1Me phendem tumenge kadala dieli, saxke te na rimon tume.
1"Nimewaambieni hayo kusudi msiiache imani yenu.
2Won shudena tume avri andal Synagoguria: ai vi avela e vriama, kai kon godi mudarela tume gindila ke kerel vorta angla Del.
2Watu watawatenga ninyi na masunagogi yao. Tena, wakati unakuja ambapo kila atakayewaua ninyi atadhani anamhudumia Mungu.
3Ai won kerena kadia, ke chi zhangle chi le Dades, ai chi man.
3Watawatendeeni mambo hayo kwa sababu hawamjui Baba, wala hawanijui mimi.
4Me phendem tumenge kadala dieli, saxke kana avela e vriama, tume serenape kai phendem tumenge. Me chi phendem tumenge pa kadala dieli de anda gor, ke me simas tumensa.
4Basi, nimewaambieni mambo haya ili saa yake itakapofika mkumbuke kwamba niliwaambieni. "Sikuwaambieni mambo haya tangu mwanzo kwa sababu nilikuwa pamoja nanyi.
5Numa akana zhavtar karing kodo kai tradia ma; ai chi iek anda tumende chi phushel ma, "Kai zhas?"
5Lakini sasa namwendea yule aliyenituma; na hakuna hata mmoja wenu anayeniuliza: Unakwenda wapi?
6Numa ke phendem tumenge kadale dieli, tumaro ilo nekezhisailo.
6Kwa kuwa nimewaambieni mambo hayo mmejaa huzuni mioyoni mwenu.
7Numa phenav tumenge o chachimos: mai mishto avela tumenge te zhavtar: ke te na zhavatar, O Zhutitori chi avela tumende; numa te zhavatar, tradava les tumende.
7Lakini, nawaambieni ukweli: afadhali kwenu mimi niende zangu, maana nisipokwenda Msaidizi hatakuja kwenu. Lakini nikienda, basi, nitamtuma kwenu.
8Ai kana avela, sikavela le narodoske ke shubinpe pa bezex, pa so si vorta, ai pai kris le Devleski.
8Naye atakapokuja atawathibitishia walimwengu kwamba wamekosea kuhusu dhambi, uadilifu na hukumu ya Mungu.
9Won shubinpe pa bezex, ke chi pachanpe ande mande;
9Wamekosea kuhusu dhambi kwa sababu hawaniamini;
10pa so si vorta, ke me zhav ka murho Dat, ai ke chi mai dikhena ma;
10kuhusu uadilifu, kwa sababu naenda zangu kwa Baba, nanyi hamtaniona tena;
11pai kris, ke o baro kadala lumiako dino lo pe kris.
11kuhusu hukumu kwa sababu mkuu wa ulimwengu huu amekwisha hukumiwa.
12Mai si ma inker but dieli te phenav tumenge, numa nashtin te haliaren le akana.
12"Ninayo bado mengi ya kuwaambieni, ila kwa sasa hamwezi kuyastahimili.
13Kana O Swunto Duxo le chachimosko avela, wo ingerela tume ande sa o chachimos: ke wo chi dela duma pa peste; numa phenela so godi ashunel: ai phenela tumenge le dieli kai avena.
13Lakini atakapokuja huyo Roho wa kweli atawaongoza kwenye ukweli wote; maana hatasema kwa mamlaka yake mwenyewe, bali atawaambieni yote atakayosikia, na atasema mambo yatakayokuwa yanakuja.
14Wo luvudila man: ke lela so si murho, ai phenela tumenge.
14Yeye atanitukuza mimi kwa kuwa atawaambieni yale atakayopata kutoka kwangu.
15So godi kai si O Dat, murho si: anda kodia phendem, "Te lel so si murho, ai te phenela tumenge."
15Vyote alivyo navyo Baba ni vyangu; ndiyo maana nimesema kwamba huyo Roho Mtakatifu atawaambieni yale atakayopata kutoka kwangu.
16"Mai xantsi vriama, ai chi mai dikhena ma; ai porme mai xantsi vriama, ai dikhena ma, ke me zhav ka Dat."
16"Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona; na baada ya kitambo kidogo tena mtaniona!"
17Pe kado divano uni anda leske disiplonge denas pe duma won de won. Ai mothonas, "So znachil so phenel amenge, mai xantsi vriama, ai chi mai dikhena ma, ai porme mai xantsi vriama, ai dikhena ma, ke me zhav ka Dat?"
17Hapo baadhi ya wanafunzi wake wakaulizana, "Ana maana gani anapotwambia: Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona; na baada ya kitambo kidogo tena mtaniona? Tena anasema: Kwa kuwa ninakwenda kwa Baba!"
18No won phende "So znachil so phenel, mai xantsi vriama? Ame chi zhanas pa soste del duma."
18Basi, wakawa wanaulizana, "Ana maana gani anaposema: Bado kitambo kidogo? Hatuelewi anaongelea nini."
