1"Antunchi e amperetsia le rhaioski si sar desh sheia baria kai line peske lampi (chediara) ai gele po drom kai o ternaxar avelas.
1"Wakati huo, Ufalme wa mbinguni utafanana na wasichana kumi waliochukua taa zao, wakaenda kumlaki bwana arusi.
2Pansh anda lende sas prosti ai pansh gojaver.
2Watano miongoni mwao walikuwa wapumbavu na watano walikuwa wenye busara.
3Le prosti kana line penge lampi, chi line vuloi pensa.
3Wale wapumbavu walichukua taa zao, lakini hawakuchukua akiba ya mafuta.
4Numa le gojaver line mai but vuloi pensa de sar so sas andel lampi.
4Lakini wale wenye busara walichukua mafuta katika chupa pamoja na taa zao.
5Ke chi avilo o ternaxar pe vriama lindraile ai lias le e lindre.
5Kwa kuwa bwana arusi alikawia kuja, wale wanawali wote wote walisinzia, wakalala.
6Numa ando mashkar la rachako ek glaso dias mui, Dikhen! O ternaxar, Aven leste!
6Usiku wa manane kukawa na kelele: Haya, haya! Bwana arusi anakuja; nendeni kumlaki.
7Antunchi le sheia baria wushtile, ai lasharde peske lampi.
7Hapo wale wanawali wote wakaamka, wakazitayarisha taa zao.
8Le prosti phende kodolenge kai sas gojaver. "Den ame anda tumaro vuloi ke amare lampi meren."
8Wale wapumbavu wakawaambia wale wenye busara: Tupeni mafuta yenu kidogo maana taa zetu zinazimika.
9Le gojaver phende, "Nashtis, ke kam chi avel dosta tumenge ai vi amenge, zhan ka kodola kai bichinen vuloi ai chinen tumenge.
9Lakini wale wenye busara wakawaambia, Hayatatutosha sisi na ninyi! Afadhali mwende dukani mkajinunulie wenyewe!
10Numa zhi pon won gele te chinen vuloi, o ternaxar avilo; le sheia baria kai sas gata gele lesa andre ka o abiav ai o wudar sas phandado.
10Basi, wale wanawali wapumbavu walipokwenda kununua mafuta, bwana arusi akafika, na wale wanawali waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye katika jumba la arusi, kisha mlango ukafungwa.
11Mai palal le kolaver sheia baria avile, ai phende, "Gazda, Gazda! Phuter amenge!"
11Baadaye wale wanawali wengine wakaja, wakaita: Bwana, bwana, tufungulie!
12Numa wo phendias, "Chachimasa phenav tumenge, me chi zhanav tumen."
12Lakini yeye akawajibu, Nawaambieni kweli, siwajui ninyi."
13Anda kodia arakhen tume, ke chi zhanen o dies vai o chaso kana O Shav le Manushesko avela."
13Kisha Yesu akasema, "Kesheni basi, kwa maana hamjui siku wala saa.
14"Ke kadia si sar ek manush kai si te zhaltar dur, ai akhardias peske slugen, ai dias ande lengo vas so sas lesko.
14"Itakuwa kama mtu mmoja aliyetaka kusafiri ng'ambo: aliwaita watumishi wake, akawakabidhi mali yake.
15Kai iek dias panzh gone sumnakai, ka aver dias dui, ai ka aver dias iek, swakones dias sode wo sai dashtil te lel sama, ai gelo pe pesko drom.
15Alimpa kila mmoja kadiri ya uwezo wake: mmoja sarafu tano za fedha ziitwazo talanta, mwingine talanta mbili na mwingine talanta moja, kisha akasafiri.
16Kodo kai lias panzh gone sumnakai, strazo gelo, kerdias buchi lensa, ai dobisardias panzh gone sumnakai mai but.
16Mara yule aliyekabidhiwa talanta tano akafanya kazi nazo akapata faida talanta tano.
17Sakadia kodo kai lias dui, gelo ai dobisardias dui mai but.
17Hali kadhalika na yule aliyekabidhiwa talanta mbili akapata faida talanta mbili.
18Numa kodo kai lias iek gono sumnakai, gelo, hunadias gropa ande phuv, ai garadias pesko gazdasko sumnakai.
18Lakini yule aliyekabidhiwa talanta moja akaenda akachimba shimo ardhini, akaificha fedha ya bwana wake.
19But vriama pala kodia o gazda kodole slugenge avilo palpale, ai manglias te sikaven leske so kerde.
