Romani: New Testament

Swahili: New Testament

Matthew

28

1Pala Sabat kana phuterdilo o dies. O pervo dies le kurkosko, e Maria Magdalena ai e kaver Maria gele te dikhen ka greposhevo.
1Baada ya Sabato, karibu na mapambazuko ya siku ile ya Jumapili, Maria Magdalene na yule Maria mwingine walikwenda kutazama lile kaburi.
2Kote izdraias e phuv zurales, ke ek angelo le Devlesko avilo tele anda rhaio, ai spidias palpale o bax, ai beshlo pe leste.
2Ghafla kutatokea tetemeko kubwa la nchi; malaika wa Bwana alishuka kutoka mbinguni, akalivingirisha lile jiwe, akalikalia.
3Strefialas sar o rhunjito, ai leske tsalia sas parne sar o iiv.
3Alionekana kama umeme na mavazi yake yalikuwa meupe kama theluji.
4Le zhene kai meklesas te len sama, daraile kadia de zurales ta izdranas ai kerdile sar mule manush.
4Walinzi wa lile kaburi wakatetemeka kwa hofu kubwa, hata wakawa kama wamekufa.
5O angelo phendias le zhuvliange, "Na daran, zhanav ke roden te dikhen le Jesusos kai mulo po trushul.
5Lakini yule malaika akawaambia wale wanawake, "Ninyi msiogope! Najua kwamba mnamtafuta Yesu aliyesulubiwa.
6Nai katse, wushtilo, sar kai phendias, Aven ai dikhen o than kai sas.
6Hayupo hapa maana amefufuka kama alivyosema. Njoni mkaone mahali alipokuwa amelala.
7Zhan sigo ai phenen leske disiplonge, ke wo wushtilo andai martia, ai zhal mai anglal tumendar ande Galilee, kote si te dikhen les, na bustren so phendem tumenge.
7Basi, nendeni upesi mkawaambie wanafunzi wake kwamba amefufuka kutoka wafu, na sasa anawatangulieni kule Galilaya; huko mtamwona. Haya, mimi nimekwisha waambieni."
8Grebisaile te zhantar katar o greposhevo ande dar numa vi veselo sas, nashle te phenen leske disiplonge.
8Wakiwa wenye hofu na furaha kubwa, hao wanawake walitoka upesi kaburini, wakakimbia kwenda kuwaambia wanafunzi wake.
9O Jesus avilo ande lengo drom, dias le dies lasho. Avile leste, ai dine changa angla leste, thode le vas pe lesko punrhe, luvudinas les ai preznainas les.
9Mara, Yesu akakutana nao, akawasalimu: "Salamu." Hao wanawake wakamwendea, wakapiga magoti mbele yake, wakashika miguu yake.
10O Jesus antunchi phendias lenge, "Na daran, zhan ai phenen murhe phralenge te zhan ande Galilee, kote si te dikhen ma."
10Kisha Yesu akawaambia, "Msiogope! Nendeni mkawaambie ndugu zangu waende Galilaya, na huko wataniona."
11Zhi pon le zhuvlia sas po drom. Uni andal ketani kai lenas sama ka greposhevo gele palpale ando foro, ai phende le bare rashange so godi kerdiliape.
11Wale wanawake walipokuwa wanakwenda zao, baadhi ya walinzi wa lile kaburi walikwenda mjini kutoa taarifa kwa makuhani wakuu juu ya mambo yote yaliyotukia.
12Le rasha le bare avile andek than le phurensa kai poronchin ai dinepe duma so te keren. Dine but love kal ketani.
12Basi, wakakutana pamoja na wazee, na baada ya kushauriana, wakawapa wale askari kiasi kikubwa cha fedha
13Ai phende lenge, "Mothon ke leske disipluria, "Avile ande riat, ai chorde lesko stato zhi pon tume sovenas."
13wakisema, "Ninyi mtasema hivi: Wanafunzi wake walikuja usiku, wakamwiba sisi tukiwa tumelala.
14Te aresela kado divano ka o guvernori Pilate, pachas les ame ai mekas te avel beda pe tumende."
14Na kama mkuu wa mkoa akijua jambo hili, sisi tutasema naye na kuhakikisha kuwa ninyi hamtapata matatizo."
15Le ketani line le love, ai kerde so phende lenge, kado divano phendo mashkar le Zhiduvuria zhi adies.
15Wale walinzi wakazichukua zile fedha, wakafanya kama walivyofundishwa. Habari hiyo imeenea kati ya Wayahudi mpaka leo.
16Le desh u dui disipluria gele ande Galilee pe plai kai O Jesus tradias le.
16Wale wanafunzi kumi na mmoja walikwenda Galilaya kwenye ule mlima aliowaagiza Yesu.
17Kana dikhle les, luvudisarde ai preznaisarde les. numa uni chi pachanas.
17Walipomwona, wakamwabudu, ingawa wengine walikuwa na mashaka.
18O Jesus avilo pasha lende ai phendias lenge, "Sa e putiera ando rhaio ai pe phuv si dini mande.
18Yesu akaja karibu, akawaambia, "Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.
19Anda kodia, zhan ai keren disipluria anda sa le thema, bolen le ando anav le Dadesko, le Shavesko, ai le Swuntone Duxosko.
19Nendeni basi, mkawafanye watu wa mataifa yote wawe wanafunzi wangu; mkiwabatiza kwa jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu.
20Sikaven le te keren so godi phendem tumenge, ai na bustren ke tumensa sim, zhi ando gor la lumiako."
20Wafundisheni kushika maagizo yote niliyowapeni. Nami nipo pamoja nanyi siku zote; naam, mpaka mwisho wa nyakati."