1Anda gor sas E Vorba, ai E Vorba sas le Devlesa, ai E Vorba sas O Del.
1Hapo Mwanzo, Neno alikuwako; naye alikuwa na Mungu, naye alikuwa Mungu.
2Wo anda gor sas le Devlesa.
2Tangu mwanzo Neno alikuwa na Mungu.
3Wo kerdia swako fielo, ai kanchi so kerdilo nas kerdo bi leste.
3Kwa njia yake vitu vyote viliumbwa; hakuna hata kiumbe kimoja kilichoumbwa pasipo yeye.
4Ande leste sas o traio, ai o traio sas e vediara le manushenge.
4Yeye alikuwa chanzo cha uhai na uhai huo ulikuwa mwanga wa watu.
5E vediara strefial ando tuniariko, ai o tuniariko shoxar chi mudardia e vediara.
5Na mwanga huo huangaza gizani, nalo giza halikuweza kuushinda.
6Sas iek manush tradino katar O Del, lesko anav sas Iovano.
6Mungu alimtuma mtu mmoja jina lake Yohane,
7Avilo o Iovano te phenel le manushenge pai vediara. Kashke savorhe te pachanape pala leste.
7ambaye alikuja kuwaambia watu juu ya huo mwanga. Alikuja ili kwa ujumbe wake watu wote wapate kuamini.
8O Iovano nas e vediara, numa wo sas tradino te phenel pai vediara.
8Yeye hakuwa huo mwanga, ila alikuja tu kuwaambia watu juu ya huo mwanga.
9Kadia chachi vediara avel ande lumia te del vediara ka swako manush kai avela ande lumia.
9Huu ndio mwanga halisi, mwanga unaokuja ulimwenguni, na kuwaangazia watu wote.
10Wo sas ande lumia, ai e lumia sas kerdi pala leste numa e lumia chi zhanglia les.
10Basi, Neno alikuwako ulimwenguni; na kwa njia yake ulimwengu uliumbwa, lakini ulimwengu haukumtambua.
11Wo avilo ka peske, ai leske chi premisarde les.
11Alikuja katika nchi yake mwenyewe, nao walio wake hawakumpokea.
12Uni premisarde les ai pachaiepe ande leste; wo dia len e putiera te aven shave Devleske.
12Lakini wale wote waliompokea na kumwamini, hao aliwapa uwezo wa kuwa watoto wa Mungu.
13Kodola kai arakhadile, na anda rat, chi andai voia le statoski, chi andai voia le manusheski, numa katar O Del.
13Hawa wamekuwa watoto wa Mungu si kwa uwezo wa kibinadamu, wala kwa nguvu za kimwili, wala kwa mapenzi ya mtu, bali Mungu mwenyewe ndiye baba yao.
14Ai E Vorba kerdile stato ai beshelas mashkar amende. Ame dikhliam lesko barimos, pherdo mishtimasa ai chachimasa, kadia sas o barimos le ieke Shavesko kai avilo katar O Dat.
14Naye Neno akawa mwanadamu, akakaa kwetu. Nasi tumeuona utukufu wake, utukufu wake yeye aliye Mwana wa pekee wa Baba; amejaa neema na ukweli.
15O Iovano phendia pa leste, phenelas, "Kado si kai phendem, 'Wo avela pala mande, numa wo si mai baro mandar, ke wo sas mai anglal arakhadilem.'"
15Yohane aliwaambia watu habari zake, akasema kwa sauti, "Huyu ndiye niliyemtaja wakati niliposema: Anakuja mtu mmoja baada yangu ambaye ni mkuu kuliko mimi, maana alikuwako kabla mimi sijazaliwa."
16Ai ame savorhe liam anda lesko baro lashimos. Mishtimos pe mishtimos.
16Kutokana na ukamilifu wake sisi tumepokea neema mfululizo.
17Ke o zakono sas dino katar o Moses, numa o mishtimos ai o chachimos avilo katar O Jesus Kristo.
17Maana Mungu alitoa Sheria kwa njia ya Mose, lakini neema na kweli vimekuja kwa njia ya Kristo.
18Khonik shoxar chi dikhlia le Devles, ferdi o iek Shav kai si le Dadesa, ai wo si kai kerdia te zhanas les.
18Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wowote ule. Mwana wa pekee aliye sawa na Mungu ambaye ameungana na Baba, ndiye aliyetujulisha habari za Mungu.
19Ai kodia si o ramomos le Iovanosko, le Zhiduvuria trade le bare rasha ai le Levituria andai Jerusalem te phushen les,
19Huu ndio ushahidi Yohane alioutoa wakati viongozi wa Wayahudi kule Yerusalemu walipowatuma makuhani wa Walawi kwake wamwulize: "Wewe u nani?"
20"Tu kon san?" Ai wo phendias lenge ai chi garadia kanch, phenelas, "Chi sim O Kristo."
20Yohane hakukataa kujibu swali hilo, bali alisema waziwazi, "Mimi siye Kristo."
