1O Theophilus: But narodo zumade te ramon pa so kerdilia mashkar amende,
1Mheshimiwa Theofilo: Watu wengi wamejitahidi kuandika juu ya mambo yale yaliyotendeka kati yetu.
2ai won ramosarde so kerdilia sar sas amenge, kodola kai dikhle de anda gor, ai kai sas lenge phendo te phenen e vorba le Devleski.
2Waliandika kama tulivyoelezwa na wale walioyaona kwa macho yao tangu mwanzo, na waliotangaza ujumbe huo.
3Ai akana me lem o gor mishto te zhanav so godi kerdilia de anda gor, miazilia mange mishto lasho te ramov tumenge pa kadala dieli kai sas.
3Inafaa nami pia, Mheshimiwa, baada ya kuchunguza kwa makini mambo yote tangu mwanzo, nikuandikie kwa mpango,
4Me kerav kadia saxke tume te sai len po gor o chachimos kai sas tumenge phendo.
4ili nawe uweze kujionea mwenyewe ukweli wa mambo yale uliyofundishwa.
5Kana o Herod sas o amperato ande Judea, sas iek rashai kai bushol Zechariah, wo sas andal rasha kai busholas Abijah. Leski rhomni busholas Elizabeth, ai woi sas andai vitsa le rashaske kai busholas Aaron, o baro rashai.
5Wakati Herode alipokuwa mfalme wa Yudea, kulikuwa na kuhani mmoja jina lake Zakaria, wa kikundi cha Abia. Mke wake alikuwa anaitwa Elisabeti, naye alikuwa wa ukoo wa kuhani Aroni.
6Won le dui zhene sas vorta angla Del, ai kerdia mishto sa le zakonuria ai sa le krisa le Devleski.
6Wote wawili walikuwa wanyofu mbele ya Mungu, wakiishi kwa kufuata amri na maagizo yote ya Bwana bila lawama.
7Nas le glati ke e Elizabeth nashti avelas le glate, ai vi le dui zhene sas phure.
7Lakini hawakuwa wamejaliwa watoto kwa vile Elisabeti alikuwa tasa, nao wote wawili walikuwa wazee sana.
8Iek dies o Zechariah kerelas peski buchi le rashaski angla Del.
8Siku moja, ilipokuwa zamu yake ya kutoa huduma ya ukuhani mbele ya Mungu,
9Ke pala zakono le rashango, o Zacharias sas alosardia te zhal ande tampla te phabarelas e thumwiia pe altari.
9Zakariya alichaguliwa kwa kura, kama ilivyokuwa desturi, kuingia hekaluni ili afukize ubani.
10Sa o narodo rhugilaspe avri ka chaso kai phabarenas e Thumwiia.
10Watu, umati mkubwa, walikuwa wamekusanyika nje wanasali wakati huo wa kufukiza ubani.
11Ek angelo le Devlesko antunchi sikadilo ka Zachariah, wo beshelas pe chachi rik kai sas o altari kai phabarenas e Thumwiia.
11Malaika wa Bwana akamtokea humo ndani, akasimama upande wa kulia wa madhabahu ya kufukizia ubani.
12Kana o Zechariah dikhlia o angelos, wo sas nekezhisailo ai darailo.
12Zakariya alipomwona alifadhaika, hofu ikamwingia.
13Numa o angelo phendia leske, "Na dara o Zechariah! O Del ashundia cho rhugimos, ai Elizabeth, chi rhomni dela tu iek shav kai akharesa les Iovano.
13Lakini malaika akamwambia, "Zakariya, usiogope, kwa maana sala yako imesikilizwa, na Elisabeti mkeo atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utampa jina Yohane.
14Ai tu avesa defial raduime, ai but narodo raduilape kana kerdiola!
14Utakuwa na furaha kubwa na watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
15Ke baro manush avela anglal iakha Devleske, ai shoxar chi pela mol ai chi iek pimos kai si alkolsa. Avela pherdo le Swuntone Duxoske kana kerdiola.
