1Ai aresle pe kaver rig le paieske, ando them kai bushol Gadarenes.
1Basi, wakafika katika nchi ya Wagerase, ng'ambo ya ziwa.
2Ai kana anklisto avri anda chuno, strazo ek manush anklisto avri andal kaplitsi kai sas les ek bi vuzho ande leste.
2Mara tu Yesu aliposhuka mashuani, mtu mmoja aliyepagawa na pepo mchafu alitoka makaburini, akakutana naye.
3Kado manush beshelas andel kaplitsi; ai khonik nashti phandel les le lansuriansa.
3Mtu huyo alikuwa akiishi makaburini wala hakuna mtu aliyeweza tena kumfunga kwa minyororo.
4Ke butivar le manush phandesas les lantsonsa ai sastrensa pel punrhe, numa wo pharhadia le lantsuria ai le sastri kai sas pel punrhe ai vas. Khonik nashtil te aterdiol les ke sas les pra but zor.
4Mara nyingi walimfunga kwa pingu na minyororo lakini kila mara aliweza kuikata hiyo minyororo na kuzivunja hizo pingu, wala hakuna mtu aliyeweza kumzuia.
5Swako riat ai swako dies phirelas andel kaplitsi ai po plaia, tsipilas, ai shinelaspe le baxensa.
5Mchana na usiku alikaa makaburini na milimani akipaaza sauti na kujikatakata kwa mawe.
6Kana o manush kai sas les ek bi vuzho ande leste dikhlian O Jesus dur lestar, nashlia ai dia le changa angle leste.
6Alipomwona Yesu kwa mbali, alimkimbilia, akamwinamia
7Ai tsipisardia zurales, ai phendias, "So manges mandar, Jesus, tu, Shav le Devlesko? Phushav tut ando anav le Devlesko, na chinuisar ma."
7akisema kwa sauti kubwa, "Una shauri gani nami, wewe Yesu Mwana wa Mungu aliye juu? Kwa jina la Mungu, nakusihi usinitese!"
8Ke O Jesus phenelas leske, "Tu, bi vuzho, ankles avri anda leste."
8(Alisema hivyo kwa kuwa Yesu alikuwa amemwambia, "Pepo mchafu, mtoke mtu huyu.")
9O Jesus phushlia le bi vuzhesko, "Sar bushos?" Wo dia atweto, phenel, "Le Legion, ke but sam."
9Basi, Yesu akamwuliza, "Jina lako nani?" Naye akajibu, "Jina langu ni Jeshi, maana sisi tu wengi."
10Ai wo rhugilaspe ka Jesus te na tradel le bi vuzhe avri anda them.
10Kisha akamsihi Yesu asiwafukuze hao pepo katika nchi ile.
11Nas dur but bale kai xanas.
11Kulikuwa na kundi kubwa la nguruwe malishoni kwenye mteremko wa mlima.
12Le beng rhugisaile ka Jesus, "Te gonisa ame avri trade ame andel bale."
12Basi, hao pepo wakamsihi, "Utupeleke kwa hao nguruwe, tuwaingie."
13O Jesus phendia lenge te zhan andel bale, ai le bi vuzhe ankliste avri ai gele andel bale. Ai sa le bale shudepe pai xar ande maria, ai tasule ando pai. Sas pashte dui mi bale.
13Naye akawaruhusu. Basi, hao pepo wachafu wakatoka, wakawaingia wale nguruwe. Kundi lote la nguruwe wapatao elfu mbili likaporomoka kwenye ule mteremko mkali mpaka ziwani, likatumbukia majini.
14Le manush kai lenas sama katar le bale sigo gele ando foro ai avrial le gave, ai phende so kerdilia. Ai sa le manush avile te dikhen so kerdilia.
14Wachungaji wa hao nguruwe walikimbia, wakatangaza jambo hilo mjini na mashambani. Watu wakafika kuona yaliyotukia.
15Avile ka Jesus ai dikhle o manush kai sas les but beng ande leste, ai beshelas tele, ai vuriardo, ai leske goji vorta; ai daraile.
