Romani: New Testament

Swahili: New Testament

Luke

21

1O Jesus vazdia le iakha, ai dikhlia le barvale manushen thonas penge love ande gono ande tampla.
1Yesu alitazama kwa makini, akawaona matajiri walivyokuwa wanatia sadaka zao katika hazina ya Hekalu,
2Ai vi dikhlia ek chorhi phivli sar tholas dui xarkune kotora.
2akamwona pia mama mmoja mjane akitumbukiza humo sarafu mbili ndogo.
3Ai phendia, "Phenav tumenge chachimasa, kacha chorhi phivli thodia mai but de sar savorhe;
3Basi, akasema, "Nawaambieni kweli, mama huyu mjane ametia zaidi katika hazina kuliko wote.
4Ke le barvale thode xantsi love anda lengo barvalimos; numa woi thodia so godi sas la te traiil.
4Kwa maana, wengine wote wametoa sadaka zao kutokana na ziada ya mali zao, lakini huyu mama, ingawa ni maskini, ametoa kila kitu alichohitaji kwa kuishi."
5Uni zhene denas duma pal tampla, sar shukarenas o tampla le lashe baxensa ai podarki kai dine ka Del, O Jesus phendia lenge,
5Baadhi ya wanafunzi walikuwa wanazungumza juu ya Hekalu, jinsi lilivyopambwa kwa mawe ya thamani, pamoja na sadaka zilizotolewa kwa Mungu. Yesu akasema,
6"Sa so dikhena avela pherdo, chi ashela iek bax po kaver." Won phushen lestar,
6"Haya yote mnayoyaona--zitakuja siku ambapo hakuna hata jiwe moja litakalosalia juu ya lingine; kila kitu kitaharibiwa."
7"Gazda, kana kerdiola kodia? Che semno avela kana kerdiona kodola?"
7Basi, wakamwuliza, "Mwalimu, mambo hayo yatatokea lini? Na ni ishara gani zitakazoonyesha kwamba karibu mambo hayo yatokee?"
8O Jesus phendia, "Arakhen tume, te na atsaven tume khonik, ke but avena ande murho anav, phenenas, "Me sim o Kristo!" E vriama pashili, na len tume pala lende.
8Yesu akawajibu, "Jihadharini, msije mkadanganyika. Maana wengi watatokea na kulitumia jina langu wakisema: Mimi ndiye, na, Wakati ule umekaribia. Lakini ninyi msiwafuate!
9Kana ashunena ke marenpe ai vieste kai marenpe ande uni thana, Na Daran; ke kodia musai te kerdiol, numa nai inker o gor.
9Basi, mtakaposikia habari za vita na misukosuko, msitishike; maana ni lazima hayo yatokee kwanza, lakini mwisho wa yote, bado."
10Antunchi O Jesus phendia lenge, "Iek them marelape aver themesa; ai iek amperetsia marelape avria amperetsiasa:
10Halafu akaendelea kusema: "Taifa moja litapigana na taifa lingine, na ufalme mmoja utapigana na ufalme mwingine.
11Ai izdrala e phuv zurales, ai ande but thana chi avela dosta te xan, ai avela but naswalimos, ai kerdionape zhungale bucha kai chi mai dichilia, ai avela bare semnuria ando cheri.
11Kila mahali kutakuwa na mitetemeko mikubwa ya ardhi, kutakuwa na njaa na tauni. Kutakuwa na vituko vya kutisha na ishara kubwa angani.
12Numa mai anglal sar kodola dieli, lena tume le manush ai chinuina tume, dena tume kal synagoguria, thona tume andel temnitsi, angerena tume anglal la amperatsi ai le bare le foroske pala murho anav.
12Lakini kabla ya kutokea hayo yote, watawatieni nguvuni, watawatesa na kuwapelekeni katika masunagogi na kuwatia gerezani; mtapelekwa mbele ya wafalme na watawala kwa ajili ya jina langu.
13Kodola kerdiona tumenge saxke te aven marturia.
13Hii itawapeni fursa ya kushuhudia Habari Njema.
14Na gindin tume mai anglal so te phenen, ai na daran.
14Muwe na msimamo huu mioyoni mwenu: hakuna kufikiria kabla ya wakati juu ya jinsi mtakavyojitetea,
15Ke dava tume le vorbi ai e goji, kai tumare duzhmaia nashti den ando gor vai te mothon ke nai kadia.
15kwa sababu mimi mwenyewe nitawapeni ufasaha wa maneno na hekima, hivyo kwamba zenu hawataweza kustahimili wala kupinga.
16Vi tumaro dat ai tumari dei purhila tume, ai tumare phral, ai tumare niamuria, ai tumare vortacha; ai mudaren buten anda tumende.
16Wazazi wenu, ndugu, jamaa na rafiki zenu watawasaliti ninyi; na baadhi yenu mtauawa.
17Avena gratsia savorhenge pala murho anav.
17Watu wote watawachukieni kwa sababu ya jina langu.
18Numa chi xasavola chi iek bal anda tumaro shero.
18Lakini, hata unywele mmoja wa vichwa vyenu hautapotea.
19Ai kai inkerena zhando gor tume skepina tumaro traio le Devlesa.
19Kwa uvumilivu wenu, mtayaokoa maisha yenu.
20Kana dikhena ke le thema chidenape te marenpe pe Jerusalem, antunchi zhanen ke Jerusalem sigo avela peradi.
