1Wushtilo savorhe ai ningerde les ka Pilate.
1Kisha, wote kwa jumla, wakasimama, wakampeleka Yesu mbele ya Pilato.
2Ai dosharenas les, phenenas, "Kado manush rimol amaro them ai vazdelpe o narodo pe amende, ai phenel le narodoske te na pochinen ka Caesar e taksa, ai phenelas ke wo si O Kristo, ek amperato."
2Wakaanza kumshtaki wakisema: "Tulimkuta mtu huyu akiwapotosha watu wetu, akipinga kulipa kodi kwa Kaisari na kujiita ati yeye ni Kristo, Mfalme."
3O Pilate phushel les, "San tu o amperato le Zhidovongo?" O Jesus phendia leske, "Tu mothos."
3Pilato akamwuliza Yesu, "Wewe ni Mfalme wa Wayahudi?" Yesu akamjibu, "Wewe umesema."
4O Pilate phendia ka le bare rashange ai le narodoske, "Me chi arakhav chi iek dosh ande kado manush.
4Pilato akawaambia makuhani wakuu na umati wa watu, "Sioni kosa lolote katika mtu huyu."
5Numa mai xoliariko sas won, phenenas, "Kado manush vazdel o narodos, ai sicharel kodolen kai si ande Judah, zhal de Galilee ai de katsar naichidisardia.
5Lakini wao wakasisitiza wakisema: "Anawachochea watu kwa mafundisho yake katika nchi yote ya Yudea; alianza Galilaya, na sasa yuko hapa."
6Kana o Pilate ashundia e vorba "Galilee," phushlia, "Kodo manush sas Galilean?"
6Pilato aliposikia hayo, akauliza, "Je, mtu huyu ni mwenyeji wa Galilaya?"
7Kana ashundia ke O Jesus sas andai Galilee ai ke o Herod poronchilas ande Galilee, tradia les ka Herod. O Herod sas ande Jerusalem ande kodia vriama.
7Alipojua kwamba Yesu alikuwa chini ya utawala wa Herode, akampeleka kwa Herode, ambaye wakati huo alikuwa Yerusalemu.
8Ai kana o Herod dikhlia O Jesus, raduisailo; ke demult mangelas te dikhel les, ke ashundia but vorbi pa leste; ai mangelas te dikhel les te kerel mirakluria angla leste.
8Herode alifurahi sana alipomwona Yesu. Alikuwa amekwisha sikia habari zake, na hivyo alikuwa anatazamia kwa muda mrefu kumwona kwa macho yake mwenyewe. Zaidi ya hayo, alikuwa anatumaini kumwona Yesu akitenda mwujiza.
9O Herod phushlia but vorbi katar o Jesusos, numa O Jesus chi phendia leske kanchi.
9Basi, akamwuliza maswali mengi kwa muda mrefu, lakini Yesu hakumjibu neno.
10Ai le bare rasha ai le Gramnoturia kotse sas, ai thonas dosh pe leste zurales.
10Makuhani wakuu na walimu wa Sheria wakajitokeza mbele, wakatoa mashtaka yao kwa nguvu sana.
11Ai o Herod peske ketanensa kerenas zhungales le Jesusosa, ai marenas mui lestar, ai dia pe leste iek rhocha shukar, ai pale tradia les ka Pilate.
11Basi, herode pamoja na maaskari wake, wakamwaibisha Yesu na kumfanyia mzaha; kisha wakamvika vazi la kifalme, wakamrudisha kwa Pilato.
12Sa kodo dies o Pilate ai o Herod kerdile vortacha, kai won mai anglal sas duzhmaia iek kavreske.
12Herode na Pilato, ambao hapo awali walikuwa maadui, tangu siku hiyo wakawa marafiki.
13Ai kana o Pilate chidia le bare rashan, ai le bare kai poronchin ai le narodos andek than,
13Basi, Pilato akaitisha mkutano wa makuhani wakuu, viongozi na watu,
14phendia lenge, "Tume andian mange kakale manushes, ke buntuil le narodos, ai me phushlem lestar angla tumende, ai chi arakhlem chi iek dosh ande leste. Nai chi iek diela kai tume dosharen les;
14akawaambia, "Mmemleta mtu huyu kwangu mkisema kwamba alikuwa anawapotosha watu. Sasa sikilizeni! Baada ya kuchunguza jambo hilo mbele yenu, sikumpata na kosa lolote kuhusu mashtaka yenu juu yake.
