1O Jesus anklisto ando chuno, nakhlo inchal e maria, ai gelo ande pesko foro.
1Yesu alipanda mashua, akavuka ziwa na kufika katika mji wake.
2Andine leste ieke manushes kai sas bango, pashliolas po than. O Jesus dikhlia lengo pachamos, ai phendias le bangeske, "Raduisavo, murho shav! Che bezexa iertime le."
2Hapo watu walimletea mtu mmoja aliyepooza mwili, amelazwa juu ya kitanda. Yesu alipoona imani yao, akamwambia huyo mtu aliyepooza, "Jipe moyo mwanangu! Umesamehewa dhambi zako."
3Antunchi le Gramnoturia phenenas peske, "Sar sai kado manush tromal te lel o than le Devlesko, ke ferdi O Del sai iertil le bezexa!"
3Baadhi ya walimu wa Sheria wakaanza kufikiri, "Mtu huyu anamkufuru Mungu!"
4O Jesus zhanglia lenge ginduria ai phendia, "Sostar si tume kasave chorhe ginduria ande tumaro ilo?
4Yesu aliyajua mawazo yao, akasema, "Kwa nini mnawaza mabaya mioyoni mwenu?
5So si mai vushoro te phenes, 'Che bezexa iertime,' vai 'Wushti opre ai phir?"
5Ni lipi lililo rahisi zaidi: kusema, Umesamehewa dhambi zako, au kusema, Simama, utembee?
6Numa te zhanen ke ka O Shav le Manushesko si e putiera pe phuv te iertil le bezexa." Antunchi phendia le bangeske, ' Wushti, le cho than, ai zha khere!'
6Basi, nataka mjue kwamba Mwana wa Mtu anao uwezo wa kuwasamehe watu dhambi duniani." Hapo akamwambia huyo mtu aliyepooza, "Inuka, chukua kitanda chako, uende nyumbani kwako."
7O manush wushtilo ai gelotar khere.
7Huyo mtu aliyekuwa amepooza akainuka, akaenda nyumbani kwake.
8Kana o narodo dikhlia kodia, daraile, chudisaile, ai luvudinas le Devles kai dias kasavi putiera ka o manush.
8Watu wote katika ule umati walipoona hayo, walishangaa na kuogopa; wakamtukuza Mungu aliyewapa binadamu uwezo wa namna hiyo.
9O Jesus gelotar kotsar, ai dikhlia ieke manushes kai busholas Mate, beshelas tele kai skafidi kai pochinenas e taksa le themeske. Ai phendia leske, "Av pala mande." Wo wushtilo ai liape pala leste.
9Yesu aliondoka hapo, na alipokuwa anakwenda zake, alimwona mtu mmoja aitwaye Mathayo, ameketi katika ofisi ya ushuru. Basi, Yesu akamwambia, "Nifuate." Naye Mathayo akainuka, akamfuata.
10Kana O Jesus xalas ande lesko kher, but manush kai chiden e taksa, ai le bezexale avile te beshen kai skafidi lesa ai leske disiplonsa.
10Yesu alipokuwa nyumbani ameketi kula chakula, watoza ushuru wengi na wahalifu walikuja wakaketi pamoja naye na wanafunzi wake.
11Le Farizeanuria dikhle kodia ai phushle leske disiplon, "Sostar tumaro gazda xal le manushensa kai chiden e taksa ai kodolensa kai si bezexale?"
11Mafarisayo walipoona hayo, wakawaambia wanafunzi wake, "Mbona mwalimu wenu anakula pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi?"
12O Jesus ashundia ai phendia lenge, "Le manush kai si saste chi trobul le dokxtoro, le naswalen trobul.
12Yesu aliwasikia, akasema, "Watu wenye afya hawahitaji daktari; wanaomhitaji ni wale walio wagonjwa. Sikuja kuwaita watu wema, ila wenye dhambi.
13Zhan ai sichon te haliaren, me mangav mila te den iekavres, ai na sakrifis, ke chi avilem te akharav kodolen kai gindinpe vorta angla Del, numa le bezexalen."
