1"Na shin kris, te na avel kris shinde pe tute.
1"Msiwahukumu wengine, msije nanyi mkahukumiwa na Mungu;
2Ke sar shinesa kris pe kavreste kadia avela kris shindi pe tute, e musura kai musurisa kolavres kodolasa avesa tu musurime.
2kwa maana jinsi mnavyowahukumu wengine, ndivyo nanyi mtakavyohukumiwa; na kipimo kilekile mnachotumia kwa wengine ndicho Mungu atakachotumia kwenu.
3Sostar dikhes e tsipiliga ande iakh chi phraleski, ai chi dikhes o stilpo kai si ande chiri iakh.
3Kwa nini wakiona kibanzi kilicho jichoni mwa ndugu yako, na papo hapo huioni boriti iliyoko jichoni mwako?
4Sar sai phenes che phraleske, Mek ma te lav e tsipliga anda chiri iakh,' kana tut si stilpo ande chiri iakh?
4Au, wawezaje kumwambia ndugu yako, Ndugu, ngoja nikuondoe kibanzi jichoni mwako, wakati wewe mwenyewe unayo boriti jichoni mwako?
5Tu manush kai ankerdios so chi san! Ankalav mai anglal o stilpo anda chiri iakh, ai porme dikhesa dosta de mishto te ankalaves e tsipliga kai si ande iakh che phraleske.
5Mnafiki wewe! Ondoa kwanza boriti iliyoko jichoni mwako na hapo ndipo utaona waziwazi kiasi cha kuweza kuondoa kibanzi kilichoko jichoni mwa ndugu yako.
6"Na den so si swunto kal zhukel, ai shuden tumare perli anglal bale, ke kham te vulin le telal punrhe, ai amboldenpe pe tumende te xan tume.
6"Msiwape mbwa vitu vitakatifu wasije wakageuka na kuwararua ninyi; wala msiwatupie nguruwe lulu zenu wasije wakazikanyaga.
7"Mangen, ai avela tume dino; roden, ai arakhena; maren, ai avela tumenge phuterdo.
7"Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtapata; bisheni, nanyi mtafunguliwa.
8Ke kon godi mangela avela les, kodo kai rodel arakhela, ai kodoleske kai marel avela phuterdo.
8Maana, aombaye hupewa, atafutaye hupata, na abishaye hufunguliwa.
9Savo anda tumende del bax peske shaves te mangela lestar manrho?
9Je, kuna yeyote miongoni mwenu ambaye mtoto wake akimwomba mkate, atampa jiwe?
10Vai te del les sap, te mangela lestar masho?
10Au je, akimwomba samaki, atampa nyoka?
11Tume kai san nasul, zhanen sar te den mishtimos tumare glaten. Sode mai but tumaro Dat kai si ando rhaio dela mishtimos kodolen kai mangen lestar?"
11Kama basi ninyi, ingawa ni waovu, mwajua kuwapa watoto wenu vitu vizuri, hakika Baba yenu wa mbinguni atafanya zaidi: atawapa mema wale wanaomwomba.
12"Ande sako fielo keren kolavrenge so tume mangen le kolaver te keren tumenge; ke kodia si o zakono ai o sicharimos le profetonge.
12"Watendeeni wengine yale mnayotaka wao wawatendee ninyi. Hii ndiyo maana ya Sheria ya Mose na mafundisho ya manabii.
13"Zhan andre pa e tang vurota; ke bufli e vurota, ai vushoro o drom kai ingerel ando iado, ai but si kai len kodo drom.
13"Ingieni kwa kupitia mlango mwembamba. Kwa maana njia inayoongoza kwenye maangamizi ni pana, na mlango wa kuingilia humo ni mpana; waendao njia hiyo ni wengi.
14Ke e vurota tang ai o drom tang kai ingerel ka traio, ai xantsi si kai arakhen les."
14Lakini njia inayoongoza kwenye uzima ni nyembamba, na mlango wa kuingilia humo ni mwembamba; ni watu wachache tu wanaoweza kuigundua njia hiyo.
