Romani: New Testament

Swahili: New Testament

Luke

4

1O Jesus pherdo sas le Swuntone Duxosko kana gelotar katar o Jordan, ai sas angerdo katar O Swunto Duxo ande pusta.
1Yesu alitoka katika mto Yordani akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akaongozwa na Roho mpaka jangwani.
2Kotse zumadia les o beng shtarvardesh dies ai chi xalia kanchi sa kodola dies, ai kana nakhle kodola dies bokhailo.
2Huko alijaribiwa na Ibilisi kwa muda wa siku arubaini. Wakati huo wote hakula chochote, na baada ya siku hizo akasikia njaa.
3Antunchi o beng phendia leske, "Te san tu O Shav le Devlesko, phen kadale bax te kerdion manrho."
3Ndipo Ibilisi akamwambia, "Kama wewe ni Mwana wa Mungu, amuru jiwe hili liwe mkate."
4O Jesus dia les atweto, "E Vorba le Devleski mothol, 'O manush nashtil traiil ferdi anda manrho,'"
4Yesu akamjibu, "Imeandikwa: Mtu haishi kwa mkate tu."
5Porme o beng angerdia les mai opre, ai sikadia leske strazo sa le amperetsi la phuviake.
5Kisha Ibilisi akamchukua hadi mahali pa juu, akamwonyesha kwa mara moja falme zote za ulimwengu. Huyo Shetani akamwambia,
6O beng phendia ka Jesus, "Dava tu sakadia putiera ai o barvalimos kadale amperetsiango, sa kadala dieli sas dini mange ai me sai dav le kaske mangav.
6"Nitakupa uwezo juu ya falme zote hizi na fahari zake, kwa maana nimepewa hivi vyote; nikitaka kumpa mtu ninaweza.
7Ferdi te desa changa angla mande dav le sa tuke."
7Hivi vyote vitakuwa mali yako wewe, kama ukiniabudu."
8O Jesus dia les atweto, "E Vorba le Devleski mothol, 'Rhugisavo ka cho Del ai ferdi les podaisar.'"
8Yesu akamjibu, "Imeandikwa: Utamwabudu Bwana Mungu wako, na utamtumikia yeye peke yake."
9Antunchi o beng angerdia les ando Jerusalem ai thodia les ta opre pe tampla, ai phendia les, "Te san tu O Shav le Devlesko, shude tu katsar tele.
9Ibilisi akamchukua mpaka Yerusalemu, kwenye mnara wa Hekalu, akamwambia, "Kama wewe ni Mwana wa Mungu,
10Ke ramome ande Vorba le Devleski, 'Ke O Del dela ordina peske angelon te arakhen tu.'
10kwa maana imeandikwa: Atawaamuru malaika wake wakulinde,
11Ai phenel, 'Ankerena tu pe penge vas te na dukhaves cho punrho po bax.'"
11na tena, Watakuchukua mikononi mwao usije ukajikwaa mguu wako kwenye jiwe."
12O Jesus dia les atweto, "E Vorba le Devleski mothol, 'Na zumav che Devles.'"
12Lakini Yesu akamjibu, "Imeandikwa: Usimjaribu Bwana Mungu wako."
13Kana o beng getosardia te zumavel le Kristos sar wo manglia, wo meklia les xantsi vriama.
13Ibilisi alipokwishamjaribu kwa kila njia, akamwacha kwa muda.
14O Jesus gelo palpale ande Galilee, ande putiera le Swuntone Duxoski. Sa o narodo delas duma pa leste kotsar.
14Yesu alirudi Galilaya akiwa amejaa nguvu za Roho Mtakatifu, na habari zake zikaenea katika sehemu zote za jirani.
15Wo sicharelas ande le synagoguria ai sa o narodo luvudisardia les.
15Naye akawa anawafundisha watu katika masunagogi yao, akasifiwa na wote.
16O Jesus gelo ando Nazareth kotse kai barilo sas, iek dies kana sas Sabato gelo ande synagogue sar kerelas butivar. Wushtilo opre te jinel E Vorba le Devleski.
16Basi, Yesu alikwenda Nazareti, mahali alipolelewa, na siku ya Sabato, aliingia katika sunagogi, kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama ili asome Maandiko Matakatifu kwa sauti.
