1Sar O Jesus nakhelas, wo dikhlia iekes manushes kai arakhadilo korho.
1Yesu alipokuwa akipita alimwona mtu mmoja, kipofu tangu kuzaliwa.
2Leske disipluria phushle les, "Gazda, sostar arakhadiol korho? Kon kerdia bezexa, kado manush vai leske dades vai leska da?
2Basi, wanafunzi wakamwuliza, "Mwalimu! Ni nani aliyetenda dhambi: mtu huyu, ama wazazi wake, hata akazaliwa kipofu?"
3O Jesus phendia lenge, "Nai wo ai chi leske dades ai chi leska da kai kerde bezexa, numa wo si korho kashte te dichol e putiera le Devleski pe leste.
3Yesu akajibu, "Jambo hili halikutukia kwa sababu ya dhambi zake yeye, wala dhambi za wazazi wake; ila alizaliwa kipofu ili nguvu ya Mungu ionekane ikifanya kazi ndani yake.
4Trobul te kerav e buchi kodaleske kai tradia man zhi kai o dies; e riat avela, kana khonik nashti kerela buchi.
4Kukiwa bado mchana yatupasa kuendelea kufanya kazi za yule aliyenituma; maana usiku unakuja ambapo mtu hawezi kufanya kazi.
5Zhi kai sim ande e lumia, me sim e vediara la lumiaki."
5Wakati ningali ulimwenguni, mimi ni mwanga wa ulimwengu."
6Kana phendia kadala vorbi, O Jesus chungardia tele pe phuv, ai kerdia chik peske cungaresa; porme thodia kodia chik pel iakha le korheske,
6Baada ya kusema hayo, akatema mate chini, akafanyiza tope, akampaka yule kipofu machoni,
7ai phendia leske, "Zha, te xalav tu ando pai kai bushol Siloam." (anav kai bushol, "Tradino"). O korho manush gelo, ai xaladiape, ai avilo palpale ai dikhelas.
7akamwambia, "Nenda ukanawe katika bwawa la Siloamu." (maana ya jina hili ni "aliyetumwa"). Basi, huyo kipofu akaenda, akanawa, kisha akarudi akiwa anaona.
8Le manush kai sas pasha leste ai kodola kai zhanenas les sar iek korhovetso, phenenas, "Nai kado kai beshelas tele ai kai mangelas?"
8Basi, jirani zake na wale waliokuwa wanajua kwamba hapo awali alikuwa maskini mwombaji, wakasema, "Je, huyu siye yule maskini aliyekuwa akiketi na kuomba?"
9Uni phenen, "Wo si," numa aver phenenas, "Wo miazolpe leste." Numa wo phendia, "Me sim."
9Baadhi yao wakasema, "Ndiye." Wengine wakasema, "La! Ila anafanana naye." Lakini huyo aliyekuwa kipofu akasema, "Ni mimi!"
10Won phenen leske, "Sarta chire iakha phuterdile?"
10Basi, wakamwuliza, "Sasa, macho yako yalipataje kufumbuliwa?"
11Wo phendia lenge, "O manush kai akharen les O Jesus kerdia chira chik, ai thodia la pe murhe iakha, ai phendia mange, "Zh ka pai kai busholas Siloam, ai xalav tu." ai gelem, ai xaladem ma, ai dikhlem.
11Naye akawajibu, "Yule mtu aitwaye Yesu alifanya tope, akanipaka machoni na kuniambia: Nenda ukanawe katika bwawa la Siloamu. Basi, mimi nikaenda, nikanawa, nikapata kuona."
12Antunchi phende leske, "Kai kodo manush?" Wo phendia, "Chi zhanav."
12Wakamwuliza, "Yeye yuko wapi?" Naye akawajibu, "Mimi sijui!"
13Ingerde karing le Farizeanuria kodales kai sas korho.
13Kisha wakampeleka huyo mtu aliyekuwa kipofu kwa Mafarisayo.
14Kana O Jesus kerdia e chik ai phuterdia leske iakha sas o dies Savatone.
14Siku hiyo Yesu alipofanya tope na kumfumbua macho mtu huyo, ilikuwa siku ya Sabato.
