1Kana O Jesus phendiasas kadala vorbi, gelo peske disiplonsa inchal o pai kai bushol Cedron, kotse sas iek sado, ai wo gelo andre peske disiplonsa.
1Yesu alipokwisha sema hayo, alikwenda ng'ambo ya kijito Kedroni, pamoja na wanafunzi wake. Mahali hapo palikuwa na bustani, naye Yesu akaingia humo pamoja na wanafunzi wake.
2Ai vi o Judas, kai purhisardia les, zhanelas kodo tsan; ke O Jesus ai leske disipluria butivar chidepe kotse andek than.
2Yuda, aliyemsaliti Yesu, alipajua mahali hapo kwani mara nyingi Yesu alikutana na wanafunzi wake huko.
3O Judas gelo ka sado, ai andia pesa ketanen ai le zhandari kai sas tradine katar le bare le rashange ai katar le Farizeanuria; won avenas le sabiensa, ai le lamponsa, ai le khashtensa kai phabonas.
3Basi, Yuda alichukua kikosi cha askari na walinzi kutoka kwa makuhani wakuu na Mafarisayo, akaja nao bustanini wakiwa na taa, mienge na silaha.
4O Jesus zhanelas so si te kerdiol pe lesa, gelo karing lende, ai phendia lenge, "Kas roden?" Le ketani phende leske,
4Yesu, hali akijua yote yatakayompata, akatokea, akawauliza, "Mnamtafuta nani?"
5"O Jesus andai Nazareth." O Jesus phendia lenge, "Me sim." Ai o Judas, kai purhisardia les, lensa sas.
5Nao wakamjibu, "Yesu wa Nazareti!" Yesu akawaambia, "Mimi ndiye." Msaliti Yuda alikuwa amesimama hapo pamoja nao.
6Kana O Jesus phendia lenge, "Me sim," won dinepe palpale, ai pele tele.
6Basi, Yesu alipowaambia: "Mimi ndiye", wakarudi nyuma, wakaanguka chini.
7O Jesus mai phushlia le, "Kas roden?" Ai won phende, "O Jesus andai Nazareth."
7Yesu akawauliza tena, "Mnamtafuta nani?" Wakamjibu, "Yesu wa Nazareti!"
8O Jesus phendia, "Me phendem tumenge ke me sim: No te sim me kai roden, meken kodolen te zhantar.
8Yesu akawaambia, "Nimekwisha waambieni kwamba mimi ndiye. Basi, kama mnanitafuta mimi, waacheni hawa waende zao."
9Wo phendia kadia saxke te kerdiolpe e vorba, kai phendiasas. Chi xasardem chi iek anda kodola kai dian ma.
9(Alisema hayo ili yapate kutimia yale aliyosema: "Wale ulionipa sikumpoteza hata mmoja.")
10O Simon Petri kai sas les iek sabia lia la, ai dia iek le bare rashaska sluga, ai shindia lako khan o chacho. Kodia sluga busholas Malchus.
10Simoni Petro alikuwa na upanga; basi, akauchomoa, akamkata sikio la kulia mtumishi wa Kuhani Mkuu. Mtumishi huyo aliitwa Malko.
11O Jesus phendia le Petreske, "Tho palpale chi sabia, so te na piiav e kuchi kai murho Dat dia ma te piiav?"
11Basi, Yesu akamwambia Petro, "Rudisha upanga wako alani. Je, nisinywe kikombe alichonipa Baba?"
12Antunchi le ketani lenge bare ai zhandari le Zhidovonge line le Jesusos, ai phangle les.
12Kile kikosi cha askari, mkuu wake na walinzi wa Wayahudi walimkamata Yesu, wakamfunga
13Ingerde les mai anglal kai Annas; ke sas o sokro le Caiaphasosko, kai sas baro rashai kodo bersh.
13na kumpeleka kwanza kwa Anasi; Anasi alikuwa baba mkwe wa Kayafa ambaye alikuwa Kuhani Mkuu mwaka huo.
14Ai o Caiaphas sas kodo kai phendiasas le Zhidovonge, "Mai mishto te merel iek manush le narodoske."
14Huyo Kayafa ndiye aliyekuwa amewashauri Wayahudi kwamba ni afadhali mtu mmoja afe kwa ajili ya taifa.
15O Simon Petri ai aver disiplo lenaspe pala Jesus, kodia disiplo zhanelas les o baro rashai, ai gelo vi wo le Jesusosa ande bar le baro rashasko.