20"Mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, ndipo mtambue ya kwamba wakati umefika ambapo mji huo utaharibiwa.
21Antunchi kodola kai si ande Judea trobula te nashen andel plaia; ai kodola kai si mashkaral ande Jerusalem trobula te zhantar; ai kodola kai si ande niva te na aven andel foruria.
21Hapo walioko Yudea wakimbilie milimani; wale walio mjini watoke; na wale walio mashambani wasirudi mjini.
22Ke kodola diesa avena diesa chorhe, ai te kerdiol so godi sas ramome.
22Kwa maana siku hizo ni siku za adhabu, ili yote yaliyoandikwa yatimie.
23Nasul le zhuvliange kai si pharia glatasa, ai kodolen kai si le glate pe chuchi ande kodola dies! Ai avela baro nekazo ando them, ai xoli pe kado narodo.
23Ole wao waja wazito na wanyonyeshao siku hizo! Kwa maana kutakuwa na dhiki kubwa katika nchi, na hasira ya Mungu itawajia watu hawa.
24Le manush avena mudarde katar e sabia, ai aver avena line ai thode ande temnitsa mashkar sa le thema; ai le manush kai Nai Zhiduvuria phiren le punrhensa pai Jerusalem, zhi kai getolpe lenge vriama.
24Wengine watauawa kwa upanga, wengine watachukuliwa mateka katika nchi zote; na mji wa Yerusalemu utakanyagwa na watu wa mataifa mengine, hadi nyakati zao zitakapotimia.
25"Kerdiola semnuria ando kham, ai ando shunuto, ai andal chererhaia; ai pe phuv avela dar mashkar le thema, kai chi mai zhanena so te keren. E maria ai le talazuria keren bunto;
25"Kutakuwa na ishara katika jua na mwezi na nyota. Mataifa duniani yatakuwa na dhiki kwa sababu ya wasiwasi kutokana na mshindo wa mawimbi ya bahari.
26le manush merena daratar ke zhanena so kerdiola pe phuv; ke e putiera le chereski izdrala.
26Watu watazirai kwa sababu ya uoga, wakitazamia mambo yatakayoupata ulimwengu; kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.
27Antunchi dikhena sar O Shav le Manushesko avela pel nuveria putierasa ai barimasa.
27Halafu, watamwona Mwana wa Mtu akija katika wingu, mwenye nguvu na utukufu mwingi.
28Kana kadala dieli nachinaina te kerdiol, antunchi dikhen opre, ai vazden tumaro shero, ke tumaro skepimos pashelo."
28Wakati mambo hayo yatakapoanza kutukia, simameni na kuinua vichwa vyenu juu, kwa maana ukombozi wenu umekaribia."
29O Jesus phendia lenge ek paramichi, "Dikhen e pruing le figengi, ai sa le khash;
29Kisha akawaambia mfano: "Angalieni mtini na miti mingine yote.
30sar barion ai anklen patria, tume dikhen ai zhanen ke o milai pashelo.
30Mnapoona kwamba imeanza kuchipua majani, mwatambua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia.
31Sakadia, kana dikhena kadala dieli ke kerdion, zhanen ke e amperetsia le Devleski pashela.
31Vivyo hivyo, mtakapoona mambo hayo yanatendeka, mtatambua kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
32Chachimasa, phenav tumenge, kadia vitsa chi nakhela zhi pon chi kerdion kadala dieli.
32Nawaambieni hakika, kizazi hiki cha sasa hakitapita kabla ya hayo yote kutendeka.
33O cheri ai e lumia nakhena, numa murhe vorbi shoxar chi nakhena.
33Mbingu na dunia vitapita, lakini maneno yangu hayatapita.
34Arakhen tume! Na meken tumaro ilo te pherdiol pachiva ai mol, ai nekazo kadale traiosko, ai kodo dies avela pe tumende kana chi zhanen.
34"Muwe macho, mioyo yenu isije ikalemewa na anasa, ulevi na shughuli za maisha haya. La sivyo, Siku ile itawajieni ghafla.
35Ke kodo dies avela sar iek selia pe sa kodola kai beshen pe sa e lumia.
35Kwa maana itawajia kama mtego, wote wanaoishi duniani pote.
36Arakhen tume! Ai rhugin tume sagda, saxke te avel tume zor te na kerdiol tumenge sa kadala dieli, ai te beshen ande punrhende angla Shav le Manushesko."
36Muwe waangalifu basi, na salini daima ili muweze kupata nguvu ya kupita salama katika mambo haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele ya Mwana wa Mtu."
37E diese O Jesus sicharelas ande tamplo; ai e riat zhalas te beshel pe plaiin kai busholas Masleni.
37Wakati wa mchana, siku hizo, Yesu alikuwa akifundisha watu Hekaluni; lakini usiku alikuwa akienda katika mlima wa Mizeituni na kukaa huko.
38Ai sa o narodo diminiatsi avile leste ande tampla te ashunen leste.
38Watu wote walikuwa wanakwenda Hekaluni asubuhi na mapema, wapate kumsikiliza.