Romani: New Testament

Swahili: New Testament

John

12

1Shov dies mai anglal O Dies O Baro le Zhidovongo, O Jesus areslo ande Bethany, kai beshlo o Lazarus, kai O Jesus zhuvindisardia les anda le mule.
1Siku sita kabla ya sikukuu ya Pasaka, Yesu alifika Bethania alikoishi Lazaro ambaye Yesu alikuwa amemfufua kutoka wafu.
2Kotse dine les te xan; e Martha podailas les; numa Lazarus sas iek anda kodala kai sas lesa ka e skafidi.
2Huko walimwandalia chakula cha jioni, naye Martha akawa anawatumikia. Lazaro alikuwa mmoja wa wale waliokuwa mezani pamoja na Yesu.
3E Maria lia dopash litre pherdi duxi kai si kuchi, thodia la pe le punrhe le Jesusoske, ai woi koslia leske punrhe peska balensa. Ai sa o kher pherdilo sunga katar e duxi.
3Basi, Maria alichukua chupa ya marashi ya nardo safi ya thamani kubwa, akampaka Yesu miguu na kuipangusa kwa nywele zake. Nyumba yote ikajaa harufu ya marashi.
4Iek anda leske disiplonge, o Judas Iscariot – kodo kai trobul te purhil les, phendia,
4Basi, Yuda Iskarioti, mmoja wa wale kumi na wawili ambaye ndiye atakayemsaliti Yesu, akasema,
5"Sostar chi bichindian kadia duxi trin shela teliara, ai le love dine kal chorhe?"
5"Kwa nini marashi hayo hayakuuzwa kwa fedha dinari mia tatu, wakapewa maskini?"
6Wo phendia kadia lenge, na ke sas leske mila anda le chorhe, numa ke sas chor, ai sas les o gono, ai lelas so sas andre ando gono.
6Alisema hivyo, si kwa kuwa alijali chochote juu ya maskini, bali kwa sababu alikuwa mweka hazina, na kwa kuwa alikuwa mwizi, mara kwa mara aliiba kutoka katika hiyo hazina.
7Numa O Jesus phendia lenge, "Mek la! Woi garadiasas kadia duxi pala e vriama kana groposarena ma.
7Lakini Yesu akasema, "Msimsumbue huyu mama! Mwacheni ayaweke kwa ajili ya siku ya mazishi yangu.
8Ke le chorhe sagda avena tumensa, numa me chi avava tumensa sagda."
8Maskini mtakuwa nao siku zote, lakini hamtakuwa nami siku zote."
9But narodo anda le Zhiduvuria ashunde ke O Jesus sas ande Bethany, ai avenas na ferdi pala O Jesus, numa vi te dikhen o Lazarus, kai O Jesus zhuvindisailo anda le mule.
9Wayahudi wengi walisikia kwamba Yesu alikuwa Bethania. Basi, wakafika huko si tu kwa ajili ya kumwona Yesu, ila pia wapate kumwona Lazaro ambaye Yesu alimfufua kutoka wafu.
10Le bare rasha dine pe duma te mudaren vi le Lazarusos,
10Makuhani wakuu waliamua pia kumwua Lazaro,
11ke but Zhiduvuria geletar lendar pala leste, ai pachanaspe ando Jesus.
11Maana kwa sababu ya Lazaro Wayahudi wengi waliwaasi viongozi wao, wakamwamini Yesu.
12Terharin but narodo avile ka O Dies O Baro le Zhidovongo, kana ashunde ke O Jesus zhal ando Jerusalem.
12Kesho yake, kundi kubwa la watu waliokuja kwenye sikukuu walisikia kuwa Yesu alikuwa njiani kuja Yerusalemu.
13Line patria katar le krenzhi, ai gele angla leste, ai tsipinas, "Hosana! Raduime O Amperato le Zhidovongo kai avel ando anav le Devlesko!"
13Basi, wakachukua matawi ya mitende, wakatoka kwenda kumlaki; wakapaaza sauti wakisema: "Hosana! Abarikiwe huyo ajaye kwa jina la Bwana. Abarikiwe mfalme wa Israeli."
14O Jesus arakhlia iek magari ai beshlo pe leste, sar sas ramome,
14Yesu akampata mwana punda mmoja akapanda juu yake kama yasemavyo Maandiko:
15"Na dara, tu foro anda Zion! Dikh! Cho Amperato avel, beshel pe iek terno magari."
15"Usiogope mji wa Sioni! Tazama, Mfalme wako anakuja, Amepanda mwana punda."
16Leske disipluria chi haliarde mai anglal kadala dieli; numa kana O Jesus lia pesko barimos, denas pe goji ke sas ramome pa leste, ai kerdilo sa so trobul te kerdiol.
16Wakati huo wanafunzi wake hawakuelewa mambo hayo, lakini Yesu alipokwisha tukuzwa, ndipo walipokumbuka kwamba hayo yalikuwa yameandikwa juu yake, na kwamba watu walikuwa wamemtendea hivyo.