15Sa anda kodia le Farizeanuria phushle le korhes, "Sar premisardian cho dikhimos?" Ai wo phendia lenge, "Thodia chik pe murhe iakha, xaladem ma, ai akana dikhav."
15Basi, Mafarisayo wakamwuliza mtu huyo, "Umepataje kuona?" Naye akawaambia, "Alinipaka tope machoni, nami nikanawa na sasa naona."
16Uni andal le Farizeanuria phende, "Kado manush chi avel katar O Del, ke chi kerel o zakono kai si Savato." Aver phenen, "Sar iek manush bezexa lo sai kerel kasave mirakluria?" Anda kodia chi haliarenas mashkar pende iek fialo.
16Baadhi ya Mafarisayo wakasema, "Mtu huyu hakutoka kwa Mungu, maana hashiki sheria ya Sabato." Lakini wengine wakasema, "Mtu mwenye dhambi awezaje kufanya ishara za namna hii?" Kukawa na mafarakano kati yao.
17Mai iek data le Farizeanuria phushen le korhes kai sastilo, "So phenes tu pa leste, kai phuterdia chire iakha?" Wo phendia lenge, "Wo si iek profeto."
17Wakamwuliza tena huyo mtu aliyekuwa kipofu, "Maadam yeye amekufungua macho, wasemaje juu yake?" Naye akawaambia, "Yeye ni nabii!"
18Le Zhiduvuria chi pachanaspe ke wo sas korho, ai ke akana dikhel, zhi kai andine leske dades ai leska da.
18Viongozi wa Wayahudi hawakusadiki kwamba mtu huyo alikuwa kipofu hapo awali na sasa anaona mpaka walipowaita wazazi wake.
19Ai phushle lendar, phenen, "Kako si tumaro shav, kai phenen ke arakhadilo korho? Sar wo dikhel akana?"
19Basi, wakawauliza hao wazazi, "Je, huyu ndiye mtoto wenu ambaye ninyi mwasema alizaliwa kipofu? Sasa amepataje kuona?"
20Leske dat ai dei phende, "Ame zhanas ke si amaro shav, ai zhanas ke arakhadilo korho.
20Wazazi wake wakajibu, "Tunajua kwamba huyu ni mtoto wetu, na kwamba alizaliwa kipofu.
21Numa chi zhanas so sai dikhel akana, ai chi zhanas kon phuterdia leske iakha. Phushen lestar, si peske bershengo , wo sai del atweto."
21Lakini amepataje kuona, hatujui; na wala hatumjui yule aliyemfumbua macho. Mwulizeni yeye mwenyewe; yeye ni mtu mzima, anaweza kujitetea mwenyewe."
22Lesko dat ai dei denas duma kadia ke daranas katar le Zhiduvuria; ke le Zhiduvuria dinepe duma mashkar pende, ke te mothona avri kon ke O Jesus si O Kristo, den les avri anda e tampla.
22Wazazi wake walisema hivyo kwa sababu waliwaogopa viongozi wa Wayahudi kwani viongozi hao walikuwa wamepatana ya kwamba mtu yeyote atakayekiri kwamba Yesu ni Kristo atafukuzwa nje ya sunagogi.
23Sa anda kodia leske dat ai dei phende, "Si peske bershengo, phushen lestar!"
23Ndiyo maana wazazi wake walisema: "Yeye ni mtu mzima, mwulizeni."
24Le Farizeanuria akharen pe duito data le manushes kai sas korho, ai phende leske, "Phen o chachimos angla Del! Ame zhanas ke kodo manush si bezexa lo."
24Basi, wakamwita tena aliyekuwa kipofu, wakamwambia, "Sema ukweli mbele ya Mungu! Sisi tunajua kwamba mtu huyu ni mwenye dhambi."
25Wo phendia lenge, "Chi zhanav te si ek bezexalo vai nai, numa zhanav iek diela, ke simas korho, akana dikhav."
25Yeye akajibu, "Kama ni mwenye dhambi mimi sijui. Lakini kitu kimoja najua: Nilikuwa kipofu, na sasa naona."
26Ai mai phushle les, "So kerdia tuke? Sar kerdia te phutrel che iakha?"
26Basi, wakamwuliza, "Alikufanyia nini? Alikufumbuaje macho yako?"