15Ai chi o Herod chi arakhlia dosh pe leste, ke wo tradia les amende. Kado manush chi kerdia kasavestar o baio kai trobul mudardo.
15Wala si mimi tu, bali hata Herode hakuona kosa lolote, kwa maana amemrudisha kwangu. Ni dhahiri kwamba mtu huyu hakufanya chochote kinachostahili adhabu ya kifo.
16Phenav le ketanenge te maren les le bichosa, ai porme mekav les te zhaltar."
16Hivyo, nitaamuru apigwe viboko, halafu nitamwachilia."
17Ka swako pachiv sas ek zakono kai trobulas te mekel avri iekes anda temnitsa.
17Kila sikukuu ya Pasaka, ilimlazimu Pilato kuwafungulia mfungwa mmoja.
18Numa savorhen tsipinas andek than, phenenas, "Mudaren les! Mekes o Barabbas te zhaltar."
18Lakini wote wakapiga kelele pamoja: "Mwondoe huyo, utufungulie Baraba!"
19O Barabbas sas ande temnitsa kai buntuisailo sas andek foro, ai kai mudardia vari kas.
19(Baraba alikuwa ametiwa ndani kwa kusababisha uasi katika mji na pia kwa sababu ya kuua.)
20OPilate mai phendia lenge, "Meken le Jesusos te zhaltar."
20Pilato alitaka kumwachilia Yesu, hivyo akasema nao tena;
21Numa narodo tsipilas, phenelas, "Karfosar les! Karfosar les!"
21lakini wao wakapiga kelele: "Msulubishe, msulubishe!"
22O Pilate mai phendia lenge e trito data, "Savestar baio kerdia kado manush? Chi arakhlem kanch ande leste te avel mudardo: No mekava les kana avela mardo."
22Pilato akawaambia mara ya tatu, "Amefanya kosa gani? Sioni kosa lolote kwake linalomstahili auawe; kwa hiyo nitampiga viboko, halafu nimwachilie."
23Numa o narodo tsipilas mai zurales, ai mangena te karfon les. Pala pengo tsipimos o Pilate kerdia pe lende.
23Lakini wao wakazidi kupiga kelele kwa nguvu sana, kwamba Yesu ni lazima asulubiwe. Mwishowe, sauti zao zikashinda.
24O Pilate phendia, "So mangen avela pe tumaro."
24Basi, Pilato akaamua kwamba matakwa yao yatimizwe.
25Meklia kodoles kai sas ande temnitsa kai kerdiasas baio ai mudardiasas kodo kai won mangenas; numa meklia le Jesusos pe lenge vas te keren so won mangen lesa.
25Akamfungua kutoka gerezani yule waliyemtaka, ambaye alikuwa ametiwa gerezani kwa sababu ya uasi na kuua; akamtoa Yesu kwao, wamfanyie walivyotaka.
26Sar ningerenas les, line pesa ieke manushes kai busholas Simon, andak foro kai busholas Cyrene, wo avelas andai them, ai thode les te ningerel o trushul pala Jesus.
26Walipokuwa wakimpeleka, walikutana na mtu mmoja, aitwaye Simoni wa Kurene, aliyekuwa anatoka shambani. Basi, walimkamata, wakamtwika ule msalaba auchukue nyuma ya Yesu.
27Ai linepe pala leste but narodo, ai zhuvlia kai rovenas ai nekezhinas pala leste.
27Watu, umati kwa umati, walimfuata; miongoni mwao wakiwemo wanawake waliokuwa wanaomboleza na kumlilia.
28O Jesus boldiape karing kodola zhuvlia, ai phendia, "Sheiale anda Jerusalem, na roven pe mande, numa roven pe tumende, ai pe tumare glate.