19"Baada ya muda mrefu, yule bwana alirudi, akaanza kukagua hesabu ya matumizi na mapato ya fedha yake.
20Kodo kai lias panzh gone sumnakai, avilo ai andias panzh mai but, ai phendias, "Gazda, tu dian ma panzh gone sumnakai. Dikh! Me dobisardem panzh mai but."
20Mtumishi aliyekabidhiwa talanta tano akaja amechukua zile talanta tano faida, akamwambia, Bwana, ulinikabidhi talanta tano, hapa pana talanta tano zaidi faida niliyopata.
21Lesko gazda phendias leske, "Mishto kerdian, lasho ai chacho sluga chachimasa sanas, xantsi dielasa si te thav tut baro pe but dieli, aidi ai hulav ande che gazdasko raduimos!"
21Bwana wake akamwambia, Vema, mtumishi mwema na mwaminifu. Umekuwa mwaminifu katika mambo madogo nitakukabidhi makubwa. Njoo ufurahi pamoja na bwana wako.
22Kodo kai lias dui gone sumnakai avilo, ai phendias, "Gazda, Tu dian ma dui. Dikh! Me dobisardem dui mai but!"
22"Mtumishi aliyekabidhiwa talanta mbili akaja, akatoa talanta mbili faida, akisema, Bwana, ulinikabidhi talanta mbili. Chukua talanta mbili zaidi faida niliyopata.
23Lesko gazda phendias leske, "Mishto kerdian, lasho ai chacho sluga chachimasa sanas, xantsi dielasa si te thav tut baro pe but dieli, aidi ai hulav ande che gazdasko raduimos!
23Bwana wake akamwambia, Vema, mtumishi mwema na mwaminifu. Umekuwa mwaminifu katika mambo madogo, nitakukabidhi makubwa. Njoo ufurahi pamoja na bwana wako.
24Kodo kai sas les iek gono sumnakai avilo ai phendias, "Gazda, Zhanglem ke zuralo ai trutno manush san, ke les katar chi thodian ai chides katar chi thodian sumuntsa.
24"Lakini yule aliyekabidhiwa talanta moja akaja, akasema, Bwana, najua wewe ni mtu mgumu; wewe huvuna pale ambapo hukupanda, na kukusanya pale ambapo hukutawanya.
25Ai darailem, gelem ai garadem cho sumnakai ande phuv, Dikh! Si tu so si chiro."
25Niliogopa, nikaificha fedha yako katika ardhi. Chukua basi mali yako.
26Lesko gazda phendias leske, "Tu nasul kandino sluga, tu zhanglian ke lav katar chi thodem ai chidav katar chi thodem sumuntsa."
26"Bwana wake akamwambia, Wewe ni mtumishi mwovu na mvivu! Unajua kuwa mimi huvuna mahali ambapo sikupanda, na hukusanya pale ambapo sikutawanya.
27Antunchi tu trobulas te thos murho sumnakai ando banko, ai kana avilemas, sas te lav murho sumnakai palpale, ai vi mai but.
27Ilikupasa basi, kuiweka fedha yangu katika benki, nami ningelichukua mtaji wangu na faida yake!
28Anda kodia le o sumnakai lestar, ai de les ka kodo kai si les le desh gone sumnakai.
28Basi, mnyang'anyeni hiyo fedha mkampe yule mwenye talanta kumi.
29Ke swakones te kai si mai but avela dino ai si te avel les but mai but opral: numa katar kodo kai nai les, vi so si les avela lino lestar.
29Maana, aliye na kitu atapewa na kuzidishiwa. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
30E sluga kai nai kanchesko shuden avri ando tuniariko ai ande kodo than kai rovena ai chiden dandendar."
30Na kuhusu huyu mtumishi asiye na faida, mtupeni nje gizani! Huko kutakuwa na kilio na kusaga meno.
31"Kana avela O Shav le Manushesko ande pesko barimos, ai sa le angeluria lesa, antunchi beshela pe pesko skamin o amperatitsko.
31"Wakati Mwana wa Mtu atakapokuja katika utukufu wake na malaika wote wakiwa pamoja naye, hapo ataketi juu ya kiti chake cha enzi kitukufu,
32Angla leste avena chidine sa le thema, ai hulavela le manushen iek katar o kaver sar o pastuxo, hulavel le bakren katar le buzhne.
32na mataifa yote yatakusanyika mbele yake, naye atawatenganisha watu kama mchungaji anavyotenganisha kondoo na mbuzi.