17Sa kodala kai sas lesa kana akhardia o Lazarus anda o greposhevo, ai wushtiardia les anda le mule, phende so dikhle ai so kerdia.
17Kundi la watu wale waliokuwa pamoja naye wakati alipomwita Lazaro kutoka kaburini, akamfufua kutoka wafu, walisema yaliyotukia.
18Ai o narodo avel angla leste, ke ashunde ke kerdia kodo miraklo.
18Kwa hiyo umati huo wa watu ulimlaki, maana wote walisikia kwamba Yesu alikuwa amefanya ishara hiyo.
19Le Farizeanuria phenenas iek kavreske, "Tume dikhen, ke chi nirin kanchi! Dikh! Sa e lumia geli pala leste!"
19Basi, Mafarisayo wakaambiana, "Mnaona? Hatuwezi kufanya chochote! Tazameni, ulimwengu wote unamfuata."
20Uni Grekuria anda kodala kai gele ando Jerusalem te rhugin po Dies O Baro le Zhidovongo:
20Kulikuwa na Wagiriki kadhaa miongoni mwa watu waliokuwa wamefika Yerusalemu kuabudu wakati wa sikukuu hiyo.
21Won avile ka Filip, wo sas anda Bethsaida ande Galilee, ai phende. "Raia, ame mangas te dikhas O Jesus."
21Hao walimwendea Filipo, mwenyeji wa Bethsaida katika Galilaya, wakasema, "Mheshimiwa, tunataka kumwona Yesu."
22O Philip gelo ai phendia o Andre, antunchi o Andre ai o Philip gele ai phende ka O Jesus.
22Filipo akaenda akamwambia Andrea, nao wawili wakaenda kumwambia Yesu.
23O Jesus phendia lenge, "O chaso avilo kai O Shav le Manushesko trobul te luvudinles.
23Yesu akawaambia, "Saa ya kutukuzwa kwa Mwana wa Mtu imefika!
24Phenav tumenge o chachimos: te na merela e sumuntsa kai peli ande e phuv ashel korkorho; numa te merela, dela but fruti.
24Kweli nawaambieni, punje ya ngano hubaki punje tu isipokuwa ikianguka katika udongo na kufa. Kama ikifa, basi huzaa matunda mengi.
25Savo kai si leske drago kado traio xasarela les; ai kodo kai gretsol kado traio ande kadia lumia garavel les te zhal ando traio le rhaiosko.
25Anayependa maisha yake, atayapoteza; anayeyachukia maisha yake katika ulimwengu huu, atayaweka kwa ajili ya uzima wa milele.
26Te si vari kon kai podail ma, mek te lelpe pala mande; ai kotse kai avava me, kotse avela vi murhi sluga; kodo kai podaila ma, murho Dat luvudila les.
26Anayetaka kunitumikia ni lazima anifuate, hivyo kwamba popote pale nilipo mimi ndipo na mtumishi wangu atakapokuwa. Mtu yeyote anayenitumikia Baba yangu atampa heshima.
27"Akana murho duxo si buntuime. Ai so sai phenav? "Murho Dat, le ma anda kado chaso?" Numa pala kodia avilem zhi ka kado chaso.
27"Sasa roho yangu imefadhaika, na niseme nini? Je, niseme: Baba, usiruhusu saa hii inifikie? Lakini ndiyo maana nimekuja--ili nipite katika saa hii.
28"Murho Dat, luvudisar chiro anav!" Ai iek glaso dia duma anda o rhaio, phenelas, "Bariardem les, ai mai luvudiva les."
28Baba, ulitukuze jina lako." Hapo sauti ikasema kutoka mbinguni, "Nimelitukuza, na nitalitukuza tena."
29O narodo kai sas kotse, ashunde o glaso, ai uni phenenas, "Iek rhonjito si!" Aver phenenas, "Iek angelo dia lesa duma!"
29Umati wa watu waliokuwa wamesimama hapo walisikia sauti hiyo, na baadhi yao walisema, "Malaika ameongea naye!"
30Numa O Jesus phendia lenge, "Na ke pala mande kado glaso ashundilo, numa pala tumende.
30Lakini Yesu akawaambia, "Sauti hiyo haikutokea kwa ajili yangu mimi, ila kwa ajili yenu.
31Akana avili e kris la lumiaki; akana o beng kai si ande lumia avela shudino avri.
31Sasa ndio wakati wa ulimwengu huu kuhukumiwa; sasa mtawala wa ulimwengu huu atapinduliwa.
32Ai me, kana avava vazdino opre katar e phuv, tsirdava sa le manushen mande."
32Nami nitakapoinuliwa juu ya nchi nitamvuta kila mmoja kwangu."
33Sar del duma kadia, sikavelas lenge sar si te merel.
33(Kwa kusema hivyo alionyesha atakufa kifo gani).
34Le manush phende leske, "Ashundian andai klishka le zakonoske ke O Kristo beshela sa data." Sar sai phenes, "O Shav le Manushesko trobul te avel vazdino? Kon si kodo Shav le Manushesko?"