15Simoni Petro pamoja na mwanafunzi mwingine walimfuata Yesu. Huyo mwanafunzi mwingine alikuwa anajulikana kwa Kuhani Mkuu, hivyo aliingia pamoja na Yesu ndani ya ukumbi wa Kuhani Mkuu.
16Numa o Petri beshlo avri pasha wudar, o kolaver disiplo kai zhanelas les o baro rashai, anklisto avri ai dia duma la zhuvliasa kai arakhelas o wudar, ai angerdia o Petri andre.
16Lakini Petro alikuwa amesimama nje, karibu na mlango. Basi, huyo mwanafunzi mwingine aliyekuwa anajulikana kwa Kuhani Mkuu alitoka nje akasema na mjakazi, mngoja mlango, akamwingiza Petro ndani.
17Antunchi e sluga kai garavelas o wudar phendia le Petreske, pate chi san vi tu iek disiplo kadale manushesko? Ai wo phendia "Nichi, chi sim."
17Huyo msichana mngoja mlango akamwuliza Petro, "Je, nawe pia ni mmoja wa wanafunzi wa mtu huyu?" Petro akamwambia, "Si mimi!"
18Ai le slugi ai zhandari beshenas anda punrhende kotse, kai kerde iag le angaresa, ke shil sas: Ai tachonas, vi o Petri sas lensa, ai tacholas vi wo.
18Watumishi na walinzi walikuwa wamewasha moto kwa sababu kulikuwa na baridi, wakawa wanaota moto. Naye Petro alikuwa amesimama pamoja nao akiota moto.
19O baro rashai phushelas le Jesusos pa leske disipluria, ai pa lesko sicharimos.
19Basi, Kuhani akamwuliza Yesu juu ya wanafunzi wake na mafundisho yake.
20O Jesus phendia leske, "Me dem duma angla savorhende le narodosa; me sichardem sagda ande synagogue, ai ando tampla, kai sa le Zhiduvuria chidenaspe; ai me chi phendem khanchi chordanes.
20Yesu akamjibu, "Nimesema na kila mtu daima hadharani. Kila mara nimefundisha katika masunagogi na Hekaluni, mahali wakutanikiapo Wayahudi wote; na wala sijasema chochote kwa siri.
21Sostar tu phushes mandar? Phush kodolendar kai ashunde man, so phendem lenge: Ashun! Won zhanen so phendem."
21Kwa nini waniuliza mimi? Waulize wale waliosikia nini niliwaambia. Wao wanajua nilivyosema."
22Pe kodo divano, iek andal zhandari kai sas kotse dia iek palma le Jesusos, ai phendia, "Kadia si sar des duma kal bare rashas?"
22Alipokwisha sema hayo mlinzi mmoja aliyekuwa amesimama hapo akampiga kofi akisema, "Je, ndivyo unavyomjibu Kuhani Mkuu?"
23O Jesus phendia leske, "Te si ke dem duma nasul, phen mange che nasulimos phendem: ai te dem duma mishto, sostar des ma iek palma?"
23Yesu akamjibu, "Kama nimesema vibaya, onyesha huo ubaya; lakini ikiwa nimesema vema, mbona wanipiga?"
24Annas tradia les phanglo ka Caiaphas o baro rashai.
24Basi, Anasi akampeleka Yesu akiwa amefungwa, kwa Kuhani Mkuu Kayafa.
25O Simon Petri kotse sas ai tacholas. Ai won phende leske, "Pate tu chi san anda kodola disipluria?" Ai wo phendia, "Nichi, me chi sim anda kodola."
25Petro alikuwa hapo akiota moto. Basi, wakamwuliza, "Je, nawe pia si mmoja wa wanafunzi wake?" Yeye akakana na kusema, "Si mimi!"
26Iek sluga le bare rashaski sas ek niamo kodolesa kai o Petri shindiasas lesko khan, phendia, "Pate chi dikhlem tu ando sado lesa?"
26Mmoja wa watumishi wa Kuhani Mkuu, jamaa wa yule aliyekatwa sikio na Petro, akamwuliza, "Je, mimi sikukuona wewe bustanini pamoja naye?"
27O Petri pale phendia, "Chi zhanav les," ai strazo o kurkorsho bashadia.
27Petro akakana tena; mara jogoo akawika.
28Porme angerde le Jesusos katar o Caiaphas ka kher la krisako le guvernorosko kai keren kris: diminiatsi sas; numa le Zhiduvuria chi gele andre ando kher, saxke te na aven marime, ai te sai xan O Dies O Baro le Zhidovongo.
