Romani: New Testament

Swahili: New Testament

Matthew

23

1Antunchi O Jesus phendia le narodoske ai peske disiplonge,
1Kisha Yesu akauambia umati wa watu pamoja na wanafunzi wake,
2"Le Gramnoturia ai le Farizeanuria thodepe ando than le Mosesosko.
2"Walimu wa Sheria na Mafarisayo wana mamlaka ya kufafanua Sheria ya Mose.
3Keren so mothon ai sikaven tumen: numa na keren sar lende, ke won sikaven tumen numa chi keren so sikaven.
3Kwa hiyo shikeni na kutekeleza chochote watakachowaambieni. Lakini msiyaige matendo yao, maana hawatekelezi yale wanayoyahubiri.
4Thon pharipe pel dume le manushenge, numa won chi mangen te vazden ek nai.
4Hufunga mizigo mizito na kuwatwika watu mabegani, lakini wao wenyewe hawataki kunyosha hata kidole wapate kuibeba.
5Ai won so godi keren keren kashte te dikhen le manush pe lende. Phiraven E Vorba le Devleski pe pengo shero ai pengo vas, ai lunzharen le chukuria ka penge tsalia!
5Wao hufanya matendo yao yote ili watu wawaone. Huvaa tepe zenye maandishi ya Sheria juu ya panda la uso na mikononi na hupanua pindo za makoti yao.
6Ai drago lenge te beshen ka shero la skafidiako kal pachiva, ai le mai lashe skamina ande synagogue.
6Hupenda nafasi za heshima katika karamu na viti vya heshima katika masunagogi.
7Ai drago lenge te den le dies lasho pel vulitsi, ai te mothon lenge le manush, "Rabbi"
7Hupenda kusalimiwa kwa heshima sokoni na kupendelea kuitwa na watu: Mwalimu.
8"Na roden te akharen tume "Rabbi" ke iek si tumaro gazda, "O Kristo" ai tume san sa phral.
8Lakini ninyi msiitwe kamwe Mwalimu, maana mwalimu wenu ni mmoja tu, nanyi nyote ni ndugu.
9Na phenen kanikaske pe phuv "Murho Dat". Ke iek ferdi si tumaro Dat kodo kai si ando rhaio.
9Wala msimwite mtu yeyote Baba hapa duniani, maana Baba yenu ni mmoja tu aliye mbinguni.
10Na roden te akharen tume "Baro", ke iek si tumaro "Baro", "O Kristo".
10Wala msiitwe Viongozi, maana kiongozi wenu ni mmoja tu, ndiye Kristo.
11"O mai baro mashkar tumende trobul te avel tumari sluga.
11Aliye mkubwa miongoni mwenu ni lazima awe mtumishi wenu.
12Kon godi bariarelape si te avel teliardo, ai kon godi mekelape tele si te avel vazdino.
12Anayejikweza atashushwa, na anayejishusha atakwezwa.
13"Nasul tumenge, Gramnoturia ai Farizeanuria! Tume manush kai ankerdion so chi san! Ke tume phandaven le manushenge, e amperetsia le rhaioski, tume chi zhan andre, ai chi meken te zhan andre kodola kai mangen te zhan andre!
13"Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnaufunga mlango wa Ufalme wa mbinguni mbele ya macho ya watu. Ninyi wenyewe hamwingii ndani, wala hamwaruhusu wanaotaka kuingia waingie.
14Nasul tumenge, Gramnoturia ai Farizeanuria Tume manush kai ankerdion so chi san! Ke tume xan le phivliange khera, ai rhugin tume lungo rhugimos, te miazol ke lashe san! Anda kodia si te pherel mai phari kris pe tumende!
14Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnawanyonya wajane na kujisingizia kuwa watu wema kwa kusali sala ndefu. Kwa sababu hiyo mtapata adhabu kali.
15Nasul tumenge, Gramnoturia ai Farizeanuria! Tume manush kai ankerdion so chi san! Tume phiren pe swako rig la phuviake ai pe maria te nirin ai te parhuven iekes manushes; antunchi, keren anda leste duvar mai but shav iadosko sar tume!