27Phendia lenge, "Phendem tumenge iek data, ai chi ashundian mande. Sostar mai mangen te ashunen? Vi tume mangen te aven leske disipluria?"
27Huyo mtu akawajibu, "Nimekwisha waambieni, nanyi hamkusikiliza; kwa nini mwataka kusikia tena? Je, ninyi pia mnataka kuwa wafuasi wake?"
28Akushle les, ai phende leske, "Tu san disiplo; ame sam le disipluria le Mosesoske.
28Lakini wao wakamtukana wakisema, "Wewe ni mfuasi wake; sisi ni wafuasi wa Mose.
29Ame zhanas ke O Del dia duma le Mosesosa; numa kado, chi zhanas katar lo!"
29Sisi tunajua kwamba Mungu alisema na Mose, lakini mtu huyu hatujui ametoka wapi!"
30O manush phendia lenge, "Shodo diela si! Ke chi zhanen katar lo, numa wo phuterdia murhe iakha!
30Naye akawajibu, "Hili ni jambo la kushangaza! Ninyi hamjui ametoka wapi, lakini amenifumbua macho yangu!
31Ame zhanas ke O Del chi ashunel le bezexalen; numa ashunel le manushes kai chetil les ai kerel leski voia.
31Tunajua kwamba Mungu hawasikilizi watu wenye dhambi, ila humsikiliza yeyote mwenye kumcha na kutimiza mapenzi yake.
32De anda gor la lumiake shoxar chi ashundian ke vari kon phuterdia le iakha le korheske kana arakhadilo korho.
32Tangu mwanzo wa ulimwengu haijasikika kwamba mtu ameyafumbua macho ya mtu aliyezaliwa kipofu.
33Kodo manush te na avilino katar O Del, nashtisardino te kerel kanchi."
33Kama mtu huyu hakutoka kwa Mungu, hangeweza kufanya chochote!"
34Ai won phende leske, "Tu arakhadilian antrego ando bezex, ai manges te sichares amen?" Ai dine les avri anda tampla.
34Wao wakamjibu, "Wewe ulizaliwa na kulelewa katika dhambi; unawezaje kutufundisha sisi?" Basi, wakamfukuzia mbali.
35O Jesus ashundia ke dine les avri, ai kana arakhlia les, phendia leske, "Pachas tu ando Shav le Manushesko?"
35Yesu alisikia kwamba walikuwa wamemfukuzia mbali, naye alipomkuta akamwuliza, "Je, wewe unamwamini Mwana wa Mtu?"
36Wo phendia ka Jesus, "Phen mange, savo si, Gazda? Kaste te sai pachav ma ande leste!"
36Huyo mtu akajibu, "Mheshimiwa, niambie yeye ni nani, ili nipate kumwamini."
37O Jesus phendia leske, "Dikhes les, wo si kai del duma tusa akana."
37Yesu akamwambia, "Umekwisha mwona, naye ndiye anayesema nawe sasa."
38Phendia leske, "Gazda, Pachav ma!" ai dia changa angla leste.
38Basi, huyo mtu akasema, "Ninaamini Bwana!" Akamsujudia.
39Porme O Jesus phendia, "Avilem ande kadia lumia te kerav e kris, kaste le korhe te sai dikhen; ai kodala kai dikhen te aven korhe.
39Yesu akasema, "Mimi nimekuja ulimwenguni kutoa hukumu, kusudi wasioona wapate kuona, na wale wanaoona wawe vipofu."
40Uni andal Farizeanuria kai sas lesa, ashunde kodala vorbi, ai phende leske, "Vi ame, sam korhe?"
40Baadhi ya Mafarisayo waliokuwa pamoja naye walisikia maneno hayo, wakamwuliza, "Je, sisi pia ni vipofu?"
41O Jesus phendia lenge, "Te avilianas korhe, nas te aven doshale: numa akana tume phenen, "Ame dikhas," sa anda kodia tumare bezexa ashen.
41Yesu akawajibu, "Kama mngekuwa vipofu, hamngekuwa na hatia; lakini sasa ninyi mwasema: Sisi tunaona, na hiyo yaonyesha kwamba mna hatia bado.