Romani: New Testament

Swahili: New Testament

John

19

1Antunchi O Pilate lia le Jesusos, ai kerdia te maren les le bichosa.
1Basi, Pilato akaamuru Yesu achukuliwe, apigwe viboko.
2Le ketani kerde andal kanrhe iek korona, ai tsode la pe lesko shero, ai dine pe leste iek rhocha brazbi.
2Nao askari wakasokota taji ya miiba, wakamtia kichwani, wakamvika na joho la rangi ya zambarau.
3Porme pashile pasha leste, ai phende, "Droboitu, Amperato le Zhidogongo!" ai denas les palmi po mui.
3Wakawa wanakuja mbele yake na kusema: "Shikamoo, Mfalme wa Wayahudi!" Wakampiga makofi.
4O Pilate pale ankliste avri, ai phendia le Zhidovonge, "Eta, anav les tumenge avri, saxke te zhanen ke chi arakhav ande leste chi iek nasulimos.
4Pilato akatoka tena nje, akawaambia, "Tazameni, namleta nje kwenu, mpate kujua kwamba mimi sikuona hatia yoyote kwake."
5Antunchi O Jesus anklisto avri la koronasa kai sas kanrhale, ai le rasha kai sas brazbi, ai o Pilate phendia lenge, "Eta, o manush!"
5Basi, Yesu akatoka nje amevaa taji ya miiba na joho la rangi ya zambarau. Pilato akawaambia, "Tazameni! Mtu mwenyewe ni huyo."
6Numa kana le bare le rashange ai zhandari dikhle les, tsipinas, phenenas, "Karfon les, karfon les." O Pilate phendia lenge, "Len les tume, ai karfon les: ke me chi arakhav chi iek nasulimos ande leste."
6Makuhani wakuu na walinzi walipomwona wakapaaza sauti: "Msulubishe! Msulubishe!" Pilato akawaambia, "Mchukueni basi, ninyi wenyewe mkamsulubishe, kwa maana mimi sikuona hatia yoyote kwake."
7Le Zhiduvuria phende leske, "Amen si ame iek zakono, ai pala amaro zakono wo trobul te merel; ke wo kerdia anda peste O Shav le Devlesko."
7Wayahudi wakamjibu, "Sisi tunayo Sheria, na kufuatana na Sheria hiyo, ni lazima afe, kwa sababu alijifanya kuwa Mwana wa Mungu."
8Kana o Pilate ashundia kodia, wo mai zurales darailo;
8Pilato aliposikia maneno hayo akazidi kuogopa.
9ai pale gelo ando kher la krisako, ai phushlia katar O Jesus, "Katar san tu?" Numa O Jesus chi phendia kanch.
9Basi, akaingia tena ndani ya ikulu, akamwuliza Yesu, "Umetoka wapi wewe?" Lakini Yesu hakumjibu neno.
10O Pilate phendia leske, "Mansa chi des duma? Pate chi zhanes ke man si ma e putiera te karfon tu po trushul, ai ke si ma vi e putiera te mekav tu?"
10Hivyo Pilato akamwambia, "Husemi nami? Je, hujui kwamba ninayo mamlaka ya kukufungua na mamlaka ya kukusulubisha?"
11O Jesus phendia, "Tut nas te avel tu chi iek putiera pe mande, te na avilino tu dini putiera opral: anda kudia kodo kai andia ma tute kerel iek mai baro bezex.
11Yesu akamjibu, "Hungekuwa na mamlaka yoyote juu yangu kama hungepewa na Mungu. Kwa sababu hiyo, yule aliyenikabidhi kwako ana dhambi kubwa zaidi."
12Pala kodia o Pilate mangelas te mekel les, numa le Zhiduvuria tsipinas, phenenas, "Te mekesa les, tu chi san o vortako le Caesarosko: ke kon godi kerel anda peste amperato, wo kerel anda peste o duzhmano le Caesarosko.
12Tangu hapo, Pilato akawa anatafuta njia ya kumwachilia, lakini Wayahudi wakapiga kelele: "Ukimwachilia huyu mtu, wewe si rafiki yake Kaisari; kila mtu anayejifanya kuwa Mfalme humpinga Kaisari!"
13O Pilate kana ashundia kodia, andia le Jesusos avri, ai beshlo tele po skamin la krisako po tsan kai bushol o Bax, ai Zhidovisko Gabbatha.
13Basi, Pilato aliposikia maneno hayo akamleta Yesu nje, akaketi juu ya kiti cha hukumu, mahali paitwapo: "Sakafu ya Mawe" (kwa Kiebrania, Gabatha).
14Antunchi sas e vriama kai lasharenas O Dies O Baro le Zhidovongo, ai pashte mizmeri sas: O Pilate phendia le Zhidovonge, "Dikh, tumaro Amperato!"
14Ilikuwa yapata saa sita mchana, siku ya maandalio ya Pasaka. Pilato akawaambia Wayahudi, "Tazameni, Mfalme wenu!"