15Wakamwendea Yesu, wakamwona na mtu yuleyule aliyekuwa amepagawa na jeshi la pepo ameketi chini, amevaa nguo na ana akili yake sawa, wakaogopa.
16Kudola kai dikhle les, phende le manush so kerdilia pa o manush kai sas le beng ande leste, ai vi pa le bale.
16Watu walishuhudia tukio hilo wakaeleza wengine mambo yaliyompata huyo mtu aliyekuwa amepagawa na pepo na juu ya wale nguruwe.
17Ai phushle les te zhaltar anda lengo them.
17Basi, wakaanza kumwomba aondoke katika nchi yao.
18Ai kana O Jesus anklisto ando chuno, o manush kai sas les le beng ande leste manglia te zhal lesa.
18Yesu alipokuwa anapanda mashuani, yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo akamwomba amruhusu kwenda naye.
19Numa O Jesus chi meklia les te zhal, ai phendia leske, "Zha khere ai phenes lenge so godi kerdia tuke O Del, ai sar sas les mila pe tute."
19Lakini Yesu akamkatalia. Badala yake akamwambia, "Nenda nyumbani kwa jamaa yako, ukawaambie mambo yote Bwana aliyokutendea na jinsi alivyokuonea huruma."
20Kodo manush gelotar ai phendia sa le manush ande Decapolis so godi kerdia leske O Jesus; ai sa le manush chudisaile.
20Basi, huyo mtu akaenda, akaanza kutangaza huko Dekapoli mambo yote Yesu aliyomtendea; watu wote wakashangaa.
21Antunchi O Jesus gelo palpale inchal e maria ando chuno, ai but narodo chidinisaile angla leste: ai wo sas po berego.
21Yesu alivukia tena upande wa pili wa ziwa kwa mashua. Umati mkubwa wa watu ukakusanyika mbele yake, naye akawa amesimama kando ya ziwa.
22Ai, eta, iek baro andai synagogue avilo kai busholas Jairus, ai kana dikhlia O Jesus, shudiape kal punrhe,
22Hapo akaja mmojawapo wa maofisa wa sunagogi, jina lake Yairo. Alipomwona Yesu, akajitupa mbele ya miguu yake,
23ai dia duma zurales leske, phenel, "Murhi shei merel akana; aidi ai tho cho vas pe late, te avela sasti ai woi traiila.
23akamsihi akisema, "Binti yangu mdogo ni mgonjwa karibu kufa. Twende tafadhali, ukamwekee mikono yako, apate kupona na kuishi."
24O Jesus gelo lesa; ai but manush lenaspe pala leste, ai pashonas pasha leste katar swako rig.
24Basi, Yesu akaondoka pamoja naye. Watu wengi sana wakamfuata, wakawa wanamsonga kila upande.
25Sas ek zhuvli kai xasarelas pesko rat de desh u dui bersh,
25Mmojawapo alikuwa mwanamke mwenye ugonjwa wa kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili.
26ai chinuisardia but. Geli ka but dokxturia, xaliasas sa peske love, numa chi iek chi sastiardia la, ai mai nasul sas.
26Mwanamke huyo alikuwa amekwisha sumbuka sana kuwaendea waganga wengi. Na ingawa alikuwa amekwisha tumia mali yake yote, hakupata nafuu bali hali yake ilizidi kuwa mbaya.
27Kana ashundia pa Jesus, avili palal pala Jesus ai azbadia e tivala leske raxamaki.
27Alikuwa amesikia habari za Yesu, na hivyo akaupenya msongamano wa watu kutoka nyuma, akagusa vazi lake.
28Ke phendiape, "Te sai azbava leske tsalia avava sasti."
28Alifanya hivyo, maana alijisemea, "Nikigusa tu vazi lake, nitapona."
29Ai strazo o rat kai xasarelas aterdilo; ai woi zhanglia ke sastilisas katar o naswalimos.
29Mara chemchemi ya damu yake ikakauka, akajisikia mwilini mwake kwamba ameponywa ugonjwa wake.
