Romani: New Testament

Swahili: New Testament

Mark

15

1Kana phuterdilo o dies sa le bare rasha, ai le phure kai poronchinas, ai le Gramnoturia avile andek than te den duma pa O Jesus. Ashshile te phanden les, ai ningerde les ka Pilate.
1Kulipopambazuka, makuhani wakuu walifanya shauri pamoja na wazee, walimu wa Sheria na Baraza lote, wakamfunga Yesu pingu, wakampeleka na kumkabidhi kwa Pilato.
2Ai o Pilato phushlia les, "Tu san O Amperato le Zhidovongo?" O Jesus phendia leske, "Sar tu phendian."
2Pilato akamwuliza Yesu, "Je, wewe ni mfalme wa Wayahudi?" Yesu akajibu, "Wewe umesema."
3Ai le bare le rasha dosharde les, numa O Jesus chi phendia khanchi.
3Makuhani wakuu wakamshtaki Yesu mambo mengi.
4Ai o Pilato mai phushlia les, "Chi phenes khanchi? Chi ashunes sa le dosha kai phenen pa tute?"
4Pilato akamwuliza tena Yesu, "Je, hujibu neno? Tazama wanavyotoa mashtaka mengi juu yako."
5Numa O Jesus chi phendia khanchi; anda kadia o Pilato chudisailo.
5Lakini Yesu hakujibu neno, hata pilato akashangaa.
6Sas ek zakono ka o guvernori Pilate po Dies O Baro le Zhidovongo te mekel avri iekes ande temnitsa savo godi mangel o narodo.
6Kila wakati wa sikukuu ya Pasaka, Pilato alikuwa na desturi ya kuwafungulia mfungwa mmoja waliyemtaka.
7Sas phandado antunchi iek kai zhanglo liaspe ke de sa nasul lo, ai mudardia vari kas, lesko anav sas Barabbas. (Ande temnitsa sas iek kai busholas o Barabbas, peske dosha lensa anda iek mudarimos kai kerde ande bunto.)
7Basi, kulikuwa na mtu mmoja aitwaye Baraba, ambaye alikuwa amefungwa pamoja na waasi wengine kwa kusababisha uasi na mauaji.
8Sa o narodo gelo ka Pilate ai mangel lestar te kerel o zakono sar kerdia swako bersh.
8Watu wengi wakamwendea Pilato wakamwomba awafanyie kama kawaida yake.
9Numa o Pilato phendia lenge, "Mangen te mekav tumenge O Amperato le Zhidovongo?"
9Pilato akawauliza, "Je, mwataka niwafungulieni Mfalme wa Wayahudi?"
10Ke wo zhanglias sostar dine les ando vas, ke le rashan sas inetsia (zhaluzo) pe leste.
10Alisema hivyo kwa sababu alijua wazi kwamba makuhani wakuu walimkabidhi Yesu kwake kwa sababu ya wivu.
11Numa le bare le rasha dziliarde le manushen, ke won mangen o Pilato te mekel Barabbas lenge.
11Lakini makuhani wakuu wakawachochea watu wamwombe Pilato awafungulie Baraba.
12Ai o Pilato magdata phendia lenge, "So mangen te kerav kadalesa O Jesus kai mothon leske O Amperato le Zhidovongo?"
12Pilato akawauliza tena, "Basi, sasa mwataka nifanye nini na mtu huyu mnayemwita Mfalme wa Wayahudi?"
13Ai savorhe phende, "Tho les po trushul!"
13Watu wote wakapaaza sauti tena: "Msulubishe!"
14Porme o Pilato phendia lenge, "Sostar, che nasulimos kerdia?" Numa won mai zurales dine mui, "Tho les po trushul!"
14Lakini Pilato akawauliza, "Kwa nini! Amefanya kosa gani?" Lakini wao wakazidi kupaaza sauti, "Msulubishe!"
15O Pilato manglia te raduin le manushen, meklia lenge o Barabbas, ai marde O Jesusosa le bichosa, antunchi dias les te karfon les po trushul.
15Pilato alitaka kuuridhisha huo umati wa watu; basi, akamwachilia Baraba kutoka gerezani. Akaamuru Yesu apigwe viboko, kisha akamtoa asulubiwe.
16Le ketani ningerde les ando kher, kai bushol Praetorium; ai chidinisaile kruglom lestar ek antrego kompania ketani.
16Kisha askari walimpeleka Yesu ndani ukumbini, katika ikulu, wakakusanya kikosi kizima cha askari.