15Numa won tsipinas, "Mudar les, Mudar les, Karfosar les po trushul." O Pilate phendia lenge, "Tume mangen ma te mudarav tumare amperatos?" Le bare rasha phenenas, "Amaro amperato si o Caesar."
15Wao wakapaaza sauti: "Mwondoe! Mwondoe! Msulubishe!" Makuhani wakuu wakajibu, "Sisi hatuna Mfalme isipokuwa Kaisari!"
16Antunchi dia les lende te karfon les. Won line le Jesus, ai ingerde les.
16Basi, hapo Pilato akamtia Yesu mikononi mwao ili asulubiwe. Basi, wakamchukua Yesu.
17O Jesus ingerelas pesko trushul, ai areslo po tsan kai bushol shero, ai Zhidovisko mothonas Golgotha:
17Naye akatoka akiwa amejichukulia msalaba wake kwenda mahali paitwapo "Fuvu la Kichwa", (kwa Kiebrania Golgotha).
18ai kotse karfosarde les, ai dui aver manush sas lesa, iek pal dui riga, ai O Jesus mashkaral.
18Hapo ndipo walipomsulubisha, na pamoja naye waliwasulubisha watu wengine wawili; mmoja upande wake wa kulia na mwingine upande wake wa kushoto, naye Yesu katikati.
19O Pilate ramosardiape vari soste, ai thodia po trushul, ai kodo ramomos motholas, "O JESUS ANDAI NAZARETH, O AMPERATO LE ZHIDOVONGO."
19Pilato aliandika ilani akaiweka juu ya msalaba. Nayo ilikuwa imeandikwa hivi: "Yesu wa Nazareti, Mfalme wa Wayahudi."
20But Zhiduvuria jinde so sas ramome: ke o than kai O Jesus sas karfome pasha foro sas: ai ramome sas Zhidovisko, Grechisko ai Latinesko.
20Wayahudi wengi waliisoma ilani hiyo, maana mahali hapo aliposulubiwa Yesu palikuwa karibu na mji. Tena ilani hiyo ilikuwa imeandikwa kwa Kiebrania, Kilatini, na Kigiriki.
21Le bare le rashange phende le Pilatoske, "Na ramosar, O Amperato Le Zhidovongo; numa ramosar ke wo phendia, 'Me sim O Amperato le Zhidovongo.'"
21Basi, makuhani wakuu wakamwambia Pilato, "Usiandike: Mfalme wa Wayahudi, ila Yeye alisema, Mimi ni Mfalme wa Wayahudi."
22O Pilate phendia, "So me ramosardem, trobul te beshel ramome."
22Pilato akajibu, "Niliyoandika, nimeandika!"
23Le ketani, kana karfosarde le Jesusos, line leske tsalia, ai kerde shtar kotora anda lende, iek kotor swakona ketanake; ai line vi leski raxami, kai nas suvdi, numa anda iek kotor sas de opral zhi tele.
23Askari walipokwisha msulubisha Yesu, walizichukua nguo zake, wakazigawa mafungu manne, fungu moja kwa kila askari. Walichukua pia na kanzu yake; kanzu hiyo ilikuwa imefumwa kwa kipande kimoja tu, bila mshono.
24Ai phende mashkar pende, "Na shinas la, numa thodepe te dikhen kon niril la," lela la: saxke te kerdiol so phendiasas E Vorba le Devleski, kai phenel, "Won hulade murhe tsalia mashkar pende, ai thodepe te dikhen kon niril murhi raxami." So kerde le ketani.
24Basi, hao askari wakashauriana: "Tusiipasue, ila tuipigie kura itakuwa ya nani." Jambo hilo lilifanyika ili yatimie Maandiko Matakatifu yasemayo: "Waligawana mavazi yangu, na nguo yangu wakaipigia kura." Basi, ndivyo walivyofanya hao askari.
25Pasha trushul le Jesusosko sas leski dei, ai e phei leska daki, e Maria e rhomni le Cleophaski, ai e Maria Magdalene.
25Karibu na msalaba wake Yesu walikuwa wamesimama mama yake, na dada ya mama yake, Maria mke wa Kleopa, na Maria Magdalene.
26Kana O Jesus dikhlia peska da, ai pasha late o disiplo, kai sas leske drago, phenel peska dake, "Zhuvlio, Eta, cho shav!"
26Yesu alipomwona mama yake, na karibu naye amesimama yule mwanafunzi aliyempenda, akamwambia mama yake: "Mama! Tazama, huyo ndiye mwanao."
27Ai porme phendia le disiploske, "Eta, chi dei! ai antunchi kodia disiplo lia la ka lesko kher te beshel leste.
27Halafu akamwambia yule mwanafunzi: "Tazama, huyo ndiye mama yako." Na tangu saa ile huyo mwanafunzi alimchukua akae nyumbani kwake.
28Pala kodia, O Jesus kai zhanelas ke vunzhe sa gata sas, saxke te kerdiol so phendia E Vorba le Devleski, wo phendia, "Trushalo sim."
28Yesu alijua kwamba yote yalikuwa yametimia; na, ili Maandiko Matakatifu yapate kutimia, akasema, "Naona kiu."