28Yesu akawageukia, akasema, "Enyi kina mama wa Yerusalemu! Msinililie mimi, ila lieni kwa ajili yenu wenyewe na kwa ajili ya watoto wenu.
29Ashun! Le diesa avena kai phenenas, "Raduime kodala zhuvlia kai nashti aven le glate, kodala kai shoxar nas le glate, ai kodala kai shoxar chi dine chuchi."
29Maana, hakika siku zitakuja ambapo watasema: Heri yao wale walio tasa, ambao hawakupata kuzaa wala kunyonyesha watoto!
30Antunchi phenena le plaienge, "Peren pe amende;" ai phenena le plaiorhange, "Garaven ame."
30Wakati huo, ndipo watu wataanza kuiambia milima: Tuangukieni! na vilima, Tufunikeni!
31Ke te kerena kadia le khashtensa kai si zeleno, so kerena kana si shuko?"
31Kwa maana, kama watu wanautendea mti mbichi namna hiyo, itakuwaje kwa mti mkavu?"
32Aver dui manush sas ningerde le Jesusosa te aven mardo.
32Waliwachukua pia watu wengine wawili, wahalifu, wauawe pamoja naye.
33Kana areslo po than, kai bushol "Calvary vai Shero," kotse karfosarde les po trushul, ai vi le duie choren, iek pe rik e chachi, ai iek pe rik o stingo.
33Walipofika mahali paitwapo, "Fuvu la Kichwa," ndipo wakamsulubisha Yesu pamoja na wale wahalifu wawili, mmoja upande wake wa kulia na mwingine upande wake wa kushoto.
34Antunchi O Jesus phendia, "Murho Dat, iertis le; ke chi zhanen so keren." Ai hulade leske tsalia, ai thodepe te dikhen kon niril leske tsalia.
34Yesu akasema, "Baba, uwasamehe kwa maana hawajui wanalofanya." Kisha wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura.
35O narodo sas kotse ai dikhelas. Ai le bare manush kai poronchin marenas mui lestar, phenenas, "Skepisardia kavren; mek te skepil pe pes, te si wo O Kristo, kai alosardia O Del."
35Watu wakawa wamesimama pale wakitazama. Nao viongozi wakamdhihaki wakisema: "Amewaokoa wengine; sasa na ajiokoe mwenyewe, kama yeye ndiye Kristo, mteule wa Mungu!"
36Ai le ketani marenas mui lestar, ai avile leste, ai denas les shut.
36Askari nao walimdhihaki pia; walimwendea wakampa siki
37Ai phenenas leske, "Te san tu o amperato le Zhidovongo, skepisar tu tut."
37wakisema: "Kama kweli wewe ni Mfalme wa Wayahudi, jiokoe mwenyewe."
38Opral pa lesko shero ramolaspe ande shiba le Greksisko, ai Latinesko, ai Zhiduviska, "Kado si O AMPERATO LE ZHIDOVONGO."
38Vilevile maandishi haya yalikuwa yameandikwa na kuwekwa juu yake: "Huyu ndiye Mfalme wa Wayahudi."
39Iek andal chor kai sas pasha leste, marelas mui lestar, phenelas, "Te san tu O Kristo, skepisar tu tut, ai ame."
39Mmoja wa wale wahalifu waliotundikwa msalabani, alimtukana akisema: "Je, si kweli kwamba wewe ndiwe Kristo? Basi, jiokoe mwenyewe, utuokoe na sisi pia."
40Numa kolaver chor phendia kolavreske, phenelas, "Chi daras katar O Del, tu kai mudardias ai avela kris pe tute?
40Lakini yule mhalifu mwingine akamkemea mwenzake akisema: "Wewe humwogopi Mungu hata kidogo? Wewe umepata adhabu hiyohiyo.
41Ame, si kris pe amende; ke ame keras amensa kadia, ke chorhe sam kai kerdiam baiuria: numa kado chi kerdia chi iek baio.
41Wewe na mimi tunastahili, maana haya ni malipo ya yale tuliyotenda. Lakini mtu huyu hakufanya chochote kibaya."
42Ai phendia le Jesusoske "Devla, desa tu goji mande kana avesa ando chi amperetsia."