28Basi, walimchukua Yesu kutoka kwa Kayafa, wakampeleka ikulu. Ilikuwa alfajiri, nao ili waweze kula Pasaka, hawakuingia ndani ya ikulu wasije wakatiwa najisi.
29O Pilate anklisto avri te zhal karing lende, ai phendia, "Savatar dosh si tume pe kado manush?"
29Kwa hiyo, Pilato aliwaendea nje, akasema, "Mna mashtaka gani juu ya mtu huyu?"
30Ai won phende leske, "Te na avilino bi lasho, nas te anas les tute."
30Wakamjibu, "Kama huyu hangalikuwa mwovu hatungalimleta kwako."
31O Pilate phendia lenge, "Len les tume ai den les pe kris pala tumaro zakono. Le Zhiduvuria phende leske, "Amenge nai slobodo te mudares vari kas:"
31Pilato akawaambia, "Haya, mchukueni ninyi wenyewe, mkamhukumu kufuatana na Sheria yenu." Wayahudi wakamjibu, "Sisi hatuna mamlaka ya kumwua mtu yeyote."
32Kodia sas saxke te kerdiol e vorba kai O Jesus phendiasas, kana sikadia sar si te merel.
32(Ilifanyika hivyo yapate kutimia maneno aliyosema Yesu kuonyesha atakufa kifo gani.)
33O Pilate gelo ando kher la krisako ai akhardia le Jesusos, ai phendia leske, "San tu o amperato le Zhidovongo?"
33Pilato akaingia tena ndani ya ikulu, akamwita Yesu na kumwuliza: "Ati wewe ndiye Mfalme wa Wayahudi?"
34O Jesus dia les atweto, "Tu anda tute mothos kodia, vai le kolaver phende tuke pa mande?"
34Yesu akamjibu, "Je, hayo ni maneno yako au wengine wamekwambia habari zangu?"
35O Pilate dia les atweto, "Pate me sim Zhidovo? Chiro narodo ai le bare rasha andine tu mande; so kerdian tu?"
35Pilato akamjibu, "Je, ni Myahudi mimi? Taifa lako na makuhani wamekuleta kwangu. Umefanya nini?"
36O Jesus phendia, "Murhi amperetsia nai ande kadia lumia; te avilino murhi amperetsia ande kadia lumia, antunchi murhe slugi marenaspe pala mande, saxke te na avav dino kal Zhiduvuria: Numa akana murhi amperetsia nai katse pe lumia.
36Yesu akamjibu, "Ufalme wangu si wa ulimwengu huu. Kama ufalme wangu ungekuwa wa ulimwengu huu watumishi wangu wangenipigania nisitiwe mikononi mwa Wayahudi. Lakini sasa ufalme wangu si wa hapa."
37O Pilate phendia leske, "No tu san amperato?" O Jesus phendia, "Tu mothos me sim amperato. Me arakhadilem ai avilem ande lumia, te phenav pa chachimos. Kon godi si le chachimasko ashunel murho glaso.
37Hapo Pilato akamwambia, "Basi, wewe ni Mfalme?" Yesu akajibu, "Wewe umesema kwamba mimi ni Mfalme. Mimi nimezaliwa kwa ajili hiyo; na kwa ajili hiyo nimekuja ulimwenguni kuwaambia watu juu ya ukweli. Kila mtu wa ukweli hunisikiliza."
38O Pilate phendia leske, "So si o chachimos?" Ai kana phendia kadia, anklisto avri pale te zhal karing le Zhiduvuria, ai phende lenge, "Me chi arakhav chi iek nasulimos ande leste."
38Pilato akamwambia, "Ukweli ni kitu gani?" Pilato alipokwisha sema hayo, aliwaendea tena Wayahudi nje, akawaambia, "Mimi sioni hatia yoyote kwake.
39Numa sar si mashkar tumende iek zakono, te mekav vari kas tumenge kana si O Dies O Baro: mangen ma te mekav tumenge O Amperato le Zhidovongo?"
39Lakini, mnayo desturi kwamba mimi niwafungulie mfungwa mmoja wakati wa Pasaka. Basi, mwataka niwafungulieni Mfalme wa Wayahudi?"
40Pale savorhe tsipinas, "Nichi, na les, numa o Barabbas." Numa o Barabbas sas ek chor.
40Hapo wakapiga kelele: "La! Si huyu ila Baraba!" Naye Baraba alikuwa mnyang'anyi.