15Atakuwa mkuu mbele ya Bwana. Hatakunywa divai wala kileo, atajazwa Roho Mtakatifu tangu tumboni mwa mama yake.
16Anelas palpale buten andal Zhiduvuria ka lenge Del.
16Atawaelekeza wengi wa watu wa Israeli kwa Bwana Mungu wao.
17Wo zhala mai anglal lestar le duxosa ai la putierasa le profetoske o Elijah te thon pale andek than le daden ai le shaven ai te anen palpale kodolen kai chi pachaie o mui ka goji le manushenge kai sas chache; wo lasharela narodos vorta angla Del."
17Atamtangulia Bwana akiongozwa na nguvu na roho kama Eliya. Atawapatanisha kina baba na watoto wao; atawafanya wasiotii wawe na fikira za uadilifu, na hivyo amtayarishie Bwana watu wake."
18O Zechariah phenel le angeloske, "Sar te zhanav ke so phenes si chaches? Ke phuro sim ai vi murhi rhomni."
18Zakariya akamwambia huyo malaika, "Ni kitu gani kitakachonihakikishia jambo hilo? Mimi ni mzee, hali kadhalika na mke wangu."
19Ai o angelo del les atweto, "Me sim o Gabriel, me beshav angla Del, vo tradia ma te dav tusa duma ai te anav tuke kadia lashi vorba.
19Malaika akamjibu, "Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele ya Mungu, na nimetumwa niseme nawe, nikuletee hii habari njema.
20Num chi pachaian murhe vorbi, kai savon avena pe kana avela e vriama. Anda kodia si te kerdios muto ai nashti desa duma zhi ka dies kai avela pe so phendem tuke."
20Sikiliza, utakuwa bubu kwa sababu huyasadiki haya maneno yatakayotimia kwa wakati wake. Hutaweza kusema mpaka hayo niliyokuambia yatakapotimia."
21Ande kodia vriama le kolaver narodo azhukerenas o Zechariah, ai chudinaspe sostar beshel kadia but vriama kotse andre tampla.
21Wakati huo, wale watu walikuwa wanamngoja Zakariya huku wakishangaa juu ya kukawia kwake Hekaluni.
22Kana anklisto avri nashti delas lensa duma, ai o narodo aliardia ke O Del sikadiasas leske vari so ande tampla. Wo sikavelas lenge le vastensa numa nashti delas duma.
22Alipotoka nje, hakuweza kusema nao. Ikawa dhahiri kwao kwamba alikuwa ameona maono Hekaluni. Lakini akawa anawapa ishara kwa mikono, akabaki bubu.
23Kana o Zechariah getosardia peski vriama kai trobulas te podail ande tampla, gelo peste khere.
23Zamu yake ya kuhudumu ilipokwisha, alirudi nyumbani.
24Xantsi vriama pala kodia e Elizabeth leski rhomni pharisas, ai garadile panzh shon ando kher.
24Baadaye Elisabeti mkewe akapata mimba. Akajificha nyumbani kwa muda wa miezi mitano, akisema:
25Woi motholas ande peste, "Eta, so kerdia O Del mange, manglia te ankalavel ma akana so sas mange lazhav anglal manush!"
25"Hivi ndivyo alivyonitendea Bwana; ameniangalia na kuniondolea aibu niliyokuwa nayo mbele ya watu."
26Ai ando shovto shon O Del tradia o angelo kai bushol Gabriel andek foro kai bushol Galilee ando Nazareth.
26Mnamo mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu aende kwenye mji uitwao Nazareti huko Galilaya,
27Kai iek shei bari kai trobulas te ansurilpe ieke manushesa kai bushol Josef, wo sas andai vitsa le amperatoski o David, o anav kodola zhuvliako kay sas shei bari busholas Maria.
27kwa msichana mmoja aitwaye Maria, mchumba wa mtu mmoja jina lake Yosefu, wa ukoo wa Daudi.
28O angelo gelo late khere ai phendia lake, "Pacha tuke, tu kai O Del andia mishtimos, O Del tusa."
