Romani: New Testament

Swahili: New Testament

Revelation

8

1Kana O Bakriorho phuterdia o eftato semno, nas ek bunto ando rhaio pala dopash chaso.
1Na Mwanakondoo alipouvunja mhuri wa saba, kukawa kimya mbinguni kwa muda wa nusu saa.
2Porme dikhlem le efta angelon beshenas anda punrhende angla Del. Won sas dine efta tuturazi.
2Kisha nikawaona wale malaika saba wanaosimama mbele ya Mungu wamepewa tarumbeta saba.
3Aver angelo avilo ai beshlo anda punrhende ka altari, ai wo inkerdia ek kuchi sumnakai pherdi duxi. Wo sas dino but duxi te amil le rhugimasa kodolenge kai sas leske shaven. Lenge rhugimata thode sas po altari kerdia andai sumnakai anglal o than kai o amperato beshel.
3Malaika mwingine akafika, akiwa anachukua chetezo cha dhahabu, akasimama mbele ya madhabahu ya kufukizia ubani. Naye akapewa ubani mwingi autoe sadaka pamoja na sala za watu wote wa Mungu, juu ya madhabahu ya dhahabu iliyo mbele ya kiti cha enzi.
4Thu katar e duxi kai phabolas ai le rhugimasa kodolenge kai si le Devleske andek than gele opre angla Del katar le angelosko vas.
4Moshi wa ubani ukapanda juu, pamoja na sala za watu wa Mungu, kutoka mikononi mwake huyo malaika aliyekuwa mbele ya Mungu.
5Porme o angelo lia e kuchi sumnakai, ai pherdia la la iagasa katar o altari ai shudia la pe phuv. Sas rhonjito, ai bunto, ai rhonjito tele, ai izdralas e phuv.
5Kisha malaika akakichukua hicho chetezo, akakijaza moto wa madhabahuni akakitupa duniani. Kukawa na ngurumo, sauti, umeme na tetemeko la ardhi.
6Le efta angeluria kai sas le efta tuturazi lasharde te phurden le.
6Kisha wale malaika saba wenye tarumbeta saba wakajiweka tayari kupiga mbiu ya mgambo.
7O pervo angelo phurdia leski tuturaza. Babitsa ai iag amime le ratesa hulelas tele pe phuv. E trito partia la phuviaki sas phabardi. E trito partia le krenzheske ai le khasheske sas phabarde. Sa le char sas phabarde.
7Malaika wa kwanza akapiga tarumbeta yake. Mchanganyiko wa mvua ya mawe na moto, pamoja na damu, ukamwagwa juu ya nchi. Theluthi moja ya nchi ikaungua, theluthi moja ya miti ikaungua, na majani yote mabichi yakaungua.
8O duito angelo phurdia leski tuturaza. Vari so sar ek bari plai phabolas la iagasa sas shudini ande maria, ai e trito partia la mariaki parhudili sas ando rat.
8Malaika wa pili akapiga tarumbeta yake. Na kitu kama mlima mkubwa unaowaka moto ukatupwa baharini. Theluthi moja ya bahari ikawa damu,
9E trito partia anda sa le dieli kai traiin ande maria sas mudarde, ai trito anda sa le paraxoduria pharhade sas.
9theluthi moja ya viumbe vya baharini vikafa na theluthi moja ya meli zikaharibiwa.
10O trito angelo phurdia leski tuturaza. Ek bari chererhai pele anda rhaio, phabola sar ek mincha la iagaki, peli pe trito partia anda le paia kai zhal ai po le thana kai o pai avela katar e phuv;
10Kisha malaika wa tatu akapiga tarumbeta yake. Na nyota kubwa ikiwaka kama bonge la moto, ikaanguka kutoka mbinguni, na kutua juu ya theluthi moja ya mito na chemchemi za maji.
11ai o anav le chererhaiesko si "Kerko". Ai trito partia le paiesko avilino votrava. But manush mule katar o pai kana pilie ke avilino votrava.
11(Nyota hiyo inaitwa "Uchungu.") Basi, theluthi moja ya maji yakawa machungu; watu wengi wakafa kutokana na maji hayo, kwa sababu yaligeuka kuwa machungu.
12O shtarto angelo phurdia leski tuturaza. Ai o trito partia le khamesko ai o trito partia le shunutosko ai o trito partia le chere rhaiange sas dukhade, ai o trito partia anda lende sas kerde tuniariko, ai o trito partia le diesesko ai eriatesko nas vediara.
12Kisha malaika wa nne akapiga tarumbeta yake. Ndipo theluthi moja ya jua, ya mwezi na ya nyota ikapata pigo; hata mwangaza ukapoteza theluthi moja ya mng'ao wake. Theluthi moja ya mchana ikakosa mwanga, hali kadhalika na theluthi moja ya usiku.
13Ando murho vizion, dikhlem ek baro vulio vurial ando cheri, ando baro glaso phendia, "Baio! Baio! Si baio kodolenge kai traiin pe phuv, kana le kaver trin angeluria phurden lenge tuturazi!"
13Kisha nikatazama, nikasikia tai akiruka juu kabisa angani anasema kwa sauti kubwa, "Ole, ole, ole kwa wanaoishi duniani wakati malaika watatu waliobaki watakapopiga tarumbeta zao!"