17Dine les e klishka le profetoske kai busholas Isaiah. Phuterdia la ai arakhlia kai si ramome,
17Akapokea kitabu cha nabii Isaya, akakifungua na akakuta mahali palipoandikwa:
18"O Swunto Duxo le Devlesko pe mandelo, wo alosardia ma te anav e lashi viasta kal chorhe. Wo tradia ma te anav o skepimos kodolenge kai si phangle, ai te sastiarav le korhen, te skepiv le manushen kai si chinuime.
18"Roho wa Bwana yu juu yangu, kwani amenipaka mafuta niwahubirie maskini Habari Njema. Amenituma niwatangazie mateka watapata uhuru, vipofu watapata kuona tena; amenituma niwakomboe wanaoonewa,
19Te mothav o bersh kai sikadiola o lashimos le Devlesko."
19na kutangaza mwaka wa neema ya Bwana."
20Porme O Jesus phandadia e klishka ai dia la kal slugi la synagogaki ai beshlo tele. Sa o narodo kai sas ande synagogue dikhenas pe leste.
20Baada ya kusoma, akafunga kile kitabu, akampa mtumishi, kisha akaketi; watu wote wakamkodolea macho.
21Ai wo antunchi mothon lenge, "So jindem ande Vorba le Devleski sikadilia adies kana tume ashundian so jindem."
21Naye akaanza kuwaambia, "Andiko hili mlilosikia likisomwa, limetimia leo."
22Savorhe raduimesas karing O Jesus ai chudinaspe andal shukar vorbi kai motholas.
22Wote wakavutiwa sana naye, wakastaajabia maneno mazuri aliyosema. Wakanena, "Je, huyu si mwana wa Yosefu?"
23Ai mothonas, "Nai kado o shav le Josefosko?" O Jesus phendia lenge, "Suguro si te mothol mange, 'Dokxtoro, sastiar tu tut.' Ai vi mothon mange, 'Ashundiam, so godi kerdian ando foro kai bushol Capernaum, kerdian sa kodola dieli katse ande cho foro.'"
23Naye akawaambia, "Bila shaka mtaniambia msemo huu: Mganga jiponye mwenyewe, na pia mtasema: Yote tuliyosikia umeyafanya kule Kafarnaumu, yafanye hapa pia katika kijiji chako."
24Porme mai phendia, "Phenav tumenge o chachimos, 'Chi iek profeto nai premisardo ande pesko foro kai kerdilo.
24Akaendelea kusema, "Hakika nawaambieni, nabii hatambuliwi katika kijiji chake.
25Ashun mange, suguro ke sas but phivlia ande Israel, ande vriama kai sas o Elijah kana o breshind chi dia trin bersh ai dopash, ai ma nas xaben ando them.
25Lakini, sikilizeni! Kweli kulikuwa na wajane wengi katika nchi ya Israeli nyakati za Eliya. Wakati huo mvua iliacha kunyesha kwa muda wa miaka mitatu na nusu; kukawa na njaa kubwa katika nchi yote.
26Ai O Del chi tradia kudules kai bushol Elisha lende numa kai ek zhuvli ka ma nas la rhom kai traiilas andek foro kai busholas Zarephath karing Sidon.
26Hata hivyo, Eliya hakutumwa kwa mjane yeyote ila kwa mwanamke mjane wa Sarepta, Sidoni.
27Ai sas vi but lepuria (manush kai chirniolas ka lenge morchi) ando Israel kana sas o profeto o Elisha, inker chi iek anda lende chi sastilo, numa iek manush kai busholas Namaan ande Syria."
27Tena, katika nchi ya Israeli nyakati za Elisha kulikuwa na wenye ukoma wengi. Hata hivyo, hakuna yeyote aliyetakaswa ila tu Naamani, mwenyeji wa Siria."
28Savorhe ande synagogue sas xoliariko kana ashunde kodola vorbi.
28Wote waliokuwa katika lile sunagogi waliposikia hayo walikasirika sana.
29Wushtilo opre, angerde O Jesus avri anda foro ai angerde les opre po plai kai lengo foro sas kerdo, te shuden les tele.
29Wakasimama, wakamtoa nje ya mji wao uliokuwa umejengwa juu ya kilima, wakampeleka mpaka kwenye ukingo wa kilima hicho ili wamtupe chini.
30Numa O Jesus nakhlo mashkar lende ai gelotar.
30Lakini Yesu akapita katikati yao, akaenda zake.
31Antunchi O Jesus gelo ando Capernaum, o foro ande Galilee, kai sicharelas le narodos dies savatosko.