28Malaika akamwendea, akamwambia, "Salamu Maria! Umejaliwa neema nyingi! Bwana yu pamoja nawe."
29E Maria daraili xantsi palal vorbia kai phendia lake, ai gindilas pa so phendia lake o angelo,
29Maria aliposikia maneno hayo alifadhaika sana, akawaza: maneno haya yanamaanisha nini?
30O angelo phendia lake, "Na dara, Maria, ke drago sanas le Devleske.
30Malaika akamwambia, "Usiogope Maria, kwa maana Mungu amekujalia neema.
31Si te aves phari ai avela tu iek shav kai desa les o anav Jesus.
31Utachukua mimba, utamzaa mtoto wa kiume na utampa jina Yesu.
32Baro avela ai akharena les O Shav le Devlesko kai si opre. O Del kerela anda leste amperato, sar sas o David, kodo kai sas mai anglal lestar.
32Yeye atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Mungu Mkuu. Bwana Mungu atampa kiti cha mfalme Daudi, babu yake.
33Ai poronchila po narodo kai si ande Israel kai bushon zhiduvuria sagda, ai leski amperetsia shoxar chi getolpe!"
33Kwa hivyo atautawala ukoo wa Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho."
34E Maria phendia le angeloske, "Sar sai kerdiola so mothos mange, ke shei bari sim?"
34Maria akamjibu, "Yatawezekanaje hayo, hali mimi ni bikira?"
35O angelo dia atweto, "O Swunto Duxo avela pe tute, ai e putiera le Devleski. Vusharela tu sar iek vushalin, anda kodia avela akhardo Swunto O Shav le Devlesko ek glata kai kerdiola.
35Malaika akamjibu, "Roho Mtakatifu atakushukia, na uwezo wake Mungu Mkuu utakujia kama kivuli; kwa sababu hiyo, mtoto atakayezaliwa ataitwa Mtakatifu, Mwana wa Mungu.
36Ai eta, Elizabeth chi vara, vi woi azhukerel iek shav. Marka ke si phuri, mothonas ke nashti avela glate, ai akana ka pesko shovto shon la.
36Ujue pia kwamba hata Elisabeti, jamaa yako, naye amepata mimba ingawa ni mzee, na sasa ni mwezi wa sita kwake yeye ambaye watu walimfahamu kuwa tasa.
37Ke kanchi nai so O Del nashti kerel."
37Kwa maana hakuna jambo lisilowezekana kwa Mungu."
38Antunchi Maria phendia, "Me sim e sluga Devleski, te avel mange sar tu phenes", ai o angelo gelotar.
38Maria akasema, "Mimi ni mtumishi wa Bwana, nitendewe kama ulivyosema." Kisha yule malaika akaenda zake.
39Ande kodia vriama e Maria sigo gelitar karing le plaia andek gav kai sas ande Judea.
39Siku kadhaa baadaye, Maria alifunga safari akaenda kwa haraka hadi mji mmoja ulioko katika milima ya Yuda.
40Geli ando kher ka Zechariah ai dia dies lasho kai Elizabeth.
40Huko, aliingia katika nyumba ya Zakariya, akamsalimu Elisabeti.
41Kana Elizabeth ashundia so phendia lake e Maria, o glata mishtisailo ande late. Elizabeth pherdo sas le Swuntone Duxosa.
41Mara tu Elisabeti aliposikia sauti ya Maria, mtoto mchanga tumboni mwake Elisabeti akaruka. Naye Elisabeti akajazwa Roho Mtakatifiu,
42Ai tsipisardia zurales. "O Del swuntsosardia tu mai but ke sar sa le zhuvlia ai lesko swuntsomos beshel pe glata kai avela tu!
42akasema kwa sauti kubwa, "Umebarikiwa kuliko wanawake wote, naye utakayemzaa amebarikiwa.
43Kon si me, kai e dei murhi Devleski avel mande?
43Mimi ni nani hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
44Ke dikhes kana ashundem ke dian ma dies lasho o glata mishtisailo raduimastar ande mande.