30Ai O Jesus, strazo zhanelaspe kai putiera ankliste avri anda leste, amboldiape ai phendia ka le manush, "Kon azbadia murhe tsalia?"
30Yesu alitambua mara kwamba nguvu imemtoka. Basi akaugeukia ule umati wa watu, akauliza, "Nani aliyegusa mavazi yangu?"
31Leske disipluria phende leske, "Tu dikhes but narodo pashon pasha tute katar swako rig, ai tu mothos, "Kon azbadia ma?"
31Wanafunzi wake wakamjibu, "Unaona jinsi watu wanavyokusonga; mbona wauliza nani aliyekugusa?"
32O Jesus amboldiape ai dikhlia pe late kai azbadia leske tsalia.
32Lakini Yesu akaendelea kutazama amwone huyo aliyefanya hivyo.
33Numa e zhuvli daralas ai izdralas, zhanelas so kerdia O Jesus lake, avili ai dia le changa angla leste, ai phendia leske sa o chachimos.
33Hapo huyo mwanamke, akifahamu yaliyompata, akajitokeza akitetemeka kwa hofu, akajitupa chini mbele ya Yesu na kusema ukweli wote.
34Ai phendia lake, "Murhi shei, cho pachamos sastiardia tu; zha pachasa, sasti san katar cho naswalimos."
34Yesu akamwambia, "Binti, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani, upone kabisa ugonjwa wako."
35Sar delas duma inker, avile manush katar o kher le baresko andai synagogue ai phende, "Chi sheiorhi muli. Sostar mai dziliares o gazda?"
35Yesu alipokuwa bado anaongea, watu walifika kutoka nyumbani kwa yule ofisa wa sunagogi, wakamwambia, "Binti yako amekwisha kufa. Ya nini kuendelea kumsumbua Mwalimu?"
36Kana O Jesus ashundia kadala vorbi, phendia le baresko andai synagogue, "Na dara, ferdi pacha tu."
36Lakini, bila kujali walichosema, Yesu akamwambia mkuu wa sunagogi, "Usiogope, amini tu."
37Ai O Jesus chi meklia khonik te zhal lesa, ferdi o Petri, ai Iakov, ai Iovano o phral le Iakovosko.
37Wala hakumruhusu mtu yeyote kufuatana naye ila Petro, Yakobo na Yohane nduguye Yakobo.
38Aresle ka kher le baresko andai synagogue, ai O Jesus dikhlia baro narodo buntuime, but mui kerenas, ai rovenas. Wo gelo andre ai phushlia le,
38Wakafika nyumbani kwa ofisa wa sunagogi naye Yesu akasikia makelele, kilio na maombolezo mengi.
39"Sostar keren kadia, ai roven? E sheiorhi nai muli, numa sovel!"
39Akaingia ndani, akawaambia, "Mbona mnapiga kelele na kulia? Msichana hakufa, amelala tu."
40Won asaie lestar, kana gonisardia le narodos, wo angerdia o dat ai e dei la sheiake, ai won kai sas lesa, ai gele ande soba kai pashliolas.
40Lakini wao wakamcheka. Basi, akawaondoa wote nje, akawachukua baba na mama ya huyo msichana na wale wanafunzi wake, wakaingia chumbani alimokuwa huyo msichana.
41Ai lia la vastestar, ai phendia lake, "Talitha cumi" kai si "Sheiorhio, phenav tuke, Wushti opre."
41Kisha akamshika mkono, akamwambia, "Talitha, kumi," maana yake, "Msichana, nakwambia, amka!"
42Ai strazo e sheiorhi wushtili, ai phiradia. Desh u dui bershengi sas. Ai chudisaile but!
42Mara msichana akasimama, akaanza kutembea. (Alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili.) Hapo watu wakashangaa kupita kiasi.
43Wo dias le trad te na mothon kanikaske; ai phendia lenge, "De la vari so te xal."
43Yesu akawakataza sana wasimjulishe mtu jambo hilo. Kisha akawaambia wampe huyo msichana chakula.