13Basi, kajifunzeni maana ya maneno haya: Nataka huruma, wala si dhabihu. Sikuja kuwaita watu wema, bali wenye dhambi."
14Le disipluria le Iovanoske o baptisto avile ka Jesus, ai phushle lestar, "Sostar ame ai le Farizeanuria zhonis butivar, numa chire disipluria chi zhonin?"
14Kisha wanafunzi wa Yohane mbatizaji walimwendea Yesu, wakamwuliza, "Sisi na Mafarisayo hufunga mara nyingi; mbona wanafunzi wako hawafungi?"
15O Jesus phendia lenge, "Sar sai zhelin le manush kai si akharde ka abiav, kana o manush kai ansurilpe lensa le? Numa avela e vriama kai o manush kai ansurilpe avela lino lendar, antunchi zhonina.
15Yesu akawajibu, "Je, walioalikwa arusini wanaweza kuomboleza wakati bwana arusi yupo pamoja nao? La hasha! Lakini wakati utafika ambapo bwana arusi ataondolewa kati yao; wakati huo ndipo watakapofunga.
16Khonik chi thol nevo kotor poxtan te lasharel phurane tsalia, ke o nevo kotor tsigniol, ai kerdiolpe mai nasul o shinimos.
16"Hakuna mtu atiaye kiraka cha nguo mpya katika vazi kuukuu. Maana kiraka hicho kitararua hilo vazi kuukuu, na pale palipokuwa pameraruka pataongezeka.
17Le manush chi thon nevi mol andel phurane morchia moliake, ke le morchia pharhadion, ai e mol shordiol, ai le morchia rimonpe. Numa thon e nevi mol andel morchia, kadia chi e mol ai chi le morchia chi rimonpe."
17Wala hakuna mtu awekaye divai mpya katika viriba vikuukuu. Akifanya hivyo, viriba hupasuka na divai ikamwagika, navyo viriba vikaharibika. Ila divai mpya hutiwa katika viriba vipya, na vyote viwili, viriba na divai, vikahifadhiwa salama."
18Sar O Jesus phenelas lenge kadala vorbi, iek baro andai synagogue avilo ai thodiape ande changende angla leste, ai phendias, " Numa so muli murhi shei; haidi tho cho vas pe late, ai woi traiila."
18Yesu alipokuwa akisema hayo, ofisa mmoja Myahudi alifika, akamwinamia na kusema, "Binti yangu amekufa sasa hivi. Lakini, tafadhali njoo umwekee mkono wako naye ataishi."
19O Jesus wushtilo, ai gelo pala leste, peske disiplonsa.
19Yesu akaondoka pamoja na wanafunzi wake, akamfuata.
20Antunchi, iek naswali zhuvli, kai xasarelas rat de desh u dui bersh, avili palal pala leste, ai azbadia e tivala leska raxamaki.
20Mama mmoja, mgonjwa wa kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili, alimfuata Yesu nyuma, akagusa pindo la vazi lake.
21Woi phenelas peske, "Numa te sai azbava leske tsalia, avava sasti."
21Alifanya hivyo kwani alifikiri moyoni: "Nikigusa tu vazi lake, nitapona."
22O Jesus amboldiape, dikhlia la, ai phendia, "Raduisavo murhi shei! Ke cho pachamos sastiardia tu." Ai ande kodo chaso sastili.
22Basi, Yesu akageuka akamwona, akamwambia, "Binti, jipe moyo! Imani yako imekuponya." Mama huyo akapona saa ileile.
23Kana O Jesus areslo ka kher le baresko andai synagogue. Dikhlia le musikanton, ai baro narodo buntuime, but mui kerenas.
23Kisha Yesu akaingia nyumbani kwa yule ofisa. Na alipowaona wapiga filimbi na umati wa watu wanaofanya matanga,
24Wo phendias lenge, "Zhantar ke e sheiorhi nai muli, numa sovel!" Won asaie lestar.