17Ai dine pe leste ek brazba raxami, ai kerde korona andal lunzhe kanrhe, ai thode la po lesko shero,
17Wakamvika vazi la rangi ya zambarau, wakasokota taji ya miiba, wakamwekea kichwani.
18ai phendias leske, "Lungo traio ka O Amperato le Zhidovongo!"
18Wakaanza kumsalimu, "Shikamoo Mfalme wa Wayahudi!"
19Ai line e rhai ai marde les pa shero lasa, ai chungarde pe leste, ai dine changa angla leste, ai luvudisarde les.
19Wakampiga kichwani kwa mwanzi, wakamtemea mate; wakampigia magoti na kumsujudia.
20Kana getosarde te maren mui lestar, line pa leste e brazba raxami, ai dine leske tsalia pe leste, ai ningerde les te karfon les po trushul.
20Baada ya kumdhihaki, walimvua lile joho, wakamvika nguo zake, kisha wakampeleka kumsulubisha.
21Po drom kai zhanas arakhle ieke manushes anda Cirene kai busholas Simon, o dat le Alexanderosko ai Rufusosko, ai thode les te ningerel o trushul.
21Walipokuwa njiani, walikutana na mtu mmoja aitwaye Simoni, mwenyeji wa Kurene. Yeye alikuwa baba wa Aleksanda na Rufo, na wakati huo alikuwa akitoka shambani. Basi, wakamlazimisha auchukue msalaba wa Yesu.
22Ai andine les ka kodo than kai bushol Golgatha. "O than kai miazol kokalo sheresko"
22Kisha wakampeleka Yesu mpaka mahali palipoitwa Golgotha, maana yake, "Mahali pa Fuvu la Kichwa."
23Dine les mol hamime drabensa te pel: chi pelias.
23Wakampa divai iliyochanganywa na manemane, lakini yeye akaikataa.
24Ai kana karfosarde les po trushul, hulade leske tsalia mashkar pende, ai thodepe te dikhen kon niril peski raxami.
24Basi, wakamsulubisha, wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura waamue nani angepata nini.
25Ai sas inia chasuria diminiatsi, ai karfosarde les.
25Ilikuwa saa tatu asubuhi walipomsulubisha.
26Opral pa lesko shero amblade ek ramomos kai phenelas che dosh ankerdesas pe leste, "O AMPERATO LE ZHIDOVONGO."
26Na mshtaka wake ulikuwa umeandikwa: "Mfalme wa Wayahudi."
27Ai lesa won karfosarde dui chor, iek ka lesko chacho vas, ai iek ka lesko stingo.
27Pamoja naye waliwasulubisha wanyang'anyi wawili, mmoja upande wake wa kulia na mwingine upande wake wa kushoto.
28Kadia kerdilia sar o ramomos phendia, won gindisarde pa leste sar iek manush kai phaglo o zakono.
28Hapo yakatimia Maandiko Matakatifu yanayosema, "Aliwekwa kundi moja na waovu."
29Le manush kai nakhenas kotsar, kerenas anda shero ai mishkirinas les, ai phenenas, "Tu kai sas te xaiis o tampla, ai ande trin dies te vazdes kadia tampla,
29Watu waliokuwa wanapita mahali hapo walimtukana, wakitikisa vichwa vyao na kusema, "Aha! Wewe mwenye kuvunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu!
30Skepisar tut, ai aidi tele pa trushul."
30Sasa, shuka msalabani ujiokoe mwenyewe!"
31Sakadia le bare le rasha ai le Gramnoturia marde mui lestar mashkar pende, "Skepisardias avren, numa nashti skepil pes."
31Nao makuhani wakuu pamoja na walimu wa Sheria walimdhihaki wakisema, "Aliwaokoa wengine, lakini kujiokoa mwenyewe hawezi!
32Mek O Kristo, O Amperato anda Israel, te avel tele pa trushul, ke mangas te dikhas ai pachas ame ande leste. Ai vi le dui kai sas thodine po trushul lesa marde mui lestar sakadia.
32Eti yeye ni Kristo, Mfalme wa Israeli! Basi, na ashuke msalabani ili tuone na kuamini." Hata watu wale waliosulubiwa pamoja naye walimtukana.
33Kal desh u dui po mashkar le diesesko avilo, tuniariko sas pe sa e lumia zhi kai trin chasuria.
33Tangu saa sita mchana mpaka saa tisa kulikuwa giza nchini kote.