21Ai won phushen les, "Kon san tu, Tu san o Elijah?" ai wo phendia, "Chi sim!" Antunchi won phushle, "Tu san o profeto?" ai wo phendia, "Nichi."
21Hapo wakamwuliza, "Basi, wewe ni nani? Je, wewe ni Eliya?" Yohane akajibu, "La, mimi siye." Wakamwuliza, "Je, wewe ni yule nabii?" Yohane akawajibu, "La!"
22Porme phende leske, "Kon san tu? Te das atweto kodolenge kai tradine ame. So phenes pa tute, kon san?"
22Nao wakamwuliza, "Basi, wewe ni nani? Wasema nini juu yako mwenyewe? Tuambie, ili tuwapelekee jibu wale waliotutuma."
23O Iovano phendia, "Me sim o glaso kodoleske kai tsipil ande pusta, "Vorton o drom le Devlesko" sar phendia o Isaiah o profeto."
23Yohane akawajibu, "Mimi ndiye yule ambaye nabii Isaya alisema habari zake: Sauti ya mtu imesikika jangwani: Nyoosheni njia ya Bwana."
24Won kai sas tradine, sas anda le Farizeanuria.
24Hao watu walikuwa wametumwa na Mafarisayo.
25Ai mai phushle les, phenenas, "Antunchi, sostar boles te chi san e Messiah vai chi o Elijah, vai chi o profeto?"
25Basi, wakamwuliza Yohane, "Kama wewe si Kristo, wala Eliya, wala yule nabii, mbona wabatiza?"
26O Iovano dia le atweto, phenelas "Me bolav ando pai, numa mashkar tumende, si vari kon kai chi zhanen.
26Yohane akawajibu, "Mimi nabatiza kwa maji, lakini yuko mmoja kati yenu, msiyemjua bado.
27Wo si kai avela pala mande, chi sim dosta lasho te phutrav le doria leske papuchenge."
27Huyo anakuja baada yangu, lakini mimi sistahili hata kumfungua kamba za viatu vyake."
28Kadala dieli kerdionas ando Bethany inchal o Jordan, kai o Iovano bolelas.
28Mambo haya yalifanyika huko Bethania, ng'ambo ya mto Yordani ambako Yohane alikuwa anabatiza.
29Pe terharin o Iovano dikhlia O Jesus sar avelas leste, ai phendia, Dikh! O Bakriorho le Devlesko, kai lel e bezex le lumiako!
29Kesho yake, Yohane alimwona Yesu akimjia, akasema, "Huyu ndiye Mwana-kondoo wa Mungu aondoaye dhambi ya ulimwengu!
30Pa kado si kai phendem, "Pala mande avel iek manush kai si mai baro mandar, ke wo sas mai anglal mandar."
30Huyu ndiye niliyesema juu yake: Baada yangu anakuja mtu mmoja aliye mkuu zaidi kuliko mimi, maana alikuwako kabla mimi sijazaliwa!
31Me chi zhanavas les; numa avilem te bolav le paiesa, kashke sai Israel te zhanel les."
31Mimi mwenyewe sikumfahamu, lakini nimekuja kubatiza kwa maji ili watu wa Israeli wapate kumjua."
32Porme o Iovano phendia, "Dikhlem O Swunto Duxo sar hulelas anda cheri sar iek gulumbo, ai beshlo pe leste.
32Huu ndio ushahidi Yohane alioutoa: "Nilimwona Roho akishuka kama njiwa kutoka mbinguni na kutua juu yake.
33Ai chi zhanavas les, numa kodo kai tradia ma te bolav ando pai, phendia mange, "Pe kodo kai dikhesa O Swunto Duxo te hulela, ai te beshela pe leste, kodo si kai bolel le Swuntone Duxosa."
33Mimi sikumjua, lakini yule aliyenituma nikabatize watu kwa maji alikuwa ameniambia: Mtu yule utakayemwona Roho akimshukia kutoka mbinguni na kukaa juu yake, huyo ndiye anayebatiza kwa Roho Mtakatifu.
34Ai dikhlem, ai phenav tumenge ke wo si O Shav le Devlesko."
34Mimi nimeona na ninawaambieni kwamba huyu ndiye Mwana wa Mungu."
35Pe terharin o Iovano mai sas pe kodo than duiensa anda leske disipluria.
35Kesho yake, Yohane alikuwa tena mahali hapo pamoja na wanafunzi wake wawili.
36Kana dikhlias O Jesus nakhelas, wo phendia, "Katse si O Bakrorho le Devlesko!"
36Alipomwona Yesu akipita akasema, "Tazameni! Huyu ndiye Mwana-kondoo wa Mungu."
37Le dui disipluria ashunenas le vorbi kai phendia, ai linepe pala Jesus.
37Hao wanafunzi walimsikia Yohane akisema maneno hayo, wakamfuata Yesu.
38Porme O Jesus boldinisailo ai dikhlia ke avenas pala leste, ai phushlia len, "So roden?" Ai won dine atweto, "Xazhainona, kai beshes?" (xazhainono znachil o manush kai sicharel).