24akasema, "Ondokeni hapa! Msichana huyu hakufa, amelala tu." Nao wakamcheka.
25Kana gonisardia le narodos, gelo ando kher, lia la vastestar, ai e shovorhi wushtili.
25Basi, umati wa watu ulipoondolewa, Yesu aliingia ndani, akamshika huyo msichana mkono, naye akasimama.
26Kodia viasta geli ande sa kodo them.
26Habari hiyo ikavuma sana katika nchi ile yote.
27Sar zhalastar O Jesus, dui korhe linepe palal leste ai tsipinas, "Al tuke mila anda amende, Shav le Davidosko."
27Yesu aliondoka hapo, na alipokuwa anakwenda, vipofu wawili walimfuata wakipiga kelele, "Mwana wa Daudi, utuhurumie!"
28Kana O Jesus areslo ando kher, le korhe avile leste, O Jesus phushlia le, "Pachan tume ke sai kerav kodia?" "Sai, Gazda," Won phende leske.
28Yesu alipoingia nyumbani, vipofu hao wawili wakamwendea, naye akawauliza, "Je, mnaamini kwamba naweza kuwafanyia jambo hilo?" Nao wakamjibu, "Naam, Mheshimiwa."
29Antunchi azbadia lenge iakha ai phendia, "Te kerdiol tumenge, so pachaian!"
29Hapo Yesu akayagusa macho yao, akasema, "Na iwe kwenu kama mnavyoamini."
30Ai lenge iakha phuterdile. O Jesus phendia lenge, "Len tume sama, te na zhanel khonik!"
30Macho yao yakafunguliwa. Naye Yesu akawaonya kwa ukali: "Msimwambie mtu yeyote jambo hili."
31Numa kana geletar, phende e viasta pe leste pe sa kodo them.
31Lakini wao wakaondoka, wakaeneza habari za Yesu katika nchi ile yote.
32Kana won zhanastar, andine leste ieke manushes kai nashti delas duma ke sas beng ande leste.
32Watu walipokuwa wanakwenda zao, wengine walimletea Yesu mtu mmoja aliyekuwa bubu kwa sababu alikuwa amepagawa na pepo.
33Kana o beng gonime anda leste, o muto dia duma. Sa o narodo chudisaile, ai phenenas, 'Shoxar chi dikhliam kadia ande Israel!"
33Mara tu huyo pepo alipotolewa, mtu huyo aliyekuwa bubu akaanza kuongea tena. Watu wakashangaa na kusema, "Jambo kama hili halijapata kuonekana katika Israeli!"
34Numa le Farizeanuria phenenas, "O baro le bengengo del les e putiera te gonil le bengen."
34Lakini Mafarisayo wakawa wanasema, "Anawatoa pepo kwa nguvu ya mkuu wa pepo wabaya."
35O Jesus gelo anda sa le foruria ai anda sa le gava, ai sicharelas ande lenge synagoguria, delas duma e lashi viasta pa e amperetsia, ai sastiarelas sa le naswalimata ai sa o nasulipe.
35Yesu alitembelea miji yote na vijiji, akafundisha katika masunagogi yao akihubiri Habari Njema ya Ufalme wa Mungu, na kuponya magonjwa yote na udhaifu wa kila namna.
36Kana wo dikhlia o narodo bari mila lia les anda lende, ke chinuinas nekezhime sas, ai nashti zhutinaspe, sar bakriorhe kai nai le pastuxo.
36Basi, alipowaona watu, makundi kwa makundi, aliwaonea huruma kwa sababu walikuwa hoi na wenye wasiwasi kama kondoo wasio na mchungaji.
37Antunchi phendias peske disiplonge, "But jiv si te chidelpe, numa xantsi bucharia si.
37Hapo akawaambia wanafunzi wake, "Mavuno ni mengi, lakini wavunaji ni wachache.
38Rhugin tume ka o gazda le chidimasko te tradel bucharia ande pesko chidimos.
38Kwa hivyo mwombeni mwenye shamba atume wavunaji shambani mwake."