34Karing le trin chasuria O Jesus dias mui andek baro glaso, "Eloi, Eloi, lema Sabachthani?" Kadia si, "Murho Del, Murho Del, Sostar meklian ma?"
34Saa tisa alasiri Yesu akalia kwa sauti kubwa, "Eloi, Eloi, lema sabakthani?" Maana yake, "Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?"
35Uni anda kodola kai sas kotse ashunde les, ai phende, "Eta, akharel o Elias."
35Baadhi ya watu waliosimama pale waliposikia hivyo, walisema, "Sikiliza! Anamwita Eliya!"
36Strazo iek anda lende grebisailo, lias ek kotor, thodias les ando lolo shut, thodias po khash ai zumadias te del ka Jesus te pel, phenel, "Mek les: Aven te dikhas te avela o Elias te skepil les."
36Mtu mmoja akakimbia, akachovya sifongo katika siki, akaiweka juu ya mwanzi, akampa anywe akisema, "Hebu tuone kama Eliya atakuja kumteremsha msalabani!"
37Antunchi O Jesus dias mui ando baro glaso ai dias pesko duxo opre, ai mulo.
37Yesu akapaaza sauti kubwa, akakata roho.
38Ai e zanaveski ande tampla ande donde de opral zhi tele (kai sas amblado opre ande tampla shindilo de opral zhi tele).
38Basi, pazia la Hekalu likapasuka vipande viwili toka juu mpaka chini.
39O fitsiri o Romano kai beshlo angla leste, dikhlia sar O Jesus dias mui ando baro glaso ai dias pesko duxo opre, ai mulo. Phendia "Chaches kado sas O Shav le Devlesko."
39Jemadari mmoja aliyekuwa amesimama mbele yake aliona jinsi Yesu alivyolia kwa sauti na kukata roho, akasema, "Kweli mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu!"
40Ai vi sas zhuvlia kotse kai dikhenas de dural: mashkar lende sas e Maria Magdalena, ai e Maria e dei le Iakovoski ai le Josefoski, ai Salomeski.
40Walikuwako pia wanawake waliotazama kwa mbali, miongoni mwao akiwa Maria toka mji wa Magdala, Salome, na Maria mama wa kina Yakobo mdogo na Yose.
41Kana wo sas ande Galilee, won linepe pala leste, ai podaisarde les; ai but kaver zhuvlia avile ka Jerusalem lesa.
41Hawa walimfuata Yesu alipokuwa Galilaya na kumtumikia. Kulikuwa na wanawake wengine wengi waliokuja Yerusalemu pamoja naye.
42Kana peli e riata, ke sas o dies mai anglal o lasharimos le Sabatosko.
42Wakati wa jioni ulikuwa umekwisha fika. Hiyo ilikuwa siku ya Maandalio, yaani siku inayotangulia Sabato.
43O Josef andai Arimathaea areslo, wo sas ek baro manush ande bar, ai vi wo azhukerelas e amperetsia le Devleski, ai tromailo te zhal ka o Pilato, te mangel le Jesusosko stato.
43Hapo akaja Yosefu mwenyeji wa Armathaya, mjumbe wa Baraza Kuu, aliyeheshimika sana. Yeye pia alikuwa anatazamia kuja kwa Ufalme wa Mungu. Basi, alimwendea Pilato bila uoga, akaomba apewe mwili wa Yesu.
44O Pilato chudisailo ke mulo kadia sigo, akhardia o kapitano anda le ketani, ai phushlia les, "Mulo kadia sigo?" Kana o Pilato ashundia so phendia o kapitano, o Pilato dias ordina te den les leste.
44Pilato alishangaa kusikia kwamba Yesu alikuwa amekwisha kufa. Basi, akamwita jemadari, akamwuliza kama Yesu alikuwa amekufa kitambo.
46O Josef lias o stato, ai vuluisardias les andek vuzho poxtan, ai thodias les ando nevo greposhevo kai sas shindo ando bax, ai spidias ek baro bax angla greposhevo.
45Pilato alipoarifiwa na huyo jemadari kwamba Yesu alikuwa amekwisha kufa, akamruhusu Yosefu auchukue mwili wake.
47Ai e Maria Magdalena, ai e Maria e dei le Josesosko dikhle kai thodia O Jesus.
46Hapo Yosefu akanunua sanda ya kitani, akauteremsha chini huo mwili, akauzungushia sanda. Akauweka katika kaburi lililokuwa limechongwa mwambani, kisha akavingirisha jiwe kubwa mbele ya mlango.
47Nao Maria Magdalene na Maria mama yake Yose walipaona hapo alipolazwa.