1O Jesus mai phendia peske slugenge, "Iek manush barvalo sas les iek manush kai lelas sama katar lesko kher ai phuvia; ai andek dies vari kon phendia leske ke o manush kai lelas sama katar lesko kher ai phuvia zidilas pesko love.
1Yesu aliwaambia wanafunzi wake: "Tajiri mmoja alikuwa na karani wake. Huyu karani alichongewa kwamba alitumia ovyo mali ya tajiri wake.
2O gazda akhardia les, ai phendia leske, "So ashunav pa tute? Phen mange sar kerdian le dielensa kai thodem tu te les sama; ke nashti mai mekav tu te le sama katar murho kher vai phuvia."
2Yule tajiri akamwita akamwambia: Ni mambo gani haya ninayosikia juu yako? Toa hesabu ya mapato na matumizi ya mali yangu, kwa maana huwezi kuwa karani tena.
3"O manush kai lelas sama katar o kher ai phuvia phenelas ande peste, "So te kerav akana? Kai murho gazda chi mai mekel ma te lav sama katar lesko kher ai phuvia: Nashti lasharav e phuv; lazhav mange te mangav zhutimos.
3Yule karani akafikiri: Bwana wangu amenifukuza kazi ya ukarani; nitafanya nini? Kwenda kulima siwezi; kwenda kuombaomba kama maskini ni aibu.
4Zhanav so kerava, kana gonila ma murho gazda, avela mange vortacha te primina ma pe lenge khera."
4Naam, najua la kufanya, ili nitakapofukuzwa kazi, watu waweze kunikaribisha nyumbani kwao.
5Antunchi akhardia iek po iek sa kukulen kai kamenas vari so peske gazdaske, ai phendia le pervoneske, "Sode kames murhe gazdaske?"
5Basi, akawaita wadeni wa bwana wake, mmoja mmoja, akamwambia yule wa kwanza: Unadaiwa kiasi gani na bwana wangu?
6"Iek shel bidoia vuloi," phendia leske. Ai wo phendia leske, "Le cho tiketo, sigo besh tele, ai ramosar panvardesh."
6Yeye akamjibu: Mapipa mia ya mafuta ya zeituni. Yule karani akamwambia: Chukua hati yako ya deni, keti haraka, andika hamsini.
7Porme phendia avreske, "Sode kames tu?" Phendia, "Iek shel musuri jiv. Ai wo phendia leske, "Le cho tiketo, ai ramosar oxtovardesh."
7Kisha akamwuliza mdeni mwingine: Wewe unadaiwa kiasi gani? Yeye akamjibu: Magunia mia ya ngano. Yule karani akamwambia: Chukua hati yako ya deni, andika themanini.
8Antunchi o manush barvalo phendia ka o bezexalo manush kai lelas sama katar lesko kher ai phuvia, "Kerdia mishto," Ke le manush anda kadia lumia si ande lengi vitsa mai gojaver de sar le manush la vediaraki.
8"Basi, yule bwana akamsifu huyo karani asiye mwaminifu, kwa kuwa alitumia busara. Kwa maana watu wa dunia hii wana busara zaidi na mambo yao kuliko watu wa mwanga."
9"Ai me phenav tumenge, keren tumenge vortacha le barvalimasa kadala phuviako, saxke, kana chi mai avela tume, won sai primina tume andek kher kai chi mai getolpe.
9Naye Yesu akaendelea kusema, "Nami nawaambieni, jifanyieni marafiki kutokana na mali ya dunia, ili zitakapowaishieni, mweze kupokewa nao katika makao ya milele.
10Kodo kai si lasho andel tsinorhe dieli si lasho vi andel bare; ai kodo kai nai lasho andel tsinorhe dieli vi andel bare nai lasho.
10Yeyote aliye mwaminifu katika mambo madogo, atakuwa mwaminifu katika mambo makubwa; na yeyote asiye mwaminifu katika mambo madogo, hatakuwa mwaminifu katika mambo makubwa.
11Te chi sanas lasho le barvalimasa la lumiako, kon jinel pe tute le barvalimasa chacho?
11Kama basi, ninyi si hamjawa waaminifu mali mbaya za dunia, ni nani atakayewakabidhi zile mali za kweli?
12Ai te chi sanas lasho andel kolavreske dieli, kon dela tume so si tumaro?
12Na kama hamjakuwa waaminifu katika mali ya mtu mwingine, ni nani atakayewakabidhi mali yenu wenyewe?
13Chi iek sluga nashti podail duie gazdan; ke wo gretsola iek ai leske drago o kolaver; astardiola ka iek, vai vurhitsila le kolavres. Nashti podais le Devles ai le love."
13"Hakuna mtumishi awezaye kuwatumikia mabwana wawili; kwa maana atamchukia mmoja na kumpenda mwingine, au ataambatana na mmoja na kumdharau mwingine. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali."
14Le Farizeanuria ashunde so phendia O Jesus, ai marenas mui lestar ke lenge drago sas le love.
14Lakini Mafarisayo waliposikia hayo, kwa vile wao walikuwa wanapenda sana fedha, wakamdharau Yesu.
15O Jesus phendia lenge, "Tume roden te kerdion vorta angal manush, numa O Del zhanel tumare ile; ke so miazol baro le manushenge nai kanch angla Del.
15Hapo akawaambia, "Ninyi mnajifanya wema mbele ya watu, lakini Mungu anaijua mioyo yenu. Kwa maana kile kinachoonekana kuwa kitukufu mbele ya watu, Mungu anakiona kuwa takataka.
