Romani: New Testament

Swahili: New Testament

John

2

1Trin dies pala kodia sas iek abiav ando gav kai bushol Cana, ando them Galilee; ai e dei le Jesusoski sas kotse.
1Siku ya tatu kulikuwa na arusi mjini Kana, mkoani Galilaya. Mama yake Yesu alikuwapo,
2Ai vi O Jesus sas akhardo peske disiplonsa ka abiav.
2naye Yesu alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake.
3Ai kana mangle mol, e dei le Jesusoski phendia leske, ma nai le mol.
3Divai ilipokwisha, mama yake akamwambia, "Hawana divai!"
4O Jesus phendia lake, "Zhuvlio, so si mashkar tute ai mande, murho chaso inker chi avilo."
4Yesu akamjibu, "Mama, usiniambie la kufanya. Saa yangu bado."
5Leski dei phenel le slugenge, "Keren so godi phenela tumenge."
5Hapo mama yake akawaambia watumishi, "Lolote atakalowaambieni, fanyeni."
6Kotse sas shov phiria chikake, thodinesas te vuzharenpe le Zhiduvuria, swako phiri sai zhalas bish tai pansh galonuria vai iek shel litre pai. (Thodinesas kotse te halaven penge vas te keren sar lenge zakono phenel.)
6Hapo palikuwa na mitungi sita ya mawe, ambayo kila mmoja uliweza kuchukua kiasi cha madebe mawili au matatu. Ilikuwa imewekwa hapo kufuatana na desturi ya Kiyahudi ya kutawadha.
7O Jesus phendia lenge, "Peren le phiria le paiesa." Line le slugi ai pherde le zhando mui.
7Yesu akawaambia, "Ijazeni mitungi hiyo maji." Nao wakaijaza mpaka juu.
8O Jesus phendia lenge, "Len akana ai angeren ka o dat la shako kai kerdia o abiav," ai ingerde leske.
8Kisha akawaambia, "Sasa choteni mkampelekee mkuu wa karamu."
9Kana o dat le shako zumadia o pai kai kerdilosas mol, wo chi zhanelas katar avelas kodia mol, numa le slugi kai linesas anda kodo pai zhanenas mishto. Porme o dat la shako akhardia le manushes kai ansurilaspe.
9Mkuu wa karamu alipoonja hayo maji, kumbe yalikuwa yamegeuka kuwa divai. Yeye hakujua ilikotoka, (lakini wale watumishi waliochota maji walijua). Mkuu wa karamu akamwita bwana arusi,
10Ai phenel leske, "Swako manush del e mai lashi mol mai anglal; ai porme kana savorhe machile, del e mai chorhi, numa tu garadian e lashi mol zhi akana."
10akamwambia, "Kila mtu huandaa divai nzuri kwanza hata wakisha tosheka huandaa ile hafifu. Lakini wewe umeiweka divai nzuri mpaka sasa!"
11Kado sas o pervo miraklo kai kerdia O Jesus ando gav kai bushol Cana ando them Galilee. Kotse sikadia pesko putiera, ai leski disipluria pachaiepe ande leste.
11Yesu alifanya ishara hii ya kwanza huko Kana, Galilaya, akaonyesha utukufu wake; nao wanafunzi wake wakamwamini.
12Pala kodia O Jesus, ai leski dei, ai leske phral, ai leske disipluria gele lesa ando foro kai bushol Capernaum, ai beshle xantsi dies.
12Baada ya hayo, Yesu alishuka pamoja na mama yake, ndugu zake na wanafunzi wake, wakaenda Kafarnaumu ambako walikaa kwa siku chache.
13Ai o dies O Baro le Zhidovongo pasholas, ai O Jesus gelo ando Jerusalem.
13Sikukuu ya Wayahudi ya Pasaka ilikuwa imekaribia; hivyo Yesu akaenda Yerusalemu.
14Ai arakhlia ande tampla manushen kai bichinenas guruven ai bakrian ai gulumburia, ai vi manush kai parhuvenas love beshenas kotse.
14Hekaluni aliwakuta watu wakiuza ng'ombe, kondoo na njiwa, na wavunja fedha walikuwa wamekaa kwenye meza zao.
15Ai kana O Jesus lia shelo ai kerdia peske bicho anda leste, wo gonisardia savorhen avri andai tampla ai vi le bakrian, ai le guruven, ai dia muial le skafidia kodolenge kai parhuvenas le love.
15Akatengeneza mjeledi wa kamba, akawafukuza wote nje ya Hekalu pamoja na kondoo na ng'ombe wao, akazimwaga sarafu za wenye kuvunja fedha na kupindua meza zao.
16Ai phendia le manushenge kai bichinenas le gulumbon, "Len kadala dieli katsar! Na keren anda kher murhe Dadesko bazari."
16Akawaambia wale waliokuwa wanauza njiwa, "Ondoeni vitu hivi hapa. Msiifanye nyumba ya Baba yangu kuwa soko!"
17Ai leske disipluria dinepe goji ke ramomesas ande Vorba le Devleski, "De drago kai si mange cho kher, Devla, phabol ande mande sar ek iag."
17Wanafunzi wake wakakumbuka kwamba Maandiko yasema: "Upendo wangu kwa nyumba yako waniua."
18Porme le Zhiduvuria phushle les, "Che miraklo sai keres tu te sikaves amenge, ke si tu putiera te keres kadia?"
18Baadhi ya Wayahudi wakamwuliza Yesu, "Utafanya muujiza gani kuonyesha kwamba unayo haki kufanya mambo haya?"
19O Jesus phendia lenge, "Peraven kadia tampla, ai ande trin dies te vazdav la."
19Yesu akawaambia, "Vunjeni Hekalu hili, nami nitalijenga kwa siku tatu."
20Le Zhiduvuria phende leske, "Trobulsardia shtarvardesh tai shov bersh te keras kadia tampla! Ai tu phenes ke ande trin dies vazdes la palpale?"
20Hapo Wayahudi wakasema, "Hekalu hili lilijengwa kwa muda wa miaka arobaini na sita. Je, wewe utalijenga kwa siku tatu?"
21Numa O Jesus delas duma pai tampla peske statosko.
21Lakini Yesu alikuwa anaongea juu ya Hekalu ambalo ni mwili wake.
22Sa anda kodia O Jesus zhuvindisailo andai martia ka traio, leske disipluria dine pe goji ke phendiasas kadia, ai won pachanaspe o ramomos ai e vorba kai phendiasas O Jesus.
22Basi, alipofufuliwa kutoka wafu, wanafunzi wake walikumbuka kwamba alikuwa amesema hayo, wakaamini Maandiko Matakatifu na yale maneno aliyokuwa akisema Yesu.
23Ande vriama kai O Jesus sas ando Jerusalem ka dies O Baro le Zhidovongo, but narodo pachanaspe ando lesko anav, kana dikhenas le mirakluria kai kerdia.
23Yesu alipokuwa Yerusalemu kwa sikukuu ya Pasaka, watu wengi walimwamini walipoona ishara alizozifanya.
24Numa O Jesus chi jinelas pe lende, ke wo zhanelas len savorhen.
24Lakini Yesu hakuwa na imani nao kwa sababu aliwajua wote.
25Ai chi trobulas vari kon te phenel leske pa manush; ke wo zhanelas korkorho si si ando manush.
25Hakuhitaji kuambiwa chochote juu ya watu, maana aliyajua barabara mambo yote yaliyomo mioyoni mwao.