38Basi, Yesu aligeuka, na alipowaona hao wanafunzi wanamfuata, akawauliza, "Mnatafuta nini?" Nao wakamjibu, "Rabi (yaani Mwalimu), unakaa wapi?"
39Phendia lenge, "Aven ai dikhen." Won avile ai dikhle kai beshelas, beshlo lesa kodo dies. Kodo sas pala miazutso karing le shtar chasuria.
39Yesu akawaambia, "Njoni, nanyi mtaona." Hao wanafunzi wakamfuata, wakaona mahali alipokuwa anakaa, wakashinda naye siku hiyo. Ilikuwa yapata saa kumi jioni.
40O Andre, phral le Simonosko Petri, sas iek andal dui manush kai ashundia so phendia o Iovano, ai liape pala Jesus.
40Andrea, nduguye Simoni Petro, alikuwa mmoja wa hao wawili waliokuwa wamemsikia Yohane akisema hivyo, wakamfuata Yesu.
41Strazo o Andre arakhlia peske phrales o Simon, ai phendia leske, "Arakhliam e Messiah,," (E vorba znachil "Kristo.")
41Andrea alimkuta kwanza Simoni, ndugu yake, akamwambia, "Tumemwona Masiha" (maana yake Kristo).
42Ai o Andre angerdia o Simon karing O Jesus. Kana O Jesus dikhlia pe leste, phendia, "Tu san o Simon o shav le Iovanosko, te aves akhardo Cephas." O anav Cephas znachil Petri vai bax.
42Kisha akampeleka Simoni kwa Yesu. Naye Yesu akamtazama Simoni akasema, "Wewe ni Simoni mwana wa Yohane. Sasa utaitwa Kefa." (maana yake ni Petro, yaani, "Mwamba.")
43Pe terharin O Jesus manglia te zhal ando them kai busholas Galilee. Wo arakhlia le Filipos, ai phendia leske, "Le tu pala mande." '
43Kesho yake Yesu aliamua kwenda Galilaya. Basi, akamkuta Filipo, akamwambia, "Nifuate."
44O Filip sas anda foro, kai busholas Bethsaida, o foro kai beshle o Andre ai o Petri.
44Filipo alikuwa mwenyeji wa Bethsaida, mji wa akina Andrea na Petro.
45O Filip arakhlia le Nathanael ai phendia leske, "Arakhliam kodoles kai o Moses ai le profeturia ramosarde ande klishka le zakonosko, wo si O Jesus andai Nazareth, o shav le Josefosko."
45Naye Filipo akamkuta Nathanieli, akamwambia, "Tumemwona yule ambaye Mose aliandika juu yake katika kitabu cha Sheria, na ambaye manabii waliandika habari zake, yaani Yesu Mwana wa Yosefu, kutoka Nazareti."
46O Nathanael phendia leske, "Sai avel anda Nazareth vari so lasho?" O Filip phendia leske, "Aidi ai Dikh."
46Naye Nathanieli akamwuliza Filipo, "Je, kitu chema chaweza kutoka Nazareti?" Filipo akamwambia, "Njoo uone."
47O Jesus dikhlia o Nathanael avelas leste, ai phenel pa leste, "Dikh! Iek chacho Zhidovo. Nai chi iek atsaimos ande leste!"
47Yesu alipomwona Nathanieli akimjia alisema juu yake, "Tazameni! Huyo ni Mwisraeli halisi: hamna hila ndani yake."
48O Nathanael phendia leske, "Katar zhanes ma tu?" O Jesus phendia leske, "Mai anglal o Filip akhardia tu, kana sanas telal pruing le figenge, Me dikhlem tu."
48Naye Nathanieli akamwuliza, "Umepataje kunijua?" Yesu akamwambia, "Ulipokuwa chini ya mtini hata kabla Filipo hajakuita, nilikuona."
49Porme o Nathanael phendia leske, "Gazda, tu san O Shav le Devlesko. Tu san O Amperato le Zhidovongo."
49Hapo Nathanieli akamwambia, "Mwalimu, wewe ni Mwana wa Mungu. Wewe ni Mfalme wa Israeli!"
50O Jesus phendia leske, "Anda kodia ke phendem tuke, "Dikhlem tu telai pruing le figenge, tu pachas? Numa dikhesa mai bare dieli sar kadala."
50Yesu akamwambia, "Je, umeamini kwa kuwa nimekwambia kwamba nilikuona chini ya mtini? Utaona makubwa zaidi kuliko haya."
51Phenel leske, Chachimasa, chachimasa, phenav tumenge chachimos, dikhena o cheri phuterdiol, ai le angeluria le Devleske anklen ai hulen tele po Shav le Manushesko.
51Yesu akaendelea kusema, "Nawaambieni kweli, mtaona mbingu zinafunguka na malaika wa Mungu wakipanda na kushuka juu ya Mwana wa Mtu."