Romani: New Testament

Swahili: New Testament

Luke

22

1Akana e pachiv le manrheski bi drozhdengi pasholas kai busholas 'O Dies O Baro le Zhidovongo'.
1Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa chachu, iitwayo Pasaka, ilikuwa inakaribia.
2Ai le bare rasha ai le Gramnoturia rodenas sar te mudaren les; ke daranas katar o narodo.
2Makuhani wakuu na walimu wa Sheria wakawa wanatafuta njia ya kumwua Yesu, lakini waliwaogopa watu.
3Antunchi o beng gelo ande Judas, kai akharenas les Iscariot, kai sas ek andal desh u dui disipluria.
3Basi, Shetani akamwingia Yuda aitwae Iskarioti, mmoja wa wale mitume kumi na wawili.
4Ai o Judas gelo kal le bare rasha ai kal le bare le ketanenge, te del les ande lenge vas.
4Yuda akaenda akajadiliana na makuhani wakuu na walinzi wa Hekalu kuhusu atakavyomsaliti Yesu kwao.
5Kodola manush raduisaile, ai shinade te den les love.
5Nao wakafurahi na kupatana naye kumlipa fedha.
6Ai o Judas shinadia te lel le love, ai rodias sar te del les ande lenge vas, bi te zhanel o narodo.
6Yuda akakubali, na akawa anatafuta nafasi nzuri ya kumkabidhi kwao bila umati wa watu kujua.
7Antunchi o dies le manrhesko bi drozhdengo avilo, kana trobulas te mudaren le bakriorhan,
7Basi, siku ya Mikate Isiyotiwa chachu ikafika. Hiyo ndiyo siku ambayo mwana kondoo wa Pasaka huchinjwa.
8ai O Jesus tradia le Petres ai le Ioanos, phenelas, "Zhan ai lasharen amende O Dies O Baro le Zhidovongo te xas."
8Hivyo Yesu akawatuma Petro na Yohane, akawaambia, "Nendeni mkatuandalie karamu ili tupate kula Pasaka."
9Ai won phende leske, "Kai manges te lasharas?"
9Nao wakamwuliza, "Unataka tuiandae wapi?"
10Wo phendia lenge, "Ashun, kana aresena ando foro, arakhena ieke manushes kai si les iek vaza paieske; len tume pala leste ando kher kai zhala.
10Akawaambia, "Sikilizeni! Mtakapokuwa mnakwenda mjini, mtakutana na mwanamume anayebeba mtungi wa maji. Mfuateni mpaka ndani ya nyumba atakayoingia.
11Ai phenena le gazdaske kodole kheresko, "Amaro gazda phenel tuke, 'Kai o than kai trobul te xav O Dies O Baro le Zhidovongo murhe displonsa?'"
11Mwambieni mwenye nyumba: Mwalimu anakuuliza, kiko wapi kile chumba ambamo nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu?
12Wo sikavela tumenge iek bari soba opre kai si swako fielo andre; kotse lasharena.
12Naye atawaonyesheni chumba kikubwa ghorofani ambacho kimepambwa. Andalieni humo."
13Geletar, ai arakhle sar phendiasas lenge; ai lasharde O Dies O Baro le Zhidovongo.
13Basi, wakaenda, wakakuta kila kitu sawa kama Yesu alivyokuwa amewaambia; wakaandaa karamu ya Pasaka.
14Ai kana o chaso avilo, wo beshlo kai skafidi le desh u do disiplonsa.
14Saa ilipotimia, Yesu akakaa kula chakula pamoja na mitume wake.
15O Jesus phendia lenge, "Drago sas mange te xav kadia Dies O Baro le Zhidovongo tumensa mai anglal sar te chinuiv.
15Akawaambia, "Nimetamani sana kula Pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu.
16Ke phenav tumenge, chi mai xava tumensa, zhi kai kerdiol ande e amperetsia le Devleski."
16Maana nawaambieni, sitaila tena hadi hapo itakapokamilika katika Ufalme wa Mungu."
17Lia e kuchi, ai dias naisimos, ai phendia, "Len, ai pen savorhe anda late."
17Kisha akatwaa kikombe, akashukuru akasema, "Pokeeni, mgawanye ninyi kwa ninyi.
18Ke phenav tumenge, chi mai piiava andai fruta le struguroski, zhi kai e amperetsia le Devleski avel.
18Kwa maana nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka Ufalme wa Mungu utakapokuja."
19Antunchi lia manrho, ai dias naisimos, phaglia les, ai dia lende, phenelas, "Kako si murho stato kai si dino tumenge; keren kadia te seren tume pa mande."
19Halafu akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa akisema, "Huu ni mwili wangu, unaotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa kunikumbuka."