15"Arakhen tume katar le profeturia kai nai chache, kai aven tumende andel bakrenge tsalia, numa andral won si divli ruv.
15"Jihadharini na manabii wa uongo. Wao huja kwenu wakionekana kama kondoo kwa nje, lakini kwa ndani ni mbwa mwitu wakali.
16Tume prinzharen le katar lenge fruta. Sai chidelpe struguro pai krenga kanrhenge, vai figi pai tsignida?
16Mtawatambua kwa matendo yao. Je, watu huchuma zabibu katika miti ya miiba, au tini katika mbigili? La!
17Swako lashi pruing del lashi fruta, numa e chori pruing del chorhi fruta.
17Basi, mti mwema huzaa matunda mema, na mti mbaya huzaa matunda mabaya.
18Ek lashi pruing nashti del chorhi fruta, ai chorhi pruing nashti del lashi fruta.
18Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mbaya hauwezi kuzaa matunda mema.
19Savi godi pruing kai chi del lashi fruta avela shindi ai shudini ande iag.
19Kila mti usiozaa matunda mema utakatwa na kutupwa motoni.
20Kadia tume prinzharena len kai nai chache katar lenge fruta."
20Kwa hiyo, mtawatambua kwa matendo yao.
21Na swako kai phenena mange 'Devla, Devla' avena ande amperetsia le rhaioski, numa kodola kai kerena e voia murhi Dadeski kai si ando rhaio.
21"Si kila aniambiaye, Bwana, Bwana, ataingia katika Ufalme wa mbinguni; ila ni yule tu anayetimiza mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.
22But ande kodo dies phenena mange, 'Devla, Devla! Chi diam profesi ande chiro anav? Chi gonisardiam le bengen ande chiro anav? Ai kerdiam but mirakluria ande chiro anav?
22Wengi wataniambia Siku ile ya hukumu: Bwana, Bwana! kwa jina lako tulitangaza ujumbe wako, na kwa jina lako tuliwatoa pepo na kufanya miujiza mingi.
23Antunchi phenava lenge, ' Shoxar, Chi zhanglem tume. Zhantar mandar, tume kai keren nasulimos!'"
23Hapo nitawaambia: Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni mbele yangu, enyi watenda maovu.
24"Anda kodia kon godi ashunela kadala vorbi kai phenav, ai kerela le, avela sar ek manush gojaver kai vazdias pesko kher pek stana baxreski.
24"Kwa sababu hiyo, kila mtu anayeyasikia maneno yangu na kuyazingatia, anafanana na mtu mwenye busara, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba.
25O breshind dias, le bare paia avile, e barval phurdias zurales pe kodo kher. Numa chi pelo, ke vazdino sas pe stana le baxreski.
25Mvua ikanyesha, mito ikafurika, pepo kali zikavuma na kuipiga nyumba hiyo. Lakini haikuanguka kwa sababu ilikuwa imejengwa juu ya mwamba.
26Numa kon godi kai ashunela le vorbi kai phenav, ai chi kerela le, avela sar ek manush prosto kai vazdias pesko kher pe chishai.
26"Lakini yeyote anayesikia maneno yangu haya bila kuyazingatia, anafanana na mtu mpumbavu aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga.
27O breshind dias, o pai o baro avilo, e barval phurdia pe kodo kher. Ai pelo zurales!"
27Mvua ikanyesha, mito ikafurika, pepo kali zikavuma na kuipiga nyumba hiyo, nayo ikaanguka; tena kwa kishindo kikubwa."
28Kana O Jesus getosardias so phenelas chudisailo o narodo katar lesko sicharimos.
28Yesu alipomaliza kusema maneno hayo, umati wa watu ukashangazwa na mafundisho yake.
29Ke wo sicharelas sar iek manush kai sas les putiera, ai na sar lenge manush kai sicharenas o zakono le Gramnturia.
29Hakuwa kama walimu wao wa Sheria, bali alifundisha kwa mamlaka.