15"Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnasafiri baharini na nchi kavu ili kumpata mtu mmoja afuate dini yenu. Mnapompata, mnamfanya astahili maradufu kwenda katika moto wa Jehanamu kuliko ninyi wenyewe.
16"Nasul tumenge, tume korhe kai ningeren le korhen! Tume phenen, "Kon godi solaxala pe tamplo, kodia nai khanchi; numa kon godi solaxala po sumnakai kai si ande tamplo, kodo phanglo lo ka peske solax!"
16"Ole wenu viongozi vipofu! Ninyi mwasema ati mtu akiapa kwa Hekalu, kiapo hicho si kitu; lakini akiapa kwa dhahabu ya Hekalu, kiapo hicho kinamshika.
17Tume prosti ai korhe manush! So si mai baro, o sumnakai vai e tamplo kai swuntsol o sumnakai?
17Enyi vipofu wapumbavu! Kipi kilicho cha maana zaidi: dhahabu au Hekalu linalofanya hiyo dhahabu kuwa takatifu?
18Ai kon godi solaxala po altari, kodia nai khanchi, numa kon godi solaxala pe soste si shinado po altari, phanglo lo ka peske solax.
18Tena mwasema ati mtu akiapa kwa madhabahu si kitu; lakini akiapa kwa zawadi iliyowekwa juu ya madhabahu, kiapo hicho humshika.
19Tume prosti ai korhe manush! So si mai baro, so si shinado po altari vai o altari kai swuntsol so si shinado po altari?
19Enyi vipofu! Ni kipi kilicho cha maana zaidi: ile zawadi, au madhabahu ambayo hufanya hiyo zawadi kuwa takatifu?
20Kon godi solaxal po altari, solaxal po altari ai pe soste godi si po altari.
20Anayeapa kwa madhabahu ameapa kwa hiyo madhabahu, na kwa chochote kilichowekwa juu yake.
21Ai kodo kai solaxal pe tamplo, solaxal vi pe tamplo ai po Del kai si ande tamplo.
21Na anayeapa kwa Hekalu ameapa kwa hilo Hekalu na pia kwa yule akaaye ndani yake.
22Ai kodo kai solaxal po rhaio, solaxal vi po skamin le Devlesko ai po Del kai beshel pe leste.
22Na anayeapa kwa mbingu ameapa kwa kiti cha enzi cha Mungu, na kwa huyo aketiye juu yake.
23"Nasul tumenge, Gramnoturia ai Farizeanuria! Tume manush kai ankerdion so chi san! Ke tume den desh anda iek shel e partia kai trobun te den andai mai tsinorhi diela, Mint, Dill, ai Cummin, numa chi keren so si mai baro ando zakono. So si vorta, Mila; ai Pachamos.
23Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnatoza watu zaka, hata juu ya majani yenye harufu nzuri, bizari na jira, na huku mnaacha mambo muhimu ya Sheria kama vile haki, huruma na imani. Haya ndiyo hasa mliyopaswa kuyazingatia bila kusahau yale mengine.
24Tume korhe kai sikaven kavren! Tume arakhen tume kaste te na nakhaven tsintsari, numa e gemula nakhavel!
24Viongozi vipofu! Mnatoa nzi katika kinywaji, lakini mnameza ngamia!
25"Nasul tumenge, tume Gramnoturia ai Farizeanuria! Tume manush kai ankerdion so chi san! Ke tume vuzharen avrial e kuchi ai o tiari, numa andral san pherde chorimos, atsaimos ai keren so si tumenge mishto.
25"Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnasafisha kikombe na bakuli kwa nje, lakini ndani mnaacha kumejaa vitu mlivyopata kwa unyang'anyi na uchoyo.
26Tume korhe Farizeanuria! Vuzharen andral mai anglal e kuchi ai o tiari, kashte te avel vuzho vi avrial!
26Mfarisayo kipofu! Kisafishe kikombe ndani kwanza na nje kutakuwa safi pia.