20Sakadia kana getosarde te xan manrho, wo lia e kuchi, phenelas, "Kacha kuchi ai o nevo kontrakto ando murho rat, kai shordilo pala tumende."
20Akafanya vivyo hivyo na kikombe, baada ya chakula, akisema, "Kikombe hiki ni agano jipya linalothibitishwa kwa damu yangu inayomwagika kwa ajili yenu.
21Ashun! Kodo kai purhila ma, katse lo kai skafidi mansa.
21"Lakini, tazameni! Yule atakayenisaliti yuko nami hapa mezani.
22Ai chaches O Shav le Manushesko trobul te merel sar O Del manglia; numa nasul avela kodoleske kai purhila les!"
22Kweli Mwana wa Mtu anakwenda kuuawa kama ilivyopangwa, lakini ole wake mtu anayemsaliti."
23Ai porme denaspe duma mashkar pende, savo si anda lende kai purhila les.
23Hapo wakaanza kuulizana wao kwa wao ni nani kati yao atakayefanya jambo hilo.
24Won marenas mui mashkar pende te zhanen savo anda lende avela o mai baro.
24Kulitokea ubishi kati ya hao mitume kuhusu nani miongoni mwao anayefikiriwa kuwa mkuu zaidi kuliko wengine.
25O Jesus phendia lenge, "Le amperatsi kadala lumiake si le putiera pe pengo narodo, ai kodola manush bushon "Vortacha le manushenge."
25Yesu akawaambia, "Wafalme wa mataifa huwatawala watu wao kwa mabavu, nao huitwa wafadhili wa watu.
26Numa te na avel tumenge sakadia; numa o mai baro kai si mashkar tumende musai avel sar o mai tsinorho; ai kuko kai si baro musai avel sar kuko sluga.
26Lakini isiwe hivyo kati yenu; bali, yule aliye mkuu kati yenu ni lazima awe mdogo wa wote, na aliye kiongozi lazima awe kama mtumishi.
27Kon si o mai baro, kodo kai beshel kai skafidi vai kodo kai podail? Kodo si kai skafidi numa me sim mashkar tumende sar kodo kai podail.
27Kwa maana, ni nani aliye mkuu: yule anayeketi mezani kula chakula, ama yule anayetumikia? Bila shaka ni yule anayeketi mezani kula chakula! Hata hivyo, mimi niko hapa kati yenu kama mtumishi.
28Tume san kodola kai rhevdisardian mansa kana avilo zumaimos pe mande.
28"Ninyi ndio mliobaki nami wakati wote wa majaribu yangu;
29Anda kodia si ma e amperetsia te dav tumen, sar murho Dat dia man.
29na, kama vile Baba yangu alivyonikabidhi Ufalme, vivyo hivyo nami nitawakabidhi ninyi Ufalme.
30Saxke te xan ai te pen kai murhi skafidi ande murhi amperetsia; ai te beshen pel bare skamina te den kris le desh u dui vitsi le Israelonge.
30Mtakula na kunywa mezani pangu katika ufalme wangu, na mtaketi katika viti vya enzi kuyahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.
31Ai O Jesus phendia, "Simon, Simon Ashun! O beng manglia te sai chinol tu, sar chinolpe o jiv te thol les rigate katar le suluma;
31"Simoni, Simoni! Sikiliza! Shetani alitaka kuwapepeta ninyi kama mtu anavyopepeta ngano.
32Numa rhugisailem anda tute, te na rimolpe cho pachamos. Ai kana avesa palpale mande. Tu musai zhutis che phralen te aven mai zurale."
32Lakini mimi nimekuombea ili imani yako isipungue. Nawe utakaponirudia, watie moyo ndugu zako."
33O Petri phendia leske, "Devla, me zhav tusa, ande temnitsa, ai kai martia!"
33Naye Petro akamjibu, "Bwana, mimi niko tayari kwenda pamoja nawe gerezani, na hata kufa."
34Ai O Jesus phendia, "Petri, phenav tuke, o kurkorsho chi bashel adies, kai tu phenesa trivar ke chi zhanes ma."
34Yesu akamjibu, "Nakwambia wewe Petro, kabla jogoo hajawika leo utakuwa umenikana mara tatu."
35Ai mai phendia lenge, "Kana tradem tumen bi lovengo, bi gonesko, ai bi papuchengo, trobulsardia tume vari so?" Won phende, "Kanchi."
35Kisha, Yesu akawauliza wanafunzi wake, "Wakati nilipowatuma bila mfuko wa fedha wala mkoba wala viatu, mlitindikiwa chochote?" Wakajibu, "La."
36Antunchi phendia lenge, "Numa, akana, kodo kai si les love, lel les, ai vi lesko gono; ai kodo kai nai les sabia, mek te bichinel peske raxami, ai chinel iek sabia.