16O zakono le Mosesoske ai o ramomos le profetonge ashile zhi kai vriama le Iovanoske o baptisto; de katar kodia vriama e lashi viasta pa e amperetsia le Devleski phendi la, ai swako zumavel peska zorasa te del andre.
16"Sheria na maandishi ya manabii vilikuweko mpaka wakati wa Yohane mbatizaji. Tangu hapo, Ufalme wa Mungu unahubiriwa, na kila mmoja anauingia kwa nguvu.
17Mai vushoro o cheri ai e phuv te naken, de sar e mai tsinorhi vorba kai si ando zakono te nakhel (te faltil).
17Lakini ni rahisi zaidi mbingu na dunia kupita, kuliko hata herufi moja ya Sheria kufutwa.
18Kon godi kai dela drom peska rhomnia ai ansurilpe avriasa, kerdia kurvia; ai kon godi ansurilape zhuvliasa kai meklia la, lako rhom pale kerdia kurvia.
18"Yeyote anayemwacha mke wake na kuoa mwingine, anazini; na yeyote anayemwoa mwanamke aliyepewa talaka, anazini.
19"Sas ek manush barvalo, kai vuriarelaspe andel mai shukar tsalia ai le mai kuchi, ai swako dies sas les shukar traio ai xalas lasho xabe.
19"Palikuwa na mtu mmoja tajiri, ambaye alikuwa anavaa mavazi ya bei kubwa sana ya rangi ya zambarau, na ya kitani safi, na kufanya sherehe kila siku.
20Sas iek manush chorho kai busholas Lazarus, beshelas pasha lesko vudar, peske pugniansa kai sas pe leste.
20Kulikuwa pia na maskini mmoja jina lake Lazaro, aliyekuwa amejaa vidonda na alikuwa analazwa mlangoni pa nyumba ya huyo tajiri.
21Kamlino te xal le kozhi kai perenas pai skafidi le barvaleske; ai inker le zhukel mai avenas te den la shibasa pa leske pugnia.
21Lazaro alitamani kula makombo yaliyoanguka kutoka meza ya tajiri; na zaidi ya hayo, mbwa walikuwa wanakuja na kulamba vidonda vyake!
22O chorho manush mulo, ai le angeluria angerde les andel vas le Abrahamoske. Vi o barvalo mulo, ai groposarde les.
22"Ikatokea kwamba huyo maskini akafa, malaika wakamchukua, wakamweka karibu na Abrahamu. Na yule tajiri pia akafa, akazikwa.
23Ai ando iado wo vazdia leske iakha, ai de dural diklia le Abrahomos ai o Lazarus sas pasha leste.
23Huyo tajiri, alikuwa na mateso makali huko kuzimu, akainua macho yake, akamwona Abrahamu kwa mbali na Lazaro karibu naye.
24O barvalo manush tsipisardia, "Murho dat, Abraham, av tuke mila anda mande, ai trades o Lazarus te chindarel o gor peske naiesko ando pai, ai te chindarel murhi shib; ke chinuiv zurales ande kadia iag!"
24Basi, akaita kwa sauti: Baba Abrahamu, nionee huruma; umtume Lazaro angalau achovye ncha ya kidole chake katika maji, auburudishe ulimi wangu, maana ninateseka mno katika moto huu.
25Numa o Abraham phendia, "Murho shav, seres tu ke sas tu lashimos ande cho traio pe phuv, ai o Lazarus chinuisardia pe phuv; akana wo raduimelo ai tu chinuis."
25Lakini Abrahamu akamjibu: Kumbuka mwanangu, kwamba ulipokea mema yako katika maisha, naye Lazaro akapokea mabaya. Sasa lakini, yeye anatulizwa, nawe unateswa.
26Inker si mashkar amende ai mashkar tumende iek bari gropa, saxke kukula kai mangen te nakhen katsar, tumende vai tumendar, amende nashtin.
26Licha ya hayo, kati yetu na ninyi kumewekwa shimo kubwa, ili wanaotaka kuja kwenu kutoka huku wasiweze, wala wanaotaka kutoka kwenu kuja kwetu wasiweze.
27Porme o barvalo manush phendia, "Rhugiv ma tute, murho dat, O Abraham, trade o Lazarus ando kher murho dadesko:
27Huyo aliyekuwa tajiri akasema: Basi baba, nakuomba umtume aende nyumbani kwa baba yangu,
28Ke si ma pansh phral; te mothol lenge te arakhenpe, te na aresen vi won ande parha."
28maana ninao ndugu watano, ili awaonye wasije wakaja huku kwenye mateso.
29O Abraham phendia leske, "Si le o ramomos le Mosesosko ai le profetongo te phenen lenge, ashunen lende." Ai o barvalo manush phendia,
29Lakini Abrahamu akamwambia: Ndugu zako wanao Mose na manabii; waache wawasikilize hao.
30"Nichi, murho dat, Abraham; numa te zhala vari kon andal mule karing lende, antunchi keinape."
30Lakini yeye akasema: Sivyo baba Abrahamu, ila kama mtu atafufuka kutoka wafu na kuwaendea, watatubu.
31Numa o Abraham phendia leske, "Te na ashunena so mothol o Moses ai le profeturia, won chi pachana vi te zhuvindil vari kon andal mule."
31Naye Abrahamu akasema: Kama hawawasikilizi Mose na manabii, hawatajali hata kama mtu angefufuka kutoka wafu."