44Nakwambia, mara tu niliposikia sauti yako, mtoto mchanga tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
45Tu raduime san kai pachaian tu so sas tuke phendo katar O Del ai kerdiola!"
45Heri yako wewe uliyesadiki kwamba yatatimia yale Bwana aliyokwambia."
46E Maria phendia, "Murho ilo naisil o barimos le Devlesko;
46Naye Maria akasema,
47Murho ilo pherdo raduimos lo pala Del murho skepitori.
47"Moyo wangu wamtukuza Bwana, roho yangu inafurahi kwa sababu ya Mungu Mwokozi wangu.
48O Del dikhlia pe mande, leski sluga kai nai kanch! Numa akana ai sagda sa o manush akharena ma raduime.
48Kwa kuwa amemwangalia kwa huruma mtumishi wake mnyenyekevu. Hivyo tangu sasa watu wote wataniita mwenye heri.
49Ke O Del kai si les e putiera kerdia mange lasho dieli. Lesko anav si Swunto.
49Kwa kuwa Mwenyezi Mungu amenitendea makuu, jina lake ni takatifu.
50Sikavel leski mila sagda ka kodola kai daran lestar, katar e vitsa po vitsa.
50Huruma yake kwa watu wanaomcha hudumu kizazi hata kizazi.
51Kerdia bare dieli leske vastesa, le zuralesa lia pal manush le barimata kai sas le ande ilo.
51Amefanya mambo makuu kwa mkono wake: amewatawanya wenye kiburi katika mawazo ya mioyo yao;
52Lia le amperaton anda penge amperetsia ai dia iek than kai si opre kal manush kai si lashe.
52amewashusha wenye nguvu kutoka vitu vyao vya enzi, akawakweza wanyenyekevu.
53Wo dia but lashimos ka kodola kai sas bokhale, ai tradia palpale le barvalen le vastensa mange.
53Wenye njaa amewashibisha mema, matajiri amewaacha waende mikono mitupu.
54Wo garado leski vorba kai shinado sas ka le Zhidovon, ai avilo te zhutil leske naroduria le Zhidovon.
54Amemsaidia Israeli mtumishi wake, akikumbuka huruma yake.
55Chi busterdia te sikavel leski mila karing o Abraham ai kodola kai sas mai palal lestar sagda.
55Kama alivyowaahidia wazee wetu Abrahamu na wazawa wake hata milele."
56E Maria beshli peska varasa Elizabeth trin shon, porme gelitar peste khere.
56Maria alikaa na Elisabeti kwa muda upatao miezi mitatu, halafu akarudi nyumbani kwake.
57Kana e vriama avili kai Elizabeth trobulas te avel la iek glata sas la iek shav.
57Wakati wa kujifungua kwake Elisabeti ulifika, akajifungua mtoto wa kiume.
58O narodo kai beshelas pashai Elizabeth ai lake naimuria dine po gor ke O Del dias la kodo mishtimos, vi won raduisaile lasa.
58Jirani na watu wa jamaa yake walipopata habari kwamba Bwana amemwonea huruma kubwa, walifurahi pamoja naye.
59Kana o tsinorho sas kurkesko avile te shinen kotor anda lesko boriko; ai mangenas te del anav peske dadesko Zechariah,
59Halafu siku ya nane walifika kumtahiri mtoto, wakataka kumpa jina la baba yake, Zakariya.
60numa leski dei phendia, "Nichi, Iovano busholas." Numa phende lake,
60Lakini mama yake akasema, "La, sivyo, bali ataitwa Yohane."
61"Na khonik ande chi familia kai si les kado anav!"
61Wakamwambia, "Mbona hakuna yeyote katika ukoo wake mwenye jina hilo?"
62Antunchi phushle le vastensa le dades, te zhanen sar mangel te akharel o shav.
62Basi, wakamwashiria baba yake wapate kujua alitaka mtoto wake apewe jina gani.
63O Zechariah manglia iek skafidi te ramol ai ramosardia, "Iovano busholas." ai savorhe chudisaile!