27"Nasul tumenge, Gramnoturia ai Farizeanuria! Tume manush kai ankerdion so chi san! Tume san sar greposhevuria vusharade, ai kerde te miazon shukar avrial, numa andral pherde mule manushenge kokala ai so godi nai vuzho.
27"Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mko kama makaburi yaliyopakwa chokaa ambayo kwa nje yanaonekana kuwa mazuri, lakini ndani yamejaa mifupa ya maiti na kila namna ya uchafu.
28Sakadia vi tume avrial miazon vorta le manushenge, numa andral bezexale san ai chi san so keren te miazon.
28Hali kadhalika ninyi mnaonekana na watu kwa nje kuwa wema, lakini kwa ndani mmejaa unafiki na uovu.
29"Nasul tumenge, Gramnoturia ai Farizeanuria! Tume manush kai ankerdion so chi san! Ke tume thon le murmunturia le profetonge, ai shukaren le greposhevuria manushenge kai sas chache;
29"Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnajenga makaburi ya manabii na kuyapamba makaburi ya watu wema.
30ai phenen, "Te traiisardiamas andel diesa amare dadenge ai paponge, nas te mudaras le profeton sar kerde won.
30Mwasema: Kama sisi tungaliishi nyakati za wazee wetu hatungalishirikiana nao katika mauaji ya manabii!
31Ke mothon kadia san marturis tumenge ke san shave kodolenge kai mudarde le profeton!
31Hivyo mnathibitisha ninyi wenyewe kwamba ninyi ni watoto wa watu waliowaua manabii.
32Tume geton so tumare dada thodepe de anda gor te keren!
32Haya, kamilisheni ile kazi wazee wenu waliyoianza!
33Tume sap, tume vitsa sapenge! Sar skepina e kris kai tradela tume ando iado?
33Enyi kizazi cha nyoka wenye sumu! Mnawezaje kuiepa hukumu ya moto wa Jehanamu?
34"Anda kodia tradav tumenge profeturia ai manush kai haliaren ai le manush kai sikaven; uni anda lende mudaren ai thona po trushul, avren si te maren bichonsa ande tumare synagoguria, ai chinuina le foro forestar.
34Ndiyo maana mimi ninawapelekea ninyi manabii, watu wenye hekima na walimu; mtawaua na kuwasulubisha baadhi yao, na wengine mtawapiga viboko katika masunagogi yenu na kuwasaka katika kila mji.
35Kadia si te perel e dosh pe tumende pala sa o rat shordo ande lumia chache manushengo, de katar o rat le Abelosko o chacho, zhi ka rat le Zachariahosko, o shav le Barachiasesko, kai tume mudardian mashkar e tamplo ai o altari.
35Hivyo lawama yote itawapateni kwa ajili ya damu yote ya watu wema iliyomwagwa juu ya ardhi. Naam, tangu kuuawa kwa Abeli ambaye hakuwa na hatia, mpaka kuuawa kwa Zakariya, mwana wa Barakia, ambaye mlimuua Hekaluni kati ya patakatifu na madhabahu.
36O chachimos me mothav tumenge, sa e dosh si te perel pe kadia vitsa!"
36Nawaambieni kweli, kizazi hiki kitapata adhabu kwa sababu ya mambo haya.
37"Jerusalem! Jerusalem! Kai mudaren le profeton ai kai shuden baxensa ande kodola kai si tumenge tradine! Sodivar manglem te chidav che shaven, sar ek kaini kai chidel peske puion tela peske paka numa chi manglian.
37"Yerusalemu, Ee Yerusalemu! Unawaua manabii na kuwapiga mawe wale waliotumwa kwako. Mara ngapi nimejaribu kuwakusanya watoto wako kwangu, kama vile kuku anavyokusanya vifaranga vyake chini ya mabawa yake, lakini hukutaka.
38Eta so ashshilo tume tumari tamplo pusto.
38Haya basi, nyumba yako itaachwa mahame.
39Me mothav tumenge, chi mai dikhena ma zhi pon chi mothona, Raduime kodo kai avel ando anav le Devlesko."
39Nakwambia kweli, hutaniona tena mpaka wakati utakaposema: Abarikiwe huyo ajaye kwa jina la Bwana."