34Basi, umati huo ukamjibu, "Sisi tunaambiwa na Sheria yetu kwamba Kristo atadumu milele. Wawezaje basi, kusema ati Mwana wa Mtu anapaswa kuinuliwa? Huyo Mwana wa Mtu ni nani?"
35O Jesus phendia lenge, "E vediara si tumensa mai xantsi vriama. Phiren zhi kai si tumen e vediara, kashte te na avela o tuniariko pe tumende, ke kodo kai phirel ando tuniariko chi zhanel kai zhal.
35Yesu akawaambia, "Mwanga bado uko nanyi kwa muda mfupi. Tembeeni mngali mnao huo mwanga ili giza lisiwapate; maana atembeaye gizani hajui aendako.
36Zhi kai si tume e vediara, pachan tume ande vediara, kashte te aven shave la vediarake." O Jesus phendia kadala dieli, gelotar, ai garadilo dur lendar.
36Basi, wakati mnao huo mwanga uaminini ili mpate kuwa watu wa mwanga." Baada ya kusema maneno hayo, Yesu alikwenda zake na kujificha mbali nao.
37Marka ke kerdia but mirakluria angla lende, chi pachanaspe ande leste,
37Ingawa Yesu alifanya miujiza hii yote mbele yao, wao hawakumwamini.
38Eta, te pherdiol e vorba le profetoski o Isaiah, kai phendiasas, "Devla, kon pachaiape ande so phendem? Ai kaske O Kristo sikadia peski putiera?"
38Hivyo maneno aliyosema nabii Isaya yakatimia: "Bwana, nani aliyeuamini ujumbe wetu? Na uwezo wa Bwana umedhihirishwa kwa nani?"
39Anda kodia won nashti pachanaspe, ke o Isaiah mai phendia,
39Hivyo hawakuweza kuamini, kwani Isaya tena alisema:
40"Korhandia lenge iakha, ai zulardia lenge ilo; te na dikhen penge iakhensa, ai te na haliaren penge ilesa, ai chi aven mande te aven skepime, ai te na sastiarav le."
40"Mungu ameyapofusha macho yao, amezipumbaza akili zao; wasione kwa macho yao, wasielewe kwa akili zao; wala wasinigeukie, asema Bwana, ili nipate kuwaponya."
41Isaiah phendia kadala dieli, kana dikhlia lesko barimos, ai dia duma pa leste.
41Isaya alisema maneno haya kwa sababu aliuona utukufu wa Yesu, akasema habari zake.
42Numa vi anda le bare le Zhidovongo pachaiepe ande leste; numa angla le Farizeanuria, chi sikavenas ke pachanpe, daratar ke den len avri anda e synagogue.
42Hata hivyo, wengi wa viongozi wa Wayahudi walimwamini Yesu. Lakini kwa sababu ya Mafarisayo, hawakumkiri hadharani kwa kuogopa kwamba watatengwa na sunagogi.
43Ke mai drago lenge o chetaimos le manushenge de sar o luvudimos katar O Del.
43Walipendelea kusifiwa na watu kuliko kusifiwa na Mungu
44O Jesus dia duma ando baro glaso, "Kodo kai pachal ande mande, pachalpe na ande mande ferdi, numa ande kodo kai tradia ma.
44Kisha Yesu akasema kwa sauti kubwa, "Mtu aliyeniamini, haniamini mimi tu, ila anamwamini pia yule aliyenituma.
45Ai kodo dikhel ma, dikhel kodales kai tradia ma.
45Anayeniona mimi anamwona pia yule aliyenituma.
46Avilem ande lumia sar iek vediara, kashte kon godi pachalape ande mande te na beshel ando tuniariko.
46Mimi ni mwanga, nami nimekuja ulimwenguni ili wote wanaoniamini wasibaki gizani.
47Te si vari kon kai ashunel murhe vorbi, numa chi pachal le, chi krisiniv les, ke me chi avilem te krisiniv e lumia, numa te skepiv la lumia.
47Anayeyasikia maneno yangu lakini hayashiki mimi sitamhukumu; maana sikuja kuhukumu ulimwengu bali kuuokoa.
48Kodo kai shudel ma, ai kai chi premil murhe vorbi si les iek kai krisinila les. E vorba kai phendem, woi dela les pe kris po paluno dies!
48Asiyeyashika maneno yangu anaye wa kumhukumu: neno lile nililosema ni hakimu wake siku ya mwisho.
49Ke chi den duma anda mande; numa O Dat kai tradia ma, phendia mange so trobul te phenav.
49Mimi sikunena kwa mamlaka yangu mwenyewe, ila Baba aliyenituma ndiye aliyeniamuru niseme nini na niongee nini.
50Ai zhanav ke anda leske vorbi si o traio le rhaiosko. Sa anda kodia le dieli kai phenav, phenav le sar O Dat phendia le mange."
50Nami najua kuwa amri yake huleta uzima wa milele. Basi, mimi nasema tu yale Baba aliyoniagiza niyaseme."