1Kana phuterdilo o dies po pervo dies le kurkoske, avile ka greposhevo te angeren le vuloia ai duxuria kai lasharde sas.
1Jumapili, alfajiri na mapema, wale wanawake walikwenda kaburini wakichukua yale manukato waliyotayarisha.
2Numa dikhle e bax spidias palpale katar o greposhevo.
2Walikuta lile jiwe limeviringishwa mbali na kaburi.
3Gele andre, numa chi arakhle o stato le Devlesko, Jesus.
3Walipoingia ndani, hawakuona mwili wa Bwana Yesu.
4Sar chi zhanenas so kerdilia, dikhle dui manushen pasha lende kai sas vuriarde andel tsalia kai strefianas;
4Walipokuwa bado wanashangaa juu ya jambo hilo, mara watu wawili waliovaa mavazi yenye kung'aa sana, wakasimama karibu nao.
5Daraile, shudepe tele le mosa pe phuv, le manush phende lenge, "Sostar roden mashkar le mule kodoles kai si zhuvindo?
5Hao wanawake wakaingiwa na hofu, wakainama chini. Ndipo wale watu wakawaambia, "Kwa nini mnamtafuta aliye hai kati ya wafu?
6Nai katse, numa wushtilo! Seren tume sar delas duma tumensa kana sas tumensa inker ande Galilee, phenelas,
6Hayuko hapa; amefufuka. Kumbukeni aliyowaambieni alipokuwa kule Galilaya:
7"O Shav le Manushesko te avel dino andel vas le bezexalenge, ai avela karfosardo po trushul, ai te zhuvindila o trito dies."
7Ni lazima Mwana wa Mtu atolewe kwa watu waovu, nao watamsulubisha, na siku ya tatu atafufuka."
8Ai won dinepe goji leske vorbi,
8Hapo wanawake wakayakumbuka maneno yake,
9ai avile palpale khere katar o greposhevo, ai phende sa kodola dieli le desh u iek disiplonge, ai le kolavrenge.
9wakarudi kutoka kaburini, wakawapa mitume wale kumi na mmoja na wengine habari za mambo hayo yote.
10Kodia kai phendia kodola dieli le slugenge sas e Maria Magdalena, ai e Ioanna, ai e Maria e dei le Iakovoske, ai le kolaver zhuvlia kai sas lensa.
10Hao waliotoa habari hizo kwa mitume ni: Maria Magdalene, Yoana na Maria mama wa Yakobo, pamoja na wanawake wengine walioandamana nao.
11Numa le disipluria gindinas ke so mothonas kodala zhuvlia nai chaches, ai chi pachaiele.
11Mitume waliyachukua maneno hayo kama yasiyo na msingi, hivyo hawakuamini.
12Antunchi o Petri wushtilo opre ai nashlo ka greposhevo; bandilo tele, ai dikhlia ferdi le tsoluria, ai gelotar khere, ai chudisailo anda so kerdilia.
12Lakini Petro alitoka, akaenda mbio hadi kaburini. Alipoinama kuchungulia ndani, akaiona tu ile sanda. Akarudi nyumbani huku akiwa anashangaa juu ya hayo yaliyotokea.
13Eta, sa kodo dies dui anda lende gele ande gav kai busholas Emmaus, kai sas desh u iek kilometeria vai efta maili anda Jerusalem,
13Siku hiyohiyo, wawili kati ya wafuasi wake Yesu wakawa wanakwenda katika kijiji kimoja kiitwacho Emau, umbali wa kilomita kumi na moja kutoka Yerusalemu.
14ai phenenas mashkar pende pa so godi kerdilia.
14Wakawa wanazungumza juu ya hayo yote yaliyotukia.
15Sar denas duma, O Jesus pashilo pasha lende, ai phirelas lensa.
15Walipokuwa wakizungumza na kujadiliana, Yesu mwenyewe akatokea, akatembea pamoja nao.
16Numa lenge iakha nashti te dikhenas ke wo si.
16Walimwona kwa macho, lakini hawakumtambua.
17Ai phendia lenge, "Pa soste divinin ando tumaro phirimos nekazosa?"
17Akawauliza, "Mnazungumza nini huku mnatembea?" Nao wakasimama kimya, nyuso zao wamezikunja kwa huzuni.
18Iek anda lende, kai busholas Cleopas, phendia leske, "Tu san ek streino ando Jerusalem, ai chi zhanes so kerdilia kadala dies."
18Mmoja, aitwaye Kleopa, akamjibu, "Je, wewe ni mgeni peke yako Yerusalemu ambaye hujui yaliyotukia huko siku hizi?"