36Naye akawaambia, "Lakini sasa, yule aliye na mfuko wa fedha auchukue; na aliye na mkoba, hali kadhalika. Na yeyote asiye na upanga, auze koti lake anunue mmoja.
37Ke phenav tumenge, o ramomos kai phenel, "Wo sas mashkar le chorenge," Musai te kerdiol vorta pa mande. Ke kadia kai sas ramome pa mande avela, chachimasa."
37Maana nawaambieni, haya maneno ya Maandiko Matakatifu: Aliwekwa kundi moja na wahalifu, ni lazima yatimie. Naam, yale yanayonihusu yanafikia ukamilifu wake."
38Won phende, "Devla, Dikh! Katse si dui sebi." O Jesus phendia leske, "Dosta si!"
38Nao wakasema, "Bwana, tazama; hapa kuna panga mbili." Naye akasema, "Basi!"
39Ai avilo avri anda foro, sar kerelas butivar, gelo po Plai le Maslinenge; ai leske disipluria linepe pala leste.
39Yesu akatoka, na kama ilivyokuwa desturi yake, akaenda katika mlima wa Mizeituni; wanafunzi wake wakamfuata.
40Kana areslo po than, phendia lenge, "Rhugin tume saxke te na peren ando zumaimos."
40Alipofika huko akawaambia, "Salini, msije mkaingia katika kishawishi."
41Ai porme durilo lendar xantsi tu sai shudes ek bax. Ai thodiape pe changende, ai rhugisailo,
41Kisha akawaacha, akaenda umbali wa mtu kuweza kutupa jiwe, akapiga magoti, akasali:
42phenelas, "Murho Dat, te sai mek te nakhel kadia kuchi mandar; numa na murhi voia, chiri voia te avel kerdi."
42"Baba, kama wapenda, ukiondoe kwangu kikombe hiki; hata hivyo, mapenzi yako yatimizwe, wala siyo yangu."
43Strazo iek angelo anda rhaio avilo leste te del les zor.
43Hapo, malaika kutoka mbinguni, akamtokea ili kumtia moyo.
44Sar chinolas, rhugilaspe mai zurales; ai le paia kai zhanas pa leste kerdionas sar bambi rateske kai perenas pe phuv.
44Akiwa katika uchungu mkubwa, alisali kwa bidii zaidi; na jasho likamtoka, kama matone ya damu, likatiririka mpaka chini.
45Kana rhugisailo wushtilo opre, ai avilo palpale ka peske disipluria, ai arakhlia le sovenas, kai nekezhinas.
45Baada ya kusali, aliwarudia wanafunzi wake, akawakuta wamelala, kwani walikuwa na huzuni.
46Ai phendia lenge, "Sostar soven? Wushten opre ai rhugin tume, te na peren ando zumaimos."
46Akawaambia, "Mbona mnalala? Amkeni msali, msije mkaingia katika kishawishi."
47Sar delas duma inker, o narodo avilo ai kodo kai busholas Judas, iek andal desh u dui disipluria, wo sas anglal, ai pashilo pasha Jesus te chumidel les.
47Alipokuwa bado anaongea, kundi la watu likaja likiongozwa na yule aliyeitwa Yuda, mmoja wa wale mitume kumi na wawili. Yuda akaenda kumsalimu Yesu kwa kumbusu.
48Ai O Jesus phendia leske, "Judas, pala kako chumidimos purhidian O Shav le Manushesko?"
48Lakini Yesu akamwambia, "Yuda! Je, unamsaliti Mwana wa Mtu kwa kumbusu?"
49Kana kodola kai sas le Jesusosa, dikhle so kerdilia, phende leske, "Devla, trobul te das la sabiasa?"
49Wale wanafunzi wake walipoona hayo wakasema, "Bwana, tutumie panga zetu?"
50Ai iek anda lende dia la sabiasa, o sluga le bare rashasko, ai shindia lesko chacho khan.
50Na mmoja wao akampiga upanga mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio lake la kulia.
51Numa O Jesus phendia, "Aterdion! Dosta si." Ai azbadia o khan pe kodole manushesko ai sastilo.
51Hapo, Yesu akasema, "Acha! Hii inatosha." Akaligusa sikio la mtu huyo akaliponya.
52Antunchi O Jesus phendia le bare le rashange, ai le barenge kai poronchinas la tamplaske, ai le mai phure, kai sas lesa. "Tume avilian, sar pala iek chor, le sabiensa, ai le khashtensa?"
52Kisha Yesu akawaambia makuhani wakuu, wakubwa wa walinzi wa Hekalu na wazee waliokuja kumkamata: "Je, mmekuja na mapanga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyang'anyi?
53Swako dies simas tumensa ande tampla, ai chi thodian o vas pe mande; numa si tumaro chaso, ai putiera le tuniarikoski."