31Kisha Yesu akashuka mpaka Kafarnaumu katika mkoa wa Galilaya, akawa anawafundisha watu siku ya Sabato.
32Kodo narodo chudimesas sar sicharelas, ke O Jesus delas duma putierasa.
32Wakastaajabia uwezo aliokuwa nao katika kufundisha.
33Ande synagogue sas iek manush kai sas ande leste ek beng; kodo manush tsipilas zurales.
33Na katika lile sunagogi kulikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na roho ya pepo mchafu; akapiga ukelele wa kuziba masikio:
34"So manges amendar, Jesus andai Nazareth? Tu avilian te mudares ame? Zhanav mishto ke O Swunto san kai si tradino karar O Del!"
34"We! Yesu wa Nazareti! Kwa nini unatuingilia? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakufahamu wewe ni nani. Wewe ni mjumbe Mtakatifu wa Mungu!"
35O Jesus dia duma zurales le bengesa, ai dia les ordina te na mai del duma ai te anklel avri anda manush! O beng peredia kodole manushes pe phuv angla sa o narodo ai anklisto avri anda leste, bi te kerel leske chi iek baio.
35Lakini Yesu akamkemea huyo pepo akisema: "Nyamaza! Mtoke mtu huyu!" Basi, huyo pepo baada ya kumwangusha yule mtu chini, akamtoka bila kumdhuru hata kidogo.
36Sa o narodo chudisailo ai mothonas iek kavreske, "Savata vorba? Kado manush del ordina putierasa ai zorasa le benges ai anklel avri!"
36Watu wote wakashangaa, wakawa wanaambiana, "Hili ni jambo la ajabu, maana kwa uwezo na nguvu anawaamuru pepo wachafu watoke, nao wanatoka!"
37Ai porme katar godi o narodo delas duma pa Jesus ande kodo foro.
37Habari zake zikaenea mahali pote katika mkoa ule.
38O Jesus gelotar andai synagogue ai gelo ka Simon leste khere. E sakra le Simonoski sas la e baro zharo, ai mangle katar O Jesus te sastiarel la.
38Yesu alitoka katika lile sunagogi, akaenda nyumbani kwa Simoni. Mama mmoja, mkwewe Simoni, alikuwa na homa kali; wakamwomba amponye.
39Pashilo karing late, ai dia duma zurales ai dia ordina le zharos, ai o zharo gelotar pa late, wushtilo opre ai podaisardia les.
39Yesu akaenda akasimama karibu naye, akaikemea ile homa, nayo ikamwacha. Mara yule mama akainuka, akawatumikia.
40Kana o kham pelo tele, sa kodola kai sa le naswale kai sas len but fialuria naswalimata. Andine le ka Jesus ai thodia le vas pe lende ai sastiardia le.
40Jua lilipokuwa linatua, wote waliokuwa na wagonjwa wao mbalimbali waliwaleta kwake; naye akaweka mikono yake juu ya kila mmoja wao, akawaponya wote.
41Ai vi but benga ankliste avri anda lende, ai tsipinas, "Tu san O Shav le Devlesko!" Numa O Jesus dias le trad te na mothon, ke zhanenas won ke wo sas o skepitori.
41Pepo waliwatoka watu wengi, wakapiga kelele wakisema: "Wewe u Mwana wa Mungu!" Lakini Yesu akawakemea, wala hakuwaruhusu kusema, maana walimfahamu kwamba yeye ndiye Kristo.
42Kana phuterdilo o dies O Jesus anklisto avri anda foro, ai gelotar vari kai te avel korkorho. But narodo rodelas les, kana arakhle les mangenas te ankeren les ai te na meken te zhaltar lendar.
42Kesho yake asubuhi Yesu aliondoka akaenda mahali pa faragha. Watu wakawa wanamtafuta, na walipofika mahali alipokuwa, wakajaribu kumzuia ili asiondoke kwao.
43Numa O Jesus phendia lenge, "Trobul te phenav e lashi viasta le rhaioski le Devleski ande kolaver foruria, ke anda kodia O Del tradia ma."
43Lakini yeye akawaambia, "Ninapaswa kuhubiri Habari Njema za Ufalme wa Mungu katika miji mingine pia, maana nilitumwa kwa ajili hiyo."
44Vi delas duma pa Del ande le synagoguria ande Galilee.
44Akawa anahubiri katika masunagogi ya Yudea.