19Ai O Jesus phendia lenge, "So kerdilia?" Ai won phende leske, "Pa Jesus anda Nazareth, kai sas iek profeto, kai sas les bari putiera kana kerelas peske bucha, ai kana divinilas angla Del ai sa le manushenge;
19Naye akawajibu, "Mambo gani?" Wao wakamjibu, "Mambo yaliyompata Yesu wa Nazareti. Yeye alikuwa nabii mwenye uwezo wa kutenda na kufundisha mbele ya Mungu na mbele ya watu wote.
20Ai sar amare bare kai poronchin dine les te den les kris, te karfon les po trushul.
20Makuhani na watawala wetu walimtoa ahukumiwe kufa, wakamsulubisha.
21Ame gindisas ke wo sas kai sas te skepil o Israel; numa sa kadale dielensa, adies si o trito dies kai kadala dieli kerdile.
21Lakini sisi tulitumaini kwamba yeye ndiye angeikomboa Israeli. Zaidi ya hayo yote, leo ni siku ya tatu tangu mambo hayo yalipotendeka.
22Ai uni zhuvlia ande amare chudisarde amen, chaches ke won gele diminiatsi ka greposhevo;
22Tena, wanawake wengine wa kwetu wametushtua. Walikwenda kaburini mapema asubuhi,
23Numa chi arakhle lesko stato, avile te phenen amenge, ke angeluria sikadile lenge, ai phende lenge ke zhuvindolo.
23wasiukute mwili wake. Wakarudi wakasema kwamba walitokewa na malaika waliowaambia kwamba alikuwa hai.
24Uni kai sas amensa gele ka greposhevo, ai arakhle le dieli sar phende sas kodola zhuvlia; numa chi dikhle le Jesusos."
24Wengine wetu walikwenda kaburini wakashuhudia yale waliyosema hao wanawake; ila yeye hawakumwona."
25Antunchi O Jesus phendia lenge, "Tume prosto manush. Ai kai o ilo lungo lo te pachal so godi phende le profeturia.
25Kisha Yesu akawaambia, "Mbona mu wapumbavu kiasi hicho na mioyo yenu ni mizito hivyo kusadiki yote yaliyonenwa na manabii?
26Pate chi trobulas O Kristo te chinuil kadia, ai te zhal ande pesko barimos?"
26Je, haikumpasa Kristo kuteswa, na hivyo aingie katika utukufu wake?"
27Porme phendia lenge so sas phendo pa leste ande Vorba le Devleski, de katar o Moses zhi ka sa le profeturia.
27Akawafafanulia mambo yote yaliyomhusu yeye katika Maandiko Matakatifu kuanzia Mose hadi manabii wote.
28Kana aresle pasha gav kai zhanas; O Jesus kerdia sar ke mangelas te zhal mai dur.
28Walipokikaribia kile kijiji walikokuwa wanakwenda, Yesu akafanya kana kwamba anaendelea na safari;
29Numa phende leske, "Besh amensa; ke perel e riat, ai o dies tsigniol." Ai gelo te beshel lensa.
29lakini wao wakamsihi wakisema, "Kaa pamoja nasi, maana kunakuchwa, na usiku unakaribia." Basi, akaingia kijijini, akakaa pamoja nao.
30Sar sas lensa kai skafidi, lia o manrho, ai kana rhugisailo, phaglia o manrho, ai dia le.
30Alipoketi kula chakula pamoja nao, akachukua mkate, akaubariki, akaumega, akawapa.
31Antunchi lenge iakha phuterdile, ai prinzharde les; numa strazo bilailo.
31Mara macho yao yakafumbuliwa, wakamtambua; lakini yeye akatoweka kati yao.
32Ai denaspe duma won de won, "Nas sar iek iag kai phabolas anda amaro ilo; kana delas duma amensa pa drom, ai kana phenelas amenge pai Vorba le Devleski?"
32Basi, wakaambiana, "Je, mioyo yetu haikuwa inawaka ndani yetu wakati alipokuwa anatufafanulia Maandiko Matakatifu kule njiani?"
33Wushtilo opre strazo, ai gele palpale ande Jerusalem, ai arakhle le kolaver desh u iek disipluria chidine andek than, ai le kolaver kai sas lensa.
33Wakaondoka saa ileile, wakarudi Yerusalemu: wakawakuta wale mitume kumi na mmoja na wale wengine waliokuwa pamoja nao, wamekusanyika
34Phenenas, "Chaches O Del zhuvindisailo, ai sikadilo le Simonoske."
