia te anklen avri le apostluria pe xantsi vriama.
34Lakini Mfarisayo mmoja aitwaye Gamalieli ambaye alikuwa mwalimu wa Sheria na aliyeheshimika sana mbele ya watu wote, alisimama mbele ya lile Baraza, akataka wale mitume watolewe nje kwa muda mfupi.
35Ai phendia lenge, "Tume manush kai san andai Israel, arakhen tume so si te keren kadale manushensa."
35Kisha akawaambia wale wajumbe wa Baraza, "Wananchi wa Israeli, tahadhari kabla ya kutekeleza hicho mnachotaka kuwatenda watu hawa!
36Ke nai de dumult sikadilia o Theudas, kai motholas kai wo si manush baro, ai shtar shela manush linepe pala leste; numa vularde les ai sa kodola kai line sas pe pala leste, xasaile ai chi mai ashilia kanch anda lende.
36Zamani kidogo, kulitokea mtu mmoja jina lake Theuda, akajisema kuwa mtu wa maana na watu karibu mia nne wakajiunga naye. Lakini aliuawa, kisha wafuasi wake wote wakatawanyika na kikundi chake kikafa.
37Ai pala leste sas o Judah andai Galilee, kai tsirdia vi wo manushen pesa, ai vi kodola xasaile, ai sa kodola kai linepe pala leste, xsaile vi won.
37Tena, baadaye, wakati ule wa kuhesabiwa watu, alitokea Yuda wa Galilaya. Huyu naye, aliwavuta watu wakamfuata; lakini naye pia aliuawa, na wafuasi wake wakatawanyika.
38Akana phenav tumenge, na len sama kadale manushenge ai meken le te zhantar; ai so keren kadala manush te avela lendar pale kadia si te xasavon
38Na sasa pia mimi nawaambieni, msiwachukulie watu hawa hatua yoyote; waacheni! Kwa maana, ikiwa mpango huu au shughuli hii yao imeanzishwa na binadamu, itatoweka yenyewe.
39Numa te avela katar O Del nashtil te xasaren kadia buchi, ai na zumaven te rimon e kris le Devleski."
39Lakini kama imeanzishwa na Mungu, siyo tu kwamba hamtaweza kuwashinda, bali mtajikuta mnapigana na Mungu." Basi, wakakubaliana naye.
40Ai vi won haliarde sar leste; ai akharde le apostluria, ai marde le, ai phende lenge te na mai den duma ando anav le Jesusosko, ai porme mekle le.
40Hivyo wakawaita wale mitume, wakaamuru wachapwe viboko na kuwaonya wasifundishe tena kwa jina la Yesu; kisha wakawaacha waende zao.
41Ai geletar kotsar le bare, ai drago sas lenge ke chinuisarde le pala anav le Jesusoske.
41Basi, mitume wakatoka nje ya ule mkutano wa halmashauri wakiwa wamejaa furaha, kwani walistahili kuaibishwa kwa ajili ya jina la Yesu.
42Ai swako dies ande khangeri, ai andel khera, savon te sicharen ai te mothon e lashi viasta pa Jesus Kristo.
42Wakaendelea kila siku kufundisha na kuhubiri Habari Njema ya Kristo, Hekaluni na nyumbani mwa watu.