19O Jesus zhanelas ke mangenas te phushen lestar, ai phendia lenge, "Tume phushen iek kavrestar so phendem. "Mai xantsi vriama ai chi mai dikhena ma, ai porme mai xantsi vriama, ai dikhena ma?"
19Yesu alijua kwamba walitaka kumwuliza, basi akawaambia, "Je, mnaulizana juu ya yale niliyosema: Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona; na baada ya kitambo kidogo tena mtaniona?
20Chachimasa, chachimasa, me phenav tumenge, tume rovena ai suspinina ai le lumia raduilape; tume avena nekezhime, numa tumaro nekazo parhudiola ai avela raduimos.
20Nawaambieni kweli, ninyi mtalia na kuomboleza, lakini ulimwengu utafurahi: mtaona huzuni lakini huzuni yenu itageuka kuwa furaha.
21E zhuvli kana si te avel la glata nekezhime la, ke lako chaso avilo: numa kana o tsinorho arakhadilo, chi mai serelpe ka chino, pala raduimos kai si la, ke iek manush kerdilo ande lumia.
21Wakati mama anapojifungua huona huzuni kwa sababu saa ya maumivu imefika; lakini akisha jifungua hayakumbuki tena maumivu hayo kwa sababu ya furaha kwamba mtu amezaliwa duniani.
22No vi tume akana san nekeshime: numa mai dikhava tume, ai tumaro ilo raduilape, ai khonik chi lela tumendar tumaro raduimos.
22Ninyi pia mna huzuni sasa; lakini nitawajieni tena, nanyi mtajaa furaha mioyoni mwenu, na furaha hiyo hakuna mtu atakayeiondoa kwenu.
23Kana avela kodo dies tume chi mai phushena mandar khanchi. Chachimasa, chachimasa, me phenav tumenge, so tume mangena katar O Dat ande murho anav, wo dela tumen.
23Siku hiyo hamtaniomba chochote. Kweli nawaambieni, chochote mtakachomwomba Baba kwa jina langu, atawapeni.
24Zhi akana tume chi manglian khanchi ande murho anav: mangen, ai avela tumen dino; saxke te pherdiol tumaro raduimos.
24Mpaka sasa hamjaomba chochote kwa jina langu. Ombeni nanyi mtapata ili furaha yenu ikamilike.
25Me phendem tumenge kadala dieli andel paramicha: numa e vriama avela, kana chi mai dava tumensa duma andel paramichi, numa dava tumensa duma vorta pa Dat.
25"Nimewaambieni mambo hayo kwa mafumbo. Lakini wakati utakuja ambapo sitasema tena nanyi kwa mafumbo, bali nitawaambieni waziwazi juu ya Baba.
26Kana kodia dies avela tume mangena ande murho anav: ai chi phenav tumenge, ke rhugiva ma ka Dat anda tumende:
26Siku hiyo mtaomba kwa jina langu, na siwaambii kwamba nitamwomba Baba kwa niaba yenu;
27Ke O Dat leske drago tumenge, ke sanas tume drazhi mange, ai tume pachaian tume ke me avilem katar Del.
27maana yeye mwenyewe anawapenda ninyi, kwa sababu ninyi mmenipenda mimi na mmeamini kwamba nimetoka kwa Mungu.
28"Me avilem katar O Dat, ai avilem ande lumia: numa akana zhavtar andai lumia, ai zhav ka Dat."
28Mimi nilitoka kwa Baba, nikaja ulimwenguni; na sasa nauacha ulimwengu na kurudi kwa Baba."
29Leske disipluria phende leske, "Eta tu des duma akana vorta, ai chi des duma andel paramichia.
29Basi, wanafunzi wake wakamwambia, "Ahaa! Sasa unasema waziwazi kabisa bila kutumia mafumbo.
30Akana zhanas ke tu zhanes swako fielo, ai ke chi trobul vari kon te phushel tu vari so: anda kodia ame pachas ame ke tu avilian katar O Del."
30Sasa tunajua kwamba wewe unajua kila kitu, na huna haja ya kuulizwa maswali na mtu yeyote; kwa hiyo tunaamini kwamba umetoka kwa Mungu."
31O Jesus phendia lenge, "Tume pachan akana?
31Yesu akawajibu, "Je, mnaamini sasa?
32Eta, e vriama avela, ai vunzhe avili, kai avela swako ande tumende respiime, pe peski rik, ai mekena ma korkorho; numa chi sim korkorho, ke O Dat si mansa.
32Wakati unakuja, tena umekwisha fika, ambapo ninyi nyote mtatawanyika kila mtu kwake, nami nitaachwa peke yangu. Kumbe, lakini mimi siko peke yangu, maana Baba yu pamoja nami.
33Me phendem tumenge kadala dieli, saxke te avel tume e pacha ande mande. Tume avena zumade ande lumia: numa na daran; ke me nirisardem pe lumia!"
33Nimewaambieni mambo haya ili mpate kuwa na amani katika kuungana nami. Ulimwenguni mtapata masumbuko; lakini jipeni moyo! Mimi nimeushinda ulimwengu!"