33Ai thola le bakren pe peski chachi rig, ai le buzhnen pe peski stingo rig.
33Atawaweka kondoo upande wake wa kulia na mbuzi upande wake wa kushoto.
34Antunchi o amperato si te mothol kodolenge ka lesko vas o chacho, "Aven tume kai san raduime katar murho Dat, len so sas tumenge shinado e amperetsia kai sas getome tumenge de sar sas e lumia kerdi.
34"Kisha Mfalme atawaambia wale walio upande wake wa kulia, Njoni enyi mliobarikiwa na Baba yangu; pokeeni Ufalme mliotayarishiwa tangu kuumbwa kwa ulimwengu.
35Ke bokhalo simas, ai dian ma te xav, trushalo simas, ai dian ma te piiva: streino simas, ai andian ma ande cho kher.
35Maana nilikuwa na njaa nanyi mkanipa chakula; nilikuwa na kiu nanyi mkanipa maji; nilikuwa mgeni nanyi mkanikaribisha;
36Nas ma tsalia, ai tu dian ma tsalia, naswalo simas, ai lian sama mandar, phandado simas, ai tu avilian te dikhes ma."
36nilikuwa uchi, mkanivika; nilikuwa mgonjwa nanyi mkaja kunitazama; nilikuwa gerezani nanyi mkaja kunitembelea.
37Antunchi le chache phenena leske, "Gazda, Kana dikhliam tu bokhalo, ai diam tu te xas? Vai trushalo, ai diam tu te pes?
37Hapo, hao watu wema watamjibu mfalme Bwana, ni lini tulikuona mwenye njaa nasi tukakupa chakula, au ukiwa na kiu nasi tukakunywesha maji?
38Kana dikhliam tu streino, ai andiam tut andre? Vai ke trobunas tut tsalia, ai diam tut?
38Ni lini tulikuona ukiwa mgeni nasi tukakukaribisha, au bila nguo nasi tukakuvika?
39Kana dikhliam tut naswalo, vai phandado, ai aviliam te dikhas tu?"
39Ni lini tulikuona ukiwa mgonjwa au mfungwa nasi tukaja kukutazama?
40Ai o amperato phenela, "O chachimos phenav tumenge, so godi kerdian kodoleske kai si mai prosto anda murho phral, kerdian mange."
40Mfalme atawajibu, Kweli nawaambieni, kila kitu mlichomtendea mmojawapo wa hawa ndugu zangu wadogo, mlinitendea mimi.
41Antunchi phenel kodolenge ka lesko stingo vas, "Zhantar mandar, tume armandine, ande iag kai chi getolpe, kai si getome le bengeske ai leske angelonge.
41"Kisha atawaambia wale walio upande wake wa kushoto, Ondokeni mbele yangu enyi mliolaaniwa! Nendeni katika moto wa milele aliotayarishiwa Ibilisi na malaika wake.
42Bokhalo simas, ai chi dian ma te xav, trushalo simas, ai tu chi dian ma te piiav.
42Maana nilikuwa na njaa nanyi hamkunipa chakula; nilikuwa na kiu nanyi hamkunipa maji.
43Streino simas, ai chi akhardian ma andre, nas ma tsalia, ai chi dian ma, naswalo, phandado, ai tu chi avilian te dikhes ma."
43Nilikuwa mgeni nanyi hamkunikaribisha; nilikuwa mgonjwa na mfungwa nanyi hamkuja kunitazama.
44Antunchi won phenen, "Gazda, kana dikhliam tut bokhalo, vai trushalo, vai streino, vai bi tsalengo, vai naswalo, vai phandado, ai chi zhutisardem tu?"
44"Hapo nao watajibu, Bwana, ni lini tulikuona ukiwa na njaa au kiu, ukiwa mgeni au bila nguo, ukiwa mgonjwa au mfungwa, nasi hatukuja kukuhudumia?
45Antunchi phendia lenge, "O chachimos phenav tumenge, sar chi kerdian le mai prostonenge, chi kerdian chi mange.
45Naye atawajibu, Nawaambieni kweli, kila mlipokataa kumtendea mambo haya mmojawapo wa hawa wadogo, mlikataa kunitendea mimi.
46Antunchi zhana ande iag kai chi getolpe, numa le chache ando traio kai chi getolpe.
46Basi, hawa watakwenda kwenye adhabu ya milele, lakini wale waadilifu watakwenda kwenye uzima wa milele."