42Kisha akasema, "Ee Yesu! Unikumbuke wakati utakapoingia katika ufalme wako."
43Ai O Jesus phendia leske, "Phenav tuke chachimasa, adies vi tu avesa mansa ando rhaio."
43Yesu akamwambia, "Nakwambia kwa hakika, leo utakuwa pamoja nami peponi."
44Kal desh u dui po mashkar le diesesko tuniariko avilo pe sa e lumia zhi kai trin chasuria.
44Ilikuwa yapata saa sita mchana; jua likaacha kuangaza, giza likafunika nchi yote mpaka saa tisa,
45Ai o kham chi mai strefialas, ai e selia (kortina) ande tampla shindili ande donde de opral zhi tele.
45na pazia lililokuwa limetundikwa Hekaluni likapasuka vipande viwili.
46Ai kana O Jesus dias mui andek baro glaso, "Murho Dat, thav murho duxo ande che vas, ai phendia kadala vorbi, mulo.
46Yesu akalia kwa sauti kubwa: "Baba, naiweka roho yangu mikononi mwako." Alipokwisha sema hayo, akakata roho.
47Akana kana o ketano diklia so kerdilia, luvudisardia O Del, phenelas, "Chaches kado manush vorta sas."
47Hapo, yule jemadari alipoona yaliyotukia akamsifu Mungu akisema: "Hakika huyu alikuwa mtu mwema."
48Ai sa o narodo kai chidelas andek than te dikhel, kana dikhle so kerdilia, marenas pe kolin ai geletar khere.
48Watu wale wote waliokuwa wamekusanyika hapo kwa ajili ya tukio hilo, walipoona hayo yaliyotukia, walirudi makwao wakijipiga vifua kwa huzuni.
49Sa leske vortacha, ai le zhuvlia kai linepe pala leste andai Galilee, de dural beshenas,dikhenas so kerdiolas.
49Marafiki zake wote pamoja na wale wanawake walioandamana naye kutoka Galilaya, walisimama kwa mbali kutazama tukio hilo.
50Sas iek manush kai busholas Josef andai foro kai bushol Arimathea, kado manush lasho sas ai vorta.
50Kulikuwa na mtu mmoja jina lake Yosefu, mwenyeji wa kijiji kimoja cha Wayahudi kiitwacho Armathaya. Alikuwa mtu mwema anayeheshimika;
51Wo nas kana dosharde le Jesusos, wo sas andek foro busholas Arimathea, o foro le Zhidovongo, wo azhukerelas e amperetsia le Devleski.
51Alikuwa akitazamia kuja kwa Ufalme wa Mungu. Ingawa alikuwa mmoja wa Baraza kuu la Wayahudi, hakuwa amekubaliana nao katika kitendo chao.
52Kodo manush gelo ka Pilate, ai manglia te len o stato le Jesusosko.
52Basi, yeye alikwenda kwa Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu.
53Gelo ai lia les tele pa trushul, ai vuluisardia les ando tsolo, ai thodia les ando greposhevo kai sas ando bax, kai inker khonik nas thodino.
53Kisha, akaushusha mwili huo kutoka msalabani, akauzungushia sanda ya kitani, akauweka katika kaburi lililokuwa limechongwa kwenye mwamba, ambalo halikuwa limetumika.
54Parashtuine sas, ai o Savato nachinuilas.
54Siku hiyo ilikuwa Ijumaa, na maandalio ya siku ya Sabato yalikuwa yanaanza.
55Ai le zhuvlia kai avile lesa andai Galilee linepe pala lende, ai dikhle o greposhevo ai sar sas thodino lesko stato.
55Wale wanawake walioandamana na Yesu kutoka Galilaya walimfuata Yosefu, wakaliona lile kaburi na jinsi mwili wake Yesu ulivyowekwa
56Porme gele palpale khere, ai lasharde le vuloia ai duxi le statoski; ai hodinisarde po dies le Savatosko, sar o zakono phenel te kerel.
56Halafu, walirudi nyumbani, wakatayarisha manukato na marashi kuyapaka mwili wa Yesu. Siku ya Sabato walipumzika kama ilivyoamriwa na sheria.