63Naye akaomba kibao cha kuandikia, akaandika hivi: "Yohane ndilo jina lake." Wote wakastaajabu.
64Strazo o Zechariah sai delas duma ai liape te naisil le Devles zurales.
64Papo hapo midomo na ulimi wake Zakariya vikafunguliwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
65Katar godi antunchi sa narodo kai beshelas pasha leste daraile, ai sa e viasta pa so kerdili geli kruglom karing le plaia ande Judea.
65Hofu ikawaingia jirani wote, na habari hizo zikaenea kila mahali katika milima ya Yudea.
66Kon godi ashunelas so kerdilia denas pe goji ai denas pe duma, so avela kodia glata e putiera le Devleski sas chaches lesa.
66Wote waliosikia mambo hayo waliyatafakari mioyoni mwao wakisema: "Mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?" Maana, hakika nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye.
67O Zechariah, o dat la glatako sas pherdo le Swuntone Duxosa, ai dia duma E Vorba le Devleski.
67Zakariya, baba yake mtoto, akajazwa Roho Mtakatifu, akatamka ujumbe wa Mungu:
68Luvudime te avel le Devles, O Del le Zhidovongo, ke andia te lia sama pe pesko narodo ai skepisardia les.
68"Asifiwe Bwana Mungu wa Israeli, kwani amekuja kuwasaidia na kuwakomboa watu wake.
69Dia ame iek putiera ai iek skepitori amenge kai sam andai vitsa le amperatoski o David leski sluga.
69Ametupatia Mwokozi shujaa, mzawa wa Daudi mtumishi wake.
70Kadia si kai phendias, de mult katar swuntso profeturia:
70Aliahidi hapo kale kwa njia ya manabii wake watakatifu,
71Phendiasas te skepil ame katar amare duzhmaia; ai katar e putiera katar kodola kai sam lenge griatsa.
71kwamba atatuokoa mikononi mwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.
72Inker sikavela peski mila amenge sar si kadia kodolenge kai sas mai anglal amendar, ai serela pe peski swinto vorba kai phendiasas te beshel amensa;
72Alisema atawahurumia wazee wetu, na kukumbuka agano lake takatifu.
73Ke O Del phendiasas le Abramoske kadala dieli kai sas mai anglal amendar.
73Kiapo alichomwapia Abrahamu baba yetu, ni kwamba atatujalia sisi
74Te ankalavel ame katar e putiera amare duzhmange, ai te podaisaras le Devles bi darako;
74tukombolewe kutoka adui zetu, tupate kumtumikia bila hofu,
75Te sai avas swintsi ai vorta angla Del, swako dies ande amaro traio.
75kwa unyofu na uadilifu mbele yake, siku zote za maisha yetu.
76Ai tu, murho tsinorho, avesa akhardo o profeto le Devlesko kai si opre, ke phiresa angla Del te lashares lesko drom;
76Nawe mwanangu, utaitwa, nabii wa Mungu Mkuu, utamtangulia Bwana kumtayarishia njia yake;
77Ai te sikaves leske narodoske ke skepila le kana iertila lenge bezexa.
77kuwatangazia watu kwamba wataokolewa kwa kuondolewa dhambi zao.
78Ke amaro Del lasholo, ai kerela te strefial pe amende iek vediara kai avel opral.
78Mungu wetu ni mpole na mwenye huruma. Atasababisha pambazuko angavu la ukombozi litujie kutoka juu,
79Te sikavel e vediara kodolenge kai si ando tuniariko ai kai si ande vushalin la martiake, te ingerel amare punrhe po drom la pachako."
79na kuwaangazia wote wanaokaa katika giza kuu la kifo, aongoze hatua zetu katika njia ya amani."
80Ai tsinorho bariolas ai o Swunto Duxo le Devlesko lel les zor ande leste. Wo beshlo ande pusta zhi ka dies kai sikadilo kal Zhiduvuria.
80Mtoto akakua, akapata nguvu rohoni. Alikaa jangwani mpaka alipojionyesha rasmi kwa watu wa Israeli.