34wakisema, "Hakika Bwana amefufuka, amemtokea Simoni."
35Ai phenenas so kerdilia lensa pa drom, ai sar prinzharde les kana phagelas o manrho.
35Basi, hao wafuasi wawili wakawajulisha yale yaliyowapata njiani, na jinsi walivyomtambua katika kumega mkate.
36Sar denas duma, O Jesus avilo mashkar lende, ai phendia lenge, "E pacha te avel tumensa,"
36Wanafunzi wote wawili walipokuwa wakiwaambia hayo, Yesu mwenyewe akasimama kati yao, akawaambia "Amani kwenu."
37Won daraile ai pherde dar sas, won gindinas ke dikhle ieke duxos,
37Wakashtuka na kushikwa na hofu wakidhani wameona mzimu.
38ai wo phendia lenge, "Sostar daran? Ai sostar kasavendar ginduria si tume ande tumaro ile?
38Lakini yeye akawaambia, "Kwa nini mnafadhaika? Mbona mnakuwa na mashaka mioyoni mwenu?
39Dikhen murhe vas ai murhe punrhe, me sim, azban ma, ai dikhen! Ke o duxo nai les, chi morchi ai chi kokola, sar dikhen tume ke si man."
39Angalieni mikono na miguu yangu, ya kwamba ni mimi mwenyewe. Nipapaseni mkanione, maana mzimu hauna mwili na mifupa kama mnionavyo."
40Sar phenelas kodo divano, sikadia lenge peske vas ai peske punrhe.
40Baada ya kusema hayo, akawaonyesha mikono na miguu.
41Ande pengo raduimos inker chi pachanas, ai chudinaspe, ai wo phendia lenge, "Si tume vari so te xav?"
41Wakiwa bado katika hali ya kutosadiki kwa sababu ya furaha yao, na wakiwa wanastaajabu, akawauliza, "Mnacho chakula chochote hapa?"
42Won dine les masho peko, ai avjin.
42Wakampa kipande cha samaki wa kuokwa.
43Lia ai xalia angla lende.
43Akakichukua, akala, wote wakimwona.
44Ai phendia lenge, "Kadala dieli kai phenavas tumenge, kana simas inker tumensa kai trobulas te kerdiol, so godi si ramome pa mande anda zakono le Mosesosko, ai andel le profetonge, ai andel Psalms."
44Halafu akawaambia, "Hii ndiyo maana ya maneno niliyowaambia nilipokuwa pamoja nanyi: kwamba ilikuwa lazima kukamilisha yote yaliyoandikwa juu yangu katika Sheria ya Mose na katika vitabu vya manabii na katika kitabu cha Zaburi."
45Antunchi phuterdia lengo ilo te sai haliaren E Vorba le Devleski.
45Kisha, akaziangazia akili zao ili wapate kuelewa Maandiko Matakatifu.
46Ai phendia lenge, "Kadia si ramome, ke O Kristo chinuila, ai zhuvindila andai martia o trito dies;
46Akawaambia, "Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na siku ya tatu atafufuka kutoka wafu,
47Ai ke o keimos ai o iertimos le bezexxengo avela phendo ande lesko anav sa le themenge, mai anglal ande Jerusalem.
47na kwamba ni lazima, kwa jina lake, mataifa yote kuanzia na Yerusalemu yahubiriwe juu ya kutubu na kusamehewa dhambi.
48Tume san marturia pe kadala dieli.
48Ninyi ni mashahidi wa mambo hayo.
49Ashun! Tradava pe tumende so murho Dat shinadia, numa tume beshen ando foro Jerusalem,zhi kai aven pherde putiera kai avel katar opral."
49Nami mwenyewe nitawapelekeeni yule ambaye Baba aliahidi kumtuma, lakini ngojeni huku mjini mpaka mtakapopewa ile nguvu itokayo juu."
50Angerdia le karing e Bethani; ai vazdia le vas, ai swuntsosardia le.
50Kisha akawaongoza nje ya mji hadi Bethania, akainua mikono yake juu, akawabariki.
51Ande kodia, kai swuntholas le, durilo lendar, ai gelotar ando rho.
51Alipokuwa anawabariki, akawaacha; akachukuliwa mbinguni.
52Won rhugisaile leste, ai geletar palpale ande Jerusalem bare raduimasa;
52Wao wakamwabudu, wakarudi Yerusalemu wakiwa na furaha kubwa:
53Ai sagda sas ande tampla, bariarenas o anav le Devlesko ai swunthonas le Devles. Amen
53wakakaa muda wote Hekaluni wakimsifu Mungu.