29Ai sas kotse iek piri chikaki pherdo shut. Le ketani bolde ieke ponzha pherdi shut, ai kana phangle la pe iek kotor khash kai bushol hisop, tsode la ka lesko wush.
29Hapo palikuwa na bakuli limejaa siki. Basi, wakachovya sifongo katika hiyo siki, wakaitia juu ya ufito wa husopo, wakamwekea mdomoni.
30Kana o shut areslo pel le Jesusoske wush, wo phendia "Sa gata"; ai kana meklia o shero tele, mulo.
30Yesu alipokwisha pokea hiyo siki, akasema, "Yametimia!" Kisha akainama kichwa, akatoa roho.
31Kodia sas iek dies mai anglal sar o Savato, ai le Zhiduvuria chi mangenas le staturia te beshen pel trushula Savatone, ke kodo Savato sas iek baro dies. Le Zhiduvuria mangenas katar o Pilate te phagen le punrhe kodolenge kai sas karfome, ai te len le pal trushula.
31Ilikuwa Ijumaa, siku ya Maandalio. Kwa hiyo, kusudi miili isikae msalabani siku ya Sabato, maana siku hiyo ya Sabato ilikuwa siku kubwa, Wayahudi walimwomba Pilato miguu ya hao waliosulubiwa ivunjwe na miili yao iondolewe.
32Antunchi le ketani avile, ai phagle le punrhe le pervoneske, porme le kolavreske kai sas karfome lesa.
32Basi, askari walikwenda, wakaivunja miguu ya yule mtu wa kwanza na yule wa pili ambao walikuwa wamesulubiwa pamoja na Yesu.
33Numa kana pashile pasha Jesus, ai dikhle ke vunzhe mulo sas, chi phagle leske punrhe.
33Lakini walipomfikia Yesu waliona kwamba alikwisha kufa, na hivyo hawakumvunja miguu.
34Numa iek andal ketani kerdia gropa ande lesko prashav la sabiasa, ai strazo anklisto rat avri ai pai.
34Lakini askari mmoja alimtoboa ubavuni kwa mkuki, na mara ikatoka damu na maji.
35O manush kai dikhlia le mothol pa kadala dieli kai kerdile, ai so mothol o chachimos si; wo zhanel ke mothol o chachimos, saxke te pachan tume.
35(Naye aliyeona tukio hilo ametoa habari zake ili nanyi mpate kuamini. Na hayo aliyosema ni ukweli, tena yeye anajua kwamba anasema ukweli.)
36Kadala dieli kerdile, saxke te kerdiol so phendia E Vorba le Devleski, chi iek kokola anda leske chi avela phaglo.
36Jambo hilo lilitendwa ili Maandiko Matakatifu yatimie: "Hapana hata mfupa wake mmoja utakaovunjwa."
37Ai ande averik E Vorba le Devleski mai phenel, "Won dikhena kodoles kai xiviarde."
37Tena Maandiko mengine yanasema: "Watamtazama yule waliyemtoboa."
38Pala kodia o Joseph andai Arimathea, kai sas ek disiplo le Jesusosko, numa chordanes ke daralas katar le Zhiduvuria, manglia katar o Pilate te sai lel o stato le Jesusosko: ai o Pilate phendia leske ke sai. Wo avilo ai lia o stato le Jesusosko.
38Baada ya hayo, Yosefu, mwenyeji wa Armathaya, alimwomba Pilato ruhusa ya kuuchukua mwili wa Yesu. (Yosefu alikuwa mfuasi wa Yesu, lakini kwa siri, maana aliwaogopa viongozi wa Wayahudi). Basi, Pilato akamruhusu. Hivyo Yosefu alikwenda, akauondoa mwili wa Yesu.
39O Nicodemus avilo, kai mai anglal avilo sas e riate ka Jesus, ai andia pashte trenda kili Mirrh ai Aloes amime andek than.
39Naye Nikodemo ambaye hapo awali alikuwa amemwendea Yesu usiku, akaja akiwa amechukua mchanganyiko wa manemane na ubani kiasi cha kilo thelathini.
40Line o stato le Jesusosko, ai vuluisarde les andek vuzho poxtan, parno ai tsode andre aromat, ke kadia si o zakono le Zhidovongo te gropon.
40Basi, waliutwaa mwili wa Yesu, wakaufunga sanda pamoja na manukato kufuatana na desturi ya Wayahudi katika kuzika.
41Ai sas iek sado pe kodo tsan kai sas O Jesus karfome; ai ande kodo sado sas iek nevo greposhevo, kai inker khonik nas thodino andre.
41Mahali hapo aliposulubiwa Yesu palikuwa na bustani, na katika bustani hiyo kulikuwa na kaburi jipya ambalo hakutiwa bado mtu yeyote ndani yake.
42Kotse thode le Jesusos ke sas O Dies O Baro le Zhidovongo mai anglal sar o Savato le Zhidovongo, ai ke o greposhevo sas pashe.
42Basi, kwa sababu ya shughuli za Wayahudi za maandalio ya Sabato, na kwa vile kaburi hilo lilikuwa karibu, wakamweka Yesu humo.