53Nilipokuwa pamoja nanyi kila siku Hekaluni hamkunitia nguvuni. Lakini, huu ndio wakati wenu hasa, ndio wakati wa utawala wa giza."
54Antunchi line les, angerde les ando kher le baro le rashasko. Ai o Petri liape pala lende de dural.
54Basi, wakamkamata, wakamchukua na kwenda naye nyumbani kwa Kuhani Mkuu. Petro akawa anamfuata nyuma kwa mbali.
55Kerde iag mashkar e bar, ai beshle tele andek than, o Petri beshelas tele mashkar lende.
55Moto ulikuwa umewashwa katikati ya ua, nao wakawa wameketi pamoja Petro akiwa miongoni mwao.
56Ek sluga dikhlia le Petres pashai iag, ai dikhelas pe leste, ai phendia, "Vi kado manush sas lesa."
56Mjakazi mmoja alipomwona Petro ameketi karibu na moto, akamkodolea macho, akasema, "Mtu huyu alikuwa pia pamoja na Yesu."
57Numa o Petri phendia, "Zhuvlio, chi zhanav les."
57Lakini Petro akakana akisema, "Wee! simjui mimi."
58Pala kodia aver sluga dikhlia les, ai phendia, "Vi tu sanas lensa." O Petri phendia, "Manusha, chi sim me."
58Baadaye kidogo, mtu mwingine akamwona Petro, akasema, "Wewe ni mmoja wao." Lakini Petro akajibu "Bwana we; si mimi!"
59Iek chaso pala kodia, aver manush phendia, "Suguro ke kado manush sas lesa; ke wo si Galilean."
59Kama saa moja baadaye, mtu mwingine akasisitiza, "Hakika huyu alikuwa pamoja naye; ametoka Galilaya ati."
60Ai o Petri phendia, "Manusha, chi zhanav so phenes, ai strazo sar delas duma o kurkorsho bashlo.
60Lakini Petro akasema, "Bwana wee; sijui hata unachosema!" Na papo hapo, akiwa bado anaongea, jogoo akawika.
61Ai O Jesus boldinisailo, dikhlia po Petri, ai o Petri diape goji ka le vorbi kai O Jesus phendiasas leske, mai anglal sar te bashel o kurkorsho, tu phenesa trivar ke chi zhanes ma."
61Bwana akageuka na kumtazama Petro, naye Petro akakumbuka yale aliyokuwa ameambiwa na Bwana: "Leo kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu."
62Ai o Petri anklisto avri, ai ruia zurales.
62Hapo akatoka nje, akalia sana.
63Ai le manush kai ankerenas le Jesusos, marenas mui lestar, ai marenas les,
63Wale watu waliokuwa wanamchunga Yesu, walimpiga na kumdhihaki.
64ai kana thode derza pe lesko mui, marde les palmi pe lesko mui ai phushle, "Kon mudardia tu?"
64Walimfunga kitambaa usoni, wakawa wanamwuliza, "Ni nani aliyekupiga? Hebu bashiri tuone!"
65Ai phende leske but zhangale vorbi ai asanas lestar.
65Wakamtolea maneno mengi ya matusi.
66Kana phuterdilo o dies, le bare rasha, ai le phure le manushenge, ai le Gramnoturia avile andek than, ai ningerde les anglai kris. Phenenas,
66Kulipokucha, kikao cha wazee wa watu kilifanyika, ambacho kilihudhuriwa na makuhani wakuu na walimu wa Sheria. Yesu akaletwa mbele ya Baraza hilo.
67"Te san tu O Kristo? Phen amenge," O Jesus phendia lenge, "Te phenava tumenge, tume chi pachan;
67Nao wakamwambia, "Twambie! Je, wewe ndiwe Kristo?" Lakini Yesu akawaambia, "Hata kama nikiwaambieni, hamtasadiki;
68Ai te phushav tumen, tume chi den atweto, vai mek ma te zhav.
68na hata kama nikiwaulizeni swali, hamtanijibu.
69Dakanara O Shav le Manushesko beshel pe rik e chachi, kai si e putiera le Devleski."
69Lakini tangu sasa, Mwana wa Mtu atakuwa ameketi upande wa kulia wa Mungu Mwenyezi."
70Antunchi savorhe phenenas, "Tu san O Shav le Devlesko?" Ai wo phendia lenge, "Tume phenen, ke sim me."
70Hapo wote wakasema, "Ndiyo kusema wewe ni Mwana wa Mungu?" Naye akasema, "Ninyi mnasema kwamba mimi ndiye."
71Ai won phende, "Chi mai trobul ame martero! Ke ame ashundiam so wo phendia anda pesko mui."
71Nao wakasema, "Je, tunahitaji ushahidi mwingine? Sisi wenyewe tumesikia akisema kwa mdomo wake mwenyewe."